Azipa
JF-Expert Member
- Mar 19, 2012
- 1,069
- 322
Chifupa atishiwa kuuawa
2006-11-16 09:03:34
Na Rosemary Mirondo na Beatrice Philemon
Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Bi. Amina Chifupa, ametishiwa kuuawa na watu wasiojulikana kupitia simu yake ya mkononi.
Madai ya mbunge huyu aliyatoa jana alipozungumza na waandishi wa habari hizi kwa njia ya simu kutoka Dodoma alikokuwa akihudhuria kikao cha Bunge kilichomalizika jana. Alisema amepokea vitisho kupitia vijikaratasi alivyoandikiwa akiwa ndani ya ukumbi wa Bunge, vikimuonya aachane na suala la wauza unga.
''Sambamba na ujumbe huo, kupitia simu yangu ya mkononi nilitumiwa ujumbe mfupi wa maneno wa kunitishia kuniua.'' Mbali na hayo, ndani ya ukumbi wa Bunge kwenyewe nimepokea ujumbe wa vikaratasi visivyo na majina vikisema kwamba ninajifanya najua kuongea'', aliongeza kusema mbunge huyo ambaye alisisitiza bado hatetereki kwa vitisho hivyo.
Ujumbe mwingine unasema "we Amina wewe acha wewe, usijifanye unajua sana, ukiwa kwenye jumba la vioo usirushe mawe wakati na wewe umo ndani, tunaanza kukuchunguza kuanzia leo unapata wapi pesa, ni SISI USALAMA WA TAIFA Hivi wewe Amina unajiona wewe ni msafi sana? Au kwa kuwa sisi tumekaa kimya. Wewe ni mchafu sana , na sisi tukiamua kuanza kukuchafua hapatakalika hapa. Dawa yako iko jikoni inachemka, ndio utajua sisi ni nani umeyataka mwenyewe usimlaumu mtu. Wameshindwa wakongwe wewe mtoto wa juzi.
Aidha Bi.Amina alipigiwa simu inayoonyesha kutoka nje ambayo ilisomeka call kwenye simu yake yenye matusi ya nguoni yakimuonya aache kuropoka. Vitisho dhidi ya mbunge huyu jasiri na chipukizi, vimekuja siku moja tu baada ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya jinai nchini, Bw.Robert Manumba kuahidi kuwa Jeshi la Polisi litamlinda na lipo tayari kupokea taarifa zinazohusu vinara wa uuzaji na usambazaji wa dawa za kulevya nchini.
Aidha, Bi. Amina alisema amepokea simu kutoka kwa mtu aliyejitaja kuwa ni polisi, akimuonya asiongee na mtu yeyote kuhusu suala hilo, mpaka atakapotoka bungeni na kumshauri mara atakapotoka Dodoma aende moja kwa moja kwa Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Bw. Robert Manumba, kuonana naye.
Hata hivyo, Bi. Amina hakutaka kutaja jina la polisi huyo. Bi. Amina alisema pamoja na kupokea vitisho hivyo, hataacha kufichua wafanyabiashara hao kwa sababu wanachangia kuwaangamiza vijana ambao ni taifa la kesho.
Alisema baada ya kutangaza bungeni kuwa yupo tayari kuwafichua vigogo wanaojihusisha na biashara haramu ya dawa za kulevya, ameanza kupata ushirikiano kutoka kwa wabunge wachache wanaochukizwa na biashara hiyo.
Nipashe ilipoongea na Kamishna Manumba jana kuhusu vitisho anavyopokea Mbunge huyo, alisema yeye hajapata taarifa zozote mbali na kusema kuwa suala hilo linahitaji kushughulikiwa kitaalamu.
Hata hivyo, alisema kwa sasa anaweza kuwasiliana na kituo cha polisi Dodoma au kikosi cha kuzuia madawa ya kulevya. "Pamoja na ujasiri wa Mbunge huyo, pia tunahitaji watu wengine wajitokeze kutoa majina ya wafanyabiashara hao ili tuweze kutokomeza biashara hiyo inayoleta madhara nchini," alisema Bw. Manumba.
Kamishna Manumba alisema kuwa ili kuweza kukabiliana na biashara hiyo nchini, unahitajika ushirikiano kutoka serikalini na watu binafsi kwani suala hilo litashughulikiwa kwa siri kwa ajili ya kuwalinda watoa taarifa. "Serikali ishirikiane kupiga vita suala hilo kisiasa na sisi tutalishughulikia kitaaluma," alisema Kamishna Manumba.
Alisema hilo ni tatizo la kimataifa hivyo inakuwa ni vugumu kuwabaini vigogo halisi wanaohusika na kilimo na kutengeneza madawa hayo kwani hapa nchini wanaohusika na madawa ya kulevya ni mawakala. Alisema kuwa wazalishaji wakubwa wapo nchi za nje kama Mashariki ya Kati, Mashariki ya Mbali, Latin America na Afghanstan.
Aliongeza kuwa kama serikali za nchi za Afrika na Bara la Ulaya zitakuwa imara, vyombo vya serikali vitaweza kufanyakazi zake vizuri katika kuweka mikakati ya kupambana hatimaye kupunguza tatizo hilo la madawa ya kulevya.
Hata hivyo, Kamishna Manumba alisema kuwa hadi sasa hawajapata ushahidi unaoonyesha kwamba vigogo wanaotoka serikalini au taasisi wanashiriki katika uuzaji wa dawa za kulevya ila wamebaini kuwa kuna wafanyabiashara wakubwa ndio wanaoongoza kuingiza madawa ya kulevya nchini kama mawakala.
SOURCE: Nipashe
2006-11-16 09:03:34
Na Rosemary Mirondo na Beatrice Philemon
Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Bi. Amina Chifupa, ametishiwa kuuawa na watu wasiojulikana kupitia simu yake ya mkononi.
Madai ya mbunge huyu aliyatoa jana alipozungumza na waandishi wa habari hizi kwa njia ya simu kutoka Dodoma alikokuwa akihudhuria kikao cha Bunge kilichomalizika jana. Alisema amepokea vitisho kupitia vijikaratasi alivyoandikiwa akiwa ndani ya ukumbi wa Bunge, vikimuonya aachane na suala la wauza unga.
''Sambamba na ujumbe huo, kupitia simu yangu ya mkononi nilitumiwa ujumbe mfupi wa maneno wa kunitishia kuniua.'' Mbali na hayo, ndani ya ukumbi wa Bunge kwenyewe nimepokea ujumbe wa vikaratasi visivyo na majina vikisema kwamba ninajifanya najua kuongea'', aliongeza kusema mbunge huyo ambaye alisisitiza bado hatetereki kwa vitisho hivyo.
Ujumbe mwingine unasema "we Amina wewe acha wewe, usijifanye unajua sana, ukiwa kwenye jumba la vioo usirushe mawe wakati na wewe umo ndani, tunaanza kukuchunguza kuanzia leo unapata wapi pesa, ni SISI USALAMA WA TAIFA Hivi wewe Amina unajiona wewe ni msafi sana? Au kwa kuwa sisi tumekaa kimya. Wewe ni mchafu sana , na sisi tukiamua kuanza kukuchafua hapatakalika hapa. Dawa yako iko jikoni inachemka, ndio utajua sisi ni nani umeyataka mwenyewe usimlaumu mtu. Wameshindwa wakongwe wewe mtoto wa juzi.
Aidha Bi.Amina alipigiwa simu inayoonyesha kutoka nje ambayo ilisomeka call kwenye simu yake yenye matusi ya nguoni yakimuonya aache kuropoka. Vitisho dhidi ya mbunge huyu jasiri na chipukizi, vimekuja siku moja tu baada ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya jinai nchini, Bw.Robert Manumba kuahidi kuwa Jeshi la Polisi litamlinda na lipo tayari kupokea taarifa zinazohusu vinara wa uuzaji na usambazaji wa dawa za kulevya nchini.
Aidha, Bi. Amina alisema amepokea simu kutoka kwa mtu aliyejitaja kuwa ni polisi, akimuonya asiongee na mtu yeyote kuhusu suala hilo, mpaka atakapotoka bungeni na kumshauri mara atakapotoka Dodoma aende moja kwa moja kwa Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Bw. Robert Manumba, kuonana naye.
Hata hivyo, Bi. Amina hakutaka kutaja jina la polisi huyo. Bi. Amina alisema pamoja na kupokea vitisho hivyo, hataacha kufichua wafanyabiashara hao kwa sababu wanachangia kuwaangamiza vijana ambao ni taifa la kesho.
Alisema baada ya kutangaza bungeni kuwa yupo tayari kuwafichua vigogo wanaojihusisha na biashara haramu ya dawa za kulevya, ameanza kupata ushirikiano kutoka kwa wabunge wachache wanaochukizwa na biashara hiyo.
Nipashe ilipoongea na Kamishna Manumba jana kuhusu vitisho anavyopokea Mbunge huyo, alisema yeye hajapata taarifa zozote mbali na kusema kuwa suala hilo linahitaji kushughulikiwa kitaalamu.
Hata hivyo, alisema kwa sasa anaweza kuwasiliana na kituo cha polisi Dodoma au kikosi cha kuzuia madawa ya kulevya. "Pamoja na ujasiri wa Mbunge huyo, pia tunahitaji watu wengine wajitokeze kutoa majina ya wafanyabiashara hao ili tuweze kutokomeza biashara hiyo inayoleta madhara nchini," alisema Bw. Manumba.
Kamishna Manumba alisema kuwa ili kuweza kukabiliana na biashara hiyo nchini, unahitajika ushirikiano kutoka serikalini na watu binafsi kwani suala hilo litashughulikiwa kwa siri kwa ajili ya kuwalinda watoa taarifa. "Serikali ishirikiane kupiga vita suala hilo kisiasa na sisi tutalishughulikia kitaaluma," alisema Kamishna Manumba.
Alisema hilo ni tatizo la kimataifa hivyo inakuwa ni vugumu kuwabaini vigogo halisi wanaohusika na kilimo na kutengeneza madawa hayo kwani hapa nchini wanaohusika na madawa ya kulevya ni mawakala. Alisema kuwa wazalishaji wakubwa wapo nchi za nje kama Mashariki ya Kati, Mashariki ya Mbali, Latin America na Afghanstan.
Aliongeza kuwa kama serikali za nchi za Afrika na Bara la Ulaya zitakuwa imara, vyombo vya serikali vitaweza kufanyakazi zake vizuri katika kuweka mikakati ya kupambana hatimaye kupunguza tatizo hilo la madawa ya kulevya.
Hata hivyo, Kamishna Manumba alisema kuwa hadi sasa hawajapata ushahidi unaoonyesha kwamba vigogo wanaotoka serikalini au taasisi wanashiriki katika uuzaji wa dawa za kulevya ila wamebaini kuwa kuna wafanyabiashara wakubwa ndio wanaoongoza kuingiza madawa ya kulevya nchini kama mawakala.
SOURCE: Nipashe