Ally M. Keissy (MP) - Michango ya harusi itozwe kodi

Uswe

JF-Expert Member
Nov 1, 2010
2,204
626
Akichangia hoja leo bungeni, Ally Mohemed Keissy mbunge wa Nkasi Kaskazini kwa ticket ya CCM ameshauri harambee zote au michango yote, ikiwepo michango ya makanisa, misikiti, harusi au chochote ili mradi watu wanachangia pesa basi itozwe kodi.

Pia aliitaka serikali ipeleke matangazo yake YOTE TBC ili kukijengea uwezo kituo hicho, amesema hata serikali ya uingereza hupeleka matangazo BBC

kujua zaidi kuhusu mh keissy, soma cv yake hapa Parliament of Tanzania
 
mi mwenyewe nashauri sadaka ziwe zinatozwa kodi na pia CAG awe anapita huko. maana zile ni pesa za umma isije ikawa wakina lusekelo wanajitajirisha tu.
 
Hatukatai ila sio sababu ya kujiongeza marupurupu na safari za kila siku.
 
Nyumba za vigogo masaki walipe kodi. Mmachinga Ana maduka mtaji laki mbili faida elfu hamsini kwa mwaka wao masaki wanapangisha kwa dolari $ au hawaoni hili
 
aache ubwege hizo posho za wabunge zinakatwa kodi? waanze na wao kwanza tena wao ndio mabingwa mwl anakatwa karibu 28% ya mshahara kisa hana TIN no.mbuge kwa sababu ana biashara only 5%.
 
Huyu mzee anapenda sana umaarufu wa kijinga. Nahisi mchawi ndiyo maana anapga vita mambo ya imani.
 
Mhe Peter Msigwa " Viongozi wa serikali ya CCM na wabunge wao wana akili zilizodumaa na Chama chao cha CCM kimechakaa. Nakubaliana nae, maana huyu Mbunge Kessy pamoja na utumbo huo wenzake walimshangilia sana.
 
Akichangia hoja leo bungeni, Ally Mohemed Keissy mbunge wa Nkasi Kaskazini kwa ticket ya CCM ameshauri harambee zote au michango yote, ikiwepo michango ya makanisa, misikiti, harusi au chochote ili mradi watu wanachangia pesa basi itozwe kodi.

Pia aliitaka serikali ipeleke matangazo yake YOTE TBC ili kukijengea uwezo kituo hicho, amesema hata serikali ya uingereza hupeleka matangazo BBC

kujua zaidi kuhusu mh keissy, soma cv yake hapa Parliament of Tanzania

Huyu mchizi kumbe hata darasa la saba hakumaliza, angesoma huyu balaa lake lingekuwa kubwa. Michango ya harusi isitozwe kodi ifutwe kabisa.
 
CCM bwanaa kila penye hela lazima mtie neno, mwishowe tutaambiwa ukipita rami lazma utoe kodi... mi nipo hawa jamaa ka watachukua nchi tena kazi tutakua nayo WA TZ.
 
Nadhani CV inajieleza vizuri pamoja na hayo uelewa na ufahamu ni sufuri-A(0).
Aongezee hata rambirambi zitozwe kodi.
Viongozi wetu hawa, shame on them.
Wafanyabiashara wakubwa, wawekezaji wakubwa wa nje wanapewa misamaha ya kodi huyu sufuri-A(0) anakuja kuongea ujinga wake, eti nae mi kiongozi??
CCM ni janga.
 
Huyu mchizi kumbe hata darasa la saba hakumaliza, angesoma huyu balaa lake lingekuwa kubwa. Michango ya harusi isitozwe kodi ifutwe kabisa.

dah SoNotorius, umenichekesha sana leo. nafikiri std 7 amemaliza mkuu, labda secondary ndo hakufika, kama kilichoandikwa katika mtandao wa bunge ni sahihi.

My Take
Huyu jamaa, wakati anachangia akili yake haikua inawaza zaidi ya M4C. haikua amewaza kuhusu michango mingine ya hiari, fikiri kazi nzuri ya vipindi kama njia panda and other charity contributions, eti kuna MP anataka zitozwe kodi, tu kwa sababu anataka kuikamata chadema....ubunge wa aina hii ni hatari!
 
Nyumba za vigogo masaki walipe kodi. Mmachinga Ana maduka mtaji laki mbili faida elfu hamsini kwa mwaka wao masaki wanapangisha kwa dolari $ au hawaoni hili

niliwahi kusema, tuwe na kiwango cha chini cha elimu mtu kuwa mbunge, mfano lazima na form six or equivalent, kuiacha wazi, kwamba hata std 7 anaweza kuwa mbuge, tutegemee michango ya hivi kwa miaka mingi ijayo
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom