Alpha na Omega ya historia ya Israeli ya kale

eden kimario

JF-Expert Member
Jun 13, 2015
10,227
16,178
6697142b5bc5420b501b369313374e0d.jpg


Izrael ilianzishwa na waizraeli waliotoka nchini misri chini ya uongozi wa musa na yoshua ambae alivamia kanaani mnamo mwaka wa 1200 kk.

Muungano wa vikundi na makabila mbalimbali yasemekana ndio chanzo cha kuundwa kwa taifa moja teule chini ya sauli na baadae daudi na Solomoni mwanae Daudi.

Baada ya kifo cha solomoni mfalme mtafaruku uliibuka kiasi kwamba izrael ilipasuka vipande viwili yaani ufalme wa kazkazini ulioendelea kujiita izraeli. Na ufalme wa Yuda ambao mji mkuu wake ukikua Yerusalemu.

Kutokana na kujitenga huku falme hizi zilikosa nguvu ya kushinda vita. Na hivyo kujikuta zikiwa chini ya falme mbalimbali za babiloni uajemi na ugiriki ya kale na hii ilikua ni kuanzia mwaka 587 kk.

Lakini kuliibuka kikundi kilichojiita wamakabayo kilichoanzisha harakati za kurudisha uhuru na waliweza kuwafukuza wagiriki waliokua wakiwatawala kwa kipindi hicho na kuanzisha ufalme na kuanzisha ufalme wa kiyahudi kati ya mwaka 140 kk.

Pamoja na hilo ufalme huo uliwekwa chini ya dola la kirumi mwaka 63kk. Na hatimae kua jimbo la kiroma mwaka 70 bk.

Maangamizi ya yerusalemu mwaka 70bk yanahesabiwa kama mwisho wa Israeli ya kale
Nikukumbushe tu wakati wa ujio wa yesu izraeli na palestina zilikua chini ya dola la kirumi ambao walitawala maeneo yote ya bahari ya mediterenian.

Nimalizie tu kwa kusema izraeli ya sasa sio ile ya taifa teule la mungu. Bali ni uzao wa ashkenazi ambae ni kizazi cha uzao wa Esau. Kama unaelewa zaidi kuhusu Israel ya kale karibu uongezee ili wengine na mimi tuelewe zaidi.
 
Mkuu unajitaabisha bure! Hakuna taifa, dola, wala nchi duniani ambayo historia yake iko very clear kama taifa la Israel. Rejea maandiko ukapate kuijua historia halisi na iliyokamilika ya taifa hili la Mungu.
 
Mkuu unajitaabisha bure! Hakuna taifa, dola, wala nchi duniani ambayo historia yake iko very clear kama taifa la Israel. Rejea maandiko ukapate kuijua historia halisi na iliyokamilika ya taifa hili la Mungu.
Hivi mkuu unajua kuna izraeli 2 ?
Kuna izrael ya kale ambayo naizungumzia hapa pia unaipata kwenye bible
Lakini pia kuna hii izraeli iliozaliwa 1948 hii sii izraeli ya taifa la mungu ni izraeli nyingine kabisa
 
Hivi mkuu unajua kuna izraeli 2 ?
Kuna izrael ya kale ambayo naizungumzia hapa pia unaipata kwenye bible
Lakini pia kuna hii izraeli iliozaliwa 1948 hii sii izraeli ya taifa la mungu ni izraeli nyingine kabisa
Wewe ni Mbumbumbu na huelewi chochote kuhusu Israel,na hakuna iSRAEL mbili labda kama umekaririshwa na sheikhe wako Uchwara ambaye naye hajui chochote kuhusu Israel na kubakiza kukaririshwa kama kasuku.
 
U
6697142b5bc5420b501b369313374e0d.jpg


Izrael ilianzishwa na waizraeli waliotoka nchini misri chini ya uongozi wa musa na yoshua ambae alivamia kanaani mnamo mwaka wa 1200 kk.

Muungano wa vikundi na makabila mbalimbali yasemekana ndio chanzo cha kuundwa kwa taifa moja teule chini ya sauli na baadae daudi na Solomoni mwanae Daudi.

Baada ya kifo cha solomoni mfalme mtafaruku uliibuka kiasi kwamba izrael ilipasuka vipande viwili yaani ufalme wa kazkazini ulioendelea kujiita izraeli. Na ufalme wa Yuda ambao mji mkuu wake ukikua Yerusalemu.

Kutokana na kujitenga huku falme hizi zilikosa nguvu ya kushinda vita. Na hivyo kujikuta zikiwa chini ya falme mbalimbali za babiloni uajemi na ugiriki ya kale na hii ilikua ni kuanzia mwaka 587 kk.

Lakini kuliibuka kikundi kilichojiita wamakabayo kilichoanzisha harakati za kurudisha uhuru na waliweza kuwafukuza wagiriki waliokua wakiwatawala kwa kipindi hicho na kuanzisha ufalme na kuanzisha ufalme wa kiyahudi kati ya mwaka 140 kk.

Pamoja na hilo ufalme huo uliwekwa chini ya dola la kirumi mwaka 63kk. Na hatimae kua jimbo la kiroma mwaka 70 bk.

Maangamizi ya yerusalemu mwaka 70bk yanahesabiwa kama mwisho wa Israeli ya kale
Nikukumbushe tu wakati wa ujio wa yesu izraeli na palestina zilikua chini ya dola la kirumi ambao walitawala maeneo yote ya bahari ya mediterenian.

Nimalizie tu kwa kusema izraeli ya sasa sio ile ya taifa teule la mungu. Bali ni uzao wa ashkenazi ambae ni kizazi cha uzao wa Esau. Kama unaelewa zaidi kuhusu Israel ya kale karibu uongezee ili wengine na mimi tuelewe zaidi.
Ulichokiandika kiko kwa bible ila umetwist kidogo baadhi ya mambo. Kwa mfano, havikuwa muunganiko wa vikundi vidogo vidogo vilivyounda Israel, bali ilianzia kwa Abraham ambaye ni babu yake na Yakobo. In fact, jina Israel ni jina alilopewa Yakobo na malaika na linamaanisha "alieshindana na Mungu na akashinda". Na waisrael ni ni jumuisho la kabila 12, ambazo zote zimetokana na watoto 12 wa Jacob au Israel.
Kilichofany8ka 1948 ni kuwarudisha Waisrael kwenye their ancestral land, ambako walikuta inakaliwa na Palestinian s
 
U

Ulichokiandika kiko kwa bible ila umetwist kidogo baadhi ya mambo. Kwa mfano, havikuwa muunganiko wa vikundi vidogo vidogo vilivyounda Israel, bali ilianzia kwa Abraham ambaye ni babu yake na Yakobo. In fact, jina Israel ni jina alilopewa Yakobo na malaika na linamaanisha "alieshindana na Mungu na akashinda". Na waisrael ni ni jumuisho la kabila 12, ambazo zote zimetokana na watoto 12 wa Jacob au Israel.
Kilichofany8ka 1948 ni kuwarudisha Waisrael kwenye their ancestral land, ambako walikuta inakaliwa na Palestinian s
Swali hapa ni kua waizraeli hawa wa 1948 ndio kizazi kile cha yakobo?
 
Swali hapa ni kua waizraeli hawa wa 1948 ndio kizazi kile cha yakobo?
Kwa mujibu wa elimu na technolojia za vinasaba, na hasa matokeo yanayoambatana na project ya Human Genome, hawa wa 1948 wanashabihiana kwa kiasi kikubwa na uzao wa Jacob.
 
Ndo kusema kipindi cha yakobo hakukuwa na utawala unaitwa israel,kile kizazi cha yusufu na kaka zake waliporudi toka misri ndo waliunda utawala wa israel,maana yake ni kuwa yakobo amekufa hakujawa na israel
 
P
Swali hapa ni kua waizraeli hawa wa 1948 ndio kizazi kile cha yakobo?
Kama Ukipata muda, pitia hiyo paper, inaitwa Jewish and Middle Eastern non-Jewish populations share a common pool of Y-chromosome biallelic haplotypes
 

Attachments

  • pq006769.pdf
    237.7 KB · Views: 72
Kwa mujibu wa elimu na technolojia za vinasaba, na hasa matokeo yanayoambatana na project ya Human Genome, hawa wa 1948 wanashabihiana kwa kiasi kikubwa na uzao wa Jacob.
ila kushabihiana si lazima pawe na record ya kulinganisha mkuu,sasa DNA ya yakobo waliipata vipi labda?.
I mean kuna madai pia wapalestina wana Dna zinazoonyesha ni wazawa wa pale,nina maana kuwa,,wazungu ni uzao wa japhet,
watu wa mashariki ya kati ni uzao wa shem,
ibrahim,isaka,yakobo wote ni uzao wa shem,

sasa wapalestina wana hizo DNA kuzidi hata hao waisrael wa leo.
Na sababu ni kuwa waisrael wa leo wamechanganya mbegu na wazungu,yaani uzao wa japhet,wakati wapalestina hawakuchanya .

Nina maana kuwa yakobo na abrahamu wana DNA sawa kwakuwa asili yao wote ni shem,na hivyo yakobo kuitwa kwake israel hakukubadili muundo wake wa DNA.

Sasa hawa wayahudi wa leo hawawezi fananisha DNA na yakobo kwani wamechanganya sana na uzao wa japhet.

Labda kama kuna mwenye maelezo zaidi atatwambia hapa
 
Hawa waizrael wa 1948 waliingia palestina iliyokua inakaliwa nA waarabu na wakaigawa palestina ili taifa jipya la israel liundwe
Sasa ina maana hakukua na mipaka iliokua inatenganisha israel na palestina? Kabla hawa jamaa hawajaletwa
 
Wewe ni Mbumbumbu na huelewi chochote kuhusu Israel,na hakuna iSRAEL mbili labda kama umekaririshwa na sheikhe wako Uchwara ambaye naye hajui chochote kuhusu Israel na kubakiza kukaririshwa kama kasuku.
Acha kutoa povu hapa tunazungumzia wazawa wa yakobo ndio hawa wa sasa au hawa wa 1948 waliotoka huko ulaya ni watu wa kizazi gani cha israeli kati ya yakobo na esau
 
Kuna Jamaa anamlaumu mtoa mada wakati yeye binafsi hakuna anachofanya,kama hajuhi mueleweshe tu mkuu
 
Kwanza kabisa bwana Eden Kimario asili ya Waebrania wote ni nchi ya Iraki ambayo kipindi hicho iliitwa ufalme wa Uru. Huu ufalme ulikuwa chini ya Wakaldayo na Abrahamu alikuwa Mkaldayo.
Ushahidi wa hili ulithibitishwa na mwanahistoria wa Kiingereza Professor J.E Taylor ambaye aliuchimba huu mji mnamo mwaka 1919.


Tena wewe unavyosema kwamba Wayahudi siyo uzao wa Abrahamu napatwa na ukakasi hasa pale unaposhindwa kufuatilia mambo kwa undani na kuzama juu juu tu.
Neno WAYAHUDI au JEWS linatokana na neno JUDEANS ambao yalikuwa makabila ya YUDA na BENJAMINI yaliyounda ufalme ya YUDA mwaka 931 K.K baada ya Mfalme JEDIDIAH kufariki.

Neno WAYAHUDI lilikuwa linatumiwa sana na WARUMI ambapo walilitumia kuwatenganisha wazao wa Ufalme wa YUDA waliloridishwa kutoka utumwa wa Waajemi. Hili lilitumika ili kuwatenganisha na kabila Wasamaria ambao walichanganyika pamoja na watu wenye asili ya ufalme wa Ashuru (Assyrians). Wayahudi walijitenga pamoja na Wasamaria kwasababu walikuwa wanaabudu dini za kipagani na huku wakimuamini YAHWEH kama ilivyoandikwa kwenye Torati. Na Wayahudi waliamini ni wao pekee ndiyo wana haki ya kutoa sadaka kwa JEHOVAH na siyo watu wengine; hivyo waliwachukia sana Wasamaria.

Ukisoma Torati yote hakuna sehemu ambapo neno WAYAHUDI limetajwa, ila ni Waebrania, Wana wa Israel na WANA WA YUDA na siyo WAYAHUDI.

Kitu cha muhimu kukumbuka ni kwamba Ufalme wa Israel uliundwa na makabila kumi na mawili ambao ulikuwa ni uzao wa Yakobo ambaye YAHWEH alimpa jina ISRAEL. Katika watoto wa Yakobo hakuna kabila la YUSUFU ila watoto wake wawili ambao ni EPHRAIM na MANASSEH.
Sasa ikumbukwe kwamba YUSUFu alipouzwa Misri alipewa mke na Farao. Mke wake alikuwa anaitwa ASENATHI ambaye alikuwa ni mtu wa MISRI. Ufalme wa Misri ulikuwa na wa watu WEUSI hivyo ASENATHI alikuwa ni mtu MWEUSI. Hivyo taifa la ISRAEL lilikuwa na mchanganyiko wa damu nyingi.

Lakini wewe umeona Wayahudi kuchanganyika na Wazungu wa Ulaya Mashariki ni tatizo sana hadi utake kuamini falsafa za kupuuzi zianzoendeshwa hapa duniani. Halafu unaongopa ulivyosema taifa la sasa la Israel linatengenezwa na ASHEKINAZI Jews pekee, hili siyo kweli hata kidogo.
Kuna Wayahudi ASHEKINAZI hawa walitokea Ulaya Mashariki kwenye Ufalme wa KHAZAR; kuna Wayahudi SEPHARDIM hawa walibaki Palestina baada ya Wayahudi kufukuzwa na Masultani wa Kiarabu; kuna Wayahudi FALASHA ambao walikuwa wanaishi kwenye utawala wa SHEBA, ABYSSINIA au ETHIOPIA.

Hawa wote rangi hata maumbile ya mwili zimetofautiana lakini baada ya kupimwa DNA wamekutwa wana undugu mkubwa kuliko unavyotaka wewe kutuaminisha. Mbali kabisa WAYAHUDI wako dunia nzima mfano mkubwa wa makabila ya KIYAHUDI duniani ni:

  1. IGBO huko Nigeria.
  2. WAHINDI WEKUNDU wa Colorado huko Marekani.
  3. WAHINDI WA KERALA, MUMBAI, KARACHI huko INDIA. (Kati ya hawa kuna wafanyabiashara wengi wa mfalme JEDEDIAH)
  4. BAADHI YA NEGROES wa Marekani ni WAYAHUDI walioishi katika ufalme wa MALI.
  5. WAAJEMI WENGI WA IRAN ni WAYAHUDI kutoka PARTHIAN EMPIRE.
Na haya yote yamefanyiwa sana uchunguzi na wanasayansi wa mataifa mbalimbali.
Sasa kuchanganyika kwa Wayahudi na Wazungu kuwaje tatizo kwako leo?
Wewe mama yako akiwa ni Mchagga baba yako akawa Mkinga wewe utaitwa MCHAGGA?


Najua WAZAYUNI wanaharibu dunia lakini tusitumie hii fimbo kuwachukia hata WAYAHIDI wasio na hatia bila sababu. Huwezi kumkatalia mtu urithi wake hata kidogo WAYAHUDI na WAPALESTINA ni ndugu kuliko wewe unavyodhani.
Hili huwezi badilisha hata kidogo na Ukweli utabaki kuwa hivyo.



 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom