Ama kweli, Tanzania itauzwa kwasababu ya mikopo

DaudiAiko

JF-Expert Member
Dec 2, 2012
302
274
Wanabodi,

Misaada na mikopo iliwahi kuwa mizuri katika kuleta maendeleo haswa katika kipindi cha baada ya vita vikuu vya pili vya dunia. Nchi kama Uingereza na Ufaransa zilipata maafa makubwa sana vitani na kwasababu hiyo ilibidi wapate misaada kujenga uchumi wao upya. Mpango wa misaada hii ilipewa Jina liitwalo "The Marshall plan" na ilitolewa na wamarekani kwa ajili ya nchi za ulaya magharibi. Malengo ya misaada kama hii ilikuwa kuwezesha nchi husika kujikwamua kutoka kwenye hali waliyokuwa nayo. Hadi sasa, tunashuhudia umuhimu wa kipindi hicho katika historia ya nchi hizo. Mpango huu wa Marshall ulifanikiwa kwa kiasi kikubwa katika kusaidia nchi hizi za ulaya kujikwamua kiuchumi.

Katika kipindi hiki, ilionekana kabisa kwamba misaada na mikopo inaweza kusaidia nchi yoyote kutatua changamoto zake na kuboresha maisha ya wananchi wake. Baada ya mafanikio ya Marshall plan,, mfumo kama huo ulitumika kusaidia nchi za dunia ya tatu zilizopo Afrika. Cha kusikitisha ni kwamba nchi za Afrika, zimeshindwa kutumia misaada na mikopo hii vizuri. Inawezekana kabisa kwamba deni la taifa Lime sababishwa na maamuzi mabaya haswa katika kukubali misaada na mikopo inayo semekana kuwa ya gharama nafuu.

Kuna umuhimu sana wa kuwa na nchi inayoweza kujiendesha yenyewe na kwasababu hiyo, sikubaliani na maoni ya Rais Samia ya kupata mikopo ya gharama nafuu kuendeleza miradi mbali mbali nchini, haswa ya ujenzi. Sio sahihi kukopa fedha kwa ajili ya matumizi ya kila siku na kwasababu hio ingependeza sana kama mikopo hii ingetumika katika sekta zinazo ingizia serikali faida. Kwa mfano, ujenzi wa madarasa mengi unasaidia wananchi lakini haiongezei serekali mapato yoyote na wakati wa kulipa ukifika lazima fungu litoke sehemu nyingine.

Je ni kweli kwamba serikali inakopa fedha kwasababu ina uhakika wa kupata fedha hizo baadaye?. Je changamoto kubwa katika kuendeleza miradi ni ukosefu wa fedha nyingi kwa mkupuo?. Je serikali ina "excess" ya fedha ambazo baada ya kusanywa kwa muda zinaweza kusaidia kwenye ulipaji wa madeni?
 
THE MARSHALL PLAN SUCCEEDED IN EUROPE BECAUSE THEY HAD STRONG INSTITUTIONS which are lacking in countries like Tanzania!! Kukosekana kwa taasisi zenye nguvu ndio chanzo cha matumizi mabaya ya rasilimali za nchi zinazohitajika kuleta maendeleo. Rasislimali hizo [ ziwe za ndani ya nchi au kutoka nje kama mikopo na misaada mingine], pale tu zitakapotumika vizuri kwa manufaa ya Wananchi ndio maendeleo yatakapopatikana!

Hivi sasa Samia hata atembee Dunia Nzima akiomba mikopo haitaleta maendeleo [ itakuwa sawa na kujaribu kujaza maji kwenye ndoo iliyotoboka ]bali kuwa zigo kwa Taifa kama madeni ;mpaka pale tu taasisi zote muhimu zitakapo pewa nguvu kwa kulindwa na sheria thabiti, hapo ndipo umuhimu wa kuwa na katiba mpya itakayozipa taasisi zetu nguvu unapojitokeza.

Nchi inapokuwa na taasisi zenye nguvu nchi hiyo inakuwa na Amani na ni Amani ambayo inavutia wawekezaji kuleta mitaji yao na kuwekeza. Hakuna kitu wawekezaji wanaogopa katika nchi kama istability kwani mitaji yao inaweza kuyeyuka wakati wa machafuko!!! Wawekezaji hawaji kuwekeza kwa kuangalia sura za viongozi, kwani wakiondoka madarakani bila kuwa na taasisi thabiti kunakuwa hakuna CONTUNUITY!
 
It was not until 2006, for example, that Britain fully repaid its lend-lease debts to the United States from World War II. Some international loans from the aftermath of World War I were never fully paid and were effectively put aside in 1934, though Britain also failed to recoup debts it was owed by other nations

Ilikuwa hadi 2006, kwa mfano, kwamba Uingereza ililipa kikamilifu madeni yake ya kukodisha kwa Marekani kutoka Vita Kuu ya II. Baadhi ya mikopo ya kimataifa kutoka baada ya Vita vya Kwanza vya Kidunia haikulipwa kikamilifu na iliwekwa kando mwaka wa 1934, ingawa Uingereza pia ilishindwa kurejesha madeni iliyokuwa iinazidai nchi nyingine.
 
Wewe jiulize kwann nchi kadhaa Asia zimeweza badili uchumi wao na kutoa mamillion ya watu kwenye umasikini? Hapa kwetu mamillion ya vijana hawana kazi, ma elfu ya vijana wanatoka vyuoni hawapati ajira, hamna access ya mikopo, masoko ya shida Yani wanasiasa hawana jipya zaidi ya kukopa.

Hivi kweli Huwa wanajua wanaongoza taifa la watu masikini? Kuna shida jinsi ya kupata viongozi "cream" kwenye hili taifa.
 
It was not until 2006, for example, that Britain fully repaid its lend-lease debts to the United States from World War II. Some international loans from the aftermath of World War I were never fully paid and were effectively put aside in 1934, though Britain also failed to recoup debts it was owed by other nations

Ilikuwa hadi 2006, kwa mfano, kwamba Uingereza ililipa kikamilifu madeni yake ya kukodisha kwa Marekani kutoka Vita Kuu ya II. Baadhi ya mikopo ya kimataifa kutoka baada ya Vita vya Kwanza vya Kidunia haikulipwa kikamilifu na iliwekwa kando mwaka wa 1934, ingawa Uingereza pia ilishindwa kurejesha madeni iliyokuwa iinazidai nchi nyingine.
Sifahamu source yako kwenye hili lakini lisitumike kama justification ya kupata mikopo holela bila ya kuwa na njia ya kulipa
 
Hana creativity yeyote ni MIKOPO TUUU ... nchi haiwezi kuendelea kwa mikopo mfululizo kiasi hichi, itakuja kua kama alivyosema yule mgogo.
 
Ndugai alikuwa Kama mpuliza filimbi alitumia nafas finyu iliyopatkana ya kidemokrasia kutujuza

Anajua hata huko enz za pombe nch ilikuwa inazama ila hakuweza kutoa mdomo kwa hofu ya uhai wake

Sasa n maamuz yetu kukubali nchi izame au tuzame wote kwa mikopo ya hovyo

Sawa na baba nyumban Hana plan b yoyote yet hata akikosa kuni ataenda kukopa badala ya kwenda msituni kuchanja zake

HUMO KWENYE MIKOPO NDIMO HUPATA 10% ZAO KUPITIA MIRADI YA HOVYO
 
Sifahamu source yako kwenye hili lakini lisitumike kama justification ya kupata mikopo holela bila ya kuwa na njia ya kulipa
Source yangu ni Sky News. Na Mimi sisapoti huu wazimu wa mikopo.
Mfundishe mtu kuvua samaki. Usimpe samaki.
 
Wanabodi,

Misaada na mikopo iliwahi kuwa mizuri katika kuleta maendeleo haswa katika kipindi cha baada ya vita vikuu vya pili vya dunia. Nchi kama Uingereza na Ufaransa zilipata maafa makubwa sana vitani na kwasababu hiyo ilibidi wapate misaada kujenga uchumi wao upya. Mpango wa misaada hii ilipewa Jina liitwalo "The Marshall plan" na ilitolewa na wamarekani kwa ajili ya nchi za ulaya magharibi. Malengo ya misaada kama hii ilikuwa kuwezesha nchi husika kujikwamua kutoka kwenye hali waliyokuwa nayo. Hadi sasa, tunashuhudia umuhimu wa kipindi hicho katika historia ya nchi hizo. Mpango huu wa Marshall ulifanikiwa kwa kiasi kikubwa katika kusaidia nchi hizi za ulaya kujikwamua kiuchumi.

Katika kipindi hiki, ilionekana kabisa kwamba misaada na mikopo inaweza kusaidia nchi yoyote kutatua changamoto zake na kuboresha maisha ya wananchi wake. Baada ya mafanikio ya Marshall plan,, mfumo kama huo ulitumika kusaidia nchi za dunia ya tatu zilizopo Afrika. Cha kusikitisha ni kwamba nchi za Afrika, zimeshindwa kutumia misaada na mikopo hii vizuri. Inawezekana kabisa kwamba deni la taifa Lime sababishwa na maamuzi mabaya haswa katika kukubali misaada na mikopo inayo semekana kuwa ya gharama nafuu.

Kuna umuhimu sana wa kuwa na nchi inayoweza kujiendesha yenyewe na kwasababu hiyo, sikubaliani na maoni ya Rais Samia ya kupata mikopo ya gharama nafuu kuendeleza miradi mbali mbali nchini, haswa ya ujenzi. Sio sahihi kukopa fedha kwa ajili ya matumizi ya kila siku na kwasababu hio ingependeza sana kama mikopo hii ingetumika katika sekta zinazo ingizia serikali faida. Kwa mfano, ujenzi wa madarasa mengi unasaidia wananchi lakini haiongezei serekali mapato yoyote na wakati wa kulipa ukifika lazima fungu litoke sehemu nyingine.

Je ni kweli kwamba serikali inakopa fedha kwasababu ina uhakika wa kupata fedha hizo baadaye?. Je changamoto kubwa katika kuendeleza miradi ni ukosefu wa fedha nyingi kwa mkupuo?. Je serikali ina "excess" ya fedha ambazo baada ya kusanywa kwa muda zinaweza kusaidia kwenye ulipaji wa madeni?
Kuna mega projects kama 5 zilianzishwa na Magufuli; SGR, JNHEPP, Dodoma Capital, Busisi -Kigongo, Ubungo Kibaha.

Mpaka Mwendazake anakufa hazikumalizika kujengwa. Je zinamalizwa kwa vyanzo vipi vya fedha?
 
Wanabodi,

Misaada na mikopo iliwahi kuwa mizuri katika kuleta maendeleo haswa katika kipindi cha baada ya vita vikuu vya pili vya dunia. Nchi kama Uingereza na Ufaransa zilipata maafa makubwa sana vitani na kwasababu hiyo ilibidi wapate misaada kujenga uchumi wao upya. Mpango wa misaada hii ilipewa Jina liitwalo "The Marshall plan" na ilitolewa na wamarekani kwa ajili ya nchi za ulaya magharibi. Malengo ya misaada kama hii ilikuwa kuwezesha nchi husika kujikwamua kutoka kwenye hali waliyokuwa nayo. Hadi sasa, tunashuhudia umuhimu wa kipindi hicho katika historia ya nchi hizo. Mpango huu wa Marshall ulifanikiwa kwa kiasi kikubwa katika kusaidia nchi hizi za ulaya kujikwamua kiuchumi.

Katika kipindi hiki, ilionekana kabisa kwamba misaada na mikopo inaweza kusaidia nchi yoyote kutatua changamoto zake na kuboresha maisha ya wananchi wake. Baada ya mafanikio ya Marshall plan,, mfumo kama huo ulitumika kusaidia nchi za dunia ya tatu zilizopo Afrika. Cha kusikitisha ni kwamba nchi za Afrika, zimeshindwa kutumia misaada na mikopo hii vizuri. Inawezekana kabisa kwamba deni la taifa Lime sababishwa na maamuzi mabaya haswa katika kukubali misaada na mikopo inayo semekana kuwa ya gharama nafuu.

Kuna umuhimu sana wa kuwa na nchi inayoweza kujiendesha yenyewe na kwasababu hiyo, sikubaliani na maoni ya Rais Samia ya kupata mikopo ya gharama nafuu kuendeleza miradi mbali mbali nchini, haswa ya ujenzi. Sio sahihi kukopa fedha kwa ajili ya matumizi ya kila siku na kwasababu hio ingependeza sana kama mikopo hii ingetumika katika sekta zinazo ingizia serikali faida. Kwa mfano, ujenzi wa madarasa mengi unasaidia wananchi lakini haiongezei serekali mapato yoyote na wakati wa kulipa ukifika lazima fungu litoke sehemu nyingine.

Je ni kweli kwamba serikali inakopa fedha kwasababu ina uhakika wa kupata fedha hizo baadaye?. Je changamoto kubwa katika kuendeleza miradi ni ukosefu wa fedha nyingi kwa mkupuo?. Je serikali ina "excess" ya fedha ambazo baada ya kusanywa kwa muda zinaweza kusaidia kwenye ulipaji wa madeni?
Kama tunaendekeza ile falsafa mbovu inayoitwa KAZI NA BATA ! Tujue kwamba kila pesa itakayopatikana iwe ni ya mikopo au ya Tozo na makusanyo ya ndani HAZITOTOSHA ASILANI !! wote tunaowaona waliopiga hatua kubwa za maendeleo walijifunga mikanda katika kuchapa kazi na kusahau habari ya kula BATA !!! hii nchi ina kila kitu tunakwama wapi wajameni ???!!!
 
Ndugai alikuwa Kama mpuliza filimbi alitumia nafas finyu iliyopatkana ya kidemokrasia kutujuza

Anajua hata huko enz za pombe nch ilikuwa inazama ila hakuweza kutoa mdomo kwa hofu ya uhai wake

Sasa n maamuz yetu kukubali nchi izame au tuzame wote kwa mikopo ya hovyo

Sawa na baba nyumban Hana plan b yoyote yet hata akikosa kuni ataenda kukopa badala ya kwenda msituni kuchanja zake

HUMO KWENYE MIKOPO NDIMO HUPATA 10% ZAO KUPITIA MIRADI YA HOVYO
Duh ! Salaaleeh !!
 
Ndugai alikuwa Kama mpuliza filimbi alitumia nafas finyu iliyopatkana ya kidemokrasia kutujuza

Anajua hata huko enz za pombe nch ilikuwa inazama ila hakuweza kutoa mdomo kwa hofu ya uhai wake

Sasa n maamuz yetu kukubali nchi izame au tuzame wote kwa mikopo ya hovyo

Sawa na baba nyumban Hana plan b yoyote yet hata akikosa kuni ataenda kukopa badala ya kwenda msituni kuchanja zake

HUMO KWENYE MIKOPO NDIMO HUPATA 10% ZAO KUPITIA MIRADI YA HOVYO
Hovyo kabisa output za Mh. Hayati magufuli huzioni au umetumwa wewe????!!
 
Mwaache akope tu huko kwa wazungu masuala ya kupokonyana pesa na matask force hatutaki Tena hii nchi itakuwepo hatatutakapo kufa sisi zitalipwa tu hizo pesa
 
Yule jiwe a.k a mzimu wa sukuma gang ndiyo amesababisha yote haya. Aliua biashara zote kubwa na ndogo kwa kupora fedha za watu. Vyanzo vyote vya Kodi vikafa. Akawa anakopa hovyo tena kwa siri kubwa mikopo ya kibiashara ambayo riba zake ni kubwa.

Mama hana namna, maana nchi imeachiwa matatizo na madeni makubwa na jiwe.

Mama anakopa mikopo yenye riba nafuu ili kuinusuru nchi. Asante mama.
 
Duuh kwa kweli it’s too much kwani Magufuli aliweza vipi na huyu kila siku yuko misele tu kukopa?
 
Back
Top Bottom