seif_tanzania
Member
- Nov 23, 2017
- 14
- 2
Imeaandaliwa na ndugu IDDY SEIF HARUNA
Tanzania oooh Tanzania kila mmoja wetu ni shahidi juu ya hili tunaelekea katika maadhimisho ya 56 ya sherehe za Uhuru nchini. Lakini lazima tuwe na maswalii juu ya kujibu kuhusiana na Uhuru wetu
1. Je Uhuru tuliopata tumeufanyia nini?
Leo naandika makala haya nikitizamia miaka 56 ya Uhuru VIJANA tumefanya nini?
Siasa ni mchezo mchafu ambao umekuwa ukipoteza wingi wa vijana katika taifa hili wenye uwezo fikra ya kinifu za kimaendeleo na uzalendo badala yake wamebaki wakiishi chini ya cheni ya utumwa wa kisiasi
Vijana wengi wamekuwa wakitumiwa kufanya kazi na kupambana kutimiza ndoto za watu wengine pasipo kuangalia ndoto zao. Vijana wamekuwa wakipoteza muda mwingi kuhama katika vyama tofauti vya kisiasa pasipo kujua au kugundua dira na misingi yakinifu ya kimaisha yao. Vijana ni miaka 56 sasa ya sherehe za Uhuru lakini bado hawajatambu fika na vyema wao ni kina nanii..? wanatakiwa kufanya nini? na ni kwa wakati gani?..
Sera ya UZALENDO sasa kwa wingi wa vijana katika taifa hili imegeuzwa ni mtaji wamekuwa wakikesha kwenye mitandao ya kijamii kuamasisha uzalendo lakini sio ule uzalendo alikuwa akiusema Baba wa Taifa Mwalimu JULIUS KAMBARAGE NYERERE wao wameona kueneza kwa njia yao ya kiutofauti ili waweze kuonekana na kutengeneza majina yao na kupambana kutafuta nafasi ya uongozi katika taifa hili
Vijana ni miaka 56 ya maadhimisho ya sherehe za Uhuru lakini wengi wanaelimu kutoka vyuo vikubwa duniania lakini wamekuwa wakitazamia kupata nafasi za uongozi katika taifa hili na kujiung kwenye vyama vya siasa ili waweze kuonekana lakini wanashindwa kutumia tunu ya ujuzi walionao kwa ajili ya kulijenga taifa na kujiajiri ili kupunguza kero ya ajira katika taifa hili
Ni miaka 56 ya sherehe za maadhimisho ya Uhuru lakini vijana bado hatujui tunaenda wapii huu ni wakati wa kujikomboa wenyewe kujenga mipango endelevu kupinga na kuepuka kero za wanasiasa ili tuweze kulijenga taifa letu
AMKA VIJANA
AMKA TANZANIA
Imeaandaliwa tarehe 07.12.2017
Na ndugu IDDY SEIF HARUNA
Tanzania oooh Tanzania kila mmoja wetu ni shahidi juu ya hili tunaelekea katika maadhimisho ya 56 ya sherehe za Uhuru nchini. Lakini lazima tuwe na maswalii juu ya kujibu kuhusiana na Uhuru wetu
1. Je Uhuru tuliopata tumeufanyia nini?
Leo naandika makala haya nikitizamia miaka 56 ya Uhuru VIJANA tumefanya nini?
Siasa ni mchezo mchafu ambao umekuwa ukipoteza wingi wa vijana katika taifa hili wenye uwezo fikra ya kinifu za kimaendeleo na uzalendo badala yake wamebaki wakiishi chini ya cheni ya utumwa wa kisiasi
Vijana wengi wamekuwa wakitumiwa kufanya kazi na kupambana kutimiza ndoto za watu wengine pasipo kuangalia ndoto zao. Vijana wamekuwa wakipoteza muda mwingi kuhama katika vyama tofauti vya kisiasa pasipo kujua au kugundua dira na misingi yakinifu ya kimaisha yao. Vijana ni miaka 56 sasa ya sherehe za Uhuru lakini bado hawajatambu fika na vyema wao ni kina nanii..? wanatakiwa kufanya nini? na ni kwa wakati gani?..
Sera ya UZALENDO sasa kwa wingi wa vijana katika taifa hili imegeuzwa ni mtaji wamekuwa wakikesha kwenye mitandao ya kijamii kuamasisha uzalendo lakini sio ule uzalendo alikuwa akiusema Baba wa Taifa Mwalimu JULIUS KAMBARAGE NYERERE wao wameona kueneza kwa njia yao ya kiutofauti ili waweze kuonekana na kutengeneza majina yao na kupambana kutafuta nafasi ya uongozi katika taifa hili
Vijana ni miaka 56 ya maadhimisho ya sherehe za Uhuru lakini wengi wanaelimu kutoka vyuo vikubwa duniania lakini wamekuwa wakitazamia kupata nafasi za uongozi katika taifa hili na kujiung kwenye vyama vya siasa ili waweze kuonekana lakini wanashindwa kutumia tunu ya ujuzi walionao kwa ajili ya kulijenga taifa na kujiajiri ili kupunguza kero ya ajira katika taifa hili
Ni miaka 56 ya sherehe za maadhimisho ya Uhuru lakini vijana bado hatujui tunaenda wapii huu ni wakati wa kujikomboa wenyewe kujenga mipango endelevu kupinga na kuepuka kero za wanasiasa ili tuweze kulijenga taifa letu
AMKA VIJANA
AMKA TANZANIA
Imeaandaliwa tarehe 07.12.2017
Na ndugu IDDY SEIF HARUNA