Wana Jambo Forum;
Salama nawatakia, wenzangu wa humu ndani
Nadhani mtapokea, salamu zenye amani
Choveki naulizia, wenzangu mu hali gani?
Amani nawatakia, wenzangu jambo foramu
Nizitoazo muhimu, salamu toka moyoni
Muondokewe magumu, moyoni pia vichwani
Nasema pia mdumu, wenzangu wa humu ndani
Amani nawatakia, wenzangu jambo foramu
Za kheri pia baraka, pokeeni nawapeni
Ziwafikie hakika, hata ikiwa mwakani
Natuma kwa kuandika, msome humu netini
Amani nawatakia, wenzangu jambo foramu
Mwendo twasema mdundo, tusiishie mwakani
Leteni, leteni nondo, tuweze mkoma nyani
Muongezee uhondo, hapa kwetu kijiweni
Amani nawatakia, wenzangu jambo foramu
Hapa hili jungu kuu, ukoko upo kwa ndani
Twazungumza makuu, yatukerayo nchini
Hatuogopi wakuu, mradi twakoma nyani!
Amani nawatakia, wenzangu jambo foramu
Mpaka kieleweke, hapa hakuna utani
Kotini tuwapeleke, mafisadi wa nchini
Kila leo tuteseke, twaulizia kwanini?
Amani nawatakia, wenzangu jambo foramu
Saba nafika tamati, siwaagii njiani
Ni mwisho si katikati, mjue wa kijiweni
Ni nyie wana kamati, nawambiya kwaherini!
Amani nawatakia, wenzangu jambo foramu
Mwana JF,
Choveki.
Salama nawatakia, wenzangu wa humu ndani
Nadhani mtapokea, salamu zenye amani
Choveki naulizia, wenzangu mu hali gani?
Amani nawatakia, wenzangu jambo foramu
Nizitoazo muhimu, salamu toka moyoni
Muondokewe magumu, moyoni pia vichwani
Nasema pia mdumu, wenzangu wa humu ndani
Amani nawatakia, wenzangu jambo foramu
Za kheri pia baraka, pokeeni nawapeni
Ziwafikie hakika, hata ikiwa mwakani
Natuma kwa kuandika, msome humu netini
Amani nawatakia, wenzangu jambo foramu
Mwendo twasema mdundo, tusiishie mwakani
Leteni, leteni nondo, tuweze mkoma nyani
Muongezee uhondo, hapa kwetu kijiweni
Amani nawatakia, wenzangu jambo foramu
Hapa hili jungu kuu, ukoko upo kwa ndani
Twazungumza makuu, yatukerayo nchini
Hatuogopi wakuu, mradi twakoma nyani!
Amani nawatakia, wenzangu jambo foramu
Mpaka kieleweke, hapa hakuna utani
Kotini tuwapeleke, mafisadi wa nchini
Kila leo tuteseke, twaulizia kwanini?
Amani nawatakia, wenzangu jambo foramu
Saba nafika tamati, siwaagii njiani
Ni mwisho si katikati, mjue wa kijiweni
Ni nyie wana kamati, nawambiya kwaherini!
Amani nawatakia, wenzangu jambo foramu
Mwana JF,
Choveki.