Dr Akili
JF-Expert Member
- Aug 21, 2011
- 4,952
- 4,326
Hii likizo ya siku saba inaonekana anaitumia vizuri kujifunza kuelewa nchi yetu sasa hivi iko hali gani baada ya kuiacha miaka mitatu iliyopita. Ndani ya siku moja tu ameshaanza kuunga juhudi za Magufuli kwamba tuko kwenye right track kuelekea kuwa kama ulaya kwa mfano:
1.Kwa mfano amekubali kuwa barabara za mwendo kasi ndizo hata huko ulaya wanatumia kwenye majiji yao. Tofauti tu ni kuwa huko ulaya ziko nyingi. Ameahidi akichaguliwa atazijenga nyingi jijini DSM. Ambacho hajajua ni kwamba JPM alishaanza kuzijenga nyingi tu jijini DSM.
2. Ameahidi pia akichaguliwa atajenga pia reli za jijini (city railways) na city ferries. Ambacho hajajua ni kuwa tayari JPM tayari alishajenga na anaendelea kujenga hizo city railways and ferries. Ingefaa katika kipindi hiki cha likizo wampeleke akazione pia.
3. Ameahidi pia kuwa atabomoa nyumba kadhaa jijini DSM ili kujenga maeneo ya kupumuzikia (city gardens) na kuegesha magari (parking areas) kama ilivyo huko ulaya. Ambacho hajajua ni kwamba JPM tayari alishaanza kufanya kazi hiyo. Aende akatembelee maeneo hayo ambayo yako tayari.
4. Alipotembelea soko la Kariakoo amejifunza kuwa hizo utitiri wa kodi alizokuwa akizilalamikia kwenye kampeni zake hazikuwa za kweli. Amejifunza kuwa mfanya biashara mkubwa (mwenye mtaji unaozidi millioni 20) kodi anayotakiwa kukusanya ni VAT tu ambayo kiwango chake huwekwa na bunge. Mfanya biashara wa kati ambaye mtaji wake ni kuanzia milioni 4 hadi ishirini kodi yake haizidi milioni 5 kwa mwaka na hukokotolewa kutokana na risiti za mauzo yake na mashine za kielekitroniki anazopewa bure na TRA.
Mfanyabiashara mdogo aka machinga ambaye mtaji wake hauzidi shilingi millioni 4 yeye hulipa gharama ya kitambulisho tu cha shillingi elfu 20 kwa mwaka. Hii wala siyo kodi bali ni gharama ya kuchapisha kitambulisho hicho. Mfanyabiashara wa aina hiyo ni kama yule dada aliyemuuzia yale maparachichi ambaye alikuwa na furaha tele kutokana na kitambulisho hicho. Anamshangaa anapokilalamikia kwenye kampeni zake.
5. Alipokuwa ndani ya bus la mwendokasi amejifunza kuwa watanzania wanaishi kwa raha na uhuru tele. Hawamuogopi mtu ye yote hadi wale dada walimuchukulia kama cerebity tu na wakaenda kukaa kuchat naye na kupiga selfie. Mke wake itakuwa roho ilimuuma. Huko ulaya hakuna kitu cha namna hiyo. Ukiingia kwenye basi hawasemazani, unasoma gazeti au kitabu tu. Halafu wanasema eti nchi yetu haina furaha eti wao ndiyo wenye furaha, nonsense.
6. Amekubali kuwa ile barabara yetu ya njia 8 hadi 12 ya kutoka Dar hadi Kibaha ni nzuri na kubwa sana ambayo hata huko ulaya hawana.
Hivyo kwa muda mfupi sana baada ya kuona machache sana yaliyofanywa na JPM katika kipindi cha miaka 3 aliyokuwa hayupo nchini, ni wazi kwamba ameshaanza kuunga juhudi. Ameshaanza kukiri maemdeleo ya vitu na kuanza kuahidi kuwa na yeye akichaguliwa atajenga mavitu. Hii likizo ya lazima aliyopewa ni blessing kwake.
1.Kwa mfano amekubali kuwa barabara za mwendo kasi ndizo hata huko ulaya wanatumia kwenye majiji yao. Tofauti tu ni kuwa huko ulaya ziko nyingi. Ameahidi akichaguliwa atazijenga nyingi jijini DSM. Ambacho hajajua ni kwamba JPM alishaanza kuzijenga nyingi tu jijini DSM.
2. Ameahidi pia akichaguliwa atajenga pia reli za jijini (city railways) na city ferries. Ambacho hajajua ni kuwa tayari JPM tayari alishajenga na anaendelea kujenga hizo city railways and ferries. Ingefaa katika kipindi hiki cha likizo wampeleke akazione pia.
3. Ameahidi pia kuwa atabomoa nyumba kadhaa jijini DSM ili kujenga maeneo ya kupumuzikia (city gardens) na kuegesha magari (parking areas) kama ilivyo huko ulaya. Ambacho hajajua ni kwamba JPM tayari alishaanza kufanya kazi hiyo. Aende akatembelee maeneo hayo ambayo yako tayari.
4. Alipotembelea soko la Kariakoo amejifunza kuwa hizo utitiri wa kodi alizokuwa akizilalamikia kwenye kampeni zake hazikuwa za kweli. Amejifunza kuwa mfanya biashara mkubwa (mwenye mtaji unaozidi millioni 20) kodi anayotakiwa kukusanya ni VAT tu ambayo kiwango chake huwekwa na bunge. Mfanya biashara wa kati ambaye mtaji wake ni kuanzia milioni 4 hadi ishirini kodi yake haizidi milioni 5 kwa mwaka na hukokotolewa kutokana na risiti za mauzo yake na mashine za kielekitroniki anazopewa bure na TRA.
Mfanyabiashara mdogo aka machinga ambaye mtaji wake hauzidi shilingi millioni 4 yeye hulipa gharama ya kitambulisho tu cha shillingi elfu 20 kwa mwaka. Hii wala siyo kodi bali ni gharama ya kuchapisha kitambulisho hicho. Mfanyabiashara wa aina hiyo ni kama yule dada aliyemuuzia yale maparachichi ambaye alikuwa na furaha tele kutokana na kitambulisho hicho. Anamshangaa anapokilalamikia kwenye kampeni zake.
5. Alipokuwa ndani ya bus la mwendokasi amejifunza kuwa watanzania wanaishi kwa raha na uhuru tele. Hawamuogopi mtu ye yote hadi wale dada walimuchukulia kama cerebity tu na wakaenda kukaa kuchat naye na kupiga selfie. Mke wake itakuwa roho ilimuuma. Huko ulaya hakuna kitu cha namna hiyo. Ukiingia kwenye basi hawasemazani, unasoma gazeti au kitabu tu. Halafu wanasema eti nchi yetu haina furaha eti wao ndiyo wenye furaha, nonsense.
6. Amekubali kuwa ile barabara yetu ya njia 8 hadi 12 ya kutoka Dar hadi Kibaha ni nzuri na kubwa sana ambayo hata huko ulaya hawana.
Hivyo kwa muda mfupi sana baada ya kuona machache sana yaliyofanywa na JPM katika kipindi cha miaka 3 aliyokuwa hayupo nchini, ni wazi kwamba ameshaanza kuunga juhudi. Ameshaanza kukiri maemdeleo ya vitu na kuanza kuahidi kuwa na yeye akichaguliwa atajenga mavitu. Hii likizo ya lazima aliyopewa ni blessing kwake.