Ni kweli huyo yuda Iscariot kashavuta mpunga.....zambi ya usaliti ni mbaya saana
Ndo maana mwanasiasa akisema anamuogopa Mungu tujiulize Mungu yupi?
Mkatoliki akifuatwa na Pengo ubavu wa kukamkatalia Pengo sio rahisi hata kama
mahitaji ya Pengo sio 'maslahi' ya Taifa kwa wakati huo
Hata mimi nimeshangaa.Mara nyingi nafuatilia mabandiko yako kwani angalau yana kuwa objective kidogo, kulinganisha na mabandiko mengi yanayoandikwa na mengine.
Hata hivyo kama wasemavyo
Waswahili "kila shetani na mbuyu wake" LOWASSA NI MBUYU WAKO WEWE PASCO
Na hilo ndio ulilosahau kutuandikia kwenye hili bandiko lako
Unamtukana na kumsema amehongwa leo Dr slaa kwa kumsema Lowassa fisadi! Unapingana na Ukweli?
hebu tuambie kwanza mtu aliye muhonga Dr slaa alipo mueka lowassa kwenye List of shame ndipo tutashughurika na huyu anayemhonga sasa.
Pasco unafanya propaganda na tayari umeshakua sehemu ya propaganda machinery ya CHADEMA
Damage imetokea na sasa mmekuja kujaribu kuokoa kwa ku employ "Damage control strategy"
Ndio maana mnashughurika na mjumbe badala ya ujumbe
Mnatulazimisha tujadili watu badala ya masuala.
Nikuonye tu vita hii utashindwa licha ya mahaba uliokua nayo Kwa Lowassa kwa sababu Ukweli daima husimama.
Pasco leo wewe wakumuita Dr slaa Yuda!? kipi hasa kisa na mkasa!?
Endelea tu kua mchekeshaji wa mfalme ipo siku utailipia gharama ya kua mchekeshaji kwani karma haitakuacha.
Usii-divert hoja hii ya msingi Ukaielekeza kwenye mlengo wa kidini.
Hebu jaribu kujibu hoja za msingi ya kuwa WHY NOW and NOT ANY OTHER TIME huyo Dr ameamua kupeleka mashambulizi mfululizo kwa Edo, tena mbaya zaidi akifanya timing na uanzaji wa utekelezaji wa cyber crime law.
Kwaiyo unataka kusema na mwaka huu ni CCM tena?Wanabodi,
Wakati wa mchakato wa kumpata mgombea wa CCM ukiendelea, 15th August 2014 nilikutana na mtu, akaniambia mgombea wa CCM ni Dr. John Pombe Magufuli na akanipa sababu za ni kwa nini Magufuli!. Mimi niliupandisha uzi huu,Mgombea wa Urais Kwa tiketi ya CCM, 2015 "Could Be" John Pombe Magufuli!, ili kuwafahamisha wana jf kuwa mgombea wa CCM ni Magufuli, lakini sikuziweka hizo sababu za kwa nini ni Magufuli na ni kweli imekuja kutokea mgombea wa CCM ni kweli ni Magufuli, lakini mpaka hii leo, hizo sababu za why ni Magufuli, ninazo, nimezihifadhi tuu bila kuzitaja, cha muhimu ni imetokea kama nilivyoeleza ila kwa wana jf waliousoma uzi ule they were the first to know!.
Hivyo tuendelee kuifuatilia jf and be the first to know.
Nawatakia Jumamosi Njema.
Pasco.
Lakiini alisema ukweli lazima uwe na egemeo na akasema kwa sasa ukweli wake una egemea CCM kwa kutoa Sababu kuwa UFISADI wa magufuri yani tuhuma za Magufuri ni Very peanut..kulinganisha na UFISADI wa LOWASA hivyo katika kuchagua kimoja kati ya VIWILI MAGUFULI NA LOWASA ...KURA YAKE YAENDA KWA MAGUFULI..Ingawa Pasco umesema kuwa Dr Slaa amepewa jezi no 33. ili kuiongezea nguvu ile timu ya makada 32 wa Sisiem wanaomfanyia kampeni Magufuli na unaendelea kueleza kuwa huyo 'Yuda Iskariote' ameelekezwa mashambulizi yote ayaelekeze kwa Lowassa na asimguse 'swahiba' wake Magufuli, lakini kwa bahati mbaya jana usiku wakati wa mahujiano maalum Star TV, mpiganaji huyo kama ambavyo wakati mwingine hutokea uwanja wa vita zile risasi ulizodhamiria kumpiga adui zika-backfire na kumpiga miongoni ya wapiganaji wa kikosi chenu.
Vivyo hivyo ndivyo iliuvyomtokea Dr Slaa wakati alipoulizwa na mwendeshaji wa kipindi hicho aeleze kama Dr Magufuli ni clean 100% ndipo Dr Slaa kwa 'ajali' akatamka hata huyo Magufuli siyo clean kihivyo, kwa kuwa naye ana skandali ya kuuza nyumba za serikali na mbaya zaidi nyumba zingine kawauzia hawara zake!
Hayo siyo maneno ninayomwekea mdomoni Dr Slaa, bali hakika aliyatamka na nadhani hata hao maccm wanaomtumia sasa hivi watakuwa wanakuna vichwa kutokana na impact itakayotokana na maneno hayo hata kama watajua kuwa 'mtu wao' aliitoa kauli hiyo kutokana na ulimi kuteleza!
Pole ujitambui nani alikwambia watu Tanzania wanachagua kwa kuanglia watu wanatoka Kanisa gani...au nyie bado mnaa amini kwa mgombea liyepita pita kwenye makanisa na misikiti ndio atapewa ukuu wa Nchi hii.Thubutu yake mwisho kwa Gwajima....Mimi ni RC lakini katu sisupport Magufuli kama mgombea wala Dr Slaa kwa usanii wake. Kwa hiyo kama wanafanya hiivyo kwa sababu ya kuamini RC watawasupport, basi wamegonga nje. Na nasema na kuomba wazi RC tafadhali msisupport CCM maana kwa hakika ndiyo chanzo cha matatizo yetuu mengi hapa Tanzania. Na kama Dr Slaa angekuwa mgombeaji wa UKAWA,ningemsupport sio kwa ajili ya RC wake bali chama (upinzani). Shida yangu lazima CCM ifike mahali iende maana inatuona watanzania wote kama hamnazo hivi kwamaba hata ikiiba, ikafanya inayo yafanya hivi sasa hatuna namna nyingine.
Hata mimi nimeshangaa.
Kwa sasa wanafanya njia zote chafu ili kupambana na hoja za Dk. Slaa.
Kwanza ametoa maelezo marefu ili kujenga hoja ya kutaka kutuaminisha kama ameongea na Dk. Mwakyembe lakini kitu muhimu anachoshindwa kukifanya ni kutueleza yeye ni nani? huyu Pasco ni nani hapa Jamiiforums. Kwa nini asije na jina lake ambalo ni verified ili ampe nafasi Mwakyembe ya kujibu hoja kama kweli alikutana naye.
Pili, anajaribu kunogesha hoja zake kwa kusema Mwakyembe alidai alikuwa na so and so huku akisahau kuwa msingi wa bandiko lake ni kutueleza yule aliyekuwa na Mwakyembe. Kwa nini asituambie huyo so and so ni nani, lakini kikubwa, anajichanganya katika maelezo yake kwa kusema kuna posibility Dk. Slaa amehongwa lakini hitimisho lake anamalizia kwa kusema Dk. Slaa amehongwa.
Hakuna suala gumu kama kuujengea hoja uwongo ili uonekane ukweli.
Hizi ni propaganda za kizamani sana ambazo haziwezi kujibu hoja za Dk. Slaa.
Nchii taasisi zenye nguvu baadaya Ccm na serikali inayofuata ni Roman Catholic Church
Magufuli,Slaa wanaunganishwa na church...mengine yote yanaongezeka tu