SHIEKA
JF-Expert Member
- Dec 20, 2011
- 8,244
- 4,258
Hki ni kisa cha kweli kilichotokea Dar es Salaam kwenye miaka ya tisini na.... Na kilishawahi kuandikwa mahali na pengine baadhi ya wanaMMU wanakifahamu. Haya tuanze.
Huyu rafiki yangu, naomba tumwite James, alikuwa mtu aliyenipita sana umri na tulifahamiana wakati mimi nasoma chuo kimoja kilichopo Dar.Alikuwa anafanya kazi wizara ya Mambo ya nje na Ushirikiano wa kimataifa na kuishi Mwenge.
Kipindi fulani alitakiwa kwenda Afrika Magharibi kuhudhuria mkutano. Safari yake ikaandaliwa vizuri na ilikuwa apande ndege toka Uwanja wa ndege wa kimataifa Dar-es-Salaam.Siku ya safari akaondoka Mwenge asubuhi kama saa tatu hivi kuelekea uwanja wa ndege akiendesha gari yake. Njiani, maeneo ya Kinondoni, akaona kundi la wanawake, mmojawao akimwashiria kuomba lift. Jamaa akaanza kuwaza, Hawa wamama wana tatizo gani? Na ntawezaje kuwasaidia ilhali nakimbilia ndege ya kwenda mkutanoni?
Kitu kikamwambia asimame awasikilize, na kweli akafanya hivyo. Kumbe mama mmoja mjamzito alikuwa kwenye hali mbaya ya uchungu alihitajika kukimbizwa Muhimbili kujifungua. James akashindwa kukataa, akamchukua mgonjwa na huyooo mpaka Muhimbili. James hakuondoka hospitali mpaka taratibu zote za kumpokea mgonjwa zilipoisha na mgonjwa kulazwa wodini.Alipotazama saa yake, ilikuwa saa tano kasoro muda ambao ndege ilikuwa imeshaondoka. kwa hiyo safari ya Afrika magharibi ikawa imekufa! Jamaa hakuwa na jingine la kufanya ila kujirudia nyumbani.Kesho yake alienda kazini akiwa na kisingizio kikali kwa nini hakuenda safari. Akaendelea na kazi mpaka kile kisa cha lift akaanza kukisahau kwa jinsi miaka ilivyosonga mbele.
Ilipofika mwaka 1999 James akastaafu kazi. Katika kumudu maisha ya kustaafu, akaamua atafute shamba ili ajenge na kulima.Akaulizia mambo ya shamba kwa marafiki zake, na mmoja akamwambia kwamba kuna shamba linauzwa maeneo ya Boko.
James na rafiki yake wakapanga kwenda Boko Jumamosi moja na rafiki akampeleka kwa muuza shamba. Muuza shamba alikuwa mwanamke, na James alistuka sana kwa jinsi yule mwanamke alivyokuwa anamtazama wakati wanazungumza.Yule mwanamke aliacha mazungumzo na kumwambia James," Kama nakufananisha naomba unwie radhi, lakini unafanana sana na baba mmoja aliyenipa lift ya kwenda muhimbili niliposhikwa na uchungu wa mwanangu Joyce" James akajibu,"Ndiyo, hiyo lift naikumbuka sana ila huyo mwanamke simkumbuki" "Ilikuwa ni mimi! Mimi!" Yule mama alisema kwa furaha huku akirukaruka na kuendelea kusema,"Kama shida yako ni shamba babangu,njoo huku kuna shamba lako nimeakuandalia na wala sitaki shilingi ya mtu." James alikabidhiwa shamba la ekari sita.
Huyu rafiki yangu, naomba tumwite James, alikuwa mtu aliyenipita sana umri na tulifahamiana wakati mimi nasoma chuo kimoja kilichopo Dar.Alikuwa anafanya kazi wizara ya Mambo ya nje na Ushirikiano wa kimataifa na kuishi Mwenge.
Kipindi fulani alitakiwa kwenda Afrika Magharibi kuhudhuria mkutano. Safari yake ikaandaliwa vizuri na ilikuwa apande ndege toka Uwanja wa ndege wa kimataifa Dar-es-Salaam.Siku ya safari akaondoka Mwenge asubuhi kama saa tatu hivi kuelekea uwanja wa ndege akiendesha gari yake. Njiani, maeneo ya Kinondoni, akaona kundi la wanawake, mmojawao akimwashiria kuomba lift. Jamaa akaanza kuwaza, Hawa wamama wana tatizo gani? Na ntawezaje kuwasaidia ilhali nakimbilia ndege ya kwenda mkutanoni?
Kitu kikamwambia asimame awasikilize, na kweli akafanya hivyo. Kumbe mama mmoja mjamzito alikuwa kwenye hali mbaya ya uchungu alihitajika kukimbizwa Muhimbili kujifungua. James akashindwa kukataa, akamchukua mgonjwa na huyooo mpaka Muhimbili. James hakuondoka hospitali mpaka taratibu zote za kumpokea mgonjwa zilipoisha na mgonjwa kulazwa wodini.Alipotazama saa yake, ilikuwa saa tano kasoro muda ambao ndege ilikuwa imeshaondoka. kwa hiyo safari ya Afrika magharibi ikawa imekufa! Jamaa hakuwa na jingine la kufanya ila kujirudia nyumbani.Kesho yake alienda kazini akiwa na kisingizio kikali kwa nini hakuenda safari. Akaendelea na kazi mpaka kile kisa cha lift akaanza kukisahau kwa jinsi miaka ilivyosonga mbele.
Ilipofika mwaka 1999 James akastaafu kazi. Katika kumudu maisha ya kustaafu, akaamua atafute shamba ili ajenge na kulima.Akaulizia mambo ya shamba kwa marafiki zake, na mmoja akamwambia kwamba kuna shamba linauzwa maeneo ya Boko.
James na rafiki yake wakapanga kwenda Boko Jumamosi moja na rafiki akampeleka kwa muuza shamba. Muuza shamba alikuwa mwanamke, na James alistuka sana kwa jinsi yule mwanamke alivyokuwa anamtazama wakati wanazungumza.Yule mwanamke aliacha mazungumzo na kumwambia James," Kama nakufananisha naomba unwie radhi, lakini unafanana sana na baba mmoja aliyenipa lift ya kwenda muhimbili niliposhikwa na uchungu wa mwanangu Joyce" James akajibu,"Ndiyo, hiyo lift naikumbuka sana ila huyo mwanamke simkumbuki" "Ilikuwa ni mimi! Mimi!" Yule mama alisema kwa furaha huku akirukaruka na kuendelea kusema,"Kama shida yako ni shamba babangu,njoo huku kuna shamba lako nimeakuandalia na wala sitaki shilingi ya mtu." James alikabidhiwa shamba la ekari sita.