Mimi na mke wangu tumebahatika kupata watoto wawili, wa kwanza 10 April, 2015, wapili 02 Feb,2019. Mtoto wa kwanza alizaliwa na 3.74 kg na wapili amezaliwa na 4.1kg. Tangu amejifungua tu mtoto wapili aliniambia hataki kuzaa tena nami siku taka kubishana nae nika mjibu hata mimi watoto wawili wananitosha japo ningetamani nipate wamwisho wakike nimpe jina la mama yangu. Alinijibu kwa utani hataki tena labda nikitaka nikazae nje ya ndoa ila yeye hataki tena kurudi leba. Baada ya kama siku 50 hivi hali yake ya kiafya ilirudi kawaida na tuliendelea na kupena uroda kama kawaida na zikifika zile siku za kupata mimba tumekuwa tukitumia kondom au kuacha kufanya. Ana cycle ya siku 28 -30 na kwa mwezi huu alitarajia kuanzia mzunguko mpya kati ya tarehe 10 hadi 12, sasa amekuwa na wasiwasi na kubwa kuliko yote aaogopa kutoa mimba na mimi pia naogopa hasa kwa kulinda afya yake.
*Swali langu kwenu naomba kujua kipi kinaweza kuwa hatari zaidi kati ya kutoa mimba ya mwezi mmoja na kuendelea kulea mimba wakati ametoaj kujifungua miezi minne iliyopita?*
*Swali langu kwenu naomba kujua kipi kinaweza kuwa hatari zaidi kati ya kutoa mimba ya mwezi mmoja na kuendelea kulea mimba wakati ametoaj kujifungua miezi minne iliyopita?*