Baba Mtu
JF-Expert Member
- Aug 28, 2008
- 870
- 168
Wana-jf juzi nilinunua losheni iitwayo CLAIRMEN FOR MEN. Kabla sijanza kuitumia nilisoma ingredients zake na jinsi ya kuitumia, nikakuta kuwa sitakiwi nikae juani pindi nitakapopakaa hiyo losheni. Nilistuka kidogo na kujiuliza itakuwaje ikiwa ntalazimika kutembea juani. Niliamua kutembelea website ya TFDA (mamlaka ya chakula na dawa tanzania) na kuperuzi, nikaona kuwa CHLOROQUINONE NA JAMII ZAKE ZOTE ZIMEPIGWA MARUFUKU; na hiyo losheni ya claire for men ina hydroquinone ndani. Kana kwamba hiyo haitoshi nikaperuzi katika google na kuona madhara ya hydroquinone, nikachoka na kuchoka. Nitaendelea kupakaa mafuta ya nazi kama yale alokuwa akipaka bibi na babu enzi zile kwani haya mafuta ya kisasa ni hatari kwa afya yangu.
Nawaasa wana-jf na jamii kwa jumla tuwe tunasoma maelezo yaliyo katika bidhaa tuzinunuazo kabla ya kuanza kuzitumia, ukiona kuna kitu huelewi uliza kwa daktari aliye karibu nawe.
Nilichokiona katika mitandao ni hiki hapa katika links hizi:
1. TANZANIA FOOD AND DRUGS AUTHORITY
2. UK Skin Lightening - Hydroquinone Skin Bleaching
3. Banned Skin Bleaching / Skin Whitening products
4. Hydroquinone Side Effects Revealed. Discover the Truth.
5. The Truth About Hydroquinone by MedicineNet.com
6. hydroquinone topical medical facts from Drugs.com
Nawaasa wana-jf na jamii kwa jumla tuwe tunasoma maelezo yaliyo katika bidhaa tuzinunuazo kabla ya kuanza kuzitumia, ukiona kuna kitu huelewi uliza kwa daktari aliye karibu nawe.
Nilichokiona katika mitandao ni hiki hapa katika links hizi:
1. TANZANIA FOOD AND DRUGS AUTHORITY
2. UK Skin Lightening - Hydroquinone Skin Bleaching
3. Banned Skin Bleaching / Skin Whitening products
4. Hydroquinone Side Effects Revealed. Discover the Truth.
5. The Truth About Hydroquinone by MedicineNet.com
6. hydroquinone topical medical facts from Drugs.com