Amri ya Magufuli yatekelezwa, jengo la TANROADS labomolewa

Huyu jamaa mimi nampinga pamoja na kupigiwa debe sana na baadhi ya watu hapa jamvini kwamba ni mtendaji mzuri na anafaa kuwa Rais 2015. Kauli yake hii kuhusu kuwalipa mafao yao wale ambao nyumba zao zitabomolewa kwa kweli ilinishangaza sana, "Kama nyumba yako imeingia nusu ndani ya eneo la barabara, itabomolewa hiyo nusu na wewe utalipwa kulingana na ulivyobomolewa, hatuwezi kulipa gharama ya nyumba nzima wakati umebomolewa nusu," alisisitiza.

Hivi nyumba ikishabomolewa nusu kuna nyumba tena hapo wandugu? au ndiyo kuwaacha walala hoi katika hali ngumu zaidi kimaisha baada ya kulipwa mafao ambayo hawawezi kufanya nayo chochote katika kujipatia makazi mapya hasa tukitilia gharama kubwa za ujenzi wa nyumba nchini.

Kaka kumbuka hata kulipwa hiyo nusu ni favour!! hawakutakiwa kulipwa kabisa!!
 
nampongeza magufuli kwa utendaji wake kwani miongoni mwa vigezo vya kiongozi bora ni yule anaeweza kufanya maamuzi magumu...bigup Mr...but my point is nilitegemea kuona wale waliousika moja kwa moja katika utoaji wa viwanja vilimo jengo la TANROAD NA TANESCO wakifikishwa mahakamani kwanza ndo uchukue hatua ya kubomoa majengo hayo...kwani kwa upeo wangu nilionao ni kwamba that reserved area were known since independence and before building any thing and especially to those high and big building u have to do survey ya kuona kama pahali hapo pako barabarani,mkondo wa maji na mengine mengi....ni pesa ya walipa kodi iliyoyajenga hayo majengo leo pesa zao ni kama zimetupwa........dont u see that this is another newly skendo to the government?...assume majengo pacha ya BOT yaliyoigharimu tanzania mabilion ya pesa achilia yale hambayo yaliingia kibindoni without doing anything...leo mtu utoke huko na kusema kwamba yako ktk hifadhi ya barabara na yanapaswa kubomolewa JE WATANZANIA TUTAKUBARI KILAHISI KAMA HAYA YA TANROARD NA TANESCO?....let u be serious to our resources.....for me naona ni tanzania tu wananchi wanaweza chekelea hili without even questining...:hungry:....liame_charm
 
Kwa hivyo munaamini kwamba raia wa kawaida kuvunjiwa kibanda chake ni sawa, lakini taasisi kubwa ni tatizo kwa vile ni resources zetu sote.

Munachosahau ni kwamba hao raia wanaovunjiwa nyumba zao ndiyo walipa kodi ambayo munaita 'resourcs zetu'.
 
Ndugu bitimkongwe binafsi simaanishi kwamba raia wa kawaida kuvunjwa kibanda chake ni sahihi! La hasha! Mantiki kuu kwenye "reply" yangu ya awali (ambapo neno "kibanda" limetumika) ni kwamba kama serikali na taasisi za kitaalamu haziwezi kujali/kung'amua makosa makubwa ya kisheria na kitaalamu kwa jengo kubwa namna hiyo na lililohusisha wataalamu na michakato mingi kiasi hicho unadhani kwa vijumba (vibanda) vyetu vya kawaida ambavyo vingi havina hata ramani zaidi ya kuwa tumevirithi kwa babu zetu hali itakuwaje? Na ndilo linalotokea nchi hii.

Vinginevyo, tusipokuwa makini, hili (la kubomoa jengo la Tanesco na majengo mengine ya serikali) linaweza kutumiwa na wanasiasa uchwara huko mbeleni kwa ajili ya kuhalalisha kuvisambaratisha vibanda vyetu hata kama vibanda hivyo vitakuwa vimejengwa kwa kufuata taratibu na kanuni sembuse vile tulivyorithi ambavyo haviko hata kwenye mipango miji! Tunachotaka kuona ni kwamba wale wote waliohusika na mchakato mzima hadi jengo likasimama pale lilipo kwa ambacho leo wanadai (Magufuli na timu yake) ni kinyume cha sheria na kanuni wanawajibishwa kwanza.

Naamini wabunge makini na wazalendo hawataacha hili lipite kihuni hivi hivi; wahoji ujinga huu.
 
Mimi huwa nashindwa kuelewa watendaji na wasomi wa nchi hii. Jengo kubwa (angalau kwa viwango vya Tz) kama la TANESCO siyo kibanda - siamini kama lilijengwa kwa kukurupuka au kwa siku moja.

Kuna "wataalam" walikaa mahali wakaandaa andiko (proposal), vikao vikakaa mara nyingi, michakato ikafanyika kwa muda mrefu, wakatafutwa wataalamu washauri wa kila fani - architectural engineers, civil engineers, urban planners, surveyers, electrical engineers, n.k. n.k.

Taasisi mbalimbali za kiserikali (pengine na binafsi) zikahusishwa - wizara yenyewe (ya nishati), jiji, wizara ya ujenzi (inayohusika na barabara), TRA, n.k. Baada ya mchakato huo mrefu ndipo hatimaye kandarasi (tender) ikatangazwa na michjo kadhaa ikafanyika hatimaye kumpata/kuwapata MAIN CONTRUCTOR, several SUB-CONTRUCTORS katika maeneo mbalimbali - civil, electrical, n.k hawa wakisimamiwa na mtu anayeitwa CONSULTANT ambaye kazi yake kuu ni kuhakikisha kazi inafanyika kwa ubora unaotakiwakwa.

At the end, tunaambiwa so simply - JENGO LIKO BARABARANI. Hivi wataalamu wote hao hakuna aliyeweza kung'amua hilo mapema? Na kama hawakung'amua, nini kifanyike? Si wamesajiliwa na Bodi ya Wahandisi (and other professional bodies)? Kama waling'amua na kushauri ila serikali (TANESCO) wakawa vichwa ngumu pengine kwa utashi wa kisiasa, hakuna wa kuwajibika? SHAME ON THEM!

Haiwezekani jengo kama la Tanesco ambalo halina hata miaka nadhani 12 leo tunaambiwa linatakiwa kubomolewa - liko barabarani. Magufuli angekuwa kweli mchapakazi angehoji hayo yote kabla ya kufikia hitimisho la kuvunja. Vinginevyo ni kulea uzembe unaoendelea kuligharimu taifa hili. Lakini inawezekana hii ni (ya kujenga na kuvunja) ni miradi yao - you never know.
Sisi wakulima na wafugaji ndo cha moto 2takiona mungu 2nusuru
 
YAANI INAUDHI SANA HII SERIKALI, MAMBO NI KAMA MAIGIZO TU, Hawa waliohusika TANROADS walitakiwa wawe gerezani kwanza wakati hilo jengo likibomolewa, hivi hii nchi inaongozwaje? duh sio siri tuna hasara na uongozi wa tz..
Kwani TANESCO ilijengwa before or after the expansion of Morogoro road (1990s).

Wao tanroads ndiyo wanaosimamia hii sheria halafu wao ndiyo wavunjaji nambari moja! serves them right.
 
Mie nadhani ifike wakati kwa kila jengo ambalo lipo kwenye hifadhi ya barabara au ambalo halipo mahali linapostahili libomolewe bila kujali gharama yake..kwani in future run ni gharama zaidi kuliacha kuliko kulibomoa sasa hivi. Ila kwa kila aliyeruhusu ujenzi wa hilo jengo wakati akijua kabisa ni sehemu ambayo haitakiwi kua na jengo..mie sidhani kama tuna haja ya kumshtaki...ni akanyee kidebe tuu moja kwa moja, sasa unamshtaki nini wakati kosa lipo wazi. Hapo ndo tutajua kuna uwajibikaji kwenye hili...sio jengo la Tanesco libomolewe tuu then hakuna aliekwenda kunyea kidebe kule segerea.
 
..napinga majengo hayo kubomolewa.

..sintoshangaa kusikia kwamba majengo hayo yalijengwa wakati Magufuli akiwa ndiye waziri wa ujenzi au waziri wa ardhi.

..waliohusika na kutoa viwanja hivyo kwa tanesco na tanroads wachukuliwa hatua za kisheria.

..zaidi watendaji wa Tanroads waliokiuka sheria yao wenyewe nao wachukuliwe hatua za kisheria.
 
Hakuna jengo linalopaswa kubomolewa bila ya kujua pesa yetu inarudije.

Aliyeamuru au kutoa vibali ni nani?
 
Back
Top Bottom