#COVID19 Amnesty International wanajaribu kuishinikiza Tanzania kununua chanjo ya Covid-19

Shilika la WHO lilikuwa la kwanza kumpongeza mama kuwa rais, unaelewa nn ktk hili na unadhani walimpongeza bure? Nchi yetu ina vibaraka wa kutosha kutimiza hili la msingi ni kuomba Mungu awatie upofu ili wasiweze kuleta uchafu wao huu
 
Kuna nchi kibao kama India zenye uhitaji wa chanjo kwanini wasianze huko?
India wako mbali sana na hili swala. Am telling you, muda si mtefu tutapata tu akili. Mwaka huu watu hakuna kwenda hija bila Chanjo. Itafika wakati tutabaki peke yetu ndio akilia itakaa sawa
 
Hatusemi kuwa hakuna aliyeathirika, bali tunasema Mungu ametuponya na kama Taifa take vizuri mara elfu nyingi ukilinganisha na mataifa mengine! Hilo halina ubishi!
Madhara hayajakuwa makubwa lakini kusema tumeponywa wakati kuna watu wamepoteza mpaka 6 members wa familia ni kuwa insensitive
 
Hakuna aliyesema hatutaki dawa wala chanjo nyingine. Ila hi ya corona haijafanyiwa utafiti wa kutosha na madhara yake tayari yameanza kuonekana! Hakuna ajuaye madhara ya muda mrefu ya hii chanjo! Uk
Ulitaka dunia isubiri miaka 7 kutafuta chanjo ya ugonjwa ambao umeshaua millions. Risk benefit analysis inasema benefits ni kubwa kuliko risks
 
Mnataka wangapi wafe ndiyo msikilize tumepoteza mpaka viongozi wa juu kabisa!!! mnashindia kusema mebeberu tulete chanjo na kupata iwe hiari tatizo liko wapi? wengine tuna wazazi wanataka chanjo.

Hatuwezi kuwanyima watanzania wote chanjo kwa mawazo ya wachache! na haziuzwi madukani au hospitalini! Mimi binafsi nimepigwa chanjo March 5, 2021 sina tatizo lolote mpala leo!
Ila Watanzania kwa ujinga tumo sana. Aliyekwambia chanjo inazuia usiumwe au kufa nani? Hizo chanjo ziko kwenye majaribio. Zinaua, zinatoa mimba zinaharibu mzunguko kwa akina mama. Hayo ni madhara yanayojulikana. Kwa sababu ni za majaribio hakuna anayejua madhara yake kesho au baada ya miaka 10.

Nawashangaa sana Watanzania kulilia chanjo ambazo hata Food and Drug Authority y Wamarekani ambao ni wanasayansi pia hawajaipitisha.

Kila anayetaka kuwageuza Watanzania kama Guinea Pigs, lab rats kufanyia majaribio ni mpumbavu. Rais wetu asiangukie kwenye mtego wa hawa wahuni wanaotaka kutugeuza panya wa majaribio. Wapiga mapambio wengi hawajui hata composition ya hizo chanjo, achilia mbali madhara yake leo na vizazi vijavyo. Wanarudia tu yaliyosemwa kama kasuku!
 
Rais Samia ajue kwamba maamuzi anayoyafanya yakileta madhara watendaji wake wengi watakuja kumruka. Tumeona walivyofanya kwa Rais Magufuli.

Kwa hiyo, mimi raia wake, ninayemtakia mema na mafanikio, akijisikia kufuata ushauri wangu, namsihi aachane tu na hii chanjo. Risk yake ni kubwa mno na hakuna faida tangible. Aache tu kila mtu aishi namna anayoona sawa. Kwa wanaotaka kuchanjwa ziwekwe chanjo za kuuza wakanunue wachanje. Wawekewe vituo maalum waende huko. Wakichanja wakafa ni wao walichagua. Na serikali isizipigie debe kukwepa liability. Watanzania wawe na uchaguzi na asilazimishwe mtu!

Ni huo tu ushauri wangu!
 
There are many humu kwenye jamii forum ambao wanasapoti chanjo ya korona as if they don't see and understand what is going on sad.
 
Hakuna hata mtu mmoja aliye chanjwa amekufa kwenye Dunia hii mpaka leo. Hapa US wamechanja zaidi ya watu milioni 150 hakuna hata mmoja kafa au kulazwa. Kuna chanjo moja tu ya kampuni ya J& J ambayo wanawake sita waliumwa kati ya milioni 7 waliochanjwa lakini wot wazima . India wamechanja wachache sana mnaona yanayotokea kule
ukiwa na nafasi:

 
Ukitembelea tovuti ya Amnesty International ukurasa wa Tanzania utakuta wamebandika andiko wakitaka kamati iliyoundwa ya corona itumike kuhakikisha kuwa Watanzania wanachanjwa chanjo ya corona.

Kinachonishangaza ni kuwa mataifa ya nje yanaongeza sana shinikizo kwa mama kuhusu corona. Wanaingia na gia ya kumsifu na kumponda Hayati Magufuli kuhusu alivyoshughulika na corona. Wanamtaka afuate sayansi na kuachana na kuamini hadithi wao wanaita "myths"!!!

Hawa inabidi tuwaambie wazi kuwa kumtanguliza Mungu siyo kuamini hadithi!! Tanzania haikudharau sayansi Bali ilimtanguliza Mungu mbele ya sayansi!! Chonde chonde huu utaratibu usivurugwe!! Mungu amejibu maombi yetu kwa sababu tulimheshimu kwa wazi na dunia yote ikasikia!! Akaamua kutuponya kwa rehema zake na kwa kulitetea Jina lake mbele ya mataifa!

Si kwamba watanzania ndio tumekuwa wema sana mbele za Mungu! Tukibatilisha hii heshima tuliyompa na kuamua kutanguliza mawazo ya mabeberu wanaotanguliza "sayansi" na kumweka Mungu pembeni, tutakutana na yanayowakuta waliofuata mwelekeo huo!! India ni Taifa LA kwanza duniani kwa kuzalizasha chanjo kwa wingi zaidi lakini hilo halijawasaidia!! Marekani wana chanjo za ziada kwa mamilioni, lakini ndilo linaloongoza kwa kufa na corona!

Tanzania tuko salama hadi sasa mpaka wanashangaa!! Wao wameamua kuabudu sayansi sisi tumeamua kumtanguliza na kumwamini Mungu kuwa atatuokoa ma korona.

Mabeberu wamekuwa wakimsimgizia marehemu Magufuli kuwa alikataa uwepo wa corona. Siyo kweli! Alitambua uwepo wa corona lakini alitumia mbinu tofauti ya kukabiliana nayo. Yeye alikataa kuiga mbinu za mabeberu na akaamua kumtamguliza Mungu kwa kuitisha maombi! Dunia nzima japo wanakataa kukiri lakini wameshuhudia Tanzania tumekuwa salama dhidi ya corona ukilinganisha na mataifa mengine ikiwa ni yale yanayotaka kuiba utukufu wa Mungu kwa kushinikiza tufuate mbinu zao ili waseme ndizo zilizotuokoa vinginevyo tungeisha!

Naomba niwakumbushe: walisema Tanzania tumekataa lockdown tutaokota miili barabarani!! Hilo halijatokea! Mataifa mengi wimbi la pili na la tatu la corona limekuwa la hatari zaidi na wengi wamekufa na mpaka sasa wanakufa! Sisi Tanzania wimbi la pili halikuwa na nguvu Kabisa ndio maana hata shule hatukufunga! Wakati wa maombolezo ya Rais Magufuli watanzania kwa mamilioni walijitokeza kumuaga kwa mamilioni na kusongamana bila barakoa!!

Wakasema baada ya wiki mbili tutaanza kuokota miili barabarani maana tutakuwa tumeambukizana sana!! Haikutokea!! Watuache! Wasitupangie wala wasimshinikize mama kwa habari ya chanjo ya corona!!

Yamewashinda kwao wasiwe wataalamu wa kutusaidia sisi.

RAI yangu: Kama wanataka kutusaidia basi watupe pesa za kumalizia SGR na Stigler's George! Nawasilisha!!
Kwenye hili la Covid, ni Mungu pekee kusimama hakuna cha sanitizer, barakoa wala chanjo hapo. Uhindini pamoja na kuwa na chanjo bora kabisa ila mdudu kawatikisa vibaya mno sisi ni kina nani kama sio Mungu kuwa pamoja nasi?.
 
Muda huu wanajifanya wanatupenda sana! Kama wana nia njema watusaidie kumalizia reli ya standard gauge na mradi wa umeme wa Stiglers George!
Hi Hivi mnakumbuka jinsi walivyoupiga vita mradi wa umeme wa Stiglers Gorge? Haya mapenzi ya Ghafla yametoka wapi?
Wasitupangie!

Unapendekeza Amnesty International watupe fedha za kumalizia miradi ya SGR na Stieglers Gorge? Ndio hao waliopiga vita mradi wa JNHPP? Na sasa wanatulazimisha chanjo?

Au unachukulia Amnesty International kama mwakilishi wa nchi za Magharibi? Wale mnaowaita mabeberu? Ni muhimu uwasilishe hoja yako vizuri tusijeonekana Watanzania kama watu hamnazo!

Hata taasisi za UN tunazishambulia kama ni za mabeberu! Tunasahau kwamba kuna wakati pia zinapambana na hizo nchi: kumbuka US vs WHO.
 
kiukweli hata ikija iwe ni chaguo la mtu na sio lazima,corona ipo ila Mungu ni mwema...hivi unajua India ndio nchi inayoongoza kuwa na dini nyingi na hasa za kuabudu sanamu na wanyama!
 
Hizo chanjo ni wizi kwa Sasa
Makampuni makubwa yanahonga wanasiasa na makundi ya kijamii kulazimisha nchi za Afrika zinunue chanjo ili wapate faida
Watanzania tupo milioni 60,wakipewa chanjo watanzania milioni 15 tu zidisha kwa Bei ya chanjo 13,000 unapata Bilioni 195!
 
Hizi kauli ongea kama Covid haijapita na mtu wako wa karibu.
Peleka chato ukazike huo Ukinjenketile Ngwale wako! Hupimi, huna takwimu utawezaje kusema tumenusurika kwa kiasi gani?! Tumbafyuu kabisa!
 
Back
Top Bottom