Amenifungulia kesi polisi,yakutishia kumuua kwa maneno,ila yote hayo chanzo yeye.

Cruel mpole

JF-Expert Member
Jul 3, 2013
282
106
Habari zenu,
¥¥¥asalaaam,
nimekuwa katika wakati mgumu,baada ya mpenzi wangu kufanya maamuzi magumu,yakunikaanga baada yakuamua kunishitaki polisi kwa Rb Kgd/Rb/90015/2013.KUTISHIA KUUA KWA MANENO.
Habari Kamili:
Nimekuwa katika mahusiano ya kimapenzi na binti mmoja mwanachuo ambaye kwasasa nimemfuta katika fikra zangu.Nimedumu naye kwa muda wa miezi sita.Awali mapenzi yetu yalikuwa ya amani na furaha tele,kiasi kwamba yanayotokea sasa,sikutegemea yatatokea.Nilimjali kwa kila kitu.Shida ndogondogo nilizitatua,akiugua namtibia,mahitaji madogomadogo nilimtimizia,ada ya shule nimemlipia,kila ki2 nimemfanyia,ili aridhike.Lakini hakuridhika.Chanzo ni mimi kumuuliza maswali kwa mambo kadhaa anayofanya ambayo mimi siyapendi.Wiki moja iliyopita,alikuwa katika mitihani,hivyo katika maandalizi ya kufanya mitihani alikuwa akijichanganya na group discussions,yenye mix ya wanaume na wanawake,ambao kila mara anafanya nao assignments za hapa na pale.Pindi wapo ktk majadiliano yao,alitokea kumshobokea kijana fulani katika hilo kundi,kiasi kwamba hata majadiliano yakiisha,members wengine waliondoka wakabaki wao wawili zaidi ya masaa ma4,to the extent,wanaweza kuondoka eneo hilo saa tano usiku,kiza kinene kikiwa kimetanda.Mimi ninaishi kwangu,kwani ni mfanya kazi taasisi fulani ya serikali,na hizi data nilizipata kutoka kwa informer wangu hapo chuo,kufuatilia nyenendo zake na mimi nilifanya reserch for the moment of time,nikaprove kwamba ni kweli kwani nilishawafumania pamoja wakiwa kwenye mapozi yakichokozi,ambayo yalifanya nigadhabike na kuondoka eneo lile nilipo wakuta na kurudi kwangu.Kweli nilikuwa nina nia yakumfanya mke wangu wa maisha,ila kwa visa anavyofanya,siamini ni kwamba niyuleyule aliyeahidi kwamba nitakuwa naye bega kwa bega maishani.Inafikia wakati ananitukana matusi makubwa pindi ninapomuuliza kwa ustaarabu kwanini anafanya mambo kama hayo.Mara ataniambia sina jipya,mara hivi na vile.Nikajua moja kwa moja nimeshanyang'anywa tonge mdomoni.Nimejaribu kila njia kumuweka sawa,lakini wapi.Ikabidi nitumie nguvu sasa.Nimemtext sms kadhaa kumtishia kwa namna yoyote ile.Binti kapanic,kasema kwamba mimi ni mchawi,mnafiki na sina mapenzi ya dhati kwake.Nikimuuliza kwanini anasema hvyo anasema kwamba mimi ni mwongo na sina future nae,kwamba namwongopea,jambo ambalo si kweli.Hivi sasa ninavyoandika haya,meseji niliyomtumia ya vitisho dhidi yake,ameisambaza kwa ndugu zake na marafiki na kiöngozi wa chuo hicho,kwamba baya lolote litakalompata chanzo ni mimi,hata akiugua mafua,chanzo ni mimi kwani amenishutumu awali kwamba mimi mchawi.Kauli hii ilinikera sana,ukitazama nimemghalamikia kwa kila hari.Kinachoniuma mimi ni kwanini hakuniambia mapema kwamba hanipendi,ila kunakitu anataka kujinufaisha kutoka kwangu then asepe zake,si bora angeniambia kweli nikamuelewa,kuliko kuchezea hisia zangu na kuniacha kwenye mataa?Eti ningefanya nini mimi Kiumbe mchanga kwenye ulimwengu wa mapenzi,kwa msichana huyu?zaidi yakugadhabika na kumtisha ili akae kwenye mstari?
 
Pole mkuu, na hayo ndo makosa tunayoyafanya sana siye vijana, kuwaamini kwa uharaka hawa viumbe. Na kosa kubwa ni kuwalipia ada ukijua siku moja atakuja kukupenda kwa dhati. Wala hukutakiwa kumtisha, ulitakiwa kumfuta katika akili yako kabisa.

Ku date na wanachuo ni risk sana. Hawaaminiki wale, waache watoke wao kwa wao, na kama unakuwa naye basi uwe kama yule aliyejenga kwenye hifadhi ya barabara, muda wowote Magufuli atapitia.
 
Dah, nimesoma kwa masiktiko sana hii thread. Pole sana kaka yangu. Mapenz ya cku hz jaman ni headache.
Nikirud kny mada, huyo mchumb wako kuna v2 viwili nawaza. 1/ huenda tangu mwanzo hakukupenda kwa dhati kama unavyompenda wew bali alikuwa nawew kma kukuchuna tu kama hvyo umemsomesha umemgharamia kwa hali na mali, sasa haoni tena umuhm wa yey kuwa nawe coz alichokuwa anataka amekpata. 2/huenda alikupenda kwa dhati icpokuwa kadanganyka tu na huyo mwanafunz mwenzie bt true love ipo kwako, so mwsho wa mchezo atakuja ku2bu umsamehe mrudiane. Ndo mchezo wa mapenz ulivyo kaka. Jikaze, mwite Mungu ktk maisha yko kwa imani yako na inshaalah atakupa mke mwema na mwenye hadhi ya kuwa mke.

NB; SI KILA MWANAMKE MREMBO ANAFAA KUWA MKE. KUWA MAKINI SANA WAKAT WA KUTAFTA MKE/MUME. UNAWEZA KUHARIBU MAISHA YAKO YOTE KWA MAAMUZI YA DK1.
 
tuwekee hiyo meseji ambayo inaonyesha ilimtishia maisha tui discuss!! so far mkuu hapo hamna mapenzi sepa ,chapa lapa such shits happen,najua uliwekeza MOYO wako yeye akawekeza KUCHA TU(yaani hata ukimwacha zitaota tu),achana nae kuna watu wengine hawajitambui na wala hawajui wanahitaji nini kwenye haya maisha ya mapenzi,PIGA MOYO KONDE after TIME utasahau tu!!
ALWAYS MARRIAGE IS A DESTINY(mpango kutoka kwa mungu) haulazimishwi
NAKUSHAURI TU KAMA MANATI YA KIZUNGU(BASTOLA) KWA MIEZI HII MIWILI KAIKABIDHISHE POLISI(kama wewe ni mchaga lakini LMAO.........................!!
 
Nimewekwa lock up kwa ujinga wa huyu binti?inaniuma sana.Nashukuru ndugu na jamaa waliotoa msaada wakanidhamini.Nipo kazini lakini akili haifanyi kazi kabisa.
 
Vijana msiwagharimie wanawake ambao hamjawaweka ndani.Mgaramie mkeo na si vinginevyo.Kama unataka kuowa mtafute mwanamke mwenye malengo kama yako na si wa kumjengea fikra ili afikirie kuolewa,hapo utachunwa sana.Nakushauri mwache huyo na anza tabia ya kugegeda mabinti tofauti tofauti atatokea mmoja atakupenda na mwenyewe atakwambia NIOWE basi hapohapo usilaze damu ila wewe usije ukamtamkia mwanamke eti nataka kukuowa.
 
tuwekee hiyo meseji ambayo inaonyesha ilimtishia maisha tui discuss!! so far mkuu hapo hamna mapenzi sepa ,chapa lapa such shits happen,najua uliwekeza MOYO wako yeye akawekeza KUCHA TU(yaani hata ukimwacha zitaota tu),achana nae kuna watu wengine hawajitambui na wala hawajui wanahitaji nini kwenye haya maisha ya mapenzi,PIGA MOYO KONDE after TIME utasahau tu!!
ALWAYS MARRIAGE IS A DESTINY(mpango kutoka kwa mungu) haulazimishwi
NAKUSHAURI TU KAMA MANATI YA KIZUNGU(BASTOLA) KWA MIEZI HII MIWILI KAIKABIDHISHE POLISI(kama wewe ni mchaga lakini LMAO.........................!!

hii kitu ipo ndugu yangu,ila sijapata wazo kama hilo.
 
Songa mbele...achana naye. Atakuepushia mengi zaidi ukichukua maamuzi sasa.
 
Jina lako lina reflect Character yako....hio ndio Falsafa ya kweli.
Pili, miezi sita tu unalalamika umegharamia? Umegharamia nini? Tatu: Binti wa Chuo si wa kumfanya Mchumba (sio wote)
NNe, umezidi sana kumfuatilia hadi anakosa at least uhuru kidogo na rafiki zake.
Tano; jiamini kuwa ni wako tu (though it is too late but for future use amini hivyo)
Sita; jifunzeni kujiweka huru na mambo yenu, achana na mambo ya kutaka kujua ana communicate na nani saa ngapi na wapi....what for? si atarudi kwako tu? kikubwa jiwekeni huru kuwa hii michezo tuayoicheza si salma kwa maisha yetu.
Aaaah ngoja niishie hapa kwanza
 
Hivi tuavyosema dont invest munakuwa wapi tena kwa demu wa chuo ambae haeleweki mbaya zaidi mumejuana kwa kipndi kifupi sana miez 6 tuu, mzee umeshachukua majukumu kama mzazi, unless kama ulikua unatoa msaada ila kama mke huyo sio ndege wako
 
Hivi tuavyosema dont invest munakuwa wapi tena kwa demu wa chuo ambae haeleweki mbaya zaidi mumejuana kwa kipndi kifupi sana miez 6 tuu, mzee umeshachukua majukumu kama mzazi, unless kama ulikua unatoa msaada ila kama mke huyo sio ndege wako

unazidi kunichang'any ndugu yangu.
 
pole saaana kaka, ushauriwangu ni kuwa achana naye hakufai ktkt maisha, wala usije hata siku moja ukakubali kumrudia, kila kitu umeshakiona
1. katika maisha yako from now usijaribu kudate au kuwa na mahusiano na wanafunzi, awe wa chuo secondary primary yeyote yule aitwayeni mwafunzi,90% ni wezi tuu, siyo waaminifu,hawako commited
2.ikitokea ukampata mwanachuo au mwanafunzi kamwe usimlipie ada hela za matumizi,mwanzo kabla hujamtokea ada alikuwa analipiwa na nani,hela za matumizi alikuwa anapewa na nani? ukijifanya mwema utakoma,kwa kizazi hiki
3. date someone of your class,wa hadhi yako,hutapata shida
ni ushauri wangu huo/nionavyo mimi,ufuate utakusaidia
 
unazidi kunichang'any ndugu yangu.

Unachanganyikiwa kwa lipi? Unadhani huna maisha tena after huyo demu wako? Dont cheat ur self, life still goes on without her. The world is full of beaut, au unadhani ana maumbile tofauti na wengine ? Wake up bro fanya kazi. Cash mpango mzima achana na vitoga uchwara.
 
Nimewekwa lock up kwa ujinga wa huyu binti?inaniuma sana.Nashukuru ndugu na jamaa waliotoa msaada wakanidhamini.Nipo kazini lakini akili haifanyi kazi kabisa.

Hili jina lako kwanza libadilishe hapa. Nahisi ndo litakuwa linakuletea majanga bila kujijua ingawa kiuhalisia yawezekana una jina lako zuri tu sema kwa sababu za ki JF umejipa hili lenye majanga.
Pili, piga moyo konde. Endelea na maisha kama kawaida huyo binti atakukumbuka kwa mabaya aliyokurudishia dhidi ya wema uliomtendea. Acha kunung'unika na kulia. Hii dunia ndivyo ilivyo aisee.
Wanawake wazuri wako wengi sana. Utapata mwingine. Songa mbele. Hilo lishapita.
Ukifocus na maisha yako kwa sasa hata hiyo kesi iliyofunguliwa itakwisha automatically.
 
unazidi kunichang'any ndugu yangu.
tatilo lote ni kumtisha,,ulitegemea aogope akurudie,badala yake kakuona mbaya zaidi....cha msingi mwache usonge mbele.haya matukio ya mauaji na polisi wanalalamikiwa kwa uzembe,ww kesi yako ishafikishwa polisi sasa naona kwa kipindi hiki lazima ufuatiliwe sana nyendo zako...hawataki ya ilala yajirudie...
 
Mapenzi hayanunuliwa wala kulazimishwa. Na mwanamke akichoka mwache aende zake, kwa nini ung'ang'ania kitu ambacho hakipo? Move on, kuna wanawake wengi wanaongojea bahati ya kupendwa na wewe.
 
Habari zenu,
¥¥¥asalaaam,
nimekuwa katika wakati mgumu,baada ya mpenzi wangu kufanya maamuzi magumu,yakunikaanga baada yakuamua kunishitaki polisi kwa Rb Kgd/Rb/90015/2013.KUTISHIA KUUA KWA MANENO.
Habari Kamili:
Nimekuwa katika mahusiano ya kimapenzi na binti mmoja mwanachuo ambaye kwasasa nimemfuta katika fikra zangu.Nimedumu naye kwa muda wa miezi sita.Awali mapenzi yetu yalikuwa ya amani na furaha tele,kiasi kwamba yanayotokea sasa,sikutegemea yatatokea.Nilimjali kwa kila kitu.Shida ndogondogo nilizitatua,akiugua namtibia,mahitaji madogomadogo nilimtimizia,ada ya shule nimemlipia,kila ki2 nimemfanyia,ili aridhike.Lakini hakuridhika.Chanzo ni mimi kumuuliza maswali kwa mambo kadhaa anayofanya ambayo mimi siyapendi.Wiki moja iliyopita,alikuwa katika mitihani,hivyo katika maandalizi ya kufanya mitihani alikuwa akijichanganya na group discussions,yenye mix ya wanaume na wanawake,ambao kila mara anafanya nao assignments za hapa na pale.Pindi wapo ktk majadiliano yao,alitokea kumshobokea kijana fulani katika hilo kundi,kiasi kwamba hata majadiliano yakiisha,members wengine waliondoka wakabaki wao wawili zaidi ya masaa ma4,to the extent,wanaweza kuondoka eneo hilo saa tano usiku,kiza kinene kikiwa kimetanda.Mimi ninaishi kwangu,kwani ni mfanya kazi taasisi fulani ya serikali,na hizi data nilizipata kutoka kwa informer wangu hapo chuo,kufuatilia nyenendo zake na mimi nilifanya reserch for the moment of time,nikaprove kwamba ni kweli kwani nilishawafumania pamoja wakiwa kwenye mapozi yakichokozi,ambayo yalifanya nigadhabike na kuondoka eneo lile nilipo wakuta na kurudi kwangu.Kweli nilikuwa nina nia yakumfanya mke wangu wa maisha,ila kwa visa anavyofanya,siamini ni kwamba niyuleyule aliyeahidi kwamba nitakuwa naye bega kwa bega maishani.Inafikia wakati ananitukana matusi makubwa pindi ninapomuuliza kwa ustaarabu kwanini anafanya mambo kama hayo.Mara ataniambia sina jipya,mara hivi na vile.Nikajua moja kwa moja nimeshanyang'anywa tonge mdomoni.Nimejaribu kila njia kumuweka sawa,lakini wapi.Ikabidi nitumie nguvu sasa.Nimemtext sms kadhaa kumtishia kwa namna yoyote ile.Binti kapanic,kasema kwamba mimi ni mchawi,mnafiki na sina mapenzi ya dhati kwake.Nikimuuliza kwanini anasema hvyo anasema kwamba mimi ni mwongo na sina future nae,kwamba namwongopea,jambo ambalo si kweli.Hivi sasa ninavyoandika haya,meseji niliyomtumia ya vitisho dhidi yake,ameisambaza kwa ndugu zake na marafiki na kiöngozi wa chuo hicho,kwamba baya lolote litakalompata chanzo ni mimi,hata akiugua mafua,chanzo ni mimi kwani amenishutumu awali kwamba mimi mchawi.Kauli hii ilinikera sana,ukitazama nimemghalamikia kwa kila hari.Kinachoniuma mimi ni kwanini hakuniambia mapema kwamba hanipendi,ila kunakitu anataka kujinufaisha kutoka kwangu then asepe zake,si bora angeniambia kweli nikamuelewa,kuliko kuchezea hisia zangu na kuniacha kwenye mataa?Eti ningefanya nini mimi Kiumbe mchanga kwenye ulimwengu wa mapenzi,kwa msichana huyu?zaidi yakugadhabika na kumtisha ili akae kwenye mstari?

Pole kijana mwenzangu! hayo yameshatokea na ulichotendewa ni uhaini juu ya maisha ya mwanadamu, huyo binti ni mwizi na ameshakuibia na kuiumiza pia roho yako na kukuharibia muda wako. cha kufanya kwanza samehe nikimaanisha muondoe akilini na rohoni mwako ki akili anza taratibu na ikitokea kukawa na maneno yoyote mabaya kutoka kwake mjibu kwa upole na usisahau kumshukuru kwa kusema asante kwa aliyokutendea! Usiruhusu hasira itumike kukupa pozo la jeraha alilokuachia kwani kufanya hivyo nikumpa ushindi zaidi, najua inauma sana tena sana ila shinda hali hii ya sasa kwa kwakutumia busara na hekima zaidi! ujue kuwa kimya nacho ni jibu wewe nyamaza kabisaa, uondoe wazo la kuwa na msichana mwingine haraka haraka kwani kwa kufanya hivi utaingia kwenye matatizo mengine kwa haraka sana, tafuta kitu cha kukufanya uwe busy wakati huna kazi ya kufanya na isiwe pombe wala mastarehe yasiyo na maana kwani hapo ndio utakuwa mwanzo wa wewe kupotea kabisaa! TULIA,MUOMBE MSAMAHA KWA SMS ULIYO MTUMIA NA UWEKE BAYANA KUWA NI HISIA ZA MAUMIVU ALIYOKUSABABISHIA NDIYO YALIYOKUSUKUMA UTUME HIYO SMS NA UMUAMBIE KUWA HUNA TENA MPANGO WA KUMFUATILIA NA UNAMPA BARAKA ZOTE AENDELEE NA HUYO KIJANA WAKE WA SASA, IKIBIDI NENDA HADI KWAO NA UENDE UKIWA NA BALOZI WA MTAANI KWAO NA MASHAHIDI WAWILI. Baada ya haya anza changamoto za maisha mapya na zaidi usali sana haita chukua muda nakuhakikishia ataanza kulia kivyake huko aliko na KUKUKUMBUKA KILA ATAKAPO DONDOSHA CHOZI katika purukushani ndani ya maisha yake hayo aliyo ya chagua. sasa hivi hawezi kuona umuhimu wako ila ukimuachila aende kwa moyo msafi hapo ndipo ataanza kuona umuhimu wako na wewe hapo ndipo pa KUFUNGA MILANGO KWA SOLEX NA USIJE KUMRUHUSU ARUDIANE NA WEWE KWANI MWANAMKE AKISHA CHEAT KAMWE HATAWEZA KUACHA zaidi atakudanganya ameacha ila ataendelea kwa siri ya hali ya juu. ni hayo tu kijana mwenzangu na pole sana.
 
Back
Top Bottom