Amos Makala analeta Ubaguzi kwenye Ofisi ya Umma

mkalamo

JF-Expert Member
Sep 7, 2013
324
347
Jana na leo taarifa ya mkuu mpya wa mkoa wa Dar esSalaam, Amos Makala kukutana na wazee wa CCM wa mkoa huo zimeenea katika mitandao mbali mbali ya kijamii.

Katika taarifa hiyo Makala amenukuliwa akisema atakuwa anakutana na wazee hao wa chama kila baada ya miezi mitatu kwa ajili ya kujadili changamoto za mkoa huo.

Suala la kukutana na wazee si jambo baya kwa kiongozi yeyote wa umma hususan wale waliopewa dhamana ya kumuwakilisha Rais katika maeneo yao.

Ubaya unakuja pale kiongozi huyo anapoamini nafasi yake ni kwa ajili ya kundi fulani pekee kama amabvyo amefanya Makala

Kuamini kuwa wazee wenye mlengo wa CCM tu ndiyo wenye kubeba changamoto za wazee wote wa Dar esSalaam, ni kutowatendea haki wazee na wakazi wa Dar kwa ujumla tena kwa kutumia ofisi ya serikali ambayo inatakiwa kuwa wazi wakati wote kupokea na kusikiliza ushauri wa wananchi wote bila kujali kada zao.

Leo hii Makala anatumia ofisi na bajeti ya serikali kukutana na wazee wa chama pekee,ilihali nafasi hiyo ya kichama wazee hao wangetumia kujadili mustakabali wao kwa viongozi wa chama kabla ya kufika serikalini.

Uamuzi huo wa Kibaguzi wa Makala ni tofauti na dhamira nzuri ya Rais Wetu Samia Suluhu Hassan ya kutobagua watanzania kwa itikadi zao.

Rais amewateua wasaidizi wake akiamini watakuwa wamejua dhamira yake lakini kwa haraka sana Amos Makala ameshindwa ama kwa kutojua au kwa kujua kuwa falsafa yake ya kutumia ofisi ya umma kibaguzi, hailingani na matamanio ya Rais
 
Chadema na wapinzani wengine subirini tuu, na nyie mtaitwa ikifika zamu yenu. Au mlifikiri ushabiki wenu maandazi kwa mama Samia utawafanya nyie muonekana ndio bora kuliko CCM? Hamkuitwa kwa hiyo hakuna haja ya lawama.

Kwanza namshangaa huyu mleta uzi kutaka wazee wote wakutane na mkuu wa mkoa. Hivi kuna mtu ana akili timamu anataka kukutana na mkuu wa mkoa? Huyo Mkuu wa mkoa akutane na wanaccm wenzake maana ndio mabingwa wa porojo, lakini huyo mkuu wa mkoa hana msaada wowote kwa hao wazee. Kama rais mwenyewe kukutana na wazee na bado shida zao ziko palepale itakuwa huyo muhuni?
 
Nimefurahishwa sana na mpango wako wa kujianika hadharani .
Huyo mbigwa juzi alisema eti Polepole sio mtu wa mchezo, maana alikuwa sijui kwenye agency gani ya waswedesh eti walitoa $300 sawa na shilingi laki 7 kujenga reli. Hapo ndio nilijua ni bonge la kilaza. Kuna wakati alikuwa anajichanganya anajifanya ni mwanacdm, ila anajisahau anarudi kwenye uccm wake.
 
Jana na leo taarifa ya mkuu mpya wa mkoa wa Dar esSalaam, Amos Makala kukutana na wazee wa CCM wa mkoa huo zimeenea katika mitandao mbali mbali ya kijamii.

Katika taarifa hiyo Makala amenukuliwa akisema atakuwa anakutana na wazee hao wa chama kila baada ya miezi mitatu kwa ajili ya kujadili changamoto za mkoa huo.

Suala la kukutana na wazee si jambo baya kwa kiongozi yeyote wa umma hususan wale waliopewa dhamana ya kumuwakilisha Rais katika maeneo yao.

Ubaya unakuja pale kiongozi huyo anapoamini nafasi yake ni kwa ajili ya kundi fulani pekee kama amabvyo amefanya Makala

Kuamini kuwa wazee wenye mlengo wa CCM tu ndiyo wenye kubeba changamoto za wazee wote wa Dar esSalaam, ni kutowatendea haki wazee na wakazi wa Dar kwa ujumla tena kwa kutumia ofisi ya serikali ambayo inatakiwa kuwa wazi wakati wote kupokea na kusikiliza ushauri wa wananchi wote bila kujali kada zao.

Leo hii Makala anatumia ofisi na bajeti ya serikali kukutana na wazee wa chama pekee,ilihali nafasi hiyo ya kichama wazee hao wangetumia kujadili mustakabali wao kwa viongozi wa chama kabla ya kufika serikalini.

Uamuzi huo wa Kibaguzi wa Makala ni tofauti na dhamira nzuri ya Rais Wetu Samia Suluhu Hassan ya kutobagua watanzania kwa itikadi zao.

Rais amewateua wasaidizi wake akiamini watakuwa wamejua dhamira yake lakini kwa haraka sana Amos Makala ameshindwa ama kwa kutojua au kwa kujua kuwa falsafa yake ya kutumia ofisi ya umma kibaguzi, hailingani na matamanio ya Rais
Rubbish. There is no such thing as Wazee wa CCM. Hivi vikao vya "Wazee wa Dar es Salaam" vilikuwapo tangu enzi za Wakoloni. Ni wazee wa Dar es Salaam - literary ni wazee, huvaa kandambili, kanzu nyeupe na baraghashia, wengi wao sifa yao pekee ni uzee, wala hawajui kusoma. Rejea Kitabu cha Sheikh Mohamed Said kiitwacho THE LIFE AND TIMES OF ABDULWAHEED SYKES, THE FORGOTTEN HISTORY OF THE STRUGGLE BY MUSLIMS IN THE LIVERATION OF TANGANYIKA. Jameni tusikubali tuharibiwe historia ya nchi yetu na hawa wanaharakati wasaliti. Kesho na kesho kutwa Yanga watasema bendera zake mbona ni za chama kimoja? Hiyo nayo ni historia.

Mhe. Makala ni CPA, kama kesho ataamua kukutana na Wahasibu wenziye, mwacheni akutane nao, hata Godbless Lema na Catherine Ruge nao pia ni CPA, waacheni tu wahudhurie. Msisingize eti matumizi ya hela ni za nani, wakitumia Wazee au Wahasibu ni matumuzi rasmi ya umma, si ya chama.

ZFZMWCCM
 
Back
Top Bottom