Sam Gidori
Senior Member
- Sep 7, 2020
- 165
- 414
Shirika la Habari linalomilikiwa na Serikali ya Uturuki, Anadolu Agency (AA) limetoa kibali cha kutumiwa kwa ofisi zake katika mji wa Gaza kwa Mashirika ya Habari ya Al Jazeera na Associated Press (AP) baada ya ofisi zao kuharibiwa na shambulio la kombora la Israel siku ya Jumamosi.
Mkurugenzi Mkuu wa AA, Serdar Karagöz amewaandikia barua Wakurugenzi wa Al Jazeera na AP akionesha kusikitishwa kwake na mashambulio ya Israel yanayolenga vyombo vya habari akisema kuwa kumekuwa na jitihada za makusudi za Jeshi la Israel kuwalenga waandishi wa habari ili kuzuia kinachoendelea Gaza kisijulikane duniani.
Karagöz amesema tangu mashambulizi yalipoanza siku ya Jumatatu, wafanyakazi 6 wa Shirika lake wamejeruhiwa na Jeshi la Israel, akiitaka dunia kusimama kupinga jaribio la kukaba uhuru wa habari linalofanywa na Israel.
“Waandishi wa Habari wanaandika taarifa za ukiukwaji wa haki za binadamu na uhalifu wa kivita unaofanyika katika eneo hilo,” ameandika Karagöz, akitoa wito pia kwa vyombo vya habari duniani kushikamana kuhakikisha usimamizi wa “uandishi wa habari usioegemea upande wowote, na kuthamini misingi ya uhuru wa habari ambao unatatizwa na Mamlaka za Israel.”
Mashambulizi ya makombora ya Israel yameendelea siku ya Jumapili katika eneo la Gaza na kusababisha vifo vya watu 42, idadi kubwa zaidi ya vifo kushuhudiwa ndani ya siku moja tangu mashambulizi yalipoanza siku ya Jumatatu, na kupelekea jumla ya idadi ya vifo kufikia watu 188 wakiwamo watoto 55. Israeli imeripoti vifo vya watu 10 wakiwamo watoto wawili.
Waziri Mkuu wa Israel, Benjjamin Netanyahu amesema mashambulio ya Israel hayatakoma licha ya jitihada za Jamii ya Kimataifa kutaka mzozo huo usitishwe.
Chanzo: Daily Sabah
Mkurugenzi Mkuu wa AA, Serdar Karagöz amewaandikia barua Wakurugenzi wa Al Jazeera na AP akionesha kusikitishwa kwake na mashambulio ya Israel yanayolenga vyombo vya habari akisema kuwa kumekuwa na jitihada za makusudi za Jeshi la Israel kuwalenga waandishi wa habari ili kuzuia kinachoendelea Gaza kisijulikane duniani.
Karagöz amesema tangu mashambulizi yalipoanza siku ya Jumatatu, wafanyakazi 6 wa Shirika lake wamejeruhiwa na Jeshi la Israel, akiitaka dunia kusimama kupinga jaribio la kukaba uhuru wa habari linalofanywa na Israel.
“Waandishi wa Habari wanaandika taarifa za ukiukwaji wa haki za binadamu na uhalifu wa kivita unaofanyika katika eneo hilo,” ameandika Karagöz, akitoa wito pia kwa vyombo vya habari duniani kushikamana kuhakikisha usimamizi wa “uandishi wa habari usioegemea upande wowote, na kuthamini misingi ya uhuru wa habari ambao unatatizwa na Mamlaka za Israel.”
Mashambulizi ya makombora ya Israel yameendelea siku ya Jumapili katika eneo la Gaza na kusababisha vifo vya watu 42, idadi kubwa zaidi ya vifo kushuhudiwa ndani ya siku moja tangu mashambulizi yalipoanza siku ya Jumatatu, na kupelekea jumla ya idadi ya vifo kufikia watu 188 wakiwamo watoto 55. Israeli imeripoti vifo vya watu 10 wakiwamo watoto wawili.
Waziri Mkuu wa Israel, Benjjamin Netanyahu amesema mashambulio ya Israel hayatakoma licha ya jitihada za Jamii ya Kimataifa kutaka mzozo huo usitishwe.
Chanzo: Daily Sabah