An Open Letter to US Ambassador: "On the Threshold of Prosperity"

Nimewapata... Nyani na Zomba... tuna uwezo gani wa kuichunguza kampuni ya Kimarekani kwa kutumia sheria zetu? Tunaweza kumleta Balali bila ya msaada wa Marekani? Fedha zetu zilizokwapuliwa kama zimewekezwa Marekani tutazipata vipi bila kuwahusisha Marekani? Nakubaliana na nyinyi kuwa kuna mambo ambayo tunaweza kuyafanya sisi wenyewe, lakini ni hiki kiburi chetu ndicho kimetufikisha hapa tukidhania kuwa watawala wetu wataamua kufanya mambo kwa maslahi ya Taifa letu. Kama wangetaka hivyo wangefanya hivyo siku nyingi zilizopita.

Hiyo Richmond ni wabongo wenyewe ndio walioingia mkataba nayo huku wakijua fika kuwa ina exist kwenye briefcase tu/ au haidili na mambo iliyodaiwa inadili nayo. Hapo tatizo ni la nani?

Balali: hivi status yake ktk serikali ya Tanzania ni ipi? Fugitive from justice or..? Has he even been indicted? If not, who's fault is it and what is the TZ Govt. waiting for?

Fedha zilizokwapuliwa: zimekwapuliwa na nani na yuko/ wako wapi hao waliozikwapua? Kama wako Tanzania, je ni nini kinachoendelea? Sisi kama taifa tumefanya nini kuwashughulikia?

Mwisho: hatuna kiburi na si kiburi chetu kilichotufikisha hapa tulipo!! Ujinga wetu ndio uliotufikisha hapa tulipo. Tunaachia mifisadi iendelee kufuja mali zetu na kutanua halafu tunaendelea kuiweka madarakani miaka nenda rudi. We have way too much tolerance for nonsense. Watanzania tuko wengi mno kuwa "pimped" na mifisadi michache. Hivi tunashindwa nini sisi kuwafanyia kweli hawa mafisadi? Mi nadhani tuna uoga wa asili that we need to overcome first in order to earnestly deal with our problems. Marekani na nchi zingine zitaweza kusaidia kwa dhati pale tu tutakapoanza kujisaidia wenyewe.
 
Tuitishe wafadhili wasitishe misaada hadi tujue nini kinaendelea katika kashfa mbalimbali za fedha? Hiyo ndiyo ilikuwa lengo langu la awali. Nilipoandika ile barua ya Rada kwa House of Commons, baadhi ya watawala walinipigia kelele kuwa wakisitisha misaada ni wakulima na watoto ndio watakaoathirika. So this time nimejaribu kuwa a little bit melancholic.. sasa sijui...
 
Tuitishe wafadhili wasitishe misaada hadi tujue nini kinaendelea katika kashfa mbalimbali za fedha? Hiyo ndiyo ilikuwa lengo langu la awali. Nilipoandika ile barua ya Rada kwa House of Commons, baadhi ya watawala walinipigia kelele kuwa wakisitisha misaada ni wakulima na watoto ndio watakaoathirika. So this time nimejaribu kuwa a little bit melancholic.. sasa sijui...

Mimi naona uandike kusitisha kabisa kufadhiliwa, iwe wakati wa kashfa au bila ya kashfa. Tuachane kabisa na kufadhiliwa. Kama alivyofanya Mahathir Muhammad Malaysia, imagine ilikuwa inashindana umasikini na sisi na kitu cha kwanza alisitisha kuomba misaada yote, western countries wakawa wanamlazimisha achukuwe misaada, why? Akakataa kata kata, akawa adui yao mkubwa, kisa? kakataa misaada. Duhh, ajabu kubwa sana, waswahili tuna msemo "akunyimae kunde akupunguzia mashuzi" sasa hawa jamaa wa western countries ni nini kilicho wakasirisha? where is Malaysia today? we have much much more natural resources than Malaysia. Dawa ni kuachana kabisa na umatonya.

And we should not mock, we should tell it as it is, hatuombi tena.
 
Mimi kuna kitu kinauonyesha moyo wangu kwa dhati kabisa kuwa mtizamo wako huu ufuatao ni sawa kabisa.

Tuitishe wafadhili wasitishe misaada hadi tujue nini kinaendelea katika kashfa mbalimbali za fedha?

Nikijitizama ndani kabisa ya ufahamu wa akili yangu nagundua kuwa hivi tunvoykwenda.... Lowasa, karamagi, mkapa, BoT..etc alafu more grants..more misaada naona pia hatutaepuka hili:

[QUOTE].. ni wakulima na watoto ndio watakaoathirika...[/QUOTE]

So far wakulima na watoto wanaadhirika. Kinachonitatiza ni kuwa Misaada imekuwa inatolewa kwa miongo mingi sasa..Lakini sijaona wakulima wakiwa bora...sijaona watoto wakipata ahueni yeyote...Ndio maana ninasita..najuliza kulikoni..!! Kweli fikra zetu bado ziko timamu?

Nimeona leo pale kiwanjani waanmbokea Bush, mawaziri wote wamehojiwa na TVT wote wanaongelea bila mshtuko wowote tutakavyofaidia Misaada....Lakini wote pale wamesomeshwa kwa misaada..wemefanya kazi kwa misaada....wanatibiwa kwa miasaada..ulimi wa kila mmjoa pale mwepesi kabisa..unakimbilia Mfadhili mfadhili..Ni ulimi mwepesi au ni fikra na akili hazijakaa vema?

Kijijini kwetu Ni heshima kuzunguka kijijini kuomba MBEGU na baada ya mazao urudishe Mbegu kwa aliyekupa msaada hu..maana HIYO NDIO HESHIMA,UTU, UBINAADAMU na USAWA. Ni mwiko kwa mwanaume kuhudumiwa kwa Chakula na familia/Nchi nyingine.

Hatari kubwa ni kuwa UTAPOTEZA MKE na wanao WA KIKE KWA YULE ALIYEKUFADHLI CHAKULA BADALA YA MBEGU!!!

Nina maana gani kama Tanzania tunalishwa na nchi nyingine kwa karibu 46% ... hii ni kama 50%...ni kuwa nusu ya ndoa za watanzania ziko hatarini. Wake zetu watawapa maji ya kunawa mikono wale waliofadhili chakula kwanza ndipo amnawishe mumewe.

Si ajabu hakuna kuaminiana kwenye ndoa nyingi sikuhizi. Tuheshimiwe kwa lipi? Kama wote tunalishwa kama hivyo .. we cant help..its human nature we have lost our wives!!!!!
 
1997 Asian financial crisis

During the Asian financial crisis of 1997, IMF had prescribed a recovery package for Malaysia, but Mahathir defied international pressure, his then Deputy Anwar Ibrahim, and conventional wisdom, in rejecting the package. Though economic prosperity has been mixed since then, Mahathir argued that Malaysia's recovery was relatively faster and better, as compared to many other Asian countries affected. After the financial crisis, the IMF and World Bank acknowledged that Mahathir's approach had worked.[17]



http://en.wikipedia.org/wiki/1997_Asian_Financial_Crisis
 
Back
Top Bottom