Showio
JF-Expert Member
- May 16, 2019
- 255
- 481
Mtoto anapotembea kwa mara ya kwanza ni tukio la kusisimua. Kila mtu nyumbani hufurahia na kusimuliana jinsi alivyopiga hatua tatu za mwanzo. Huwa hawasimuliani kuwa amepiga hatua chache au ameanguka baada ya hatua tatu. Wote husimulia kuwa anatembea. Wazazi hufurahi zaidi maana mtoto wao ametembea.
Iwe hivyo tunapomwona mtu akiwa anayumba na kujitahidi kupiga hatua chache za maendeleo. Amefata mzigo ameuza, amepata faida kiduchu au imemkata, usimzomee na kuona hawezi. Usimvunje moyo kuwa hawezi kabisa. Furahia kwa vile amepiga hatua za mwanzo. Ameweza kunyanyua miguu na kuubeba mwili wake.
Iwe hivyo tunapomwona mtu akiwa anayumba na kujitahidi kupiga hatua chache za maendeleo. Amefata mzigo ameuza, amepata faida kiduchu au imemkata, usimzomee na kuona hawezi. Usimvunje moyo kuwa hawezi kabisa. Furahia kwa vile amepiga hatua za mwanzo. Ameweza kunyanyua miguu na kuubeba mwili wake.