ADC Party
Member
- Sep 14, 2020
- 28
- 29
Chama Cha Alliance for Democratic Change (ADC) kupitia Mgombea wake wa Kiti cha Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Bi. Queen Cuthbert Sendiga, kinapenda kukuletea taarifa ya muendelezo wa Kampeni zake kuelekea tarehe 28/10/2020 huku akiwa mgombea mwanamke pekee kuanza kampeni zake hizi.
Kesho Jumatano, tarehe 16 Septemba atazindua kampeni zake Mjini Pemba - Zanzibar katika viwanja vya Shame Mmata, Soko la Mjini Micheweni.
Mgombea wetu ameshaanza kampeni na huu utakuwa ni mkutano wake wa tatu. Miwili aliifanya visiwa vya Unguja.
Mkutano wa kwanza ulizinduliwa pamoja na Ilani ya uchaguzi 2020-2025 siku ya tarehe 11/09/2020 katika viwanja vya Mnazi Mmoja huko Unguja. Mkutano wa Pili ulifanyika siku ya tarehe 13/09/2020 huko Unguja kusini, Makunduchi.
Tunapenda kutoa shukrani za dhati kwa support kubwa mnayompa mgombea wetu
Imetolewa na
Devilsi Method
Meneja wa Kampeni
ADC DIRA YA MABADILIKO