Katika hali ya kuonyesha CCM hapako shwari leo mkuu wa Wilaya Gabriel Kimolo amevua gamba na kuvaa Gwanda hii leo ni kwenye Kongamano linaloendelea muda huu katika hotel ya Land mark ambapo wangeni rasmi ni Tundu Lisu, Mnyika, Lema, Msigwa, Heche na Kilewo.
Akiongea na watanzania waliojana kwenye kongamano hilo Kimolo amesema CCM inakufa na kuna kila ishara za CCM kufa mfano kuuwa waandishi wa habari, kutesa wana harakati, kutumia nguvu nyingi kuzoofisha upinza hasa CHADEMA pia amewaomba watanzania kujiunga na chadema kwani kwasasa ni tumaini la watanzania na kuna kila ishara kuwa inaenda kuongoza nchi...
Nawasilisha
============
Gabriel Kimolo, alijiuzulu mwezi Mei 2012 (Ref
https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/262111-mkuu-wa-wilaya-ya-mbozi-atangaza-kujiuzulu.html ) kufuatia madai kuwa alikuwa akikejeliwa na wafanyabiashara wakimwita Mbwa!