Ambaye ana uzoefu na biashara za Dar-Zanzibar

We peleka mchele wako wa BAHI au Wa KAHAMA uone kama hujaumwaga baharini.

Kule ni wazee wa Bismat rice.
Mnapoizungumzia Zanzibar ya sasa mkumbuke pia kuwa kuna mchanganyiko mkubwa sana wa raia wake kwa miaka ya sasa.

Hivyo basi mchele kama wa Mbeya unauzika sana tena sana. Maharage. Sembe/dona. Na baadhi ya nafaka ambazo tumezoea zinapatikana huko bara.

Raia wa bara ni wengi huku kuliko mnavyodhani. Na hata Wazanzibar wanaojua hasa kula vyakula vyenye afya wanatumia zaidi mchele wa mbeya.

Pia huo mchele wa basmat aina nyingi ni bei ghali sio watu wengi wanaomudu izo bei sana sana wakikosa mbeya wanatumia mapembe.
 
Nataka nifanye biashara ya mayai mkula! Sema naona kwa Dar soko lipo saturated sana. Mayai ya jumla yale. Nikawaza what if naweza kuyavusha maji incase Zanzibar bado soko sio tight
Zanzibar pia mayai ni mengi. Watu wengi wanafuga.

Labda labda uangalie na majira ambayo mayai huwa yanapungua.

Au msimu wa sikukuu hasa za eid mayai huwa yanauzika sana sana. Mpaka huwa hayapatikani hasa.
 
wazenji kibao wanakuja moro kucheki mchele, wengine wanaenda hadi mbeya kuchukua mchele super, acha kudanganywa watu
Sawa wanakwenda lakini, mchele wa bara kwa zanzibar, mzunguko wake ni mdogo sana kutokana na bei yake kuwa juu, kulinganisha na hayo ma michele ya pakistani/brazili, ambayo wapemba wengi ndio wanatumia, ile super ya mbeya ikifika zanzibar si itakuwa zaidi ya 3000/- ni wangapi wenye uwezo huo??kuna kipindi nilikuja znb, nikashindwa kabisa kula wali, kila sehemu ni ule nadhani walikuwa wanauita pembe kutoka brazil!!
 
Niko katika mchakato wa kuangalia fursa za kibiashara maeneo tofauti tofauti ila nimefikia muda wa tathmini ya biashara Zenji.

Nina hamu ya kujua biashara ambazo zinashamiri za kutoka Dar kwenda Zanzibar hasa za vyakula. Naomba ushirikiano wenu ili niweze kupata tathmini halisi ya mambo ya changamoto, gharama na kodi ikibidi kwa wazoefu.

Biashara nayolenga mojawapo ni ya kusafirisha mayai ya jumla. Kutoka Dar to Zenji. Karibuni.

Hlw mimi ni mzanzibar kabisa may b i can tell you kwa mayai siyo sana ila biashara ya nyama kma unaweza kupeleka ng’ombe inshort nyama bei kubwa kilo tunanunua 9,500 mpka 10000.

Biashara nyengine ni nafaka tukisemea mchele mchele unauza sawq lakini waznz tulio wengi tunakula michele ya asia jasmin basmat mapembe na myengine bt you can try pia.

Ila mboga mboga imean tungule,viazi utauza pia sana sabab vipo bei za juu.
 
Hlw mimi ni mzanzibar kabisa may b i can tell you kwa mayai siyo sana ila biashara ya nyama kma unaweza kupeleka ng’ombe inshort nyama bei kubwa kilo tunanunua 9,500 mpka 10000
Biashara nyengine ni nafaka tukisemea mchele mchele unauza sawq lakini waznz tulio wengi tunakula michele ya asia jasmin basmat mapembe na myengine bt you can try pia
Ila mboga mboga imean tungule,viazi utauza pia sana sabab vipo bei za juu
vipi kuhusu usafirishaji
 
vipi kuhusu usafirishaji

Fatilia bandarini uko sehmu ulipo afu ss bandari ya huku unaeza kusaidia sema sijajua vizuri ila kwetu huku kuna bodi ya dawa na chakula ukifnya biashara ya kuingiza vyakula unajisajili kila mwaka ithnk unalipia laki ila bandarini wana visheria sheria bt sijaulizia maana sijawah kufnya biashara bt ulizia dar kwanza
 
Mnapoizungumzia Zanzibar ya sasa mkumbuke pia kuwa kuna mchanganyiko mkubwa sana wa raia wake kwa miaka ya sasa.

Hivyo basi mchele kama wa Mbeya unauzika sana tena sana. Maharage. Sembe/dona. Na baadhi ya nafaka ambazo tumezoea zinapatikana huko bara.

Raia wa bara ni wengi huku kuliko mnavyodhani. Na hata Wazanzibar wanaojua hasa kula vyakula vyenye afya wanatumia zaidi mchele wa mbeya.

Pia huo mchele wa basmat aina nyingi ni bei ghali sio watu wengi wanaomudu izo bei sana sana wakikosa mbeya wanatumia mapembe.

Basmati kuna aina nyingi basmat kg 2500 unanunua ambapo mbeya ni bei zaidi kidgo
 
Kuhusu mayai...funga safari nenda Zanzibar katafute mnunuzi kule mkubaliane terms na bei....cha msingi uwe serious usibip Leo unapeleka kesho hamna ..msimu wa mfungo wa ramadhani ndio unakaribia biashara ya mayai inakuwa kubwa na demand n price inapanda....kingine lazima ukubaliane na mnunuzi kuhusu kibali....elewa kuna vibali pande zote mbili za muungano huku bara unakata wizara ya kilimo...kwa kila trei ushuru wake ni 1000....
 
Kuhusu mayai...funga safari nenda Zanzibar katafute mnunuzi kule mkubaliane terms na bei....cha msingi uwe serious usibip Leo unapeleka kesho hamna ..msimu wa mfungo wa ramadhani ndio unakaribia biashara ya mayai inakuwa kubwa na demand n price inapanda....kingine lazima ukubaliane na mnunuzi kuhusu kibali....elewa kuna vibali pande zote mbili za muungano huku bara unakata wizara ya kilimo...kwa kila trei ushuru wake ni 1000....
mkuu naomba niweke sawa kidogo
vibali gan hivyo vinavyohitajika?
 
Basmati rice..

Sio kweli sana mkuu. Ule ni kwaajiri ya mapishi ya biriani. Ila unapotaka kupika pilau au wali wa kawaida then mchele mzuri ni huu wetu wa bara especially ile mbegu ya Mchele wa mbeya au shinyanga huwa inadatisha sana.
Mkuu siongei kwa kusoma maandishi.

Nimeishi Zanzibar (Unguja). Unguja usiku watu wakula Kachori, sambusa, maandazi, n.k hayo mawali wanakula watu wa bara.

Ukienda maeneo ya Bububu watu mchana wanakula urojo. Unaweza kutembea umbali wa kilomita hata 4 hujaona sehemu wanapika wali.

Sasa Kama huamini peleka huo mchele wako utuletee mrejesho.

Zanzibar usirogwe ukapeleka biashara yoyote ambayo wao wanaingiza kutokea Bara Asia.
 
Hlw mimi ni mzanzibar kabisa may b i can tell you kwa mayai siyo sana ila biashara ya nyama kma unaweza kupeleka ng’ombe inshort nyama bei kubwa kilo tunanunua 9,500 mpka 10000
Biashara nyengine ni nafaka tukisemea mchele mchele unauza sawq lakini waznz tulio wengi tunakula michele ya asia jasmin basmat mapembe na myengine bt you can try pia
Ila mboga mboga imean tungule,viazi utauza pia sana sabab vipo bei za juu
Maana yake unamshauri afungue Bucha la nyama? maana nyama huwezi iuza kama bidhaa zingine hii inahtaji Sehemu yake nikimaanisha frem kabisa.
 
Hahaha Hakuna sehemu Zanzibar nyama ya mifupa inauzwa 15,000 kwa kilo.

Acheni kudanganyana vijana.


Nyama ya mifupa mitaani kwa Bei ya leo ni 8,500 kwa kilo na Nyama ya stake ni 9,500 kwa kilo.


Hiyo Bei ya 15,000 naomba uniambie ni Zanzibar ipi
Kizimkazi, paje nyama kilo 15k.
 
Back
Top Bottom