Replica
JF-Expert Member
- Aug 28, 2017
- 1,426
- 7,736
Mkuu wa Mkoa wa Dar, Amos Makalla amempongeza Rais Samia kwa kazi Nzuri anayoifanya ikiwemo tukio alilofanya leo kuendelea kuboresha huduma za Afya.
Makalla amemuhakikishia Rais Samia, yeye kama mkuu wa Moka wa Dar na mwenyekiti wa Kamati ya ulinzi na Usalama kwamba Mkoa uko Salama na kazi aliyompa, wamejipanga na kazi waliyoianza kuhakikisha wananchi wako salama Uhalifu utabaki Historia.
Pia, Makalla amemshukuru Rais Samia kwa kumpa heshma, kumkumbuka na kumpa ukuu wa Mkoa wa Dar es Salaam na kusema hatomuangusha na ameanza kwa kukimbia badala ya kutembea.
Makalla amesema Rais amemrudisha nyumbani kwani yeye ni mtoto wa Dar, amezaliwa na kukulia hivyo kama shughuli imepata mwenyeji.
Makalla amemuhakikishia Rais Samia, yeye kama mkuu wa Moka wa Dar na mwenyekiti wa Kamati ya ulinzi na Usalama kwamba Mkoa uko Salama na kazi aliyompa, wamejipanga na kazi waliyoianza kuhakikisha wananchi wako salama Uhalifu utabaki Historia.
Pia, Makalla amemshukuru Rais Samia kwa kumpa heshma, kumkumbuka na kumpa ukuu wa Mkoa wa Dar es Salaam na kusema hatomuangusha na ameanza kwa kukimbia badala ya kutembea.
Makalla amesema Rais amemrudisha nyumbani kwani yeye ni mtoto wa Dar, amezaliwa na kukulia hivyo kama shughuli imepata mwenyeji.