Mwita Maranya
JF-Expert Member
- Jul 1, 2008
- 10,564
- 7,970
Wana JF,
Hivi karibuni nilikuwa Morogoro kwenye shughui zangu binafsi. Katika mizunguko yangu wilayani Mvomero nikajikuta nimevutiwa kutaka kujua hali ya kisiasa ikoje. Maeneo/vijiji nilivyobahatika kufika ni pamoja na Turiani, madizini, manyinga, Kidudwe, Magole, Mvomero na maeneo mengine ambayo majina yake yamenitoka.
Nilifanikiwa kuzungumza na wakazi wa maeneo hayo kuhusiana na uchaguzi mkuu wa mwaka huu. Nilichoshuhudia huko ni kwamba wananchi wana mwamko mkubwa sana juu ya uchaguzi wa mwaka huu, na zaidi ni kwamba wanataka mabadiliko ya kweli.
Na pasipo kuumauma maneno wanasema mwaka huu Amos Makala imekula kwake, kuna kijana wa Chadema anaitwa Matokeo Owden Manyeta almaarufu "Mau" ndio chaguo lao. Kutokana na hali hiyo nikaambiwa kuwa bw. Makala ameamua kuwatumia hadi viongozi wa kanisa analosali pale turiani kumsaidia kampeni kwa waumini wenzake, hususani wanakwaya kwakuwa aliwahi kuisaidia kwaya hiyo kwa kuinunulia vyombo vya muziki na ufadhili mwingine mwingi tu.
Bahati mbaya kwake ni kuwa bw. Mau naye ni muumini wa kanisa hilo, kwahiyo hata wanakwaya wamegawanyika wengine wanamuunga mkono bw. Makala na wengine bw. Mau. Pia nikaambiwa bw. Makala amekuwa "mkarimu sana" kama anavyofanya mama wa arusha mjini na takukuru ya mvomero wanaimba nyimbo zile zile wanazoimba wenzao wa arusha mjini.
Haya wapiga kura wa Mvomero kazi kwenu.
Nawasilisha.
Hivi karibuni nilikuwa Morogoro kwenye shughui zangu binafsi. Katika mizunguko yangu wilayani Mvomero nikajikuta nimevutiwa kutaka kujua hali ya kisiasa ikoje. Maeneo/vijiji nilivyobahatika kufika ni pamoja na Turiani, madizini, manyinga, Kidudwe, Magole, Mvomero na maeneo mengine ambayo majina yake yamenitoka.
Nilifanikiwa kuzungumza na wakazi wa maeneo hayo kuhusiana na uchaguzi mkuu wa mwaka huu. Nilichoshuhudia huko ni kwamba wananchi wana mwamko mkubwa sana juu ya uchaguzi wa mwaka huu, na zaidi ni kwamba wanataka mabadiliko ya kweli.
Na pasipo kuumauma maneno wanasema mwaka huu Amos Makala imekula kwake, kuna kijana wa Chadema anaitwa Matokeo Owden Manyeta almaarufu "Mau" ndio chaguo lao. Kutokana na hali hiyo nikaambiwa kuwa bw. Makala ameamua kuwatumia hadi viongozi wa kanisa analosali pale turiani kumsaidia kampeni kwa waumini wenzake, hususani wanakwaya kwakuwa aliwahi kuisaidia kwaya hiyo kwa kuinunulia vyombo vya muziki na ufadhili mwingine mwingi tu.
Bahati mbaya kwake ni kuwa bw. Mau naye ni muumini wa kanisa hilo, kwahiyo hata wanakwaya wamegawanyika wengine wanamuunga mkono bw. Makala na wengine bw. Mau. Pia nikaambiwa bw. Makala amekuwa "mkarimu sana" kama anavyofanya mama wa arusha mjini na takukuru ya mvomero wanaimba nyimbo zile zile wanazoimba wenzao wa arusha mjini.
Haya wapiga kura wa Mvomero kazi kwenu.
Nawasilisha.