Leo hapa jijini kunafanyika kongamano la miaka 100 tangia kuzaliwa kwa Baba wa Taifa letu, Mwl. Julius Kambarage Nyerere, 1922 huko Butiama mkoani Mara
Vijana wengi wa sasa hatukubahatika kumuona Mwl. Nyerere Bali tunamsoma tu vitabuni na kuskia masimulizi kumhusu.
Mfano:
1. Kwamba Mwl. Nyerere alipigania Uhuru wa Taifa letu
2. Kwamba Mwl. Nyerere hakutaka wazungu watuibie madini yetu na rasilimali zinginezo
3. Kwamba Mwl. Nyerere alitoa Elimu bure kwa watanzania kuanzia msingi hadi sekondari
4. Kwamba Mwl. Nyerere alijenga miundo mbinu ya reli, bandari na Barabara
5. Kwamba Mwl. Nyerere alianzisha mashirika ya Umma kama Air Tanzania, TRC, Tazara n.k
6. Kwamba Mwalimu Nyerere hakuwa na aibu kwa mafisadi wala wahujumu uchumi wa Taifa hili
7. Kwamba Mwl. Nyerere hakuwa tayari kutii maagizo ya Mabeberu.
8. Kwamba Mwalimu Nyerere ni Mzalendo aliyekuwa tayari kufa kwaajili ya Taifa lake.
Mambo hayo mazito, kuna vijana wanaodhani kwamba ni porojo, hayakufanyika na hakuna Mtanzania awezaye kuwatenda.
Tunapoadhimisha miaka100 tangia kuzaliwa Mzalendo wetu, ni dhahiri kwamba Mheshimiwa Hayati JPM ndiye Nyerere wa zama zetu.
Kama JPM aliweza kufufua mashirika ya umma, kukomesha wizi wa madini, kupitia upya mikataba ya madini, kuzuia hujuma ktk miradi ya umeme, kuhuisha reli ya kati na Tazara na ile ya Kilimanjaro, kununua meli mpya, vivuko na ndege, kukomesha ujangili wa tembo, kutumbua mafisadi, kukataa maagizo ya mabeberu na kurejesha heshima ya nchi
Ni Faraja kwamba Matendo ya Nyerere na Magufuli ni fundisho kwetu kuwa wazalendo, wachapa kazi na kuutetea Uhuru na kulinda rasilimali za Taifa.
Mwl. Nyerere alikuwa tayari kufa kwaajili ya Taifa lake, katika Hotuba nyingi za JPM, alisisitiza kwamba amejitoa mhanga kwaajili ya watanzania, alisimamia alichokiamini, alikemea mabeberu weupe na vibaraka wao, alikubali kufa kishujaa kuliko kusalim Amri.
Alisisitiza, Tutamkumbuka kwa Wema na kweli tumeanza kumkumbuka na tunaendelea kumkumbuka, hata waliimchukia wameanza kumkumbuka kutokana na hali halisi ya sasa
Nawatakia Kumbukizi njema yenye Tafakuri kwetu na kwenu mlioko hapo Ukumbini. Jifunzeni Mema ya Mwalimu na Mema ya Magufuli ili mumshauri vyema mheshimiwa Samia katika kuliongoza Taifa. Tanzania ni yetu Sote
Vijana wengi wa sasa hatukubahatika kumuona Mwl. Nyerere Bali tunamsoma tu vitabuni na kuskia masimulizi kumhusu.
Mfano:
1. Kwamba Mwl. Nyerere alipigania Uhuru wa Taifa letu
2. Kwamba Mwl. Nyerere hakutaka wazungu watuibie madini yetu na rasilimali zinginezo
3. Kwamba Mwl. Nyerere alitoa Elimu bure kwa watanzania kuanzia msingi hadi sekondari
4. Kwamba Mwl. Nyerere alijenga miundo mbinu ya reli, bandari na Barabara
5. Kwamba Mwl. Nyerere alianzisha mashirika ya Umma kama Air Tanzania, TRC, Tazara n.k
6. Kwamba Mwalimu Nyerere hakuwa na aibu kwa mafisadi wala wahujumu uchumi wa Taifa hili
7. Kwamba Mwl. Nyerere hakuwa tayari kutii maagizo ya Mabeberu.
8. Kwamba Mwalimu Nyerere ni Mzalendo aliyekuwa tayari kufa kwaajili ya Taifa lake.
Mambo hayo mazito, kuna vijana wanaodhani kwamba ni porojo, hayakufanyika na hakuna Mtanzania awezaye kuwatenda.
Tunapoadhimisha miaka100 tangia kuzaliwa Mzalendo wetu, ni dhahiri kwamba Mheshimiwa Hayati JPM ndiye Nyerere wa zama zetu.
Kama JPM aliweza kufufua mashirika ya umma, kukomesha wizi wa madini, kupitia upya mikataba ya madini, kuzuia hujuma ktk miradi ya umeme, kuhuisha reli ya kati na Tazara na ile ya Kilimanjaro, kununua meli mpya, vivuko na ndege, kukomesha ujangili wa tembo, kutumbua mafisadi, kukataa maagizo ya mabeberu na kurejesha heshima ya nchi
Ni Faraja kwamba Matendo ya Nyerere na Magufuli ni fundisho kwetu kuwa wazalendo, wachapa kazi na kuutetea Uhuru na kulinda rasilimali za Taifa.
Mwl. Nyerere alikuwa tayari kufa kwaajili ya Taifa lake, katika Hotuba nyingi za JPM, alisisitiza kwamba amejitoa mhanga kwaajili ya watanzania, alisimamia alichokiamini, alikemea mabeberu weupe na vibaraka wao, alikubali kufa kishujaa kuliko kusalim Amri.
Alisisitiza, Tutamkumbuka kwa Wema na kweli tumeanza kumkumbuka na tunaendelea kumkumbuka, hata waliimchukia wameanza kumkumbuka kutokana na hali halisi ya sasa
Nawatakia Kumbukizi njema yenye Tafakuri kwetu na kwenu mlioko hapo Ukumbini. Jifunzeni Mema ya Mwalimu na Mema ya Magufuli ili mumshauri vyema mheshimiwa Samia katika kuliongoza Taifa. Tanzania ni yetu Sote