Themagufulianz
JF-Expert Member
- Apr 15, 2017
- 4,548
- 1,990
Na bado kuna wajinga walisoma anyway
Viva Magu 2020 to 2030
Viva Magu 2020 to 2030
umeandika utopolo mtupu.
umeandika utopolo mtupu.
Kwa iyo wewe ulivhofanyiwa Kabendera na Mama yake unaona uhuru na haki???Uhuru ?
Tanganyika 1961 pioneers TANU, wewe unasema uhuru gani?
Haki - kwani Mahakama hazipo? Na ni haki unazizungumzia mbona wananchi haki zao zinazingatiwa?
Maendeleo- Muulize Lisu jana alikuwa picnic atakupa mrejesho na hiyo ni Dar tuu.
Sasa hivi unatoka Mtwara mpaka Bukoba mkeka tuu yaani unaweza kukodi hadi Taxi.
October 28 kura zote ni kwa JPM
JPM ANATOSHA
CCM KWA MAENDELEO YA TANZANIA
Yapo dar pekee,vipi mikoani Wana kipi Cha kunufaika na Utawala huu
Hahahahaha endeleeni kuweweseka tu!! Jana watu waliacha biashara zao na wakawa wanamfuata Tundu Lissu na kuimba Raisi, Raisi???? Au umevaa miwani ya mbao hujaona??!Ila ile ziara ya miguu ukimwangalia Lisu alikuwa kama frustrated Fulani hivi hakutarajia ile cold reception aliyopata toka kwa wananchi
Alienda kariakoo akitegemea labda shughuli zingesimama ingekuwa patashika nguo kuchanika lakini watu wala hawakumshobokea wala kuonyesha kuwa yeye no special Fulani walimchukulia kawaida tu
Halafu alipita pale karibu na kituo cha polisi msimbazi makusudi akitarajia labda kuna polisi wata mind waka mshit alitaka akatafutie umaarufu wa ghafla kariakoo kwenye watu wengi single imebuma
Ndio maaa hata ukiangalia alipohojiwa body language inaonyesha wazi kapanick kafrustrate kuwa I didn't expect to be treated so low kwenye eneo la watu wengi kama hili la kariokoo
Alitegemea kupata grand reception ndio maana aka target kariakoo
Kilichomkuta kimempa jibu la ategemee nini October 28
Ile ziara sio siri ime do more harm to him than benefit /Aliyemshauri aende kariakoo kamharibia kuanzia mood had I ego yake ndio maana hats ule ubabe babe wake wa kuongea uliyeyukia hewani
His ego from now will be so low
Heri angesikia ushauri wa kubaki ndani tu kipindi hiki cha kufungiwa na tume.Sasa katoka kaenda tu kuibua frustration
Ile confidence aliyokuwa nayo imekuwa shaken up .Kaanza kuwajua vizuri sasa watanzania walioko mtaani sio wale wa mikutanoni walivyo
Kawaona wa mitaani kuwa hawamuoni kama presidential material.
Lisu hao ndio wenyewe wapiga kura wa October 28 wa Dar es salaam
Acha uongo weweHahahahaha endeleeni kuweweseka tu!! Jana watu waliacha biashara zao na wakawa wanamfuata Tundu Lissu na kuimba Raisi, Raisi???? Au umevaa miwani ya mbao hujaona??!
Project ni idea ya Kikwete na kikwete ndiye aliyepeleka proposal world bank. Na Kuna Awamu Kama 4 kwenye hili jiji la Dar. Leo Eti wanasema ni mradi wa Magufuli vilaza hawaKwani mwendo kasi zimejengwa kipindi cha Mzee meko?
Kabendera kafanyiwaje kwani?Kwa iyo wewe ulivhofanyiwa Kabendera na Mama yake unaona uhuru na haki???
Walichofanyiwa Azory Gwanda, Mdude Nyangali, Tito magoti, Ben Saanane na walikuwa sema kutupwa Coco beach kwenye viloba unaona ndo uhuru na haki???
Alichofanyiwa Tundu Antiphas Lissu kupigwa risasi 16 na nyie unaona uhuru na haki???
walichofanyiwa wafanyakazi wa serikali zaidi ya 10,000 kufukuzwa kazi kwa vyeti feki huku Paul Makonda akiachwa pamoja na kuwa na vyeti feki unaona uhuru na haki???
Walichofanyiwa wakazi wa kagera kukatazwa kuuza kahawa uganda kwa bei Nzuri na kulazimishwa kuuza amicos kwa bei ndogo hadi kuwa masikini unaona uhuru na haki???
Wanachofanyiwa wakulima wa mbaazi, korosho na tu mbali, kukatazwa kuuza mazao yao sehemu wanazotaka na kulazimishwa kuuza kwa stakabadhi ghalani huku hawalipwi kwa wakati unaona ndo Uhuru na haki??!
Walichofanyiwa wakulima wa mpunga kilombero na wa mananasi bagamoyo ya kuzuiwa kuuza mazao yao kwa wakenya jambo lililopelekea wamekuwa masikini we unaona ndo uhuru na haki???
Lie ni kundi aliloliandaa la vijana wa kuhamasisha waliokuwa wakimsindikizaHahahahaha endeleeni kuweweseka tu!! Jana watu waliacha biashara zao na wakawa wanamfuata Tundu Lissu na kuimba Raisi, Raisi???? Au umevaa miwani ya mbao hujaona??!
Imekuchoma eeh???? Jibu maswali hayo??? Huo ndo uhuru na haki???Kabendera kafanyiwaje kwani?
Na hilo kundi kubwa limefanyiwaje maana sijui?
Unaonekana unayafahamu mengi kama unaona Haki za watu zimevunjwa fanya kuwahi MAHAKAMANI Chaaap.
Humu JF sio Mahakama kama una ushahidi wa hayo nenda Mahakamani huko ndipo HAKI upatikana.
Usisahau kumpigia kura JPM October 28 sababu kura yako ni muhimu.
JPM ANATOSHA
CCM KWA MAENDELEO YA TANZANIA
Hahahahaha!! Kilihamasiswa sa ngapi?? Weka ushahidi ??? Safari za jana za Lissu zimeoneshwa kuanzia alipoanzia Morroco hadi Kariakoo!! Sema huo uhamasishaji Uko wapi na ulikuwa wapi???Lie ni kundi aliloliandaa la vijana wa kuhamasisha waliokuwa wakimsindikiza
Angalia anamopita response ya watu walio upande wa kushoto na kulia wako cold wapiga miyowe ni hicho kikundi kilicho nyuma yake tu cha wapambe .
The rest of the people wanamtizama tu
Kipi cha kujibu hapo Kabendera si ni kweli alikiri na kuomba msamaha alipe fidia sasa kuna kipi hapo cha kujibu?Imekuchoma eeh???? Jibu maswali hayo??? Huo ndo uhuru na haki???
Hivi ni kwanini unahangaika sana? Halafu ukweli hata hutaki kuusikia.Lie ni kundi aliloliandaa la vijana wa kuhamasisha waliokuwa wakimsindikiza
Angalia anamopita response ya watu walio upande wa kushoto na kulia wako cold wapiga miyowe ni hicho kikundi kilicho nyuma yake tu cha wapambe .
The rest of the people wanamtizama tu
Kafeli sana, manake saiv Mwendo kasi ya mjini mbagala ilitakiwa iwe inafanya kazi , mwendo kasi ya goms gongo la mboto ilitakiwa na yenyewe iwe kwenye hatua za mwsho, hajafanya kituMagufuli ni mwaribifu tu wa pesa za Umma, mwizi na fisadi hawezi kuliendeleza JIJI kwa namna yoyote ile.
Magufuli alipokua Waziri aliiba pesa za MV Bagamoyo - Dar. Akaleta meli mbovu.
Magufuli na MaCCM yote hayajawahi kuitakia mema nchi yetu.
Hii likizo ya siku saba inaonekana anaitumia vizuri kujifunza kuelewa nchi yetu sasa hivi iko hali gani baada ya kuiacha miaka mitatu iliyopita. Ndani ya siku moja tu ameshaanza kuunga juhudi za Magufuli kwamba tuko kwenye right track kuelekea kuwa kama ulaya kwa mfano:
1.Kwa mfano amekubali kuwa barabara za mwendo kasi ndizo hata huko ulaya wanatumia kwenye majiji yao. Tofauti tu ni kuwa huko ulaya ziko nyingi. Ameahidi akichaguliwa atazijenga nyingi jijini DSM. Ambacho hajajua ni kwamba JPM alishaanza kuzijenga nyingi tu jijini DSM.
2. Ameahidi pia akichaguliwa atajenga pia reli za jijini (city railways) na city ferries. Ambacho hajajua ni kuwa tayari JPM tayari alishajenga na anaendelea kujenga hizo city railways and ferries. Ingefaa katika kipindi hiki cha likizo wampeleke akazione pia.
3. Ameahidi pia kuwa atabomoa nyumba kadhaa jijini DSM ili kujenga maeneo ya kupumuzikia (city gardens) na kuegesha magari (parking areas) kama ilivyo huko ulaya. Ambacho hajajua ni kwamba JPM tayari alishaanza kufanya kazi hiyo. Aende akatembelee maeneo hayo ambayo yako tayari.
4. Alipotembelea soko la Kariakoo amejifunza kuwa hizo utitiri wa kodi alizokuwa akizilalamikia kwenye kampeni zake hazikuwa za kweli. Amejifunza kuwa mfanya biashara mkubwa (mwenye mtaji unaozidi millioni 20) kodi anayotakiwa kukusanya ni VAT tu ambayo kiwango chake huwekwa na bunge. Mfanya biashara wa kati ambaye mtaji wake ni kuanzia milioni 4 hadi ishirini kodi yake haizidi milioni 5 kwa mwaka na hukokotolewa kutokana na risiti za mauzo yake na mashine za kielekitroniki anazopewa bure na TRA. Mfanyabiashara mdogo aka machinga ambaye mtaji wake hauzidi shilingi millioni 4 yeye hulipa gharama ya kitambulisho tu cha shillingi elfu 20 kwa mwaka. Hii wala siyo kodi bali ni gharama ya kuchapisha kitambulisho hicho. Mfanyabiashara wa aina hiyo ni kama yule dada aliyemuuzia yale maparachichi ambaye alikuwa na furaha tele kutokana na kitambulisho hicho. Anamshangaa anapokilalamikia kwenye kampeni zake.
5. Alipokuwa ndani ya bus la mwendokasi amejifunza kuwa watanzania wanaishi kwa raha na uhuru tele. Hawamuogopi mtu ye yote hadi wale dada walimuchukulia kama cerebity tu na wakaenda kukaa kuchat naye na kupiga selfie. Mke wake itakuwa roho ilimuuma. Huko ulaya hakuna kitu cha namna hiyo. Ukiingia kwenye basi hawasemazani, unasoma gazeti au kitabu tu. Halafu wanasema eti nchi yetu haina furaha eti wao ndiyo wenye furaha, nonsense.
6. Amekubali kuwa ile barabara yetu ya njia 8 hadi 12 ya kutoka Dar hadi Kibaha ni nzuri na kubwa sana ambayo hata huko ulaya hawana.
Hivyo kwa muda mfupi sana baada ya kuona machache sana yaliyofanywa na JPM katika kipindi cha miaka 3 aliyokuwa hayupo nchini, ni wazi kwamba ameshaanza kuunga juhudi. Ameshaanza kukiri maemdeleo ya vitu na kuanza kuahidi kuwa na yeye akichaguliwa atajenga mavitu. Hii likizo ya lazima aliyopewa ni blessing kwake.