‘Ambulance’ nusura ichomwe moto

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,299
33,082
bulance.jpg


Wananchi hao walidai kuwa gari hilo la wagonjwa halina msaada kwani muda mwingi haliko kituoni hapo hivyo kutaka kulichoma moto.



KWA UFUPI

  • Ni baada ya kuchelewa kumchukua mgonjwa, ambaye baadaye alifariki dunia.


Sumbawanga. Wananchi waliotaka kujichukulia sheria mikononi, nusura walichome moto gari la wagonjwa lilitolewa msaada Kituo cha Afya Mtowisa wilayani Sumbawanga mkoani Rukwa kutokana na madai ya kuchangia kifo cha mwalimu mmoja aliyekosa msaada wa haraka wakati wa kujifungua.

Wananchi hao wanadaiwa kulishambulia gari hilo kwa mawe na kuvunja moja ya kioo.

Gari hilo linadaiwa kuchelewa kuja kumchukua Mwalimu Leah Mgaya wa Shule ya Msingi Mtowisa ‘A', ambaye alifariki baada ya kutokwa na damu nyingi wakati wa kujifungua.

Habari kutoka sehemu ya tukio zilizothibitishwa na Ofisa Tarafa ya Mtowisa, Peter Masindi zinaeleza kuwa, awali mwalimu huyo alipelekwa katika kituo hicho cha afya juzi saa 3 asubuhi akiwa katika hali uchungu wa kujifungua, lakini baadaye ilionekana anahitaji kupewa rufaa kwenda Hospitali ya Mkoa wa Rukwa mjini hapa.

Masindi alisema kutokana na hali hiyo ililazimu kupiga simu Ofisi ya Mganga Mkuu wa Wilaya saa 6 mchana ili kuomba msaada wa gari, lakini gari hiyo ilichelewa kufika kutokana na kudaiwa ilisafiri kwenda wilayani Nkasi, na hata iliporejea jioni ilikwama njiani kutokana na hali ya mvua.

Mmoja ya wananchi waliozungumza na gazeti hili, Mwaipungu alisema kifo cha mwalimu huyo kiliwakera wananchi wa eneo hilo, ambapo walikusanyika kwenye makundi na kuanza kujadiliana.

Wananchi hao walidai kuwa gari hilo la wagonjwa halina msaada kwani muda mwingi haliko kituoni hapo hivyo kutaka kulichoma moto.

Hasira za wananchi hao zilionekana baada ya kufika kwa dereva wa gari hiyo aliyefika, huku akiliza king'ora lakini alipokelewa kwa mabango, kabla ya kumsimamishwa kumtaka kuwapa funguo za gari, jambo lililopingwa na dereva. huyo huku wananchi hao wakilishambulia kwa mawe. ‘Ambulance’ nusura ichomwe moto - Kitaifa - mwananchi.co.tz






 
bulance.jpg


Wananchi
hao walidai kuwa gari hilo la wagonjwa halina msaada kwani muda mwingi
haliko kituoni hapo hivyo kutaka kulichoma moto.



KWA
UFUPI


  • Ni baada ya kuchelewa kumchukua mgonjwa, ambaye baadaye
    alifariki dunia.


Sumbawanga. Wananchi
waliotaka kujichukulia sheria mikononi, nusura walichome moto gari la
wagonjwa lilitolewa msaada Kituo cha Afya Mtowisa wilayani Sumbawanga
mkoani Rukwa kutokana na madai ya kuchangia kifo cha mwalimu mmoja
aliyekosa msaada wa haraka wakati wa kujifungua.


Wananchi hao wanadaiwa kulishambulia gari hilo kwa mawe na
kuvunja moja ya kioo.


Gari hilo linadaiwa kuchelewa kuja kumchukua Mwalimu Leah Mgaya
wa Shule ya Msingi Mtowisa ‘A’, ambaye alifariki baada ya kutokwa na
damu nyingi wakati wa kujifungua.


Habari kutoka sehemu ya tukio zilizothibitishwa na Ofisa Tarafa
ya Mtowisa, Peter Masindi zinaeleza kuwa, awali mwalimu huyo alipelekwa
katika kituo hicho cha afya juzi saa 3 asubuhi akiwa katika hali uchungu
wa kujifungua, lakini baadaye ilionekana anahitaji kupewa rufaa kwenda
Hospitali ya Mkoa wa Rukwa mjini hapa.


Masindi alisema kutokana na hali hiyo ililazimu kupiga simu
Ofisi ya Mganga Mkuu wa Wilaya saa 6 mchana ili kuomba msaada wa gari,
lakini gari hiyo ilichelewa kufika kutokana na kudaiwa ilisafiri kwenda
wilayani Nkasi, na hata iliporejea jioni ilikwama njiani kutokana na
hali ya mvua.


Mmoja ya wananchi waliozungumza na gazeti hili, Mwaipungu
alisema kifo cha mwalimu huyo kiliwakera wananchi wa eneo hilo, ambapo
walikusanyika kwenye makundi na kuanza kujadiliana.


Wananchi hao walidai kuwa gari hilo la wagonjwa halina msaada
kwani muda mwingi haliko kituoni hapo hivyo kutaka kulichoma
moto.


Hasira za wananchi hao zilionekana baada ya kufika kwa dereva wa
gari hiyo aliyefika, huku akiliza king’ora lakini alipokelewa kwa
mabango, kabla ya kumsimamishwa kumtaka kuwapa funguo za gari, jambo
lililopingwa na dereva. huyo huku wananchi hao wakilishambulia kwa mawe.

‘Ambulance’
nusura ichomwe moto - Kitaifa - mwananchi.co.tz








miundo mbinu mibovu magari machache ya kubebea wagonjwa, ndiyo janga la nchi hii kwa wagonjwa, Mungu ailaze mahala sitahiki mwalimu Amena
 
they have points this people, kwa sababu hiyo ambulence ilitolewa na watu wa AMREF katika kituo hicho kwa ajiri ya emergence zote za akinamama wajawazito ili kupunguza vifo vya mama na mtoto ila mdada wote hiyo gari ipo mjin haikai kituoni.
 
bulance.jpg


Wananchi hao walidai kuwa gari hilo la wagonjwa halina msaada kwani muda mwingi haliko kituoni hapo hivyo kutaka kulichoma moto.



KWA UFUPI

  • Ni baada ya kuchelewa kumchukua mgonjwa, ambaye baadaye alifariki dunia.


Sumbawanga. Wananchi waliotaka kujichukulia sheria mikononi, nusura walichome moto gari la wagonjwa lilitolewa msaada Kituo cha Afya Mtowisa wilayani Sumbawanga mkoani Rukwa kutokana na madai ya kuchangia kifo cha mwalimu mmoja aliyekosa msaada wa haraka wakati wa kujifungua.

Wananchi hao wanadaiwa kulishambulia gari hilo kwa mawe na kuvunja moja ya kioo.

Gari hilo linadaiwa kuchelewa kuja kumchukua Mwalimu Leah Mgaya wa Shule ya Msingi Mtowisa ‘A', ambaye alifariki baada ya kutokwa na damu nyingi wakati wa kujifungua.

Habari kutoka sehemu ya tukio zilizothibitishwa na Ofisa Tarafa ya Mtowisa, Peter Masindi zinaeleza kuwa, awali mwalimu huyo alipelekwa katika kituo hicho cha afya juzi saa 3 asubuhi akiwa katika hali uchungu wa kujifungua, lakini baadaye ilionekana anahitaji kupewa rufaa kwenda Hospitali ya Mkoa wa Rukwa mjini hapa.

Masindi alisema kutokana na hali hiyo ililazimu kupiga simu Ofisi ya Mganga Mkuu wa Wilaya saa 6 mchana ili kuomba msaada wa gari, lakini gari hiyo ilichelewa kufika kutokana na kudaiwa ilisafiri kwenda wilayani Nkasi, na hata iliporejea jioni ilikwama njiani kutokana na hali ya mvua.

Mmoja ya wananchi waliozungumza na gazeti hili, Mwaipungu alisema kifo cha mwalimu huyo kiliwakera wananchi wa eneo hilo, ambapo walikusanyika kwenye makundi na kuanza kujadiliana.

Wananchi hao walidai kuwa gari hilo la wagonjwa halina msaada kwani muda mwingi haliko kituoni hapo hivyo kutaka kulichoma moto.

Hasira za wananchi hao zilionekana baada ya kufika kwa dereva wa gari hiyo aliyefika, huku akiliza king'ora lakini alipokelewa kwa mabango, kabla ya kumsimamishwa kumtaka kuwapa funguo za gari, jambo lililopingwa na dereva. huyo huku wananchi hao wakilishambulia kwa mawe. ‘Ambulance’ nusura ichomwe moto - Kitaifa - mwananchi.co.tz







lilikua ziara ya kichama jamani tuvumiliane tu ni mambo yakawaida tu jamani si unajua akija kiongozi mkubwa kutoka makao makuu lazima tuandamane nalo
 
they have points this people, kwa sababu hiyo ambulence ilitolewa na watu wa AMREF katika kituo hicho kwa ajiri ya emergence zote za akinamama wajawazito ili kupunguza vifo vya mama na mtoto ila mdada wote hiyo gari ipo mjin haikai kituoni.

Kwa mtindo huo walikuwa na haki yakufanya walichokifanya'
 
Wakilichoma linaungua, then....? marehemu atafufuka au?
Litaungua serikali itapata hasara then kodi yao waliochoma itanunua then....|?
Baadhi wanaweza wakasotajela miaka kadhaa kwa kitendo walichofanya cha saa moja then....?
Suluhisho la kuhamisha kivuli sio kukata mti bali ni wewe kukifuata kivuli
 
Wakilichoma linaungua, then....? marehemu atafufuka au?
Litaungua serikali itapata hasara then kodi yao waliochoma itanunua then....|?
Baadhi wanaweza wakasotajela miaka kadhaa kwa kitendo walichofanya cha saa moja then....?
Suluhisho la kuhamisha kivuli sio kukata mti bali ni wewe kukifuata kivuli
kwa nini uwe na ambulance isiyokuwa na msaada wakati wa emergence?Tusiwafanye wananchi ni wapuuzi kiasi hiki kwamba hawajui kufanya maamuzi.
This community will be praised for being in line with MDG4&5.....
 
Back
Top Bottom