Ally Bananga: Nikifika mbinguni (peponi) nikikuta Mama Samia hayupo natoka peponi

mtoto wa mchungaji

JF-Expert Member
Oct 24, 2020
279
480
Kunausemi unasemaga ukistaajabu ya Musa.

Leo katika jiji la Arusha aliyekuwa kamanda wa chama cha Demcrasia na Maendeleo Chadema Ally Bananga alirudisha kadi ya chama hicho katika mkutana mkubwa wa adhala wa Raisi wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania mama Samia Hassan, Kamanda huyo wa zamani ametoa kauli ya ajabu na kushangaza.

Pamoja na kuongea vizuri katika hotuba yake kisiasa lakini ametoa kauli ya ajabu sana hasa kwetu sisi viongozi wa dini imetupa ukakasi mkubwa sana kwa ndugu huyo. Bananga amesema kuwa kama akifika mbinguni na kukuta mama Samia hayupo huko peponi atatoka huko peponi yeye. Sijui atatoka kumtafuta wapi.

Kauli hii nzito na yakushangazana ya kipagani na ya fedhea kwa Mungu wetu imeleta gumzo katika makundi yetu mengi ya wasapu ya viongozi wa dini wakiwemo wachungaji, mashekh, maaskofu, mitume na manabii. Katika haya magrupu viongozi wengi wamebaki midomo wazi na wengine kutatoa macho kanakwamba wanatengeneza saa kwa kukosa pakuanzia kujadili.

Kwa msikilizaji wa kufikiri na akili aliyekuwa anamsikiliza Bananga katika hotuba yake alikuwa kama au likuwa anafanya intavyuu ya kuomba kazi kwa Mhs. Rais na si vinginevyo. Katika maongezi yake alionyesha uzoefu wake wa kazi kuwa anaweza na amekaa katika uongozi kwa vipindi kadhaa na amefanya kadha wa kadha ikiwemo uwazishwaji wa jambo fulani. Alizidi kwenda mbali kwa kusema anauwezo wa kufanya mambo magumu na mchapakazi hivyo anaomba asiachwe benchi atumike katika serikali.

Bananga ambaye mara nyingi amekuwa akitishia kurudisha kadi hiyo ya Chadema lakini leo ametumia mwanya huo kama fulsa kurudisha kadi hiyo na kuomba kazi kwani amekuwa benchi kwa muda sasa kisiasa ukilinganisha na mkewe kuwa mbunge wa viti maarumu kupitia Chadema.

Bananga ambaye Mungu amempa neema ya kutembelea upepo kwani zamani alikuwa mwanachama mtiifu wa CCM na baada ya kuona chama hicho ilikuwa ikidorola mika ya 2013 alibadili gia na kuhamia Chadema, lakini leo kilichotokea CCM kinatokea Chadema hivyo anabadili tena gia na kurudi CCM kusaka fulsa kama alivyosikika katika hotuba yake ya kuombakazi.

Mimi kama mtumishi wa Mungu namshauri Bananga kuomba kitubio kwa Mwenyezi Mungu kwa kauli yake ya kibuli cha uzima, kauli yake ni chukizo kwa Mungu kwani haikubaliki kanisa, haikubaliki msikitini na haikubaliki hata kindagateni mpaka chuo kikuu.
 
Mtume S.a.w alitutahadharisha sana kupenda (kujipendekeza) kupitiliza kwa kuwa utajikuta unakufuru tu!

Huyu Mtoto anadhan issue ya Kuingia Peponi ni kama kuingia Bungeni tu

Swahaba Mkubwa sana wa Bw. Mtume s.a.w ambae alikuwa Mweusi (Bilal bin Rabbah) alisema hata akiwa kishaingiza Mguu mmoja ndani ya Pepo bado hatokuwa na uhakika wa kuingia Peponi lakin anatokea mtu kwa kujipendekeza tu anakufuru kwa kumpa Mungu Masharti eti akitaka kumuingiza Peponi lazima na fulani nae aingie…

vyeo vya Kidunia vinaishia huku huku huko hakutakuwa na mambo ya 'kupita bila ya kupingwa'
 
Hata kama ni kujipendekeza lakini sio kwa maneno haya!

Angesifia yote mazuri aliyofanya. Mfano 1.5T ilivyogawanywa kwenye maendeleo, uhuru wa vyombo vya habari, Kukemea TRA kutokutumia nguvu kwenye ukusanyaji wa kodi na n.k

Haya mambo ya peponi hata huyo unayemsifia anaweza kuona huyu ni wale “handle with care”!!
 
Bananga ni nani? nisaidie, elimu yake, anafanya nini etc
Ni mhuni mmoja tu wa hapo Mbauda hana jipya mke wake ni mmoja wa wale covid 19 walipo mle bungeni kinyume cha sheria.

Huwa anaburuzwa sana na mkewe baada ya kukosa ulaji (alichukua form kugombea ubunge Arusha kupitia CDM ila Lema ndie aliepitishwa) na hana mishe yoyote zaidi ya kulewa bar asubuhi mpaka usiku.

Binafsi namfahamu vizuri tu maana nimezaliwa na kukulia mtaa moja na yeye.
 
Back
Top Bottom