Amina Chifupa kupokea vitisho na hatimae kufariki. COINCIDENCE?

Azipa

JF-Expert Member
Mar 19, 2012
1,069
322
Chifupa atishiwa kuuawa
2006-11-16 09:03:34
Na Rosemary Mirondo na Beatrice Philemon

Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Bi. Amina Chifupa, ametishiwa kuuawa na watu wasiojulikana kupitia simu yake ya mkononi.
Madai ya mbunge huyu aliyatoa jana alipozungumza na waandishi wa habari hizi kwa njia ya simu kutoka Dodoma alikokuwa akihudhuria kikao cha Bunge kilichomalizika jana. Alisema amepokea vitisho kupitia vijikaratasi alivyoandikiwa akiwa ndani ya ukumbi wa Bunge, vikimuonya aachane na suala la wauza unga.

''Sambamba na ujumbe huo, kupitia simu yangu ya mkononi nilitumiwa ujumbe mfupi wa maneno wa kunitishia kuniua.'' Mbali na hayo, ndani ya ukumbi wa Bunge kwenyewe nimepokea ujumbe wa vikaratasi visivyo na majina vikisema kwamba ninajifanya najua kuongea'', aliongeza kusema mbunge huyo ambaye alisisitiza bado hatetereki kwa vitisho hivyo.

Ujumbe mwingine unasema "we Amina wewe acha wewe, usijifanye unajua sana, ukiwa kwenye jumba la vioo usirushe mawe wakati na wewe umo ndani, tunaanza kukuchunguza kuanzia leo unapata wapi pesa, ni SISI USALAMA WA TAIFA Hivi wewe Amina unajiona wewe ni msafi sana? Au kwa kuwa sisi tumekaa kimya. Wewe ni mchafu sana , na sisi tukiamua kuanza kukuchafua hapatakalika hapa. Dawa yako iko jikoni inachemka, ndio utajua sisi ni nani umeyataka mwenyewe usimlaumu mtu. Wameshindwa wakongwe wewe mtoto wa juzi.

Aidha Bi.Amina alipigiwa simu inayoonyesha kutoka nje ambayo ilisomeka call kwenye simu yake yenye matusi ya nguoni yakimuonya aache kuropoka. Vitisho dhidi ya mbunge huyu jasiri na chipukizi, vimekuja siku moja tu baada ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya jinai nchini, Bw.Robert Manumba kuahidi kuwa Jeshi la Polisi litamlinda na lipo tayari kupokea taarifa zinazohusu vinara wa uuzaji na usambazaji wa dawa za kulevya nchini.

Aidha, Bi. Amina alisema amepokea simu kutoka kwa mtu aliyejitaja kuwa ni polisi, akimuonya asiongee na mtu yeyote kuhusu suala hilo, mpaka atakapotoka bungeni na kumshauri mara atakapotoka Dodoma aende moja kwa moja kwa Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Bw. Robert Manumba, kuonana naye.

Hata hivyo, Bi. Amina hakutaka kutaja jina la polisi huyo. Bi. Amina alisema pamoja na kupokea vitisho hivyo, hataacha kufichua wafanyabiashara hao kwa sababu wanachangia kuwaangamiza vijana ambao ni taifa la kesho.

Alisema baada ya kutangaza bungeni kuwa yupo tayari kuwafichua vigogo wanaojihusisha na biashara haramu ya dawa za kulevya, ameanza kupata ushirikiano kutoka kwa wabunge wachache wanaochukizwa na biashara hiyo.

Nipashe ilipoongea na Kamishna Manumba jana kuhusu vitisho anavyopokea Mbunge huyo, alisema yeye hajapata taarifa zozote mbali na kusema kuwa suala hilo linahitaji kushughulikiwa kitaalamu.

Hata hivyo, alisema kwa sasa anaweza kuwasiliana na kituo cha polisi Dodoma au kikosi cha kuzuia madawa ya kulevya. "Pamoja na ujasiri wa Mbunge huyo, pia tunahitaji watu wengine wajitokeze kutoa majina ya wafanyabiashara hao ili tuweze kutokomeza biashara hiyo inayoleta madhara nchini," alisema Bw. Manumba.

Kamishna Manumba alisema kuwa ili kuweza kukabiliana na biashara hiyo nchini, unahitajika ushirikiano kutoka serikalini na watu binafsi kwani suala hilo litashughulikiwa kwa siri kwa ajili ya kuwalinda watoa taarifa. "Serikali ishirikiane kupiga vita suala hilo kisiasa na sisi tutalishughulikia kitaaluma," alisema Kamishna Manumba.

Alisema hilo ni tatizo la kimataifa hivyo inakuwa ni vugumu kuwabaini vigogo halisi wanaohusika na kilimo na kutengeneza madawa hayo kwani hapa nchini wanaohusika na madawa ya kulevya ni mawakala. Alisema kuwa wazalishaji wakubwa wapo nchi za nje kama Mashariki ya Kati, Mashariki ya Mbali, Latin America na Afghanstan.

Aliongeza kuwa kama serikali za nchi za Afrika na Bara la Ulaya zitakuwa imara, vyombo vya serikali vitaweza kufanyakazi zake vizuri katika kuweka mikakati ya kupambana hatimaye kupunguza tatizo hilo la madawa ya kulevya.

Hata hivyo, Kamishna Manumba alisema kuwa hadi sasa hawajapata ushahidi unaoonyesha kwamba vigogo wanaotoka serikalini au taasisi wanashiriki katika uuzaji wa dawa za kulevya ila wamebaini kuwa kuna wafanyabiashara wakubwa ndio wanaoongoza kuingiza madawa ya kulevya nchini kama mawakala.


SOURCE:
Nipashe
 
Hatuwezi kujua tunakokwenda kama hatujui tunakotoka
 
stick to the point! Mtu anatishiwa na usalama wa taifa halafu anakufa kifo cha ajabu.Crazy govt invòlved!

Hivi kila siku Serikali za dunia zinatangaza kuwa UKIMWI unaua, unatisha. Bado huoni wala husikii na wala hujui kuwa Amina na Mumewe Mpondamali walikufa kwa UKIMWI?

Nini mnachotaka kukificha au kujidai hamjui?
 
Hivi kila siku Serikali za dunia zinatangaza kuwa UKIMWI unaua, unatisha. Bado huoni wala husikii na wala hujui kuwa Amina na Mumewe Mpondamali walikufa kwa UKIMWI?

Nini mnachotaka kukificha au kujidai hamjui?

Hivi mume wake bado yupo?
 
Hivi kila siku Serikali za dunia zinatangaza kuwa UKIMWI unaua, unatisha. Bado huoni wala husikii na wala hujui kuwa Amina na Mumewe Mpondamali walikufa kwa UKIMWI?

Nini mnachotaka kukificha au kujidai hamjui?

come to your senses
 
Alinyonyoka nywele na kubabuka ngozi wafukue mwili wapime mifupa nina mashaka...............................................
 
Hatuwezi kujua tunakokwenda kama hatujui tunakotoka

quote frm dci Manumba "jeshi la polisi litamlinda" how comes alikufa ktk mazingira km yale?mikono ya serikali hii inanuka damu za watu.
 
Muanzisha hii thread umeleta thread ili ufananishe na kutishiwa kuuwawa kwa Slaa, na Mnyika...Amin alifariki kwa maradhi ya kibinadamu wala hakuwawa.
 
mizimu ya mauaji yanaizonga sana ccm. Sokoine....Kolimba....Amina....nk
 
Hivi kila siku Serikali za dunia zinatangaza kuwa UKIMWI unaua, unatisha. Bado huoni wala husikii na wala hujui kuwa Amina na Mumewe Mpondamali walikufa kwa UKIMWI?

Nini mnachotaka kukificha au kujidai hamjui?
Mtu anaweza kuumwa malaria akadungwa sindano yenye virusi vya ukimwi makusudi ili aonekane amekufa kio cha kawaida.
 
Hivi kila siku Serikali za dunia zinatangaza kuwa UKIMWI unaua, unatisha. Bado huoni wala husikii na wala hujui kuwa Amina na Mumewe Mpondamali walikufa kwa UKIMWI?

Nini mnachotaka kukificha au kujidai hamjui?

Aids? Sure? Thibitisha with documents.Are u a doctor?
 
Muanzisha hii thread umeleta thread ili ufananishe na kutishiwa kuuwawa kwa Slaa, na Mnyika...Amin alifariki kwa maradhi ya kibinadamu wala hakuwawa.

Mkuu Ritz, binafsi sijui kama aliuawa ama la, ila naelewa kuna maradhi ya 'kibinadamu' yanayosababishwa na binadamu kwa kusudi la kuua bila kuchochea udadisi.
Say Renal failure sababu ya sumu labda (kumbuka, inaweza kuwa na sababu zingine za kibinadamu) au hata wale wanaosema UKIMWI, coz basically ukimwi ni upungufu wa kinga mwilini, ambapo kuna several causes to this as well za 'kibinadamu', lakini pia sumu inayoweza kuathiri sehemu seli za mwili zinapotengenezwa (bone marrow) ikiwa moja wapo. Hapa mtu hupata upungufu wa kinga na dalili zote ambazo zinahusika nao.

Kwa hiyo basi unaweza kuuwawa kitaalamu kwa kupewa kitu kinachoweza kusababisha maradhi ambayo bila uchunguzi wa kutosha, hasa katika mazingira kama yetu (yasiyo na vipimo mahsusi na yaliyojawa na magonjwa yanayodhaniwa kuwa ya 'kawaida kwa watu fulani') huonekana ni 'matatizo ya kibinadamu' na hivyo kufifisha udadisi zaidi.

 
Mkuu Ritz, binafsi sijui kama aliuawa ama la, ila naelewa kuna maradhi ya 'kibinadamu' yanayosababishwa na binadamu kwa kusudi la kuua bila kuchochea udadisi.
Say Renal failure sababu ya sumu labda (kumbuka, inaweza kuwa na sababu zingine za kibinadamu) au hata wale wanaosema UKIMWI, coz basically ukimwi ni upungufu wa kinga mwilini, ambapo kuna several causes to this as well za 'kibinadamu', lakini pia sumu inayoweza kuathiri sehemu seli za mwili zinapotengenezwa (bone marrow) ikiwa moja wapo. Hapa mtu hupata upungufu wa kinga na dalili zote ambazo zinahusika nao.

Kwa hiyo basi unaweza kuuwawa kitaalamu kwa kupewa kitu kinachoweza kusababisha maradhi ambayo bila uchunguzi wa kutosha, hasa katika mazingira kama yetu (yasiyo na vipimo mahsusi na yaliyojawa na magonjwa yanayodhaniwa kuwa ya 'kawaida kwa watu fulani') huonekana ni 'matatizo ya kibinadamu' na hivyo kufifisha udadisi zaidi.


Kwi kwi kwi.

Dokta, Lema na Mnyika mmesha wapima?
 
Back
Top Bottom