mtoto wa mchungaji
JF-Expert Member
- Oct 24, 2020
- 279
- 480
Kunausemi unasemaga ukistaajabu ya Musa.
Leo katika jiji la Arusha aliyekuwa kamanda wa chama cha Demcrasia na Maendeleo Chadema Ally Bananga alirudisha kadi ya chama hicho katika mkutana mkubwa wa adhala wa Raisi wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania mama Samia Hassan, Kamanda huyo wa zamani ametoa kauli ya ajabu na kushangaza.
Pamoja na kuongea vizuri katika hotuba yake kisiasa lakini ametoa kauli ya ajabu sana hasa kwetu sisi viongozi wa dini imetupa ukakasi mkubwa sana kwa ndugu huyo. Bananga amesema kuwa kama akifika mbinguni na kukuta mama Samia hayupo huko peponi atatoka huko peponi yeye. Sijui atatoka kumtafuta wapi.
Kauli hii nzito na yakushangazana ya kipagani na ya fedhea kwa Mungu wetu imeleta gumzo katika makundi yetu mengi ya wasapu ya viongozi wa dini wakiwemo wachungaji, mashekh, maaskofu, mitume na manabii. Katika haya magrupu viongozi wengi wamebaki midomo wazi na wengine kutatoa macho kanakwamba wanatengeneza saa kwa kukosa pakuanzia kujadili.
Kwa msikilizaji wa kufikiri na akili aliyekuwa anamsikiliza Bananga katika hotuba yake alikuwa kama au likuwa anafanya intavyuu ya kuomba kazi kwa Mhs. Rais na si vinginevyo. Katika maongezi yake alionyesha uzoefu wake wa kazi kuwa anaweza na amekaa katika uongozi kwa vipindi kadhaa na amefanya kadha wa kadha ikiwemo uwazishwaji wa jambo fulani. Alizidi kwenda mbali kwa kusema anauwezo wa kufanya mambo magumu na mchapakazi hivyo anaomba asiachwe benchi atumike katika serikali.
Bananga ambaye mara nyingi amekuwa akitishia kurudisha kadi hiyo ya Chadema lakini leo ametumia mwanya huo kama fulsa kurudisha kadi hiyo na kuomba kazi kwani amekuwa benchi kwa muda sasa kisiasa ukilinganisha na mkewe kuwa mbunge wa viti maarumu kupitia Chadema.
Bananga ambaye Mungu amempa neema ya kutembelea upepo kwani zamani alikuwa mwanachama mtiifu wa CCM na baada ya kuona chama hicho ilikuwa ikidorola mika ya 2013 alibadili gia na kuhamia Chadema, lakini leo kilichotokea CCM kinatokea Chadema hivyo anabadili tena gia na kurudi CCM kusaka fulsa kama alivyosikika katika hotuba yake ya kuombakazi.
Mimi kama mtumishi wa Mungu namshauri Bananga kuomba kitubio kwa Mwenyezi Mungu kwa kauli yake ya kibuli cha uzima, kauli yake ni chukizo kwa Mungu kwani haikubaliki kanisa, haikubaliki msikitini na haikubaliki hata kindagateni mpaka chuo kikuu.
Leo katika jiji la Arusha aliyekuwa kamanda wa chama cha Demcrasia na Maendeleo Chadema Ally Bananga alirudisha kadi ya chama hicho katika mkutana mkubwa wa adhala wa Raisi wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania mama Samia Hassan, Kamanda huyo wa zamani ametoa kauli ya ajabu na kushangaza.
Pamoja na kuongea vizuri katika hotuba yake kisiasa lakini ametoa kauli ya ajabu sana hasa kwetu sisi viongozi wa dini imetupa ukakasi mkubwa sana kwa ndugu huyo. Bananga amesema kuwa kama akifika mbinguni na kukuta mama Samia hayupo huko peponi atatoka huko peponi yeye. Sijui atatoka kumtafuta wapi.
Kauli hii nzito na yakushangazana ya kipagani na ya fedhea kwa Mungu wetu imeleta gumzo katika makundi yetu mengi ya wasapu ya viongozi wa dini wakiwemo wachungaji, mashekh, maaskofu, mitume na manabii. Katika haya magrupu viongozi wengi wamebaki midomo wazi na wengine kutatoa macho kanakwamba wanatengeneza saa kwa kukosa pakuanzia kujadili.
Kwa msikilizaji wa kufikiri na akili aliyekuwa anamsikiliza Bananga katika hotuba yake alikuwa kama au likuwa anafanya intavyuu ya kuomba kazi kwa Mhs. Rais na si vinginevyo. Katika maongezi yake alionyesha uzoefu wake wa kazi kuwa anaweza na amekaa katika uongozi kwa vipindi kadhaa na amefanya kadha wa kadha ikiwemo uwazishwaji wa jambo fulani. Alizidi kwenda mbali kwa kusema anauwezo wa kufanya mambo magumu na mchapakazi hivyo anaomba asiachwe benchi atumike katika serikali.
Bananga ambaye mara nyingi amekuwa akitishia kurudisha kadi hiyo ya Chadema lakini leo ametumia mwanya huo kama fulsa kurudisha kadi hiyo na kuomba kazi kwani amekuwa benchi kwa muda sasa kisiasa ukilinganisha na mkewe kuwa mbunge wa viti maarumu kupitia Chadema.
Bananga ambaye Mungu amempa neema ya kutembelea upepo kwani zamani alikuwa mwanachama mtiifu wa CCM na baada ya kuona chama hicho ilikuwa ikidorola mika ya 2013 alibadili gia na kuhamia Chadema, lakini leo kilichotokea CCM kinatokea Chadema hivyo anabadili tena gia na kurudi CCM kusaka fulsa kama alivyosikika katika hotuba yake ya kuombakazi.
Mimi kama mtumishi wa Mungu namshauri Bananga kuomba kitubio kwa Mwenyezi Mungu kwa kauli yake ya kibuli cha uzima, kauli yake ni chukizo kwa Mungu kwani haikubaliki kanisa, haikubaliki msikitini na haikubaliki hata kindagateni mpaka chuo kikuu.