Amos Makalla una sababu ya msingi ya kuendelea kuwa RC Mkoa wa Dar es Salaam?

Good Father

JF-Expert Member
Feb 28, 2014
10,275
18,352
Naandika uzi huu kwa masikitiko makubwa.

Mhe. Amos Makala ukiwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam na mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Dar es salaam.

Huu Mkoa ni kitovu cha biashara kwenye nchi hii, huu mkoa ndio una image kubwa ya nchi kibiashara, wageni zaidi ya 90% wako Dar es salaam.

Pamoja na mambo yote hayo mkoa huu ghafla umegeuka kuwa sio salama kabisa watu wanakatwa mapanga kila siku, hawa vijana wa Panyaroad wanavamia maeneo mbalimbali ya mkoa huu na kuua, kujeruhi, kuiba na kuharibu mali ambazo wananchi wamezitafuta kwa tabu.

Juzi kati kulikuwa na tukio Kinyerezi, jana kulikuwa na tukio Kawe na mtu mmoja aliuwawa, leo usiku huko Dovya Temeke watu wamekatwa mapanga mengi sana.

Mhe. Makala una sababu gani ya msingi kuendelea kuwa RC na Mkuu wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wa mkoa wa Dar es Salaam?

Unaamka asubuhi unaenda ofisini kwa gari la watanzania, unawekewa mafuta, unalipwa vizuri, unapewa dereva, una PS una jeshi la Polisi, una JWTZ, una TISS, Fire, Magereza, immigration n.k ivi kweli umefeli Mheshimiwa?

Hawa vijana ni mpaka wamuue mwanao wa kumzaa ndio utajua kuna tatizo?

Mpaka wamuu mkeo ndio utajua kuna tatizo mkoani kwako?

Mheshimiwa Makala acha kuongea maneno marahisi, ingia kazini, tumia vyombo ulivyokabidhiwa watu katika mkoa huu hawana amani na wewe upo.

Kama unaona umefeli resign Mzee aje mtu mwingine hapa.

Nadhani huu mkoa upewe RC sawa na wale wenye sifa za ziada waliopo mikoa ya mipakani kama Mtwara, Kigoma n.k

Nawasilisha.
 
Panya Road wakianza kuvamia masaki na Oysterbay ndio wataanza kuchukua hatua.

Panya Road wakianza kuwapiga mawe barabarani ndio watachukua hatua.

Bado naendelea kusisitiza, tunaweza kuona watu wanafanya makusudi lakini kumbe tunaongozwa na watu wenye upeo mdogo sana kichwani.
 
panya road wakianza kuvamia masaki na Oysterbay ndio wataanza kuchukua hatua.

Panya road wakianza kuwapiga mawe barabarani ndio watachukua hatua.

Bado naendelea kusisitiza, tunaweza kuona watu wanafanya makusudi lakini kumbe tunaongozwa na watu wenye upeo mdogo sana kichwani.
Dar si tumeambiwa kila mtu anaishi masaki na oyster bay au? Kwani wengine mnaishi wapi?
 
Yaani tunashindwa kuchunguza na kujua Panya road ni akina nani na wanatokea wapi ili tuchukue hatua?.

Yaani kitengo cha CID jeshi la polisi, na hata task force fulani ya TISS wanashindwa kufanya intelejensia for a week na kukamata wote pamoja na kukata mzizi kabisa?

Yaani vitoto vidogo ndio vinasumbua mijitu tuliyoisomesha kwa hela nyingi nje na ndani na kuwapa majukumu ya kutulinda na kututumikia huku wengine tukifanya kazi kwa bidii kulipa kodi na kujenga nchi halafu yenyewe inakuwa mipumbavu tu.
 
Yaani inashindwa kutoka amri ya mwezi mmoja kwa RC, IGP, bosi wa TISS nk asisikie huu ujinga vinginevyo watatumbuliwa. Yaani kabisa inashindwa kutoka hiyo amri na kuhakikisha watu wanakuwa salama.
 
Ni aibu kuwa kwa taifa na jeshi la police panya road wanafanya matukio mfululizo, na kuna mahali wamefanya tukio kwa zaidi ya masaa 2 pasipo police kujitokeza embu tujiulize panya road wanavamia nyumba kwa zaid ya masaa mawili Je nani yupo salama? ujasiri wa kukaa masaa mawili wanautoa wapi? taifa lipo yatima hili ni ovyo.

Wanasiasa wanafikili wao wapo salama, ila siku zao zinahesabika ni pale ambapo baada ya vijana wapambanaji wanaojitaftia kwa nguvu zao tena kwa tabu na wakaadhirika na panya road kiuchumi na kiafya woote waamue kuona hii njia ya uporaji ni njia saahihi kwao basi taifa litabadilika ndani ya Usiku mmoja tu!
 
Ni aibu kuwa kwa taifa na jeshi la police panya road wanafanya matukio mfululizo, na kuna mahali wamefanya tukio kwa zaidi ya masaa 2 pasipo police kujitokeza embu.
Ni hatari sana, kama hao vijana wanaweza kuvamia eneo na kukaa masaa mawili na kuondoka bila bughudha yoyote hakuna haja ya kuwa na polisi, labda kila mtu ajiwekee ulinzi wake.
 
Hili tatizo alaumiwe Mama tozo,kwa kukataza Askari kuua majambazi,enzi za Magufuli tulishuhudia majambazi wote wakiúawa
 
Naandika uzi huu kwa masikitiko makubwa.

Mhe. Amos Makala ukiwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam na mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Dar es salaam...
Alaumiwe aliyemrudisha makala kuwa rc na kumweka dar ilhali anajua kuwa hata katavi alishindwa
 
Yaani inashindwa kutoka amri ya mwezi mmoja kwa RC, IGP, bosi wa TISS nk asisikie huu ujinga vinginevyo watatumbuliwa. Yaani kabisa inashindwa kutoka hiyo amri na kuhakikisha watu wanakuwa salama.
Mpaka unahisi hawa panya road watakua na baraka kutoka kwa wakubwa..mana wamekaa kimya kama hawaoni kinachoendelea.

#MaendeleoHayanaChama
 
Mimi naanza kupata wasiwasi na uwezo wetu kama taifa kiusalama kama vijana wadogo wanaweza kujiunga na kusumbua eneo kama Dar es Salaam na kushindwa kudhibitiwa mpaka sasa basi kwa uhakika vyombo vyetu vya usalama vijitafakari hatuko salama kama taifa.
 
Naandika uzi huu kwa masikitiko makubwa.

Mhe. Amos Makala ukiwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam na mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Dar es salaam...
WaNasemaga usipoziba Ufa utajenga ukuta !! Hata mbuyu ulianza Kama mchicha !
 
Hili tatizo alaumiwe Mama tozo,kwa kukataza Askari kuua majambazi,enzi za Magufuli tulishuhudia majambazi wote wakiúawa
Kiongozi mzuri huwa hadumu kwa nchi Kama Tanzania. Wakati wa Makonda Mkoa ulikuwa salama Ila alichukiwa na kila fisadi na wauza ngadu.
 
Siyo RC tu. Hata Sirro na Makamanda wote wa Polisi Dar. Waondolewe. Yaani Panya Road tu vitoto havina silaha. Je mtiti wa Alshabab ukizama ndani? Afu shida ya mama ana penda sna kudanganywa. Watu wazuri ana fanya kuwakomoa. Mpe Dar...Bw. Antony Mtaka. Hao Panya Road watakuwa rafiki zake. Na atawapa kazi. Jamaa huwa anacheza na mental change.
 
Huu mkoa arudi makonda tuu!alipambana nao vilivyo! Hata Muliro nae akae pembeni!anawashindwaje hawa madogo, mbona walipotea kipindi cha CHUMA JPM!!
 
Anzeni na asiyejulikana makazi yake yako wapi hasa! Zenji, Dom au Dar?

Ili tuone uhalifu huu unashika hatamu yeye akiwa wapi!

Pili, maono yake ni kuwa na wasaidizi walio bize kuhondomola tu, masuala mengine yote yameachwa yaende kwa gravity tu, yasipopanda mlima, yatafute level yake, yakae hapo.

Tatu, kama mnajinadi kuwa mnaenda kisomi, tayari mna sensa, anuani za makazi, nida, serikali za mitaa, shule, urasimishwaji wa makazi n.k, nini kinawashind kujua umri wa watu, kwa majina, mitaa na shughuli wafanyazo? Anzeni na wale wenye umri kati ya 12 na 45, kama hawapo shule kimahudhurio, hawana shughuli maalum, mtaa haujui mienendo yao, wanafanya mawasiliano, n.k chukua listi, waweke kwenye Possible suspect, anza udukuzi kwao! Si ndio kazi ya Polisi na TISS au?

Angalau mtakuwa bize, muachane na kutufanyia fujo barabarani, hamna shughuli, mnajazana kwenye gari zetu, kututishia na mataa, ving'ora kuwahi kwenda kukaa kwenye benchi. Muda wa kutuuliza kama tunawafambua nyie kina nani utapungua, Pumbavu.
 
Back
Top Bottom