Anachokitetea Lissu kwenye mchanga ndio kinachotokea IPTL

Kidamva

JF-Expert Member
Dec 3, 2013
2,581
1,981
Kumekuwa na malumbano kuhusu hatua ya Rais Magufuli kukomalia mchanga wa dhahabu (makinikia).

Mwanasheria Mkuu wa Chadema Tundu Lissu amekosoa hatua hiyo akisema kinachotakiwa ni kufunga mikataba kwanza vibginevyo tutashitakiwa na tutashindwa.

Hali hiyo ndio inayojitokeza kwenye mkataba wa IPTL na Serikali ulioingiwa mwaka 1994.
Kila mwezi Tanesco inailipa IPTL zaidi ya sh3 billion kama service charge. Ni mkataba uliozua Maneno mengi kwa miaka mingi.

Lakini juzi Ewura wameitisha maoni ikiwa ni mchakato wa kuongeza leseni ya IPTL. Kelele zimeanza, wanaharakati na wanasiasa wanahoji kwanini IPTL ipewe leseni wakati mkataba wake una harufu ya ufisadi.

Lakini Ewura wanasema IPTL ina mkataba wa kuzalisha umeme hadi mwaka 2022, hivyo wanatakiwa waongezewe leseni.
Issue hapa ni sheria. Kosa tulilofanya ni kuingia mikataba mibovu na waliohusika wapo wanadunda tu.

Ndicho anachokisema Lissu, sheria sheria sheria.
 
Kumekuwa na malumbano kuhusu hatua ya Rais Magufuli kukomalia mchanga wa dhahabu (makinikia).
Mwanasheria Mkuu wa Chadema Tundu Lissu amekosoa hatua hiyo akisema kinachotakiwa ni kufunga mikataba kwanza vibginevyo tutashitakiwa na tutashindwa.
Hali hiyo ndio inayojitokeza kwenye mkataba wa IPTL na Serikali ulioingiwa mwaka 1994.
Kila mwezi Tanesco inailipa IPTL zaidi ya sh3 billion kama service charge. Ni mkataba uliozua Maneno mengi kwa miaka mingi.
Lakini juzi Ewura wameitisha maoni ikiwa ni mchakato wa kuongeza leseni ya IPTL. Kelele zimeanza, wanaharakati na wanasiasa wanahoji kwanini IPTL ipewe leseni wakati mkataba wake una harufu ya ufisadi.
Lakini Ewura wanasema IPTL ina mkataba wa kuzalisha umeme hadi mwaka 2022, hivyo wanatakiwa waongezewe leseni.
Issue hapa ni sheria. Kosa tulilofanya ni kuingia mikataba mibovu na waliohusika wapo wanadunda tu.
Ndicho anachokisema Lissu, sheria sheria sheria.
Nimefurahi umeanzisha huu uzi kwa sababu utaelezea kwa nini mimi simuelewi Lissu.

Lissu ni mwanasheria aliebobea. Anafahamu sheria za mikataba na kwamba itachukua muda mrefu sana kujipanga kukabili hii mikataba mibovu ya madini. Kurekebisha mikataba sio kitu cha kufanyika kwa papara ama sivyo tutashindwa mahakamani.

Lakini wizi uliofanywa na ACACIA (kudanganya kilichomo kwenye makinikia) ni kosa la jinai na hauhusiki na mkataba mbovu. Hili tatizo liko kwenye uwezo wetu kulikabili kama hivi kuzuia mchanga mpaka tutakapojiridhisha ni kiasi gani cha madini kimo na kama wametudanganya au la katika declaration zao. Sijui kwa nini Lissu - mwanasheria ngangari - haliongelei hili bali anatutisha kuwa tutashitakiwa na huyu mwizi.

Mawili, ama anakula na huyu mwizi au uanasheria wake una walakin.
 
Nimefurahi umeanzisha huu uzi kwa sababu utaelezea kwa nini mimi simuelewi Lissu.

Lissu ni mwanasheria aliebobea. Anafahamu sheria za mikataba na kwamba itachukua muda mrefu sana kujipanga kukabili hii mikataba mibovu ya madini. Kurekebisha mikataba sio kitu cha kufanyika kwa papara ama sivyo tutashindwa mahakamani.

Lakini wizi uliofanywa na ACACIA (kudanganja kilichomo kwenye makinikia) ni kosa la jinai na hauhusiki na mkataba mbovu. Hili tatizo liko kwenye uwezo wetu kulikabili kama hivi kuzuia mchanga mpaka tutakapojiridhisha ni kiasi gani cha madini kimo na kama wametudanganya au la katika declaration zao. Sijui kwa nini Lissu - mwanasheria ngangari - haliongelei hili bali anatutisha kuwa tutashitakiwa na huyu mwizi.

Mawili, ama anakula na huyu mwizi au uanasheria wake una walakin.


Duh umejichanganya hadi sijui nikusaidieje? Pole kaka
 
Only the intelligent ones will understand Lissu and not otherwise.The rest will understand when it is already too late.
Only people with least clear minds do fall or get entrapped into Lissu's snare - Bush lawyers in a Kangaroo Court.
 
Lissu hana jipya. Kazi yake kubwa ni kutetea majizi ili mradi tu atapata chake kwanza.
Wote mtakuwa mashahidi, Lowassa aliwahi kushutumiwa vikali kuwa ni fisadi hadi akawekwa kwenye LIST OF SHAME. Mwaka juzi alipoonekana kuwa ni mtaji kwao ghafla akageuka kuwa MALAIKA.
Katika issue ya mchanga (makinikia ) hivi kuna sheria gani ya kimataifa inayoruhusu wawekezaji kutudanganya kuhusu uwepo wa madini mengi kwenye mchanga?
Lissu kazi yake kubwa ni kushabikia tu sisi kuibiwa.
 
Nimefurahi umeanzisha huu uzi kwa sababu utaelezea kwa nini mimi simuelewi Lissu.

Lissu ni mwanasheria aliebobea. Anafahamu sheria za mikataba na kwamba itachukua muda mrefu sana kujipanga kukabili hii mikataba mibovu ya madini. Kurekebisha mikataba sio kitu cha kufanyika kwa papara ama sivyo tutashindwa mahakamani.

Lakini wizi uliofanywa na ACACIA (kudanganja kilichomo kwenye makinikia) ni kosa la jinai na hauhusiki na mkataba mbovu. Hili tatizo liko kwenye uwezo wetu kulikabili kama hivi kuzuia mchanga mpaka tutakapojiridhisha ni kiasi gani cha madini kimo na kama wametudanganya au la katika declaration zao. Sijui kwa nini Lissu - mwanasheria ngangari - haliongelei hili bali anatutisha kuwa tutashitakiwa na huyu mwizi.

Mawili, ama anakula na huyu mwizi au uanasheria wake una walakin.
Unajuaje kama wamedanganya kilichomo kwenye makinikia wakati hawakushirikishwa kwenye utafiti?
 
Nimefurahi umeanzisha huu uzi kwa sababu utaelezea kwa nini mimi simuelewi Lissu.

Lissu ni mwanasheria aliebobea. Anafahamu sheria za mikataba na kwamba itachukua muda mrefu sana kujipanga kukabili hii mikataba mibovu ya madini. Kurekebisha mikataba sio kitu cha kufanyika kwa papara ama sivyo tutashindwa mahakamani.

Lakini wizi uliofanywa na ACACIA (kudanganja kilichomo kwenye makinikia) ni kosa la jinai na hauhusiki na mkataba mbovu. Hili tatizo liko kwenye uwezo wetu kulikabili kama hivi kuzuia mchanga mpaka tutakapojiridhisha ni kiasi gani cha madini kimo na kama wametudanganya au la katika declaration zao. Sijui kwa nini Lissu - mwanasheria ngangari - haliongelei hili bali anatutisha kuwa tutashitakiwa na huyu mwizi.

Mawili, ama anakula na huyu mwizi au uanasheria wake una walakin.
anayepima kilichomo kwenye makinikia ni ACACIA au TMAA ?
 
Lissu hana jipya. Kazi yake kubwa ni kutetea majizi ili mradi tu atapata chake kwanza.
Wote mtakuwa mashahidi, Lowassa aliwahi kushutumiwa vikali kuwa ni fisadi hadi akawekwa kwenye LIST OF SHAME. Mwaka juzi alipoonekana kuwa ni mtaji kwao ghafla akageuka kuwa MALAIKA.
Katika issue ya mchanga (makinikia ) hivi kuna sheria gani ya kimataifa inayoruhusu wawekezaji kutudanganya kuhusu uwepo wa madini mengi kwenye mchanga?
Lissu kazi yake kubwa ni kushabikia tu sisi kuibiwa.
1. wakati lowassa anashutumiwa kuwa fisadi MAGUFULI alikuwa upande upi? Wa lowassa au wa Tundu Lissu?
2. Unaijua TMAA na kazi zake?
 
Unajuaje kama wamedanganya kilichomo kwenye makinikia wakati hawakushirikishwa kwenye utafiti?
Unajuaje kama walichosema ACACIA ni sahihi? Ulikuwepo ACACIA walipokuwa wanafanya vipimo vyao?

Yaani tunawaamini wageni zaidi ya serikali yetu jamani. Hivi nyie mkoje lakini? Sisi kwa kweli tuna haki ya kupokonywa hata hii nchi kama huu ndio utashi wetu.
 
50 Reactions
Reply
Back
Top Bottom