Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 21,050
- 50,997
KAULI YA BANANGA INATISHA; "MWIZI KARUDISHA VITU VYETU ALAFU ANALAZIMISHA TUMSIFU"
Na, Robert Heriel
Moja ya watu waliotisha siku ya jana kwenye mkutano wa Kampeni wa CHADEMA huko Tabata Segerea ni pamoja Ally Bananga. Sikuwahi kumjua huyu Bananga, siku ya jana ndio nimemuona na kumsikia. Hakika huyu ni mtu muhimu sana kwa CHADEMA kwa wakati huu. CHADEMA mchukueni huyu mtu, angalau apewe Dakika kumi au kumi na tano kabla ya saa kumi na moja.
Kauli zote za Bananga ni muhimu, Kauli zote za Bananga zinashtua ubongo uliolala. Kauli zote za Bananga zinahamasisha, zinachangamsha, zinatia uchungu, na pia zinamfanya msikilizaji achukue hatua.
Bananga kila alichoongea kiliingia katika akili ya aliyekisikia. Ni watu wachache kama Bananga wenye uwezo wa kuwasilisha hoja kwa namna yake.
Kwa Mujibu wa Bananga, ameomba Muongozo kwa Mgombea wake wa Urais, kisha na wasikilizaji waliokuwa wakimsikia kuwa; Mwizi karudisha vitu alivyotuibia, alafu analazimisha tumsifu, hiyo imekaaje.
Bananga anajaribu kuzishtua akili za wasikilizaji kuwa, Mambo mengi ambayo CCM wameyasema wameyafanya yalikuwepo, ametoa mfano wa ndege, treni na reli,
Bananga anasema, mambo hayo yalikuwepo lakini yaliuawa na haohao CCM, kisha leo wanarudisha vitu vilivyokuwepo wanajisifu. Hiyo imekaaje.
Kuhusu Ndege sikuwepo, lakini Treni ya kaskazini nilikuwepo kipindi ikiwa inafanya kazi zake. Baadaye Treni ile iendayo Moshi ilikufa chini ya utawala uliowekwa na CCM. Sasa kitendo cha Serikali ya awamu hii chini ya CCM kusema imeleta maendeleo katika ufufuaji wa Reli iliyokufa chini ya utawala wao huohuo wa CCM, ni mfano wa mwizi kukurudishia kitu alichokuibia kisha akalazimisha umsifu.
Hii ni kama muda huu ambapo serikali ya awamu hii imesitisha nyongeza ya mishahara kwa wafanyakazi wa serikalini alafu baadaye serikali hiyo hiyo iongeze mishahara ambayo yenyewe ilisitisha nyongeza alafu ilazimishe kusifiwa.
Ni sawa na mtu anayekupiga kofi kisha anakubembeleza kisha anajisifu kwa kukubembeleza.
Au ni sawa na mtoto umchape kisha umpe pipi ya kumrubuni ili anyamaze.
Au ni sawa na Mwizi kakuibia Gari Kisha anakurudishia akiwa kalipaka rangi muda huo umechapika. Alafu anajisifu nimelipaka rangi, hasemi yeye ni mwizi wala haombi samahani kwa kukuibia hamna yeye anajisifu kakurudishia gari lako.
Ally Bananga apewe Dakika 10 hadi 15 kuongea, anaweza kuwafikisha CHADEMA Somewhere. Jamaa anajua kuongea, anajua kuhamasisha.
Nashukuru CHADEMA kwa kuweza kufuata baadhi ya ushauri wangu wa namna ya kuwasilisha hoja zenu Jukwaani. Kule Segerea Mlifanya vizuri kwa 80%.
Tafuteni kama kina BANANGA 3
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300