Spanishboy
Senior Member
- Apr 24, 2011
- 118
- 65
Habari ndugu, mimi na mchumba wangu tumedumu kwa miaka 8 sasa, hatukufunga ndoa kwa sababu ya kutaka kutimiza malengo ya kimasomo, mwenzangu amemaliza chuo mwezi wa sita mwaka huu na mimi ndo nimemaliza mwezi uliopita, kinachosubiriwa ni kwenda kulipa mahari ili kufunga ndoa, kwa kuwa nilikuwa masomoni sijajipanga vizuri kwa maana ya pesa za kulipa mahari, nimemwambia mpenzi wangu anivumilie nigangegange maana hata mahari najilipia mwenyewe, lakini cha ajabu ameniambia amechoka kusubiri, amenipa mwezi mmoja niwe nimekamilisha taratibu za kumuoa, vinginevyo ataniacha, nifanyeje ndugu zangu, nisaidieni!