Ambrose Dunga: Producer aliyezivunja vunja Bongo Records, MJ Records kwa ma-beat makali yenye 'back vocals'

Nako 2 Nako, Weusi pia kawapatia sana

MANDUGU DIGITAL NI BALAA

DUNGA ANAJUA AISEE TUMPE CREDITS ZAKE.... KWENYE TOP TEN YANGU YA MUSIC PRODUCERS YUPO
 
Kwenye wimbo wa MANUVA wa Joh Makini..

Mwishoni Joh anasema -: DUNGA UTAWAUA..
Dunga anajibu -: MY CONDOLOSENCE..

Jamaa alikuwa na swagger sana..

Msafwa,
Uporoto, Mbeya..
 
Hii ndio raha ya JF


Mkuwe unaweka nyuzi ka hizi kila siku.

Jana usiku wakati nachapa code za JavaScript (hii language siipendi basi tu!!) huku nasikiliza album ya Joyner Lucas -ADHD kuna wimbo mmoja unaitwa 10 Bands uli-popup. Ndani ya ngoma hii ameshirikishwa the Legend Producer Timberland.

View attachment 1451643

Kwa ambao hamumjui producer Timberland tafuteni ngoma za marehemu Aaliyah (sio huyu wa Wasafi), Aaliyah msanii aliyefariki kwa ajali ya ndege akiwa na crew yake wakitoka ku-shoot video ya "Rock the Boat" kule visiwa vya Bahamas. Karibu 98% ya nyimbo za Aaliyah zilitengenezwa na legendary Timbeland 'Mzee wa Back vocals'.

Karibu nyimbo zote alizotengeneza Timberland, kuna kitu 'common' na very 'unique' kwenye beats za Timberland, zile 'back vocals' ambazo alikua anaimba Timberland mwenyewe. Okey tufanye hivi, tafuta nyimbo zifuatazo sikiliza halafu utagundua nachoongelea:

Aaliyah - Try Again
Aaliyah - Are you that somebody
Aaliyah - More than a woman
Justin Timberlake - My love
Missy Elliott - Get Ur Freak On (Napenda zile back vocals 'Piki piki donsee')
Ginuwine - Same OL G (Aisee ukiwa na stress sikiliza hii ngoma, Timberland nyoko!!)

Sikiliza beats za hizo nyimbo hapo juu. Umesikia hizo back-vocals? Basi huyo ndio Timberland mzee wa ma-beat!

Hii ikanikumbusha miaka ya 2004 mpaka 2012 kipindi Bongo Records na MJ Records bado wanatawala 'music production industry' ya Bongo, kuna producer Mkenya alikuja kuleta mapinduzi akawavunja vunja kina P-Funk Majani na Master Jay wakapotea kwenye production ya muziki wa Bongo-Fleva mpaka kesho!!

Unakumbuka miaka ya 2005 - 2010 karibu kila ngoma mpya ya Bongo-Fleva unasikia wanataja "Mandugu Digitoooo" au wakati mwingine unasikia "41 Recordssssss". Kama umesahau basi sikiliza ngoma ya Prof. Jay "Hapo Vipi" au ngoma ya Mwasiti na Chid Benz "Hao" utasikia hizo jingles. Nyuma ya pazia alikuepo 'Timberland wa Bongo' Ambrose Dunga.

Jamaa kwa muonekano ni kama mshamba mshamba hivi, lakini kazi zake zilikuwa ni nyoko!

Unaikumbuka ngoma ya Nakaaya - Mr. Politician? Basi yule 'Mr. Politician' kwenye video ndio Producer Dunga huyo! Unacheki alivo na msuti ule!! Mshamba kweli.

View attachment 1451649

Fanya hivi, angalia video ya Matonya - Anita pale beat linaanza yule anasema "Tusichongole chongole" ndio Producer Dunga huyo. Umecheki anavookena mshamba na hilo Tishet lake la njano nyuma ya nyumba yenye ukuta wa tofali za kuchoma halafu inataka kubomoka?

View attachment 1451647

Ikafika kipindi wasanii wote waliokua wateja wazuri wa Bongo Records na studio zingine wakawa wanamiminika Mandugu Digital. Producer Lamar nae akaona isiwe tabu, akamkimbia P-Funk ajifie na Bongo Records yake akaenda kuongeza maufundi kwa Producer Dunga. Aisee Lamar na Dunga waliunda 'Duo" moja kali sana.

Akina Prof. Jay wakaona isiwe tabu, wakafuata midundo yenye "back vocals' kwa 'Timberland wa Bongo'. Marehemu Ngwair aliyekua msanii 'Loyal' kwa P-funk na yeye akaona isiwe tabu. Kwanza alikua ameshapotea hasikiki tena, lakin alivoenda kwa 'Timberland wa Bongo' ndipo akaja na "Nipeni Dili Masela" ndio akarudi kwenye mainstream. Hii ngoma ukisikiliza zile 'back vocals' za Dunga utaelewa kwanini Dunga namfananisha na "Timberland wa Aaliyah"

Chini ni baadhi ya ngoma zilizopikwa na producer Dunga akisaidiwa na Lamar (kabla ya kuiva na kuunda 'Fish Crab'):

1. MB Dogg - Natamani (Kule mwishon Dunga anaimba "dumba dumba dumba dumbe")
2. Mwasiti ft. Chid Benz- Hao (Utamsikia Dunga anaimba "Tunadunda dunda duundaaa")
3. Nakaaya - Mr. Politician (Utamsikia Dunga "Nipeni kura zenu.. Nivotieni.. Put your hands up")
4. Prof Jay - Hapo Vipi
5. Ngwair - Nipeni Dili
6. Nako 2 Nako ft Loon - Bayeyo (beat linadunda hili ni nyoko)
7. Matonya - Anita (Tusichongole chongole)
8. Noorah - Baba styles
8. Ngwair ft. TID - She Performs ("Thi..This should be played at high volume")
9. Temba ft. Ray C - Nipe Mimi
10. Fatma ft. Jay Moe - Chozi la kusimuliwa

Kila kitu kina muda wake. Nani anaikumbuka match ya EPL iliopewa nickname ya "Battle of the Buffet"?

October 29, mwaka 2004 katika uwanja wa Old Traford, mabao mawili kutoka kwa Ruud van Nistelrooy na Wayne Roon yali-hitimisha "49 unbeaten record" ya washika mtutu wa London Arsenal. Mechi hiyo ilitawaliwa na vurugu kama zoteee. Hadi kupelekea Cesc Fabregas kumrushia kipande cha Pizza kocha Alex Ferguson wakat wanatoka uwanjani. Na ndio sababu ya mechi hiyo kubatizwa "Battle of the BUffet".

Leo hii May 16, 2020 mechi kati ya Man U na Arsenal inaonekana kama Aston Villa anacheza na Norwich. Mechi haina tena impact. Hakuna ile amsha amsha kama ya 2004.

Kila kitu na muda wake. Battle of the Buffet imehamia kwa Man City vs Liverpool.

Producer Dunga hatimaye (sijui kwa sababu zipi) alisepa Bongo akarudi kwao Kenya.

Lamar nae akafungua Studio yake Fish Crab. Uzuri akaendeleza ufundi aliopata kutoka kwa 'Timberland wa Bongo' kwa kutengeneza beats za kipekee zenye identity, zenye "back vocals' na jingles. Ukisikia tu "Talk of the town... Lamar.. Aaaaaaaaauu" unajua huyu ni Lamar.

Siku hizi mambo yamebadilika. Hakuna tena 'monopoly' ya music production.

Studio na Producers wamejaa Bongo yoteee... Hakuna tena 'Timberland wa Bongo' kama ilivokua miaka hiyo.

Ngoja niendelee kusikiliza ngoma za Joyner Lucas hapa, kuna ngoma inaitwa Will. Anamsifia na kumu-appreciate mwanamuziki na muigizaji Will Smith akielezea kuwa Will Smith ndio 'Role Model' wake tangu enzi hizo Joyner Lucas ana struggle kutoka.

Ingia Youtube search Joyner Lucas - Will, uone alivojivika uhusika kwenye movies za Will Smith alizoigiza zamani!!

-------- UPDATES--------
Kuna mdau kachangia amesema Dunga yupo Tanga bado anafanya production (japo sio intensive kama enzi zile). Nimeangalia video ya msanii Galatone - Samaki (ipo Youtube) nimemuona Dunga kama kawaida yake na 'back vocals' :D :D:D:D
View attachment 1451874


-------------UPDATES 2--------------
Asante mdau josephmasamaki kwa kunipa update nilikua sijui kama ngoma ya Chege na Temba - Go Down ya mwaka 2017 imetengenezwa na Dunga. Nimeicheki Youtube 'back vocals' zake kama kawaida. "Mama yanguuu.. Tembelee"
Dunga ananifurahisha sana halafu amekula suti kaliii :D :D:D
View attachment 1452188

Mama Debora
 
Jana usiku wakati nachapa code za JavaScript (hii language siipendi basi tu!!) huku nasikiliza album ya Joyner Lucas -ADHD kuna wimbo mmoja unaitwa 10 Bands uli-popup. Ndani ya ngoma hii ameshirikishwa the Legend Producer Timberland.

View attachment 1451643

Kwa ambao hamumjui producer Timberland tafuteni ngoma za marehemu Aaliyah (sio huyu wa Wasafi), Aaliyah msanii aliyefariki kwa ajali ya ndege akiwa na crew yake wakitoka ku-shoot video ya "Rock the Boat" kule visiwa vya Bahamas. Karibu 98% ya nyimbo za Aaliyah zilitengenezwa na legendary Timbeland 'Mzee wa Back vocals'.

Karibu nyimbo zote alizotengeneza Timberland, kuna kitu 'common' na very 'unique' kwenye beats za Timberland, zile 'back vocals' ambazo alikua anaimba Timberland mwenyewe. Okey tufanye hivi, tafuta nyimbo zifuatazo sikiliza halafu utagundua nachoongelea:

Aaliyah - Try Again
Aaliyah - Are you that somebody
Aaliyah - More than a woman
Justin Timberlake - My love
Missy Elliott - Get Ur Freak On (Napenda zile back vocals 'Piki piki donsee')
Ginuwine - Same OL G (Aisee ukiwa na stress sikiliza hii ngoma, Timberland nyoko!!)

Sikiliza beats za hizo nyimbo hapo juu. Umesikia hizo back-vocals? Basi huyo ndio Timberland mzee wa ma-beat!

Hii ikanikumbusha miaka ya 2004 mpaka 2012 kipindi Bongo Records na MJ Records bado wanatawala 'music production industry' ya Bongo, kuna producer Mkenya alikuja kuleta mapinduzi akawavunja vunja kina P-Funk Majani na Master Jay wakapotea kwenye production ya muziki wa Bongo-Fleva mpaka kesho!!

Unakumbuka miaka ya 2005 - 2010 karibu kila ngoma mpya ya Bongo-Fleva unasikia wanataja "Mandugu Digitoooo" au wakati mwingine unasikia "41 Recordssssss". Kama umesahau basi sikiliza ngoma ya Prof. Jay "Hapo Vipi" au ngoma ya Mwasiti na Chid Benz "Hao" utasikia hizo jingles. Nyuma ya pazia alikuepo 'Timberland wa Bongo' Ambrose Dunga.

Jamaa kwa muonekano ni kama mshamba mshamba hivi, lakini kazi zake zilikuwa ni nyoko!

Unaikumbuka ngoma ya Nakaaya - Mr. Politician? Basi yule 'Mr. Politician' kwenye video ndio Producer Dunga huyo! Unacheki alivo na msuti ule!! Mshamba kweli.

View attachment 1451649

Fanya hivi, angalia video ya Matonya - Anita pale beat linaanza yule anasema "Tusichongole chongole" ndio Producer Dunga huyo. Umecheki anavookena mshamba na hilo Tishet lake la njano nyuma ya nyumba yenye ukuta wa tofali za kuchoma halafu inataka kubomoka?

View attachment 1451647

Ikafika kipindi wasanii wote waliokua wateja wazuri wa Bongo Records na studio zingine wakawa wanamiminika Mandugu Digital. Producer Lamar nae akaona isiwe tabu, akamkimbia P-Funk ajifie na Bongo Records yake akaenda kuongeza maufundi kwa Producer Dunga. Aisee Lamar na Dunga waliunda 'Duo" moja kali sana.

Akina Prof. Jay wakaona isiwe tabu, wakafuata midundo yenye "back vocals' kwa 'Timberland wa Bongo'. Marehemu Ngwair aliyekua msanii 'Loyal' kwa P-funk na yeye akaona isiwe tabu. Kwanza alikua ameshapotea hasikiki tena, lakin alivoenda kwa 'Timberland wa Bongo' ndipo akaja na "Nipeni Dili Masela" ndio akarudi kwenye mainstream. Hii ngoma ukisikiliza zile 'back vocals' za Dunga utaelewa kwanini Dunga namfananisha na "Timberland wa Aaliyah"

Chini ni baadhi ya ngoma zilizopikwa na producer Dunga akisaidiwa na Lamar (kabla ya kuiva na kuunda 'Fish Crab'):

1. MB Dogg - Natamani (Kule mwishon Dunga anaimba "dumba dumba dumba dumbe")
2. Mwasiti ft. Chid Benz- Hao (Utamsikia Dunga anaimba "Tunadunda dunda duundaaa")
3. Nakaaya - Mr. Politician (Utamsikia Dunga "Nipeni kura zenu.. Nivotieni.. Put your hands up")
4. Prof Jay - Hapo Vipi
5. Ngwair - Nipeni Dili
6. Nako 2 Nako ft Loon - Bayeyo (beat linadunda hili ni nyoko)
7. Matonya - Anita (Tusichongole chongole)
8. Noorah - Baba styles
8. Ngwair ft. TID - She Performs ("Thi..This should be played at high volume")
9. Temba ft. Ray C - Nipe Mimi
10. Fatma ft. Jay Moe - Chozi la kusimuliwa

Kila kitu kina muda wake. Nani anaikumbuka match ya EPL iliopewa nickname ya "Battle of the Buffet"?

October 29, mwaka 2004 katika uwanja wa Old Traford, mabao mawili kutoka kwa Ruud van Nistelrooy na Wayne Roon yali-hitimisha "49 unbeaten record" ya washika mtutu wa London Arsenal. Mechi hiyo ilitawaliwa na vurugu kama zoteee. Hadi kupelekea Cesc Fabregas kumrushia kipande cha Pizza kocha Alex Ferguson wakat wanatoka uwanjani. Na ndio sababu ya mechi hiyo kubatizwa "Battle of the BUffet".

Leo hii May 16, 2020 mechi kati ya Man U na Arsenal inaonekana kama Aston Villa anacheza na Norwich. Mechi haina tena impact. Hakuna ile amsha amsha kama ya 2004.

Kila kitu na muda wake. Battle of the Buffet imehamia kwa Man City vs Liverpool.

Producer Dunga hatimaye (sijui kwa sababu zipi) alisepa Bongo akarudi kwao Kenya.

Lamar nae akafungua Studio yake Fish Crab. Uzuri akaendeleza ufundi aliopata kutoka kwa 'Timberland wa Bongo' kwa kutengeneza beats za kipekee zenye identity, zenye "back vocals' na jingles. Ukisikia tu "Talk of the town... Lamar.. Aaaaaaaaauu" unajua huyu ni Lamar.

Siku hizi mambo yamebadilika. Hakuna tena 'monopoly' ya music production.

Studio na Producers wamejaa Bongo yoteee... Hakuna tena 'Timberland wa Bongo' kama ilivokua miaka hiyo.

Ngoja niendelee kusikiliza ngoma za Joyner Lucas hapa, kuna ngoma inaitwa Will. Anamsifia na kumu-appreciate mwanamuziki na muigizaji Will Smith akielezea kuwa Will Smith ndio 'Role Model' wake tangu enzi hizo Joyner Lucas ana struggle kutoka.

Ingia Youtube search Joyner Lucas - Will, uone alivojivika uhusika kwenye movies za Will Smith alizoigiza zamani!!

-------- UPDATES--------
Kuna mdau kachangia amesema Dunga yupo Tanga bado anafanya production (japo sio intensive kama enzi zile). Nimeangalia video ya msanii Galatone - Samaki (ipo Youtube) nimemuona Dunga kama kawaida yake na 'back vocals' :D :D:D:D
View attachment 1451874


-------------UPDATES 2--------------
Asante mdau josephmasamaki kwa kunipa update nilikua sijui kama ngoma ya Chege na Temba - Go Down ya mwaka 2017 imetengenezwa na Dunga. Nimeicheki Youtube 'back vocals' zake kama kawaida. "Mama yanguuu.. Tembelee"
Dunga ananifurahisha sana halafu amekula suti kaliii :D :D:D
View attachment 1452188

Mama Debora
Dunga pia alifanya kazi ya Nikki Mbishi feat Collo na V-Money inaitwa Toast to life Collo na V-Money, ambapo track hiyo imetumiwa kama reference na P the MC kwenye futi 6 kumshangaa Nikki kwa nini hakutusua licha ya kupata collabo na wasanii wakubwa tena waliopo katika chart kwa nyakati hizo. Ilikuwa ni Collabo isiyotegemewa kufanywa na msanii kama Nikki Mbishi.


Pia alifanya ile ngoma tamu ya Enika inaitwa Changanya Changanya - background vocals zake " Mama eeh ohaa"


Joh Makini alifanyiwa mikono hatari kama Chochote Popote, Zamu Yangu na Manuva

TMK wanaume ile kazi ipo ukichanganya na ile kutengana kwao iliwatingisha kwelikweli kina Juma Nature (TMK Asilia), ile beat iliwafanya wakune sana vichwa namna ya kurudisha mashambulizi.

Kwa kweli umefanya uchambuzi vyema sana, umerudisha kumbukumbu wakati muziki ukiwa muziki.
 
Iyo Baba Style Ya Noorah Asee Si Mchezo Beat Yakee---
Jamaa Aligonga Base Apo


Sent from my iPhone using JamiiForums
Hii ngoma nimeitafutaga sana sijaipata aisee, mwenye nayo ninaomba anitumie hapa au kwa PM au hata kama ni link. Ngoma kali sana ile aisee
 
Hivi producer effector na ile lebo yake nimeisahau jina yuko wapi?

Sent using Jamii Forums mobile app
Studio ilikuwa inaitwa Serious Records ilikuwa Maili moja Kibaha nadhani. Alikuwa ndio Chief Producer akisaidiana na Marco Chali pamoja na Amba. Effector alifanya kazi kali hizo za ECT, alifanya kazi na Pig Black, akafanya ngoma ya Dark Master feat Ngwair inaitwa Dark master pia. Baadae studio ilikufa maprodusa wakatawanyika, Marco Chali nafikiri ndio akaenda Kama Kawa records ya G Solo na Amba kafungua studio yake AB records Iringa, Effector kama sikosei alikwenda tena kusoma mambo ya Sound South Africa.
 
Katika production za miaka ya karibuni nimeielewa sana ngoma yake Say Something aliyo feature na Drake.
Pia kuna moja aliitoa 2016 hivi inaitwa Dont Get No Betta, ni kali sana ina beat moja tamu sana
 
Huyu jamaa aliwagongaga beat kali sana kwenye 'itikadi zetu' ya East Cost.

Pia kuna dogo mmoja mwenye melody nzuri sana aliyefanya chorus ya itikadi zetu nadhani alikua anaitwa 'Stand boy'(kama skosei). Huyu bwana mdogo alifanyiwaga beat moja very heavy na huyo Effector kwenye wimbo wake 'sweet girl'...sijui huyu bwana mdogo alikujaga kuishia wapi

Sent from my TECNO B1f using Tapatalk
Jina la yule jamaa alikuwa anaitwa Stan Boy, kuna video aliiweka youtube mwaka 2009 akiwa USA, alikuwa anatangaza muziki wake na kusema unapatikana myspace.com ambayo kwa sasa haipo file zilikuwa corrupted zote na tovuti ikafa kabisa (hata mimi nilipoteza baadhi ya kazi zangu huko). Ukiangalia video anasema pia anapatikana facebook na site nyingine


Mbali ya track za ECT kama crew pia alifanyaga collabo na AY ile track ya mademu watafutaji
 
Ndio maana wanakushutumu kuwa wewe ni dume tena la mbegu, mwanamke anachambuaje muziki namna hii!

Au Modds mnasemaje?
Kama kweli ni mgonga code. Weledi wake wa uchambuzi unashabihiana kabisa. Hivyo anaweza kuwa ni mwanamke. Kiufupi ukishakuwa mtu wa code anakuwa na uelewa mpana wa jambo ambalo anakuwa na interest nalo.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Timberland mtu mbaya sana kwenye beat na back ground vocal.
Kwenye beat yeye na Dr. Dre wana kitu flani cha kipekee, ile ukisikia tu unajua huyu flani.

BTW, umechambua vizuri sana.
Unaijua game ya muziki kama wadada flani amazing, Salama Jabir na Dj Fetty.
Nahisi wewe ni mmoja wa hao wadada, hiyo rangi yako kwenye pic uliyo tuma, white flani kama ya Dubai na uelewa wako wa game ya music ndiyo vimenishawishi kukufaninisha na hao watu.
Timbaland ana mabalaa, anaujua muziki mpaka amepitiliza. Nafikiri ndio producer aliyeanza kutoa sample za kutumia mdomo wake (human sound) na zikawa kama accoustic safi kabisa kwenye wimbo. Mbali ya hiyo alikwa anafanya Dj-ing skills ya kuchezea nyimbo au kupandishia na wakati huo music software hazikuwa na effects au automation za kufanya kwa urahisi mambo hayo. Kuna track ya Get your Freaky On ya Missy Eliot, beat inapokaribia kumalizika anapandishia kama mara 3 hivi beat ya BUBBA SPARXXX - Ugly ambayo nayo kaitengeneza yeye mwenyewe, dah fleva yake sio ya kitoto. Wakati ule muziki wa Hip Hop umepata Crunk kama sub genre alikuja kutengeneza track ya 50 Cents ft. Justin Timberlake - Ayo Technology, zile appregiations anazijua mwenyewe na bado mwishoni ckaichezea chezea beat na kuirudisha kwenye melody ya awali, Hapo kuna ilre track ya The Game inaitwa Put you on the game, nayo alifanya beat hatari na akaichezea chezea ki-Dj. Halafu ametoka kutoa midude mikavu ya HipHop ghafla anaswitck kukupa Rehab ya Rihanna, kuna gitaa tamu sana kama lile la What's Goes Around Comes Around ya Justin Timberlake...

Tuliowahi kutumia Fruity Loops 3 moja ya tutorials ilikuwa ni beat ya Try Again ya Aaliyah..Na ukitaka kujipa stress na kukata tamaa ilikuwa uisikilize hiyo beat halafu ufananishe na unazotengeneza, unaona kama Image-Line wanataka kuua hivi, unabaki kujiuliza huyu Timbaland alifanyaje beat kama hii, mbona haiwezekani kabisa kufanywa.

Itoshe kusema Timbaland ni zaidi ya Music Producer, sio mtu wa kawaida.
 
Jina la yule jamaa alikuwa anaitwa Stan Boy, kuna video aliiweka youtube mwaka 2009 akiwa USA, alikuwa anatangaza muziki wake na kusema unapatikana myspace.com ambayo kwa sasa haipo file zilikuwa corrupted zote na tovuti ikafa kabisa (hata mimi nilipoteza baadhi ya kazi zangu huko). Ukiangalia video anasema pia anapatikana facebook na site nyingine


Mbali ya track za ECT kama crew pia alifanyaga collabo na AY ile track ya mademu watafutaji
Respect sajo

Unaweza kuwa na Sweet girl ya huyu Stan Boy?

Pia pole kwa kupoteza kazi zako sheikh

Sent using Jamii Forums mobile app
 
ebwana eeeh track ya ya 50 ile ya ayo technolog ninyokooo balaa tupuuu....
Timbaland ana mabalaa, anaujua muziki mpaka amepitiliza. Nafikiri ndio producer aliyeanza kutoa sample za kutumia mdomo wake (human sound) na zikawa kama accoustic safi kabisa kwenye wimbo. Mbali ya hiyo alikwa anafanya Dj-ing skills ya kuchezea nyimbo au kupandishia na wakati huo music software hazikuwa na effects au automation za kufanya kwa urahisi mambo hayo. Kuna track ya Get your Freaky On ya Missy Eliot, beat inapokaribia kumalizika anapandishia kama mara 3 hivi beat ya BUBBA SPARXXX - Ugly ambayo nayo kaitengeneza yeye mwenyewe, dah fleva yake sio ya kitoto. Wakati ule muziki wa Hip Hop umepata Crunk kama sub genre alikuja kutengeneza track ya 50 Cents ft. Justin Timberlake - Ayo Technology, zile appregiations anazijua mwenyewe na bado mwishoni ckaichezea chezea beat na kuirudisha kwenye melody ya awali, Hapo kuna ilre track ya The Game inaitwa Put you on the game, nayo alifanya beat hatari na akaichezea chezea ki-Dj. Halafu ametoka kutoa midude mikavu ya HipHop ghafla anaswitck kukupa Rehab ya Rihanna, kuna gitaa tamu sana kama lile la What's Goes Around Comes Around ya Justin Timberlake...

Tuliowahi kutumia Fruity Loops 3 moja ya tutorials ilikuwa ni beat ya Try Again ya Aaliyah..Na ukitaka kujipa stress na kukata tamaa ilikuwa uisikilize hiyo beat halafu ufananishe na unazotengeneza, unaona kama Image-Line wanataka kuua hivi, unabaki kujiuliza huyu Timbaland alifanyaje beat kama hii, mbona haiwezekani kabisa kufanywa.

Itoshe kusema Timbaland ni zaidi ya Music Producer, sio mtu wa kawaida.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Timbaland ana mabalaa, anaujua muziki mpaka amepitiliza. Nafikiri ndio producer aliyeanza kutoa sample za kutumia mdomo wake (human sound) na zikawa kama accoustic safi kabisa kwenye wimbo. Mbali ya hiyo alikwa anafanya Dj-ing skills ya kuchezea nyimbo au kupandishia na wakati huo music software hazikuwa na effects au automation za kufanya kwa urahisi mambo hayo. Kuna track ya Get your Freaky On ya Missy Eliot, beat inapokaribia kumalizika anapandishia kama mara 3 hivi beat ya BUBBA SPARXXX - Ugly ambayo nayo kaitengeneza yeye mwenyewe, dah fleva yake sio ya kitoto.

Tuliowahi kutumia Fruity Loops 3 moja ya tutorials ilikuwa ni beat ya Try Again ya Aaliyah..Na ukitaka kujipa stress na kukata tamaa ilikuwa uisikilize hiyo beat halafu ufananishe na unazotengeneza, unaona kama Image-Line wanataka kuua hivi, unabaki kujiuliza huyu Timbaland alifanyaje beat kama hii, mbona haiwezekani kabisa kufanywa.

Itoshe kusema Timbaland ni zaidi ya Music Producer, sio mtu wa kawaida.

Kwa maelezo haya, sajo unaujua muziki.
Respect kaka. Usiwe kama @RHONDO, yeye amekazania kujua magari na pafyumu tu!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom