AMIMI USIAMINI - Hii ndiyo fomu ya kuombea viza ya kuja Tanzania!

Massenberg

JF-Expert Member
Jun 4, 2011
1,173
1,370
Mara nyingi huwa tunazungumzia namna ambavyo nchi ya Tanzania inaendeshwa katika utaratibu wenye kutia aibu na fedheha kwa taifa na wananchi wake na inastaajabisha pale unapotafiti aina ya watu wenye madaraka ukilinganisha na uwezo wao.

Atachment iliyopo kwenye mada hii ndiyo fomu raia wa kigeni anayojaza pale anapoomba viza ya kuja nchini kwetu. Ni ukurasa mmoja tu ambao sehemu anayojaza ni theluthi moja tu ya kurasa hiyo.

Kwa wale ambao mmewahi kuomba viza kwenda nchi zingine naamini mtaweza kulinganisha information unazotakiwa kutoa kuhusu wewe ni nani na unafanya nini, una mahusiano gani, viambatanisho muhimu, n.k.

Ukiangalia fomu hii unaweza sasa kuelewa ni kwa nini hapa nchini kuna raia wengi wa kigeni ambao hawakupaswa kuingia nchini, watu ambao wasingethubutu kuomba viza nchi zingine, lakini kwa vile serikali imeifanya nchi kuwa shamba la bibi kwa kupitia upumbavu wa namna hii, matokeo yake ni nchi kudharaulika.

Hii ndiyo fomu iliyobuniwa na wataalam wetu waliopo uhamiaji>
Jioneeni wenyewe!
 

Attachments

  • tanzania_visa.pdf
    576.2 KB · Views: 2,660
Kuna jamaa m1 nshamsahau alishawahi kusema wataalamu na wasomi ndio wanaoifirisi hii nchi.
 
Maaaavi kweli ......kwa style hii wachina watauza vibanio na penseli kule kariakoo kishenzi.....hakyamungu serikali yetu imejaa mazezeta!!...
 
ninavyojua mimi ni kwamba ukiwa raia wa kigeni unalipia dola 100 pale airport bila maswali au longolongo, au hii kuomba visa imeanza jana?
 
Mara nyingi huwa tunazungumzia namna ambavyo nchi ya Tanzania inaendeshwa katika utaratibu wenye kutia aibu na fedheha kwa taifa na wananchi wake na inastaajabisha pale unapotafiti aina ya watu wenye madaraka ukilinganisha na uwezo wao.
Atachment iliyopo kwenye mada hii ndiyo fomu raia wa kigeni anayojaza pale anapoomba viza ya kuja nchini kwetu. Ni ukurasa mmoja tu ambao sehemu anayojaza ni theluthi moja tu ya kurasa hiyo. Kwa wale ambao mmewahi kuomba viza kwenda nchi zingine naamini mtaweza kulinganisha information unazotakiwa kutoa kuhusu wewe ni nani na unafanya nini, una mahusiano gani, viambatanisho muhimu, n.k.
Ukiangalia fomu hii unaweza sasa kuelewa ni kwa nini hapa nchini kuna raia wengi wa kigeni ambao hawakupaswa kuingia nchini, watu ambao wasingethubutu kuomba viza nchi zingine, lakini kwa vile serikali imeifanya nchi kuwa shamba la bibi kwa kupitia upumbavu wa namna hii, matokeo yake ni nchi kudharaulika.
Hii ndiyo fomu iliyobuniwa na wataalam wetu waliopo uhamiaji>
Jioneeni wenyewe!

Mkuu mbona ingekuwa heri kama ungelikuwa unajaza yote, Siku moja nilifika hapo kumuombea rafiki yangu visa..tatizo likaja hakujua nini cha kujaza basi nikaenda mapokezi kuuliza nijaze nini hapa? kuna mama mmoja nimemsahau jina akaniambia hapo hakuna umuhimu wa kujaza.....sehemu yenyewe inahusiana na details za msafiri au muombaji wa visa, aisee nilicheka sana.
 
Hii ni scandal! Kwanini waziri wa mambo ya ndani asitangaze kabisa kuwa hakuna haja ya visa wageni waingie tuu. Aibu!
 
china ni nchi ya pili kwa ukumbwa wa kiuchumi duniani,so hata wakiuza vibanio na pencil k,koo ni poa tuu,bcoz hatuna uwezo wa kuvitengeneza,tumekalia wimbo wa "ufisadi ufisadi"this is a magic county bwana,kila ki2 zero ingawa tuna utajiri mkubwa wa madini!
 
Hakuna haja ya ukiritimba. Wangekuwa na form ya kijitabu cha kurasa kumi kuomba visa mngewasema wanakimbiza watalii, wanafuja fedha na maliasili.

Wamekuja na form simple ya kurasa moja mnawasema. Wewe ulitaka information gani zaidi hapo?

Kama unajali sana watu wanavyoingia Tanzania kitu cha kuangalia ni jinsi hati za kusafiria za Tanzania (passports) zinavyogawiwa ovyo kama njugu. Hizi habari za visa nchi ambayo hata haina border control ni kichekesho tu.
 
Da hii ni kali mkuu....nadhani kwa hali hii nchi inaweza kuwa imeuzwa muda mrefu.
 
Mkuu mbona ingekuwa heri kama ungelikuwa unajaza yote, Siku moja nilifika hapo kumuombea rafiki yangu visa..tatizo likaja hakujua nini cha kujaza basi nikaenda mapokezi kuuliza nijaze nini hapa? kuna mama mmoja nimemsahau jina akaniambia hapo hakuna umuhimu wa kujaza.....sehemu yenyewe inahusiana na details za msafiri au muombaji wa visa, aisee nilicheka sana.

Angalia kwenye hiyo fomu hata sehemu ambazo unatakiwa kujaza maelezo marefu kidogo, mfano hapo kwenye Date and place of birth au hapo kwenye Residence address; hivi nafasi ndogo kama hiyo mtu unajaza kitu gani ambacho kitasomeka kwa urahisi?
 
Hakuna haja ya ukiritimba. Wangekuwa na form ya kijitabu cha kurasa kumi kuomba visa mngewasema wanakimbiza watalii, wanafuja fedha na maliasili.

Wamekuja na form simple ya kurasa moja mnawasema. Wewe ulitaka information gani zaidi hapo?

Kama unajali sana watu wanavyoingia Tanzania kitu cha kuangalia ni jinsi hati za kusafiria za Tanzania (passports) zinavyogawiwa ovyo kama njugu. Hizi habari za visa nchi ambayo hata haina border control ni kichekesho tu.

Kujijibu mwenyewe swali lako kwamba mimi ninataka information gani zaidi hapo, nenda mtandaoni katafute fomu za viza za nchi zingine halafu utaelewa tunachokijadili.
 
Inatia uchungu kwa kweli.. Ndiyo maana takataka za kila aina zinaingia nchi.. Yani masharti ya kwenda kukopa mkopo benki ni magumu kuliko kuomba visa.
 
Back
Top Bottom