Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,906
- 22,027
Alizwa Pesa na Hawara, Arudi Kwa Mkewe Kuomba Radhi | |
Tuesday, July 26, 2011 6:09 PM HASSAN ABDUL [39] mkazi wa Sinza jijini Dar es Salaam, amemuangukia mke wake kwa kutembea kwa kutumia magoti kwa lengo la kuomba radhi baada ya kufilisiwa na kuibiwa fedha na aliyekuwa hawara yake | |
Hatua hiyo ya kuomba radhi imekuja baada ya mwanaume huyo kugundua kuwa alikuwa ameibiwa fedha kiasi cha shilingi milioni ishirini na tano na mwanamke aliyekuwa na uhusiano nae wa kimapenzi aliyemtaja kwa jina la Husna [27] kwa kuiba kadi ya ATM na kwenda kuiba fedha hizo na kutimkia kusikokujulikana. Mwanamke huyo aliiba kadi ya kutolea fedha bila mwanaume huyo kutambua kwa kuwa siku aliyoiba alizidiwa na kinywaji na kufanikiwa kwenda kutoa fedha hizo na kutimka nazo kusikojulikana. Abduli alidai kuwa, mwanamke huyo alifanikiwa kuiba fedha hizo kwa kuwa alikuwa anafahamu namba yake ya siri na mara kwa mara huitumia kwa kuwa walikuwa wakiaminiana na kudai hata namba ya siri ya kadi ya mwanamke huyo alikuwa anaifahamu. Mara baada ya mwanamke huyo kutoa fedha hizo alirudisha kadi hiyo nyumbani kwake ili mwanaume huyo akija aikute na kuchukua vitu muhimu ambavyo aliona vingemsaidia na kuacha kila kitu kama kilivyo ndani ya chumba hicho na kutokomea mitaani. Hatua hiyo ya kuomba radhi imekuja baada ya baadhi ya marafiki wa karibu na Abduli kumpa hongera mke wa Abduli kwakuwa Abduli alinunua shamba na kiwanja kwa wakati pamoja na pia walimtaka mke huyo wa Abduli awe makini na mkopo aliyochukua Abduli. Ndipo mke huyo Khadija [29] aliyebahatika kuzaa nae watoto wapatao wawili alipofahamu mambo hayo na kumbana mume wake kuhusu manunuzi ya viwanja hivyo ikiwemo na mikakati ya kutumia mkopo huo. Ndipo Abduli hakuwa na cha kuongea kuhusiana na fedha hizo kwa kuwa hawara yake alishamuibia ikiwemo na hati ya manunuzi ya shamba ambalo alikuwa amemnunulia. Abduli aliitisha kikao cha wazee na kumuomba radhi mke wake na kufafanua jinsi alivyoibiwa fedha hizo na kufafanua hati ya kiwanja ameihifadhi na kubainisha shamba alikuwa amemnunulia mwanamke huyo ambaye amemuibia kwa kuwa alikuwa na ujauzito wake. Hata hivyo mke wa Abduli alilia kwa uchungu kusikia maneno hayo na ghafla alianguka chini na kupoteza fahamu kwa dakika kadhaa na kupelekea awahishwe zahanati kwa matibabu. Haijajulikana kama mke wa Abduli amekubali kumsamhehe mumewe kwa aliyoyafanya au la. |