Lunyungu
JF-Expert Member
- Aug 7, 2006
- 8,873
- 1,890
KATIKA historia ya mahusiano ya watawala na
watawaliwa na hasa pale ambako yanawahusisha watu
wenye historia moja na ambao wanatoka damu moja na
hatma yao ni moja au watu ambao historia ya maisha yao
imefungamana tangu enzi za enzi; endapo mahusiano hayo
baina ya pande hizo mbili hayana budi kukomeshwa na
kuvunjwa, basi sababu za kuvunja na kuyakomesha kwa
njia ya kidemokrasia au ya kimapinduzi ni lazima
zisemwe wazi, kwa ukweli na bayana.
Kwa vile kuvunja uhusiano huo ni jambo ambalo
litawaathiri watu wa pande zote hizo mbili, basi hoja
za kwanini uhusiano huo uvunjwe hazina budi kuwekwa
hadharani.
Hili ni lazima lifanyike ili mahusiano hayo
yatakapovunjwa kusitafutwe kisingizio kingine cha
kuvunjika kwake. Kwa kutangaza hadharani sababu hizo
basi hisia za chuki, uonevu, kisasi, uzandiki, au uovu
wowote zitaweza kuepukwa.
Mahusiano na watawala yaweza kuvunjwa
Kuvunja mahusiano na watawala si jambo geni wala
jepesi kufanywa. Jamii mbalimbali duniani zimeweza
kushuhudia kuvunjwa kwa mahusiano yaliyodumu kwa muda
mrefu kati ya watawala na watawaliwa.
Mahusiano ya namna hiyo yameweza kuvunjwa Marekani na
utawala wa Uingereza (waliandika Azimio la Uhuru),
Ukraine (Mapinduzi ya Chungwa), Lebanon (Mapinduzi
ya Mierezi), Georgia (Mapinduzi ya Waridi) na Kenya
(Ushirikiano wa Upinde wa Mvua). Hivyo, si jambo geni
na si la pekee kwa watu kuamua kuvunja uhusiano na
watawala wao, hata kama ni ndugu zao.
Dhamira ya kuingoa CCM
Kwa kuzingatia historia yetu ya mahusiano kati ya
Watanzania na chama chetu tawala cha CCM, tunaweza
kudhamiria kukiondoa madarakani ifikapo uchaguzi wa
mwaka 2010 kwa kuchukua Bunge la Jamhuri na ifikapo
2015 kuchukua kiti cha urais.
Vyote viwili vikiwezekana mwaka 2010, basi azma ya
kuanza hatua za kulibadili taifa letu na kujenga taifa
jipya la kisasa, lenye kuheshimu katiba, na lenye
kuhakikisha kuwa wana na mabinti wa Tanzania
wanafurahia haki sawa na nafasi sawa katika nchi yao,
itatimia. Kuiondoa CCM madarakani kutafanyika endapo
mkataba na vyama vya upinzani utakubaliwa na vyama
hivyo.
Sababu za kuingoa CCM madarakani
Ni kutokana na dhamira hiyo basi, nimeamua kuainisha
sababu ambazo zinatufanya sisi wana na mabinti wa
Tanzania bila kujali itikadi zetu, hali zetu za
maisha, vyeo na hadhi zetu na vitu vingine
vinavyotutofautisha kama mtu mmoja mmoja kama vile
rangi, kabila, au dini kuvunja mahusiano yanayotufunga
sisi na Chama Cha Mapinduzi na kukiondoa madarakani
kwa njia ya kidemokrasia, kwa nguvu ya sanduku la
kura, kwa kutumia sheria na taratibu zilizopo.
Tumeazimia kufanya hivyo kwa sababu zifuatazo:
Chama Cha Mapinduzi kimeenda kinyume kabisa na katiba
yake, iliyotangaza kuwa Azimio la Arusha ndiyo dira ya
taifa letu na iliyoweka maono ya kitaifa na hata
tafsiri ya azimio hilo iliyotolewa Zanzibar.
Kwa kufanya hivyo serikali ya CCM imeiingiza nchi
katika siasa za kibepari (zenye msingi wa unyonyaji)
bila kuwaambia wananchi wenyewe wakati katiba ya chama
hicho na ile ya nchi bado vinatamka wazi na bayana
kuwa Tanzania ni nchi ya kijamaa, yenye kujenga ujamaa
(usoshalisti) kwa misingi ya kujitegemea.
Chama Cha Mapinduzi kimeruhusu viongozi wake kuvunja
Azimio la Arusha na maelekezo yaliyotolewa na Rais
mstaafu Ali Hassan Mwinyi kuhusu Azimio la Zanzibar
kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee Aprili 25 mwaka 1991.
Miongoni mwa mambo ambayo viongozi wa chama hicho
wanajihusisha nayo licha ya kukatazwa na Azimio la
Zanzibar (Likifafanua Azimio la Arusha) ni pamoja na
kupangisha majumba, kuwa na shamba la zaidi ya hekta
20, kupokea mishahara zaidi ya mmoja wakiwa wamevaa
kofia zaidi ya mbili za serikali au chama.
Chama hiki hivi karibuni kimefurahia kutimiza miaka 30
tangu kuzaliwa kwake, na bila hata hofu wameshindwa
kutaja kabisa miaka 40 ya Azimio la Arusha na hivyo
kuthibitisha kuwa azimio hilo limekufa kiujanja na
kuzikwa kinyemela. Kama CCM ingekuwa na wasema kweli
angalau wangelisema kuwa Azimio la Arusha limekufa, na
maelezo ya azimio hilo ya kule Zanzibar nayo yamekufa,
kila mtu na lwake.
Chama Cha Mapinduzi kwa kupitia Bunge la Jamhuri ya
Muungano na wabunge wake ambao ndio wengi bungeni,
kimeshindwa kuisimamia serikali ya Jamhuri ya Muungano
na hivyo kuifanya isiwajibike kwa wananchi kama
inavyopaswa.
Ni Bunge lenye wingi wa wabunge wa CCM ambalo
limeiacha serikali yake kuingia katika mikataba mibovu
na isiyo na maslahi kwa nchi kama ile ya madini na
nishati (mifano ya IPTL, Richmond, na Buzwagi iko
mawazoni), na mikataba ya uendeshaji wa kampuni za
Kitanzania kama ile ya Tanesco na Dawasco na mingine
ya ubinafsishaji.
Ni wabunge hao ambao wamegoma kutunga sheria ambayo
ingewapa uwezo wa kuiangalia na hata kuitengua
mikataba yoyote ambayo haina maslahi kwa taifa au
yenye athari mbalimbali kwa wananchi, mazingira, na
usalama wa taifa.
Ni bunge hili ambalo licha ya vyanzo vingi vya kodi,
limeshindwa kupitisha vyanzo vipya vya kodi ambavyo
vingelifanya taifa letu kuwa na uchumi huru zaidi na
si tegemezi. Bunge letu bado limeshindwa kubuni vyanzo
vipya vya mapato ili hatimaye bajeti yetu iwe huru
kutoka kwa wafadhili na wahisani.
Ni Bunge hilo hilo la wingi wa wabunge wa CCM
lililoshindwa kabisa kuikemea serikali hasa
ilipojihusisha na ununuzi wa ndege ya kifahari ya rais
pamoja na rada isiyokidhi mahitaji yetu, na yenye
gharama kubwa.
Bunge hili limeshindwa kumtaka rais kuruhusu ripoti ya
Benki ya Dunia kupinga ununuzi wa rada hiyo kuwekwa
hadharani ili wananchi wajue ni jinsi gani ununuzi huo
ulikosa busara na sababu ya msingi.
Serikali ya CCM imeshindwa kukemea viongozi wake
waliotumia ofisi zao za umma vibaya na kuwavumilia kwa
kuwalinda. Kitendo cha Serikali ya CCM kukubali na
kutoa baraka yake kwa rais mstaafu kufanya shughuli
binafsi Ikulu, na kuruhusu maafisa wake kuwa na hisa
katika kampuni ambazo wao wana maslahi, na kitendo cha
kutaka wananchi wapuuzie hoja zinazohoji utaratibu
huo, ni kitendo kinachoonyesha ni jinsi gani chama
hiki kimelewa madaraka. Kwa kufanya hicho CCM si tu
imejenga misingi mibovu ya maadili, bali pia
imeonyesha mfano mbaya kabisa kwa viongozi wa mbeleni.
Chama Cha Mapinduzi kwa kupitia serikali zake,
kimeshindwa kuipa sekta ya elimu mkazo na msisitizo
unaostahili na hivyo kushindwa kuleta mabadiliko ya
kielimu yanayotakiwa katika kuleta mageuzi makubwa ya
kiuchumi na kijamii.
Licha ya kuongeza idadi ya shule, madarasa, wanafunzi
na vyuo, serikali ya CCM imeshindwa kuinua ubora wa
elimu ya kati na ya juu na hivyo kushindwa kuandaa
taifa la wasomi waliobobea, watafiti mahiri, na
wachunguzi wa mambo waliofuzu.
Badala yake wasomi wale wachache ambao Tanzania inao
wameishia kuwa wanasiasa, na wale walioko katika
taaluma maslahi yao ni duni sana na hivyo wengine
kuamua kwenda nje ya nchi na wengine kutokujihusisha
kabisa na mambo ya ndani ya maendeleo ya Tanzania.
Hili linadumaza elimu ya kizazi kijacho cha wasomi.
Matokeo yake ni kuwa Serikali ya CCM imeshindwa kubuni
mikakati inayowezekana ya kuiinua Tanzania kitaaluma
na kuipatia faida ya kiushindani katika soko la ajira
za ndani na za kimataifa.
Serikali ya Chama Cha Mapinduzi imeshindwa kujenga na
kuendeleza sekta nzuri, ya kisasa, na iliyo endelevu
ya afya na badala yake matatizo ya magonjwa ya
milipuko yasiyo ya lazima bado yanaendelea kuua watu
wetu na kudhalilisha utu wa Watanzania.
Licha ya mafanikio kidogo ya hapa na pale ya ujenzi wa
majengo ya hospitali na kliniki, Serikali ya CCM
imeshindwa kupunguza kwa kiasi kikubwa maambukizi ya
magonjwa makubwa, kupunguza vifo vya watoto na hasa
kuhakikisha upatikanaji wa chanjo za watoto ambazo
zimepungua kwa kiasi kikubwa sasa hivi.
Ni serikali ya chama hicho ambayo imeshindwa kufanya
sekta ya afya kuwa ya kisasa zaidi na inayowafikia
watu wengi zaidi na kwa muda mfupi zaidi.
Ni kutokana na kushindwa huku ndio maana Serikali ya
CCM imejiwekea utaratibu wa kupeleka viongozi wake nje
ya nchi huku watu wa kawaida wakiendelea kuhangaika
kila kukicha kutafuta huduma bora za afya. Hata
zinapotokea ajali, viongozi wao watapelekwa nje, na
wale waliokuwa nao watatibiwa humu humu nchini.
Kwa kukimbilia uwekezaji katika madini na utalii na
kutokuweka mazingira mazuri ya uwekezaji katika sekta
ya sfya, Serikali ya CCM inatengeneza taifa la watu
dhaifu na walio goigoi na ambao afya zao ziko shakani.
Licha ya kuendelea kuimba wimbo wa Kilimo ndio uti wa
mgongo wa taifa na licha ya kutambua kuwa wananchi
wetu wengi wameajiriwa katika kilimo, Serikali ya CCM
imeshindwa kabisa kubadilisha kilimo chetu na
kukifanya kuwa cha kisasa na kinachotosheleza mahitaji
yetu na ziada.
Serikali ya chama hiki imeshindwa kuongoza mapinduzi
ya kilimo licha ya ahadi nyingi, ambayo yangesababisha
tuachane na jembe la mkono na kuleta kilimo ambacho
kimeanza kutumia mashine za kisasa, utaalamu wa
kisasa, na taratibu za kisasa za kilimo na hivyo
kukifanya kisiwe cha kujihifadhi tu bali kiwe cha
kutosheleza mahitaji ya nyumbani na ziada. Wameshindwa
kufanya hivi licha ya nchi yetu kuwa na Chuo Kikuu cha
Kilimo na taasisi mbalimbali za utafiti wa mazao na
mifugo ambazo zinafanya kazi chini ya uwezo wake
kupita kiasi.
Serikali ya CCM inaamini kuwa Tanzania pasipo CCM
madarakani haiwezekani. Tabia ya baadhi ya viongozi wa
chama hicho na vyombo ambavyo vimo kwenye mikono yao
kuendelea kutishia wananchi kuwa endapo chama kingine
kitashika madaraka basi nchi itaingia matatani na
kutatokea machafuko makubwa ni tabia ya watu
walioishiwa hoja na yenye lengo la kutishia watu.
Vitisho hivyo vya mara kwa mara vinavyofanywa na
baadhi ya viongozi hawa vina lengo la kutaka kuendelea
kujikita zaidi madarakani kwa kutumia hofu na mbinu za
vitisho. Kwa kuendeleza mbinu hizi zilizopotoka,
serikali ya CCM inataka kuendeleza utawala wake kwa
kuchezea hisia na vionjo vya wananchi kwa mbinu chafu
za kuwatishia.
Kwa makusudi kabisa wameamua kuziacha na kuzitupilia
mbali fikra za Mwalimu Nyerere, fikra ambazo msingi
wake ulikuwa ni kujenga taifa la watu walio huru na
sawa, na taifa ambalo kila mtu ana haki ya
kutambuliwa na kuthaminiwa utu wake. CCM wamejikuta
wakibadili maana ya maendeleo kutoka maendeleo ya watu
na kuwa maendeleo ya vitu.
Kwa kufanya hivyo, wametilia mkazo umwagaji wa mapesa
na vitu bila kuathiri maisha ya mtu wa kawaida.
Matokeo yake ni tofauti ya maisha ikiendelea kuonekana
kati ya watu na vitu, huku wachache wakiendelea
kunufaika kwa vitu huku wengi wakiendelea kutaabika.
Azimio
Kwa kuzingatia sababu zote hizo na nyingine ambazo mtu
mmoja mmoja anaweza kuwa nazo, tukitambua kuwa Chama
Cha Mapinduzi kimepewa nafasi nyingi za kujirekebisha,
na kimeshindwa kufanya hivyo na badala yake kuendelea
kutawala bila kujali hisia na maslahi ya wananchi,
tukifahamu kuwa nchi yetu haiwezi kusonga mbele na
kupiga hatua ya haraka ya maendeleo kwa kadiri ya
kwamba CCM bado iko madarakani, tunajikuta
tunakabiliwa na uamuzi mmoja tu wa makusudi, wazi, na
dhahiri, ambao tunaweza kuuchukua.
Sisi wananchi wa Tanzania, tulio nyumbani na
ughaibuni, tukiwa na vingi vinavyotutofautisha kama
mtu mmoja mmoja, kama vile rangi, dini, nasaba,
makabila, vyeo, hadhi, nk na ambao tuko ndani na nje
ya CCM, ndani na nje ya upinzani na wale ambao
hatufungamani na chama chochote au itikadi yoyote ya
kisiasa tukiunganishwa na tunu za utii kwa nchi na
uzalendo kwa taifa, na tukisukumwa na matamanio kuwa
siku moja watoto na watoto wa watoto wetu wataikuta
nchi hii iliyojaa fanaka na neema, tunajikuta
tukitangaza mara moja na daima kuwa:
Chama Cha Mapinduzi, ni lazima kiondolewe madarakani
kwa kutumia njia za kidemokrasia na kwa kutumia nguvu
ya sanduku la kura kwenye uchaguzi wa 2010 kwa
kuwanyima wagombea wao kura za ubunge na uwakilishi
mwingine wowote ule.
Na pia tunakoelekea huko tutaanza kuwanyima kura za
uwakilishi katika chaguzi ndogondogo zinazofanyika
kuanzia sasa kama za madiwani, kama ishara ya
kuonyesha kuwakataa kwetu na kukataa sera zao ambazo
zimeifikisha nchi yetu hapa ilipo.
Azimio hilo tunaliingia sisi kama mtu mmoja mmoja na
kama jumuiya, tukijua kwa hakika kuwa kuondoka kwa CCM
madarakani kunawezekana, na tukitambua kuwa kushindwa
kuiondosha CCM madarakani ni kuendeleza utawala wa
chama kisichojirudi na ambacho kimebadili sera zake za
kujali wakulima na wafanyakazi wa nchi hii, na badala
yake kukumbatia kundi la watu wachache wenye kujali
maslahi binafsi zaidi kuliko ya taifa na mwongozo wa
katiba.
Tunaweza kuazimia hayo tukiwa na akili timamu, bila
shurti, vitisho, ahadi ya cheo au madaraka, tukijua
wazi kuwa kwa kuweka majina yetu hadharani tutakuwa
tumeonyesha kitendo kikuu cha kutowakubali CCM.
Tunaweza kufanya hivi kwa ajili ya mapenzi ya nchi
zaidi kuliko kitu kingine chochote. Mungu atusaidie.
Pindi azimio hili likikubalika na wananchi wengi,
tutaweka hadharani mkataba na vyama vya upinzani ambao
ni lazima waukubali wote au waukatae wote.
Wakiukubali tutawapa Bunge mwaka 2010; wakiukataa
tutawapa tena nafasi CCM lakini tutaendeleza mapambano
ya kifikra hadi CCM ibadilike au chama kingine
kiimarike na kuweza kuchukua nafasi ya CCM kwa
kuzingatia misingi ya mkataba huo.
Mungu ibariki Afrika, Mungu ibariki Tanzania.
watawaliwa na hasa pale ambako yanawahusisha watu
wenye historia moja na ambao wanatoka damu moja na
hatma yao ni moja au watu ambao historia ya maisha yao
imefungamana tangu enzi za enzi; endapo mahusiano hayo
baina ya pande hizo mbili hayana budi kukomeshwa na
kuvunjwa, basi sababu za kuvunja na kuyakomesha kwa
njia ya kidemokrasia au ya kimapinduzi ni lazima
zisemwe wazi, kwa ukweli na bayana.
Kwa vile kuvunja uhusiano huo ni jambo ambalo
litawaathiri watu wa pande zote hizo mbili, basi hoja
za kwanini uhusiano huo uvunjwe hazina budi kuwekwa
hadharani.
Hili ni lazima lifanyike ili mahusiano hayo
yatakapovunjwa kusitafutwe kisingizio kingine cha
kuvunjika kwake. Kwa kutangaza hadharani sababu hizo
basi hisia za chuki, uonevu, kisasi, uzandiki, au uovu
wowote zitaweza kuepukwa.
Mahusiano na watawala yaweza kuvunjwa
Kuvunja mahusiano na watawala si jambo geni wala
jepesi kufanywa. Jamii mbalimbali duniani zimeweza
kushuhudia kuvunjwa kwa mahusiano yaliyodumu kwa muda
mrefu kati ya watawala na watawaliwa.
Mahusiano ya namna hiyo yameweza kuvunjwa Marekani na
utawala wa Uingereza (waliandika Azimio la Uhuru),
Ukraine (Mapinduzi ya Chungwa), Lebanon (Mapinduzi
ya Mierezi), Georgia (Mapinduzi ya Waridi) na Kenya
(Ushirikiano wa Upinde wa Mvua). Hivyo, si jambo geni
na si la pekee kwa watu kuamua kuvunja uhusiano na
watawala wao, hata kama ni ndugu zao.
Dhamira ya kuingoa CCM
Kwa kuzingatia historia yetu ya mahusiano kati ya
Watanzania na chama chetu tawala cha CCM, tunaweza
kudhamiria kukiondoa madarakani ifikapo uchaguzi wa
mwaka 2010 kwa kuchukua Bunge la Jamhuri na ifikapo
2015 kuchukua kiti cha urais.
Vyote viwili vikiwezekana mwaka 2010, basi azma ya
kuanza hatua za kulibadili taifa letu na kujenga taifa
jipya la kisasa, lenye kuheshimu katiba, na lenye
kuhakikisha kuwa wana na mabinti wa Tanzania
wanafurahia haki sawa na nafasi sawa katika nchi yao,
itatimia. Kuiondoa CCM madarakani kutafanyika endapo
mkataba na vyama vya upinzani utakubaliwa na vyama
hivyo.
Sababu za kuingoa CCM madarakani
Ni kutokana na dhamira hiyo basi, nimeamua kuainisha
sababu ambazo zinatufanya sisi wana na mabinti wa
Tanzania bila kujali itikadi zetu, hali zetu za
maisha, vyeo na hadhi zetu na vitu vingine
vinavyotutofautisha kama mtu mmoja mmoja kama vile
rangi, kabila, au dini kuvunja mahusiano yanayotufunga
sisi na Chama Cha Mapinduzi na kukiondoa madarakani
kwa njia ya kidemokrasia, kwa nguvu ya sanduku la
kura, kwa kutumia sheria na taratibu zilizopo.
Tumeazimia kufanya hivyo kwa sababu zifuatazo:
Chama Cha Mapinduzi kimeenda kinyume kabisa na katiba
yake, iliyotangaza kuwa Azimio la Arusha ndiyo dira ya
taifa letu na iliyoweka maono ya kitaifa na hata
tafsiri ya azimio hilo iliyotolewa Zanzibar.
Kwa kufanya hivyo serikali ya CCM imeiingiza nchi
katika siasa za kibepari (zenye msingi wa unyonyaji)
bila kuwaambia wananchi wenyewe wakati katiba ya chama
hicho na ile ya nchi bado vinatamka wazi na bayana
kuwa Tanzania ni nchi ya kijamaa, yenye kujenga ujamaa
(usoshalisti) kwa misingi ya kujitegemea.
Chama Cha Mapinduzi kimeruhusu viongozi wake kuvunja
Azimio la Arusha na maelekezo yaliyotolewa na Rais
mstaafu Ali Hassan Mwinyi kuhusu Azimio la Zanzibar
kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee Aprili 25 mwaka 1991.
Miongoni mwa mambo ambayo viongozi wa chama hicho
wanajihusisha nayo licha ya kukatazwa na Azimio la
Zanzibar (Likifafanua Azimio la Arusha) ni pamoja na
kupangisha majumba, kuwa na shamba la zaidi ya hekta
20, kupokea mishahara zaidi ya mmoja wakiwa wamevaa
kofia zaidi ya mbili za serikali au chama.
Chama hiki hivi karibuni kimefurahia kutimiza miaka 30
tangu kuzaliwa kwake, na bila hata hofu wameshindwa
kutaja kabisa miaka 40 ya Azimio la Arusha na hivyo
kuthibitisha kuwa azimio hilo limekufa kiujanja na
kuzikwa kinyemela. Kama CCM ingekuwa na wasema kweli
angalau wangelisema kuwa Azimio la Arusha limekufa, na
maelezo ya azimio hilo ya kule Zanzibar nayo yamekufa,
kila mtu na lwake.
Chama Cha Mapinduzi kwa kupitia Bunge la Jamhuri ya
Muungano na wabunge wake ambao ndio wengi bungeni,
kimeshindwa kuisimamia serikali ya Jamhuri ya Muungano
na hivyo kuifanya isiwajibike kwa wananchi kama
inavyopaswa.
Ni Bunge lenye wingi wa wabunge wa CCM ambalo
limeiacha serikali yake kuingia katika mikataba mibovu
na isiyo na maslahi kwa nchi kama ile ya madini na
nishati (mifano ya IPTL, Richmond, na Buzwagi iko
mawazoni), na mikataba ya uendeshaji wa kampuni za
Kitanzania kama ile ya Tanesco na Dawasco na mingine
ya ubinafsishaji.
Ni wabunge hao ambao wamegoma kutunga sheria ambayo
ingewapa uwezo wa kuiangalia na hata kuitengua
mikataba yoyote ambayo haina maslahi kwa taifa au
yenye athari mbalimbali kwa wananchi, mazingira, na
usalama wa taifa.
Ni bunge hili ambalo licha ya vyanzo vingi vya kodi,
limeshindwa kupitisha vyanzo vipya vya kodi ambavyo
vingelifanya taifa letu kuwa na uchumi huru zaidi na
si tegemezi. Bunge letu bado limeshindwa kubuni vyanzo
vipya vya mapato ili hatimaye bajeti yetu iwe huru
kutoka kwa wafadhili na wahisani.
Ni Bunge hilo hilo la wingi wa wabunge wa CCM
lililoshindwa kabisa kuikemea serikali hasa
ilipojihusisha na ununuzi wa ndege ya kifahari ya rais
pamoja na rada isiyokidhi mahitaji yetu, na yenye
gharama kubwa.
Bunge hili limeshindwa kumtaka rais kuruhusu ripoti ya
Benki ya Dunia kupinga ununuzi wa rada hiyo kuwekwa
hadharani ili wananchi wajue ni jinsi gani ununuzi huo
ulikosa busara na sababu ya msingi.
Serikali ya CCM imeshindwa kukemea viongozi wake
waliotumia ofisi zao za umma vibaya na kuwavumilia kwa
kuwalinda. Kitendo cha Serikali ya CCM kukubali na
kutoa baraka yake kwa rais mstaafu kufanya shughuli
binafsi Ikulu, na kuruhusu maafisa wake kuwa na hisa
katika kampuni ambazo wao wana maslahi, na kitendo cha
kutaka wananchi wapuuzie hoja zinazohoji utaratibu
huo, ni kitendo kinachoonyesha ni jinsi gani chama
hiki kimelewa madaraka. Kwa kufanya hicho CCM si tu
imejenga misingi mibovu ya maadili, bali pia
imeonyesha mfano mbaya kabisa kwa viongozi wa mbeleni.
Chama Cha Mapinduzi kwa kupitia serikali zake,
kimeshindwa kuipa sekta ya elimu mkazo na msisitizo
unaostahili na hivyo kushindwa kuleta mabadiliko ya
kielimu yanayotakiwa katika kuleta mageuzi makubwa ya
kiuchumi na kijamii.
Licha ya kuongeza idadi ya shule, madarasa, wanafunzi
na vyuo, serikali ya CCM imeshindwa kuinua ubora wa
elimu ya kati na ya juu na hivyo kushindwa kuandaa
taifa la wasomi waliobobea, watafiti mahiri, na
wachunguzi wa mambo waliofuzu.
Badala yake wasomi wale wachache ambao Tanzania inao
wameishia kuwa wanasiasa, na wale walioko katika
taaluma maslahi yao ni duni sana na hivyo wengine
kuamua kwenda nje ya nchi na wengine kutokujihusisha
kabisa na mambo ya ndani ya maendeleo ya Tanzania.
Hili linadumaza elimu ya kizazi kijacho cha wasomi.
Matokeo yake ni kuwa Serikali ya CCM imeshindwa kubuni
mikakati inayowezekana ya kuiinua Tanzania kitaaluma
na kuipatia faida ya kiushindani katika soko la ajira
za ndani na za kimataifa.
Serikali ya Chama Cha Mapinduzi imeshindwa kujenga na
kuendeleza sekta nzuri, ya kisasa, na iliyo endelevu
ya afya na badala yake matatizo ya magonjwa ya
milipuko yasiyo ya lazima bado yanaendelea kuua watu
wetu na kudhalilisha utu wa Watanzania.
Licha ya mafanikio kidogo ya hapa na pale ya ujenzi wa
majengo ya hospitali na kliniki, Serikali ya CCM
imeshindwa kupunguza kwa kiasi kikubwa maambukizi ya
magonjwa makubwa, kupunguza vifo vya watoto na hasa
kuhakikisha upatikanaji wa chanjo za watoto ambazo
zimepungua kwa kiasi kikubwa sasa hivi.
Ni serikali ya chama hicho ambayo imeshindwa kufanya
sekta ya afya kuwa ya kisasa zaidi na inayowafikia
watu wengi zaidi na kwa muda mfupi zaidi.
Ni kutokana na kushindwa huku ndio maana Serikali ya
CCM imejiwekea utaratibu wa kupeleka viongozi wake nje
ya nchi huku watu wa kawaida wakiendelea kuhangaika
kila kukicha kutafuta huduma bora za afya. Hata
zinapotokea ajali, viongozi wao watapelekwa nje, na
wale waliokuwa nao watatibiwa humu humu nchini.
Kwa kukimbilia uwekezaji katika madini na utalii na
kutokuweka mazingira mazuri ya uwekezaji katika sekta
ya sfya, Serikali ya CCM inatengeneza taifa la watu
dhaifu na walio goigoi na ambao afya zao ziko shakani.
Licha ya kuendelea kuimba wimbo wa Kilimo ndio uti wa
mgongo wa taifa na licha ya kutambua kuwa wananchi
wetu wengi wameajiriwa katika kilimo, Serikali ya CCM
imeshindwa kabisa kubadilisha kilimo chetu na
kukifanya kuwa cha kisasa na kinachotosheleza mahitaji
yetu na ziada.
Serikali ya chama hiki imeshindwa kuongoza mapinduzi
ya kilimo licha ya ahadi nyingi, ambayo yangesababisha
tuachane na jembe la mkono na kuleta kilimo ambacho
kimeanza kutumia mashine za kisasa, utaalamu wa
kisasa, na taratibu za kisasa za kilimo na hivyo
kukifanya kisiwe cha kujihifadhi tu bali kiwe cha
kutosheleza mahitaji ya nyumbani na ziada. Wameshindwa
kufanya hivi licha ya nchi yetu kuwa na Chuo Kikuu cha
Kilimo na taasisi mbalimbali za utafiti wa mazao na
mifugo ambazo zinafanya kazi chini ya uwezo wake
kupita kiasi.
Serikali ya CCM inaamini kuwa Tanzania pasipo CCM
madarakani haiwezekani. Tabia ya baadhi ya viongozi wa
chama hicho na vyombo ambavyo vimo kwenye mikono yao
kuendelea kutishia wananchi kuwa endapo chama kingine
kitashika madaraka basi nchi itaingia matatani na
kutatokea machafuko makubwa ni tabia ya watu
walioishiwa hoja na yenye lengo la kutishia watu.
Vitisho hivyo vya mara kwa mara vinavyofanywa na
baadhi ya viongozi hawa vina lengo la kutaka kuendelea
kujikita zaidi madarakani kwa kutumia hofu na mbinu za
vitisho. Kwa kuendeleza mbinu hizi zilizopotoka,
serikali ya CCM inataka kuendeleza utawala wake kwa
kuchezea hisia na vionjo vya wananchi kwa mbinu chafu
za kuwatishia.
Kwa makusudi kabisa wameamua kuziacha na kuzitupilia
mbali fikra za Mwalimu Nyerere, fikra ambazo msingi
wake ulikuwa ni kujenga taifa la watu walio huru na
sawa, na taifa ambalo kila mtu ana haki ya
kutambuliwa na kuthaminiwa utu wake. CCM wamejikuta
wakibadili maana ya maendeleo kutoka maendeleo ya watu
na kuwa maendeleo ya vitu.
Kwa kufanya hivyo, wametilia mkazo umwagaji wa mapesa
na vitu bila kuathiri maisha ya mtu wa kawaida.
Matokeo yake ni tofauti ya maisha ikiendelea kuonekana
kati ya watu na vitu, huku wachache wakiendelea
kunufaika kwa vitu huku wengi wakiendelea kutaabika.
Azimio
Kwa kuzingatia sababu zote hizo na nyingine ambazo mtu
mmoja mmoja anaweza kuwa nazo, tukitambua kuwa Chama
Cha Mapinduzi kimepewa nafasi nyingi za kujirekebisha,
na kimeshindwa kufanya hivyo na badala yake kuendelea
kutawala bila kujali hisia na maslahi ya wananchi,
tukifahamu kuwa nchi yetu haiwezi kusonga mbele na
kupiga hatua ya haraka ya maendeleo kwa kadiri ya
kwamba CCM bado iko madarakani, tunajikuta
tunakabiliwa na uamuzi mmoja tu wa makusudi, wazi, na
dhahiri, ambao tunaweza kuuchukua.
Sisi wananchi wa Tanzania, tulio nyumbani na
ughaibuni, tukiwa na vingi vinavyotutofautisha kama
mtu mmoja mmoja, kama vile rangi, dini, nasaba,
makabila, vyeo, hadhi, nk na ambao tuko ndani na nje
ya CCM, ndani na nje ya upinzani na wale ambao
hatufungamani na chama chochote au itikadi yoyote ya
kisiasa tukiunganishwa na tunu za utii kwa nchi na
uzalendo kwa taifa, na tukisukumwa na matamanio kuwa
siku moja watoto na watoto wa watoto wetu wataikuta
nchi hii iliyojaa fanaka na neema, tunajikuta
tukitangaza mara moja na daima kuwa:
Chama Cha Mapinduzi, ni lazima kiondolewe madarakani
kwa kutumia njia za kidemokrasia na kwa kutumia nguvu
ya sanduku la kura kwenye uchaguzi wa 2010 kwa
kuwanyima wagombea wao kura za ubunge na uwakilishi
mwingine wowote ule.
Na pia tunakoelekea huko tutaanza kuwanyima kura za
uwakilishi katika chaguzi ndogondogo zinazofanyika
kuanzia sasa kama za madiwani, kama ishara ya
kuonyesha kuwakataa kwetu na kukataa sera zao ambazo
zimeifikisha nchi yetu hapa ilipo.
Azimio hilo tunaliingia sisi kama mtu mmoja mmoja na
kama jumuiya, tukijua kwa hakika kuwa kuondoka kwa CCM
madarakani kunawezekana, na tukitambua kuwa kushindwa
kuiondosha CCM madarakani ni kuendeleza utawala wa
chama kisichojirudi na ambacho kimebadili sera zake za
kujali wakulima na wafanyakazi wa nchi hii, na badala
yake kukumbatia kundi la watu wachache wenye kujali
maslahi binafsi zaidi kuliko ya taifa na mwongozo wa
katiba.
Tunaweza kuazimia hayo tukiwa na akili timamu, bila
shurti, vitisho, ahadi ya cheo au madaraka, tukijua
wazi kuwa kwa kuweka majina yetu hadharani tutakuwa
tumeonyesha kitendo kikuu cha kutowakubali CCM.
Tunaweza kufanya hivi kwa ajili ya mapenzi ya nchi
zaidi kuliko kitu kingine chochote. Mungu atusaidie.
Pindi azimio hili likikubalika na wananchi wengi,
tutaweka hadharani mkataba na vyama vya upinzani ambao
ni lazima waukubali wote au waukatae wote.
Wakiukubali tutawapa Bunge mwaka 2010; wakiukataa
tutawapa tena nafasi CCM lakini tutaendeleza mapambano
ya kifikra hadi CCM ibadilike au chama kingine
kiimarike na kuweza kuchukua nafasi ya CCM kwa
kuzingatia misingi ya mkataba huo.
Mungu ibariki Afrika, Mungu ibariki Tanzania.