nasrimgambo
JF-Expert Member
- Jan 10, 2017
- 1,858
- 2,348
Yote ni aina ya muziki wa kiafrika kutoka mitaani wanakoishi Waafrika wa hali ya kawaida.
Amapiano nasikia inatokea mitaa kama Soweto, Katlehong, Vosloorus ama Mamelodi huko Afrika Kusini.
Tena ulionekana muziki wa watu wa mitaani. Lakini hatimaye huu mziki umekubalika na kuigwa na watu wa mataifa mengine
ila umebakia utambulisho wa wasauzi kwasababu huu mziki unapendeza zaidi ukiimbwa kwa lugha na lafudhi za huko huko Afrika Kusini na jinsi ya kuucheza wenyewe wasauzi ndio mahodari zaidi, yani hata tuige vipi amapiano ikichezwa na msauzi ndio inapendeza zaidi.
Tukirudi singeli huu muziki nao umeanzia mitaani kabisa, ambapo tunaambiwa asili yake ni ma-emcee wa mitaani walipoanza ku 'play' isha nyimbo za taarabu kwa kasi ili zichezeke kisha wakaongezea na mitindo inayofanana na mchiriku na mdundiko.
Moja ya nyimbo zilizoinua muziki huu ni ulikuwa wimbo wa msanii msaga sumu ulioitwa Lowassa, ambao ulikuwa ni wimbo wa kampeni ya uraisi wa muheshimiwa Edward Lowassa back in 2015.
Nao kama ilivyo kwa Amapiano, singeli imekuja kuwa maarufu na sidhani kama kuna watu wa nchi nyengine wanaiwezea kuliko sisi. Japo kwenye kucheza naamini mtu wa asili yeyote anaweza icheza labda wasio Waafrika ndio watachekesha wakicheza singeli.
Ila amapiano na singeli zinaenda njia tofauti
Amapiano imeanza kuvuka toka kuwa mziki wa mitaani na kuwa mziki unaoheshimika na kuigwa kimataifa, ila singeli bado haijaanza kuigwa. Pia mashairi ya singeli yanazidi kuipoteza.
Hivi nani atachukulia serious nyimbo zinazoimba juu ya mtu anayeheshimu madanga ya mke wake kuwa ndio yanampa kula, yani uma"""lay$&a wa mke mume anajivunia.
Ama nani atachukulia serious nyimbo yenye mashairi ya kishangingi kama vile wimbo wenye mashairi ya mwanamke nyumba ndogo anayeenda kwa mke mkubwa kujitambulisha na mabendibati
Ama wimbo wa mwanamke anayeimbia juu ya ex wake huku anamtambia mwanamke mwengine kuwa kama yeye mume kwake (huyo mwanamke mwengine) basi naye ni danga lake.
Kama haitoshi singeli ya siku hizi ni video za makalio makalio makalio yani ni mata__k__ooo tu na kukata viuno nyimbo zikitoka total class less
Halafu ndio hii singeli ndio itashindana na amapiano ambayo ni mziki unaoweza imbwa, tazamwa na kuchezwa kokote na hauna mashairi na video za Konsepti za hovyohovyo
Safari ya tanzania kuwa na utambulisho wetu kama taifa ina vikwazo vingi ikiwemo hili la wasanii kukosa ubunifu na kuimbaimba mashairi ya kukenulisha meno ila in long run yanafanya miziki ionekane haina class huku ubunifu wa nje ukiendelea kuonekana kuwa ni bora kuliko wa hapa kwetu nyumbani.
Amapiano nasikia inatokea mitaa kama Soweto, Katlehong, Vosloorus ama Mamelodi huko Afrika Kusini.
Tena ulionekana muziki wa watu wa mitaani. Lakini hatimaye huu mziki umekubalika na kuigwa na watu wa mataifa mengine
ila umebakia utambulisho wa wasauzi kwasababu huu mziki unapendeza zaidi ukiimbwa kwa lugha na lafudhi za huko huko Afrika Kusini na jinsi ya kuucheza wenyewe wasauzi ndio mahodari zaidi, yani hata tuige vipi amapiano ikichezwa na msauzi ndio inapendeza zaidi.
Tukirudi singeli huu muziki nao umeanzia mitaani kabisa, ambapo tunaambiwa asili yake ni ma-emcee wa mitaani walipoanza ku 'play' isha nyimbo za taarabu kwa kasi ili zichezeke kisha wakaongezea na mitindo inayofanana na mchiriku na mdundiko.
Moja ya nyimbo zilizoinua muziki huu ni ulikuwa wimbo wa msanii msaga sumu ulioitwa Lowassa, ambao ulikuwa ni wimbo wa kampeni ya uraisi wa muheshimiwa Edward Lowassa back in 2015.
Nao kama ilivyo kwa Amapiano, singeli imekuja kuwa maarufu na sidhani kama kuna watu wa nchi nyengine wanaiwezea kuliko sisi. Japo kwenye kucheza naamini mtu wa asili yeyote anaweza icheza labda wasio Waafrika ndio watachekesha wakicheza singeli.
Ila amapiano na singeli zinaenda njia tofauti
Amapiano imeanza kuvuka toka kuwa mziki wa mitaani na kuwa mziki unaoheshimika na kuigwa kimataifa, ila singeli bado haijaanza kuigwa. Pia mashairi ya singeli yanazidi kuipoteza.
Hivi nani atachukulia serious nyimbo zinazoimba juu ya mtu anayeheshimu madanga ya mke wake kuwa ndio yanampa kula, yani uma"""lay$&a wa mke mume anajivunia.
Ama nani atachukulia serious nyimbo yenye mashairi ya kishangingi kama vile wimbo wenye mashairi ya mwanamke nyumba ndogo anayeenda kwa mke mkubwa kujitambulisha na mabendibati
Ama wimbo wa mwanamke anayeimbia juu ya ex wake huku anamtambia mwanamke mwengine kuwa kama yeye mume kwake (huyo mwanamke mwengine) basi naye ni danga lake.
Kama haitoshi singeli ya siku hizi ni video za makalio makalio makalio yani ni mata__k__ooo tu na kukata viuno nyimbo zikitoka total class less
Halafu ndio hii singeli ndio itashindana na amapiano ambayo ni mziki unaoweza imbwa, tazamwa na kuchezwa kokote na hauna mashairi na video za Konsepti za hovyohovyo
Safari ya tanzania kuwa na utambulisho wetu kama taifa ina vikwazo vingi ikiwemo hili la wasanii kukosa ubunifu na kuimbaimba mashairi ya kukenulisha meno ila in long run yanafanya miziki ionekane haina class huku ubunifu wa nje ukiendelea kuonekana kuwa ni bora kuliko wa hapa kwetu nyumbani.