Amini usiamini: Dar ni UKAWA na UKAWA ni Dar

Quinine

JF-Expert Member
Jul 26, 2010
21,271
47,271
Zaidi ya asilimia 80 ya wakazi wa Dar es salaam ni wanachama au mashabiki wa vyama vinavyounda UKAWA. CCM Dar ni kama 20% tu matokeo ya uchaguzi uliopita ni shahidi mzuri.

Bila serikali kutumia nguvu za ziada nina imani wabunge wote wangetoka UKAWA, madiwani wote wangetoka UKAWA, wenyeviti wote wa mitaa wangetoka UKAWA, na Mameya wote wangetoka UKAWA.

UKAWA Dar ni sawa na CHADEMA Arusha, inaweza kushinda uchaguzi wowote bila kufanya hata mkutano mmoja.

RC peke yake hawezi kuliongoza jiji la Dar, hawezi kusimamia usafi kila sehemu, hawezi kufanikisha ulinzi na amani wakati wote, hawezi kuyajua matatizo ya wakazi kwa kufanya ziara ya siku mbili bila kuwashirikisha Wenyeviti wa Mitaa.

Kwa hiyo Rais na Makonda wajue kuwa Dar ni UKAWA na UKAWA ndiyo Dar es salaam yenyewe hata wafanye vipi labda waamue kutawala.

Karibu kwa mjadala.
 
Siku mkiweza kuidhibiti kanda ya ziwa ambayo ndiyo ina wapiga kura wengi mtachukua nchi mapema lakini mkitegemea hao wa dar tu matakalia kusema mnaongoza majiji ili hali juu wapo wengini ni hayo
 
Ukweli uko wazi, CCM inabidi waje na mbinu modern sana kushawishi wakazi wa jiji. maana idadi ya watu wanofuata mikumbo ni wachache kuliko wanaojitambua. mkakati wowote wa kulirudisha jiji chini yao inabidi uwe wa mahesabu ya hali ya juu sio ubabe na nguvu
 
Zaidi ya asilimia 80 ya wakazi wa Dar es salaam ni wanachama au mashabiki wa vyama vinavyounda UKAWA. CCM Dar ni kama 20% tu matokeo ya uchaguzi uliopita ni shahidi mzuri.

Bila serikali kutumia nguvu za ziada nina imani wabunge wote wangetoka UKAWA, madiwani wote wangetoka UKAWA, wenyeviti wote wa mitaa wangetoka UKAWA, na Mameya wote wangetoka UKAWA.

UKAWA Dar ni sawa na CHADEMA Arusha, inaweza kushinda uchaguzi wowote bila kufanya hata mkutano mmoja.

RC peke yake hawezi kuliongoza jiji la Dar, hawezi kusimamia usafi kila sehemu, hawezi kufanikisha ulinzi na amani wakati wote, hawezi kuyajua matatizo ya wakazi kwa kufanya ziara ya siku mbili bila kuwashirikisha Wenyeviti wa Mitaa.

Kwa hiyo Rais na Makonda wajue kuwa Dar ni UKAWA na UKAWA ndiyo Dar es salaam yenyewe hata wafanye vipi labda waamue kutawala.

Karibu kwa mjadala.
Dar hawana wapiga kura waaminifu kama Arusha. Dar wanapiga kura kwa maslahi tu na siyo ushabiki.
 
Zaidi ya asilimia 80 ya wakazi wa Dar es salaam ni wanachama au mashabiki wa vyama vinavyounda UKAWA. CCM Dar ni kama 20% tu matokeo ya uchaguzi uliopita ni shahidi mzuri.

Bila serikali kutumia nguvu za ziada nina imani wabunge wote wangetoka UKAWA, madiwani wote wangetoka UKAWA, wenyeviti wote wa mitaa wangetoka UKAWA, na Mameya wote wangetoka UKAWA.

UKAWA Dar ni sawa na CHADEMA Arusha, inaweza kushinda uchaguzi wowote bila kufanya hata mkutano mmoja.

RC peke yake hawezi kuliongoza jiji la Dar, hawezi kusimamia usafi kila sehemu, hawezi kufanikisha ulinzi na amani wakati wote, hawezi kuyajua matatizo ya wakazi kwa kufanya ziara ya siku mbili bila kuwashirikisha Wenyeviti wa Mitaa.

Kwa hiyo Rais na Makonda wajue kuwa Dar ni UKAWA na UKAWA ndiyo Dar es salaam yenyewe hata wafanye vipi labda waamue kutawala.

Karibu kwa mjadala.

ni ukweli mtupu.. ndo maana katika mikutano yake mteule wa mkulu anawaweka watu mbaroni wakimuuliza maswali yasiyoifurahisha ccm na makada wao. matokeo ya ubabe huu mikutano iyo watu hawaudhurii.

jana uko Goba ktk mkutano wake walijaa watoto walokua uwanjan hapo wakicheza mpira na makada wenzake wa ccm. . ati ana kazi maalum ya kupambana na ukawa duh kweli kwa miitikio kt mikutano yake real naye wananchi wanamsomesha nambali
 
Dar hawana wapiga kura waaminifu kama Arusha. Dar wanapiga kura kwa maslahi tu na siyo ushabiki.
Nilitaka kumjibu hivihivi, itakuwa ni kosa kubwa sana kulinganisha Dar na mikoa ya Moshi na Arusha. Kule kaskazini hata uwe mwendawazimu ila ukigombea kwa tiketi ya CDM utashinda kwa sababu ya ukabila.
Naomba CDM wasijisahau, Musoma napo waliamini hivi hivi, Tarime baada ya Chacha Wangwe CDM walishinda wakaamini huko kushinda ni lazima,ni kosa kubwa sana mtakalofanya kuamini Dar ni ya UKAWA.
 
Zaidi ya asilimia 80 ya wakazi wa Dar es salaam ni wanachama au mashabiki wa vyama vinavyounda UKAWA. CCM Dar ni kama 20% tu matokeo ya uchaguzi uliopita ni shahidi mzuri.

Bila serikali kutumia nguvu za ziada nina imani wabunge wote wangetoka UKAWA, madiwani wote wangetoka UKAWA, wenyeviti wote wa mitaa wangetoka UKAWA, na Mameya wote wangetoka UKAWA.

UKAWA Dar ni sawa na CHADEMA Arusha, inaweza kushinda uchaguzi wowote bila kufanya hata mkutano mmoja.

RC peke yake hawezi kuliongoza jiji la Dar, hawezi kusimamia usafi kila sehemu, hawezi kufanikisha ulinzi na amani wakati wote, hawezi kuyajua matatizo ya wakazi kwa kufanya ziara ya siku mbili bila kuwashirikisha Wenyeviti wa Mitaa.

Kwa hiyo Rais na Makonda wajue kuwa Dar ni UKAWA na UKAWA ndiyo Dar es salaam yenyewe hata wafanye vipi labda waamue kutawala.

Karibu kwa mjadala.
Toeni mfano ili mkabidhiwe nchi.
Hadi sasa Far ni ile ile Kama kawa
 
Siku mkiweza kuidhibiti kanda ya ziwa ambayo ndiyo ina wapiga kura wengi mtachukua nchi mapema lakini mkitegemea hao wa dar tu matakalia kusema mnaongoza majiji ili hali juu wapo wengini ni hayo
ubabe si ulitumika kupata majimbo, na ukerewe washukuru ziwa la sivyo kungekuwa na barabara wangeibuka kama walivyoibuka nyamagana na buzilayombo kutumia ubabe, ukerewe ndo likabaki jimbo pekee lililo chini ya ukawa,
 
ni ukweli mtupu.. ndo maana katika mikutano yake mteule wa mkulu anawaweka watu mbaroni wakimuuliza maswali yasiyoifurahisha ccm na makada wao. matokeo ya ubabe huu mikutano iyo watu hawaudhurii.

jana uko Goba ktk mkutano wake walijaa watoto walokua uwanjan hapo wakicheza mpira na makada wenzake wa ccm. . ati ana kazi maalum ya kupambana na ukawa duh kweli kwa miitikio kt mikutano yake real naye wananchi wanamsomesha nambali
nimependa
 
Nilitaka kumjibu hivihivi, itakuwa ni kosa kubwa sana kulinganisha Dar na mikoa ya Moshi na Arusha. Kule kaskazini hata uwe mwendawazimu ila ukigombea kwa tiketi ya CDM utashinda kwa sababu ya ukabila.
Naomba CDM wasijisahau, Musoma napo waliamini hivi hivi, Tarime baada ya Chacha Wangwe CDM walishinda wakaamini huko kushinda ni lazima,ni kosa kubwa sana mtakalofanya kuamini Dar ni ya UKAWA.
labda utumike ubabe na kanjanja, we mshabomolea watu nyumba zao mnategemea kweli utapendwa, mnalazimisha watu wawapende kwa ubabe, mnaweza mkalipata lakini lazma demography itokee manake hamtakubali,
 
labda utumike ubabe na kanjanja, we mshabomolea watu nyumba zao mnategemea kweli utapendwa, mnalazimisha watu wawapende kwa ubabe, mnaweza mkalipata lakini lazma demography itokee manake hamtakubali,
Huko Musoma kwani ulitumika ubabe...ni mahesabu tu, naomba viongozi wasijisahau kabisa la sivyo majimbo yote yatarudi CCM. Musoma mfano Vicent aligawia mpaka wananchi vibanda vya biashara kwa kumnyang'anya Mathayo, na halmashauri ilikuwa chini ya CDM lakini madiwani karibia wote walipigwa chini pamoja na mbunge. Dar sio Arusha na Moshi. Jana nilikuwa bar moja hapa Dar wakawa wamefungulia Clouds FM Makonda akawa anaongea baada ya kama dkk kumi hivi meneja( badaye nilikuja kusikia akiitwa Masawe) akatokea akazima redio wateja walianza kumshambulia arudishe waendelee kumsikiliza Makonda mteja mmoja kwa dharau akamwambia meneja au wewe ni CDM. Hii hali mwaka jana kipindi cha uchaguzi isingetokea.
Viongozi wa CDM inabidi wafanye kazi maana strategy ya kusubiria makapi ya CCM sijui kama itafanya kazi tena.
 
Kiuhalisia wajipange vizuri. Mi niko Arusha lakin dalili zinaonyesha wazi kuwa wasipojipanga 2020 Arusha inaweza kurudi ccm. Strategy wanazotumia ccm chin ya magufuli ni mpumbavu tu anaeweza kuzidharau lakin wenye akili wameshajua kuwa inahitajika nguvu ya ziada kulinda majimbo yaliyochin ya ukawa.

Kuishi kwa matumain hakutawasaidia. Ccm ni mabingwa wa huu mchezo wa siasa. Ukiwadharau utakuwa unalia kila siku kama akina obama wanavolia uko Marekani. Ukiangalia kura walizopata ccm na Cdm Arusha na moshi utaelewa kuwa kazi ipo. Sehemu ambayo unaweza kusema una uhakika kwa kutumia records za uchaguzi uliopita ni mbeya mjini kwa sugu. Huyo ndo alipata kura nyingi sana kuliko mbunge yeyote Tanzania hii. Labda uko ndo unaweza kusema records hizo zinatia moyo ingawa historia pia haiwapi guarantee akina sugu kushinda tena. Stil wanayo kazi ya kufanya.
 
Nakubaliana na mleta mada...

Dar ni UKAWA...

Haya majamaa hata yafanyaje jiji ndio wameshalipoteza, kulirudisha hata wafanyaje haiwezekani.
 
Zaidi ya asilimia 80 ya wakazi wa Dar es salaam ni wanachama au mashabiki wa vyama vinavyounda UKAWA. CCM Dar ni kama 20% tu matokeo ya uchaguzi uliopita ni shahidi mzuri.

Bila serikali kutumia nguvu za ziada nina imani wabunge wote wangetoka UKAWA, madiwani wote wangetoka UKAWA, wenyeviti wote wa mitaa wangetoka UKAWA, na Mameya wote wangetoka UKAWA.

UKAWA Dar ni sawa na CHADEMA Arusha, inaweza kushinda uchaguzi wowote bila kufanya hata mkutano mmoja.

RC peke yake hawezi kuliongoza jiji la Dar, hawezi kusimamia usafi kila sehemu, hawezi kufanikisha ulinzi na amani wakati wote, hawezi kuyajua matatizo ya wakazi kwa kufanya ziara ya siku mbili bila kuwashirikisha Wenyeviti wa Mitaa.

Kwa hiyo Rais na Makonda wajue kuwa Dar ni UKAWA na UKAWA ndiyo Dar es salaam yenyewe hata wafanye vipi labda waamue kutawala.

Karibu kwa mjadala.
NDOTO ZA MLEVI !
 
Katika uchaguzi kila kitu kinawezekana, sitashangaa endapo 2020 CDM wasipopata mbunge hata mmoja achilia mbali kura za uraisi, nahii ni kutokana na aina ya siasa za kipindi hiki. Chama cha siasa ni watu. Unapozuiwa kufanya mikutano ya kisiasa unategemea nini?? Unaporuhusu chama tawala pekee kufanya mkutano ya kisiasa na kuvinyima haki vyama vya siasa unategemea miujiza gani kwa vyama vya upinzani kuendelea kuishi?? Mfano mzuri Rwanda, kagame anasifika kwa sababu hakuna mtu anayethubutu kumnyoshea kidole, Leo anauhakika wa kushinda kila changuzi kutokana na mazingira aliyoyaweka. Hivyo kwa jinsi mazingira yanavyoandaliwa hakuna ubishi lazima tukubali CCM kushinda kwa kishindo tena kuvunja record zote za watangulizi wake. Tusubiri na tujiandae kuyapokea.
 
Zaidi ya asilimia 80 ya wakazi wa Dar es salaam ni wanachama au mashabiki wa vyama vinavyounda UKAWA. CCM Dar ni kama 20% tu matokeo ya uchaguzi uliopita ni shahidi mzuri.

Bila serikali kutumia nguvu za ziada nina imani wabunge wote wangetoka UKAWA, madiwani wote wangetoka UKAWA, wenyeviti wote wa mitaa wangetoka UKAWA, na Mameya wote wangetoka UKAWA.

UKAWA Dar ni sawa na CHADEMA Arusha, inaweza kushinda uchaguzi wowote bila kufanya hata mkutano mmoja.

RC peke yake hawezi kuliongoza jiji la Dar, hawezi kusimamia usafi kila sehemu, hawezi kufanikisha ulinzi na amani wakati wote, hawezi kuyajua matatizo ya wakazi kwa kufanya ziara ya siku mbili bila kuwashirikisha Wenyeviti wa Mitaa.

Kwa hiyo Rais na Makonda wajue kuwa Dar ni UKAWA na UKAWA ndiyo Dar es salaam yenyewe hata wafanye vipi labda waamue kutawala.

Karibu kwa mjadala.
Msichokijua ni kwamba DAR ni CCM damu damu ila Kilichotokea mwaka jana ni LOWASSA Impact.

- Lowassa aliwekeza muda mrefu sana kwa mama ntilie na bodaboda wa dar, kama wewe ni mkazi wa dar utakuwa umekutana na bodaboda zimeandikwa Donated by Edward Lowassa.


- Kipindi cha uchaguzi Lowassa amefanya kampeni kubwa sana ndani ya DAR zaidi ya mara nne na bado kuna wabunge 5 wa CCM wamebaki.

Sasa mkiendelea kupiga porojo humu 2020 hamtaamii macho yenu maana hata pesa za kugawa kwenye makanisa na misikiti kwa sasa hazipo .
 
Back
Top Bottom