Ama kweli, Tanzania itauzwa kwasababu ya mikopo

Alafu tatizo kama saa hivi ambapo mfumuko wa bei umepanda hawa wote walioingia mikataba ambayo (tuseme ukweli) wanajua wazi inatuumiza wao wanatumia misaada hii hii kujifanyia 'uwekezaji', kwa hiyo hata mafuta yafikie 5000 au kilo ya sukari ifike 7000 wao wanapata peza kutoka kwenye 'uwekezaji' wao walioufanya hivyo mzigo kuendelea kumelemea mtu wa kawaida.

Ndio maana ukihoji wako tayari hata kukuondoa maana wanadhani njia pekee ya kuwaongolea matatizo ni hiyo pekee. Ila kna njia mbadala ambayo tukikubali kujibana kwa pamoja baada ya muda unafuu utakuja sio kwa watu wote milioni 60 lakini walau 60% yao
 
JK alishawahi kuulizwa hilo swali Tanzania inakwama wapi akajibu hajui…

Km kiongozi wako anajibu hivyo na yeye yupo jikoni kilichobaki wewe lima zako mchicha siku ukiambiwa wewe ni msukule wa waarabu utakachovuna chochote kiende kwao uwe mpole tu
Duh! Kweli iko kazi !
 
JK alishawahi kuulizwa hilo swali Tanzania inakwama wapi akajibu hajui…

Km kiongozi wako anajibu hivyo na yeye yupo jikoni kilichobaki wewe lima zako mchicha siku ukiambiwa wewe ni msukule wa waarabu utakachovuna chochote kiende kwao uwe mpole tu
Tatizo lililopo ni kwamba ubadhirifu umetamalaki, kila MTU anataka ajilimbikizie Mali, na ile falsafa ya kazi na bata !!! Waziri mkuu alikuta Ofisi imejengwa kwa gharama ya milioni mia moja !! Lakini ukiiangalia hiyo ofisi haifiki hata milioni kumi !! Hiyo ni sehemu moja tu !!
 
Well said
Wanabodi,

Misaada na mikopo iliwahi kuwa mizuri katika kuleta maendeleo haswa katika kipindi cha baada ya vita vikuu vya pili vya dunia. Nchi kama Uingereza na Ufaransa zilipata maafa makubwa sana vitani na kwasababu hiyo ilibidi wapate misaada kujenga uchumi wao upya. Mpango wa misaada hii ilipewa Jina liitwalo "The Marshall plan" na ilitolewa na wamarekani kwa ajili ya nchi za ulaya magharibi. Malengo ya misaada kama hii ilikuwa kuwezesha nchi husika kujikwamua kutoka kwenye hali waliyokuwa nayo. Hadi sasa, tunashuhudia umuhimu wa kipindi hicho katika historia ya nchi hizo. Mpango huu wa Marshall ulifanikiwa kwa kiasi kikubwa katika kusaidia nchi hizi za ulaya kujikwamua kiuchumi.

Katika kipindi hiki, ilionekana kabisa kwamba misaada na mikopo inaweza kusaidia nchi yoyote kutatua changamoto zake na kuboresha maisha ya wananchi wake. Baada ya mafanikio ya Marshall plan,, mfumo kama huo ulitumika kusaidia nchi za dunia ya tatu zilizopo Afrika. Cha kusikitisha ni kwamba nchi za Afrika, zimeshindwa kutumia misaada na mikopo hii vizuri. Inawezekana kabisa kwamba deni la taifa Lime sababishwa na maamuzi mabaya haswa katika kukubali misaada na mikopo inayo semekana kuwa ya gharama nafuu.

Kuna umuhimu sana wa kuwa na nchi inayoweza kujiendesha yenyewe na kwasababu hiyo, sikubaliani na maoni ya Rais Samia ya kupata mikopo ya gharama nafuu kuendeleza miradi mbali mbali nchini, haswa ya ujenzi. Sio sahihi kukopa fedha kwa ajili ya matumizi ya kila siku na kwasababu hio ingependeza sana kama mikopo hii ingetumika katika sekta zinazo ingizia serikali faida. Kwa mfano, ujenzi wa madarasa mengi unasaidia wananchi lakini haiongezei serekali mapato yoyote na wakati wa kulipa ukifika lazima fungu litoke sehemu nyingine.

Je ni kweli kwamba serikali inakopa fedha kwasababu ina uhakika wa kupata fedha hizo baadaye?. Je changamoto kubwa katika kuendeleza miradi ni ukosefu wa fedha nyingi kwa mkupuo?. Je serikali ina "excess" ya fedha ambazo baada ya kusanywa kwa muda zinaweza kusaidia kwenye ulipaji wa madeni?
Tanzania tusipokuwa makini tutakuwa kama wenzetu Sri Lanka ambao deni la taifa halishikiki wala kukamatika.

Jamaa wanadaiwa mabilioni ya dola na China.

Wamejikuta wameshanyanganywa moja ya bandari yao kubwa na mdeni wao.

Hali ya uchumi kwa sasa nchini humoni mbaya sana.

Watu wanapanga foleni ili kupata mahitaji ya kawaida (mafuta, sukari,nk).

Watu wanakufa kwa dhiki, njaa na magonjwa.

Serikali haina akiba fedha za kigeni.

Mpaka wameanza kufunga balozi zao katika mataifa mbalimbali kama vile Iraq, Norway, and Australia, na kuanza punguza idadi ya wanadiplomasia wake katika balozi zake mbalimbali.

Karibu China itajitwalia Sri Lanka sasa ili kufidia deni lake.


Zaidi ya yote inasikitisha kuona na sisi tukipita mule mule alikopita Sri Lanka.

Serikali ya CCM, someni alama za nyakati, mshaurini M/kiti wenu, maana kazi kubwa anayoiweza kwa sasa tangu aingie madarakani ni kukopa fedha na kuzunguka na bakuli huku akidai analifungua taifa.
 
11 Reactions
Reply
Back
Top Bottom