Ameuteka Moyo Wangu!!!!

BelindaJacob

Platinum Member
Nov 24, 2008
6,474
4,022
Huyu kaka nafanya nae kazi ametokea kweli kuuteka moyo wangu, sidhani kama anaelewa hilo ila ninaongea nae kama marafiki wa kawaida. Yani sijawahi kujisikia kama hivi kwa mwanaume mwingine.
So far nimevutiwa nae kwa jinsi alivyo pia hobbies zetu zinaendana. Ni kaka mcheshi, mkarimu, anavaa vizuri&smart(sidhani kama ni mzaire yani anang'aa nje ya nyumba tu).
Sijui kama yupo ''attached'' japo hajaoa kutokana na maongezi tunayokuwa nayo.
Je nimwambie ukweli? au atanifikiriaje?Nitaanzaje?Au nimsubiri azisome hisia?how?

NB: Nipo serious mana naamini hisia zangu za nguvu, namuwazia kuwa baba wa watoto wangu tukijaliwa kuwa wote:)))
 
Hizi ni zama za ukweli na uwazi kama ni understanding atakuelewa tu ukimweleza hisia zako lakini uwe makini asije kukuona kicheche.
 
vunja ukimyaaa!...'mtokee'....au tukupe mistari???hahahahah
 
Mweleze tu BJ unaogopa nini akikuona mcharuko poa tu lakini roho yako itatulia unajua ukisema ukweli unatoa dukuduku moyoni linalokutesa
 
Hizi ni zama za ukweli na uwazi kama ni understanding atakuelewa tu ukimweleza hisia zako lakini uwe makini asije kukuona kicheche.

Kweli kabisa, mi mwenyewe naamini mtu ukiwa na hisia juu ya mtu unamwambia ili uwe free ila akinifikiria hivyo je na mimi ni mwanamke?! Inabidi niwe na kifua kweli kweli cha kumwambia.
 
Huyu kaka nafanya nae kazi ametokea kweli kuuteka moyo wangu, sidhani kama anaelewa hilo ila ninaongea nae kama marafiki wa kawaida. Yani sijawahi kujisikia kama hivi kwa mwanaume mwingine.
So far nimevutiwa nae kwa jinsi alivyo pia hobbies zetu zinaendana. Ni kaka mcheshi, mkarimu, anavaa vizuri&smart(sidhani kama ni mzaire yani anang'aa nje ya nyumba tu).
Sijui kama yupo ''attached'' japo hajaoa kutokana na maongezi tunayokuwa nayo.
Je nimwambie ukweli? au atanifikiriaje?Nitaanzaje?Au nimsubiri azisome hisia?how?

NB: Nipo serious mana naamini hisia zangu za nguvu, namuwazia kuwa baba wa watoto wangu tukijaliwa kuwa wote:)))


Duh, hapo kwenye red inayonyesha unalo jibu tayari, uko serious, unaamini hisia zako na tayari umeshaenda mpaka kuwaza habari za watoto....yaani watoto si ni mapenzi ya Mungu. What if hutawapata, je utamchukia huyo ambaye sasa hivi unamfia....mmmmhhhhhh patience, wisdom, prayer....dada haraka haraka zitakupeleka kubaya. Upendo wa kweli hauna speed hiyo yako. Ila nahushangaa unauliza wakti unasema unaamini hisia zako, basi mwambie ila akisema yuko booked tayari angali isije ikawa sasa ni kulia na kupata hysteria, ita-affect kazi yako...ndio maana ni vizuri kuwa na busara na kwenda slow....
 
BJ Acha kuugulia moyoni hebu tema hizo lyrics kusudi mauzo ya singo yaende platinum
 
Tafuta mahali na muda muafaka umueleze ukweli atakuelewa tu, ukishindwa tumia njia nyingine za indirect kama kuwa naye close mara nyingi sio tu ofisini bali hata siku za weekend tafuta jinsi ya kukutana naye, pia tumia vizuri mawasiliano ya simu baada ya muda wa kazi kumuandikia sms kumjulia hali yake na mambo mengine ya kawaida atakusoma tu baadae.
 
We mweleze 2 ila tatizo la sisi vidume hata akiwa na mpenzi mtalajiwa hawezi kukueleza zaidi atataka ukumege mchezo uishe uwe makini kwa hilo angalia kwanza msimaso wake!
 
nakushauri usimwambie!
kama anakuhitaji atakwambia sbb lazima tu kuna vidalili umemuonesha!
kumuanza mwanaume ni big no nooo hamna cha zama za uwazi wala cha nini nioneni mshamba tu lkn huo ni mtazamo wangu!
wengine hata kama alikua anapanga jinsi ya kukuanza ukimtongoza tu unamkata stimu zote.
anyway Belinda huu ni ushauri tu wewe ndio utakayeamua upi wa kufuata na upi wa kupotezea ila nakutakia kila la kheri!
 
Mweleze tu BJ unaogopa nini akikuona mcharuko poa tu lakini roho yako itatulia unajua ukisema ukweli unatoa dukuduku moyoni linalokutesa

Dena Amsi nina wakati mgumu sana..ipi bora kumtext au live? au nifanye viji-actions kama kutoka wote anaweza kuwa connected na yeye?
 
mwaya usimueleze jikaze tu ila kuwa nae karibu ili ujue nae anahisia zozote na ww au,unajua siku hizi wanawake tumekuwa warahisi sana unaweza kumueleza akaona nawe ndiyo walewale so avunjike moyo kabisa please jikaze my dear ushauri wa cheusi mangala pia muhim
 
BJ unaogopa kutekwa?
Naogopa mana huyu mtu amezingira kichwa changu.. Niambie ukweli wewe mwanaume ukiambiwa unapendwa unamchukuliaje mwanamke?


Duh, hapo kwenye red inayonyesha unalo jibu tayari, uko serious, unaamini hisia zako na tayari umeshaenda mpaka kuwaza habari za watoto....yaani watoto si ni mapenzi ya Mungu. What if hutawapata, je utamchukia huyo ambaye sasa hivi unamfia....mmmmhhhhhh patience, wisdom, prayer....dada haraka haraka zitakupeleka kubaya. Upendo wa kweli hauna speed hiyo yako. Ila nahushangaa unauliza wakti unasema unaamini hisia zako, basi mwambie ila akisema yuko booked tayari angali isije ikawa sasa ni kulia na kupata hysteria, ita-affect kazi yako...ndio maana ni vizuri kuwa na busara na kwenda slow....

Asante mkuu, kweli mambo mengine ni majaliwa na always tunafikiria kujaliwa..nitaenda polepole japo naziamini hisia zangu!!..nitakuwa mwngalifu kwa utendji wangu kazini ambao mpaka sasa haujatetereka...busara mbele, shukrani za dhati


BJ Acha kuugulia moyoni hebu tema hizo lyrics kusudi mauzo ya singo yaende platinum
Yani natamani ingekuwa rahisi hivyo..au nifanye ile liwalo na liwe!!..hata akisema huyo na mtu ningependa tuendelee marafiki, sijui itawezekana?!! haya najiandaa na singo


Tafuta mahali na muda muafaka umueleze ukweli atakuelewa tu, ukishindwa tumia njia nyingine za indirect kama kuwa naye close mara nyingi sio tu ofisini bali hata siku za weekend tafuta jinsi ya kukutana naye, pia tumia vizuri mawasiliano ya simu baada ya muda wa kazi kumuandikia sms kumjulia hali yake na mambo mengine ya kawaida atakusoma tu baadae.

Sawa Mfarisayo, labda kuwa nae karibu inaweza kumletea automatic hisia juu yangu pia..Haonyeshi kujisikia ila asijekunifuta kwenye ramani ya ubongo wake na kuwa maadui..

mwambie ukweli usiogope
Haya nitajitahidi sana..huenda ikanisaidia kushusha mzigo hata kama mwelekeo sijajua


We mweleze 2 ila tatizo la sisi vidume hata akiwa na mpenzi mtalajiwa hawezi kukueleza zaidi atataka ukumege mchezo uishe uwe makini kwa hilo angalia kwanza msimaso wake!

Usiniambie, kwahiyo anaweza kuona chakula hichoo na kukubali kumbe ana wake? hapo pia pagumu nikiwaza..nitakuwa makini,thanx


Dinner could a good plan there is a way as you go on lazima atajua tu you are interested in him usiogope
Yani acha tu, naona vitendo viongee zaidi ya live ila bado najipanga..akikubali dinner itakuwa walaaah
 
Mtoe out usiku, usiongee mengi, kuwa msikivu zaidi, msifie, mwambie unapenda uwe na mtu kama yeye... ataelewa somo
Huyu kaka nafanya nae kazi ametokea kweli kuuteka moyo wangu, sidhani kama anaelewa hilo ila ninaongea nae kama marafiki wa kawaida. Yani sijawahi kujisikia kama hivi kwa mwanaume mwingine.
So far nimevutiwa nae kwa jinsi alivyo pia hobbies zetu zinaendana. Ni kaka mcheshi, mkarimu, anavaa vizuri&smart(sidhani kama ni mzaire yani anang'aa nje ya nyumba tu).
Sijui kama yupo ''attached'' japo hajaoa kutokana na maongezi tunayokuwa nayo.
Je nimwambie ukweli? au atanifikiriaje?Nitaanzaje?Au nimsubiri azisome hisia?how?

NB: Nipo serious mana naamini hisia zangu za nguvu, namuwazia kuwa baba wa watoto wangu tukijaliwa kuwa wote:)))
 
Back
Top Bottom