AMIMI USIAMINI - Hii ndiyo fomu ya kuombea viza ya kuja Tanzania!

Mkuu mbona ingekuwa heri kama ungelikuwa unajaza yote, Siku moja nilifika hapo kumuombea rafiki yangu visa..tatizo likaja hakujua nini cha kujaza basi nikaenda mapokezi kuuliza nijaze nini hapa? kuna mama mmoja nimemsahau jina akaniambia hapo hakuna umuhimu wa kujaza.....sehemu yenyewe inahusiana na details za msafiri au muombaji wa visa, aisee nilicheka sana.

Nchi za wenzetu, unapewa VISA baada ya kujaza maelezo mengi sana mpaka yanachosha. Na wanataka kujua mpaka unakotarajia kufikia na zababu zinazo kupeleka kwao. Kwa form hiyo ya bongo ni cha mtoto na bado mtu anakwambia haina umuhimu na kama haina umuhimu ipo pale kwa ajili ya nini? Hata wafanyakazi wengine wapo tu kwa sababu waliambiwa wakaye hapo wangoje mshiko mwisho wa mwezi basi!! Wageni waje tu kuvuna shamba la bibi.

Hao waliandaa hiyo form nadhani ni wavivu wa kufikiri. Haiwezekani hiyo form iwe iliandaliwa na mtu mwenye uzalendo na nchi yake.
 
Nchi za wenzetu, unapewa VISA baada ya kujaza maelezo mengi sana mpaka yanachosha. Na wanataka kujua mpaka unakotarajia kufikia na zababu zinazo kupeleka kwao. Kwa form hiyo ya bongo ni cha mtoto na bado mtu anakwambia haina umuhimu na kama haina umuhimu ipo pale kwa ajili ya nini? Hata wafanyakazi wengine wapo tu kwa sababu waliambiwa wakaye hapo wangoje mshiko mwisho wa mwezi basi!! Wageni waje tu kuvuna shamba la bibi.

Hao waliandaa hiyo form nadhani ni wavivu wa kufikiri. Haiwezekani hiyo form iwe iliandaliwa na mtu mwenye uzalendo na nchi yake.

Kwanini unakuwa na fikra wageni waje kuvuna, mbona wewe huvuni?
 
Tafuta fomu za viza za nchi zingine utapata jibu lako.

Kwa nini unamtaka mtu mwingine akufanyie kazi ambayo wewe uliyeleta madai kwamba fomu hii haitupi habari za kutosha unatakiwa kutufahamisha?

Duniani kuna nchi nyingi sana, hizo "nchi nyingine" unazozizungumzia ni nchi gani? Nchi tofauti zina vigezo tofauti katika kupanga matakwa shurti ya fomu, utasemaje tu "tafuta fomu za viza za nchi nyingine"? Na kwa nini Mtanzania atake kupanga matakwa ya fomu ya viza ya Tanzania kwa kuangalia nchi nyingine? Utataka kutuambia na zile nchi zisizotaka kabisa mtu kuwa na viza nazo tuzigeze? Na zile zenye kutoza mamia na maelfu ya dola kama viza processing fee nazo?

Mbona hamjajibu swala la kusema kwamba nchi masikini inayotaka kukuza utalii haiwezi ku-afford kuwa na unnecessary and bureaucratic paperwork?

Hao vinara wa dunia wana ma "paperwork reduction acts", Marekani wamekuwa so bureaucratic kwa paperwork mpaka wametunga sheria ya kupunguza paperwork. Na hata hapo nasoma "The Economist" la wiki hii, gazeti linawabalasa Wamarekani kwamba moja ya mambo yanayosababisha uchumi kuwa stagnant ni bureaucracy na a Vogon-like overkill in paperwork kiasi kwamba, the Economists correspondent says in jest kwamba hiyo 800+ page Dodd-Frank Act hakuna mtu aliyeisoma yote outside of Beijing na huyo muandishi.

Hivi itasaidia nini kama utakuwa na ki booklet cha fomu za viza wakati watu wanauza pasipoti za bongo kama njugu? Si unaongeza gharama za uendeshaji balozi tu?

United States' economy: Over-regulated America | The Economist

20120220195350439893270.jpg
 
Siku hizi passport karibu zote dunia zinasomwa kwa computer (machine readerble) ukifika mpakani wanaswap tu information zako zote kwenye data base kutoka kwenye barcode ya passport yako. Wanakuchukua finger print basi unapata visa yako. Hata huko ubalozini kuna machine za kusoma finger print. Tatizo mleta maada kaamsha morali za watu kwa kuleta maada kama vile hayo makatasi yana umuhimu sana kwa karne hii. Hilo fomu halina Umuhimu wowote kwa karne ya Computer, enzi za Mwalimu ndio kulikuwa na mambo hayo ya mahard copy, siku hizi ni soft copy tu. Jamani tokeni kidogo Tanzania ili muone procedure za kutoka na kuingia zikoje, sio mnakuja na kitu ambacho hujui hata practically kinafanyika vipi mnaleta kelele.
 
Sasa si tunahitaji watalii fomu ndefu ya nini?.Hizo ndizo sifa za fomu ya visa ya viinchi maskini kama Tanzania. Hebu nenda linganisha Kenya, Uganda, zao zikoje ndio uje hapa. Kamwe fomu ya kuomba visa kwa Mtanzania kwenda Marekani au China haiwezi kuwa sawa na wao wanavyoomba kuja kwetu. Mimi lishaenda Rwanda hizo visa tunagongewa tu mpakani
 
Fomu za utalii wa muda mfupi katika nchi nyingi hata zilizoendea zaidi ya kwetu nazo ni fupi tu

Singapore, Malaysia, Cambodia, Vietnam, South Korea, China, Japan, Ugiriki, Ureno, Indonesia, Urussi, Dubai, ....kote fomu ni page moja tu ama unagongea airport

Hamna cha ajabu hata kimoja kwenye hiyo form ya Tanzania
 
Mara nyingi huwa tunazungumzia namna ambavyo nchi ya Tanzania inaendeshwa katika utaratibu wenye kutia aibu na fedheha kwa taifa na wananchi wake na inastaajabisha pale unapotafiti aina ya watu wenye madaraka ukilinganisha na uwezo wao.

Atachment iliyopo kwenye mada hii ndiyo fomu raia wa kigeni anayojaza pale anapoomba viza ya kuja nchini kwetu. Ni ukurasa mmoja tu ambao sehemu anayojaza ni theluthi moja tu ya kurasa hiyo.

Kwa wale ambao mmewahi kuomba viza kwenda nchi zingine naamini mtaweza kulinganisha information unazotakiwa kutoa kuhusu wewe ni nani na unafanya nini, una mahusiano gani, viambatanisho muhimu, n.k.

Ukiangalia fomu hii unaweza sasa kuelewa ni kwa nini hapa nchini kuna raia wengi wa kigeni ambao hawakupaswa kuingia nchini, watu ambao wasingethubutu kuomba viza nchi zingine, lakini kwa vile serikali imeifanya nchi kuwa shamba la bibi kwa kupitia upumbavu wa namna hii, matokeo yake ni nchi kudharaulika.

Hii ndiyo fomu iliyobuniwa na wataalam wetu waliopo uhamiaji>
Jioneeni wenyewe!

sasa mkuu unatakiwa ueleze details nyingine ambazo unahisi zinamiss kwenye hii fomu ziongezwe ila kwa upande wangu naona ipo clear na details zote muhimu zipo sawa na nchi zingine labda US na UK ndio zina a lot of complications!1
 
Kwa nini unamtaka mtu mwingine akufanyie kazi ambayo wewe uliyeleta madai kwamba fomu hii haitupi habari za kutosha unatakiwa kutufahamisha?

Duniani kuna nchi nyingi sana, hizo "nchi nyingine" unazozizungumzia ni nchi gani? Nchi tofauti zina vigezo tofauti katika kupanga matakwa shurti ya fomu, utasemaje tu "tafuta fomu za viza za nchi nyingine"? Na kwa nini Mtanzania atake kupanga matakwa ya fomu ya viza ya Tanzania kwa kuangalia nchi nyingine? Utataka kutuambia na zile nchi zisizotaka kabisa mtu kuwa na viza nazo tuzigeze? Na zile zenye kutoza mamia na maelfu ya dola kama viza processing fee nazo?

Mbona hamjajibu swala la kusema kwamba nchi masikini inayotaka kukuza utalii haiwezi ku-afford kuwa na unnecessary and bureaucratic paperwork?

Hao vinara wa dunia wana ma "paperwork reduction acts", Marekani wamekuwa so bureaucratic kwa paperwork mpaka wametunga sheria ya kupunguza paperwork. Na hata hapo nasoma "The Economist" la wiki hii, gazeti linawabalasa Wamarekani kwamba moja ya mambo yanayosababisha uchumi kuwa stagnant ni bureaucracy na a Vogon-like overkill in paperwork kiasi kwamba, the Economists correspondent says in jest kwamba hiyo 800+ page Dodd-Frank Act hakuna mtu aliyeisoma yote outside of Beijing na huyo muandishi.

Hivi itasaidia nini kama utakuwa na ki booklet cha fomu za viza wakati watu wanauza pasipoti za bongo kama njugu? Si unaongeza gharama za uendeshaji balozi tu?

United States' economy: Over-regulated America | The Economist

20120220195350439893270.jpg

Angalia jibu nililolitoa hapo juu muda wa 01.05 kwa Kibunango, nadhani unaweza kuona nini ninachozungumza. Suala si mlolongo wa paperwork ila ni jinsi fomu yenye isivyo ya kisasa kwa maana kwamba kwa mfano unalazimika kui-print na kuituma au kuipeleka kwa mkono ubalozini.
 
Angalia jibu nililolitoa hapo juu muda wa 01.05 kwa Kibunango, nadhani unaweza kuona nini ninachozungumza. Suala si mlolongo wa paperwork ila ni jinsi fomu yenye isivyo ya kisasa kwa maana kwamba kwa mfano unalazimika kui-print na kuituma au kuipeleka kwa mkono ubalozini.

Samahani Mkuu labda ungetueleza unatumia reference nchi gani?

Manake hayo ya kwenda ubalozini kurudisha form mbona ni kawaida mno!
 
Fomu za utalii wa muda mfupi katika nchi nyingi hata zilizoendea zaidi ya kwetu nazo ni fupi tu

Singapore, Malaysia, Cambodia, Vietnam, South Korea, China, Japan, Ugiriki, Ureno, Indonesia, Urussi, Dubai, ....kote fomu ni page moja tu ama unagongea airport

Hamna cha ajabu hata kimoja kwenye hiyo form ya Tanzania

Nadhani ukizingatia kichwa cha habari cha uzi huu pengine utaona tatizo ninalozungumzia. Hii fomu si ya viza ya utalii tu, ni viza yoyote mtu anayokusudia kuomba ili aje Tanzania; ukiwa unakuja kibiashara, kitalii, likizo, n.k. unajaza fomu hiyo hiyo. Moja ya matatizo yaliyo wazi ni namna ambavyo hizo sehemu za kujaza zilivyo ndogo; zaidi tena hiyo fomu inaonekana aliyeitengeneza aliwaza kuwa viza huombwa na mtu mmoja mmoja tu. Chukua mfano familia moja kubwa yenye watoto wadogo inapohitaji viza kuja Tanzania, ni kwamba kila mtu atatakiwa kujaza fomu yake na kuifikisha ubalozini wakati angejaza mzazi mmoja tu fomu moja na kuorodhesha majina ya wote anaoambatana nao.
 
Nadhani ukizingatia kichwa cha habari cha uzi huu pengine utaona tatizo ninalozungumzia. Hii fomu si ya viza ya utalii tu, ni viza yoyote mtu anayokusudia kuomba ili aje Tanzania; ukiwa unakuja kibiashara, kitalii, likizo, n.k. unajaza fomu hiyo hiyo. Moja ya matatizo yaliyo wazi ni namna ambavyo hizo sehemu za kujaza zilivyo ndogo; zaidi tena hiyo fomu inaonekana aliyeitengeneza aliwaza kuwa viza huombwa na mtu mmoja mmoja tu. Chukua mfano familia moja kubwa yenye watoto wadogo inapohitaji viza kuja Tanzania, ni kwamba kila mtu atatakiwa kujaza fomu yake na kuifikisha ubalozini wakati angejaza mzazi mmoja tu fomu moja na kuorodhesha majina ya wote anaoambatana nao.

Mkuu ushasema fomu inajazwa theluthi moja tu sasa tatizo ni lipi kama na kila mtoto kwenye familia atatakiwa kujaza yake?

Kuna mtu amesema kuwa visa ya kuombea ukazi au biashara unatakiwa ujaze na form nyengine. Lakini wewe unapingana nae wazi

Wewe una uhakika kuwa karatasi ni hii hii TU hata kwa mtu anaeomba ukazi na biashara?
 
Mkuu ushasema fomu inajazwa theluthi moja tu sasa tatizo ni lipi kama na kila mtoto kwenye familia atatakiwa kujaza yake?

Kuna mtu amesema kuwa visa ya kuombea ukazi au biashara unatakiwa ujaze na form nyengine. Lakini wewe unapingana nae wazi

Wewe una uhakika kuwa karatasi ni hii hii TU hata kwa mtu anaeomba ukazi na biashara?

Sijui kama umeiangalia hiyo fomu; niliposema theluthi moja nilimaanisha ukubwa wa section ambayo muombaji anajaza, theluthi nyingine ni matumizi ya ofisi na nyingine ndiyo ina nembo ya nchi, anuani ya ubalozi na vinginevyo.
Ipitie tena utaona kuwa wameweka aina za viza: Transit, holiday, tourist na business. Tovuti ya ubalozi wetu Uingereza inasema bayana kabisa kuwa fomu hiyo inatumika kwa viza zote. Sasa kwa mfano mtu anayekuja Tanzania kuungana na familia yake ambayo ilikuja kuishi huku anajazaje fomu hiyo?
 
Fomu za utalii wa muda mfupi katika nchi nyingi hata zilizoendea zaidi ya kwetu nazo ni fupi tu

Singapore, Malaysia, Cambodia, Vietnam, South Korea, China, Japan, Ugiriki, Ureno, Indonesia, Urussi, Dubai, ....kote fomu ni page moja tu ama unagongea airport

Hamna cha ajabu hata kimoja kwenye hiyo form ya Tanzania

Kwanza kabisa hii fomu si ya viza ya utalii tu bali ni viza zote. Halafu kuna kitu kinaitwa "visa regime", yaani mfumo wa viza kati ya nchi moja na nyingine. Kutokana na mfumo huu utakuta kuna nchi ukienda huna haja ya kuomba viza ubalozini bali unagongewa tu pale unapoingia, wakati zingine inakubidi uombe ubalozini.
Kwa mfano unapoenda Rwanda unabeba tu passport yako lakini huwezi kufanya hivyo unapotaka viza yoyote kwenda Canada.
 
ninavyojua mimi ni kwamba ukiwa raia wa kigeni unalipia dola 100 pale airport bila maswali au longolongo, au hii kuomba visa imeanza jana?

Mara nyingi kulipia airport ni zile nchi ambazo hatuna ubalozi kwenye hizo nchi
 
Mbona iko sawa tu na ya nchi zingine si unajua form nyingi ni za kudesa tu, ungeongelea utaratibu wa kupata visa ningekuelewa
 

Attachments

  • kenya_visa_application_form.pdf
    27.4 KB · Views: 65
Sijui kama umeiangalia hiyo fomu; niliposema theluthi moja nilimaanisha ukubwa wa section ambayo muombaji anajaza, theluthi nyingine ni matumizi ya ofisi na nyingine ndiyo ina nembo ya nchi, anuani ya ubalozi na vinginevyo.
Ipitie tena utaona kuwa wameweka aina za viza: Transit, holiday, tourist na business. Tovuti ya ubalozi wetu Uingereza inasema bayana kabisa kuwa fomu hiyo inatumika kwa viza zote. Sasa kwa mfano mtu anayekuja Tanzania kuungana na familia yake ambayo ilikuja kuishi huku anajazaje fomu hiyo?

Hiyo fomu sio kuiangalia tu, nishawahi kuwasaidia watu kujaza mara kadhaa

Nijuavyo ni hivi, kwa viza ya utalii ndio inabaki fomu hiyo hiyo tu lakini kwa viza nyengine kama kazi unaambiwa ukabidhi na stakabadhi nyengine

Vigezo vyote vya msingi (hadi suala la fedha) limeshaanishwa, tunataka nini tena jengine?
 
Mbona iko sawa tu na ya nchi zingine si unajua form nyingi ni za kudesa tu, ungeongelea utaratibu wa kupata visa ningekuelewa
angalia ya ethiopia na ya china
 

Attachments

  • visa_form ethiopia.pdf
    66.6 KB · Views: 37
  • visa application form china.pdf
    514.3 KB · Views: 76
Mara nyingi huwa tunazungumzia namna ambavyo nchi ya Tanzania inaendeshwa katika utaratibu wenye kutia aibu na fedheha kwa taifa na wananchi wake na inastaajabisha pale unapotafiti aina ya watu wenye madaraka ukilinganisha na uwezo wao.

Atachment iliyopo kwenye mada hii ndiyo fomu raia wa kigeni anayojaza pale anapoomba viza ya kuja nchini kwetu. Ni ukurasa mmoja tu ambao sehemu anayojaza ni theluthi moja tu ya kurasa hiyo.

Kwa wale ambao mmewahi kuomba viza kwenda nchi zingine naamini mtaweza kulinganisha information unazotakiwa kutoa kuhusu wewe ni nani na unafanya nini, una mahusiano gani, viambatanisho muhimu, n.k.

Ukiangalia fomu hii unaweza sasa kuelewa ni kwa nini hapa nchini kuna raia wengi wa kigeni ambao hawakupaswa kuingia nchini, watu ambao wasingethubutu kuomba viza nchi zingine, lakini kwa vile serikali imeifanya nchi kuwa shamba la bibi kwa kupitia upumbavu wa namna hii, matokeo yake ni nchi kudharaulika.

Hii ndiyo fomu iliyobuniwa na wataalam wetu waliopo uhamiaji>
Jioneeni wenyewe!

Form za kurasa tatu na kuendelea zimepitwa na wakati! Si lazima kila kitu cha nchi za nje ni kizuri kuigwa! Mi nimeipenda hii form..ni simple na ime-cover the basics. AFteralll, ukubwa wa form haumzuii mtu mwenye nia mbaya kughusi taarifa!

Kama form zao ziko so efficient..mbona ndo zinaongoza kwa wahamiaji haramu!
 


Sioni tatizo. Niliijaza application form ya kuingia India, ni kama hiyo tu, kurasa moja. Tofauti ni ndogo. Angalia ya India hapa chini:


attachment.php
 
Back
Top Bottom