Jembe Jembe
JF-Expert Member
- Jun 9, 2016
- 749
- 1,797
Mamia ya wakazi wa jimbo la Arumeru Magharibi wilaya ya Arumeru Mkoa wa Arusha mapema jana wamejitokeza kumzika aliyewahi kuwa mbunge wa jimbo hilo Marehemu Elisa David Mollel aliyefariki kwa ugonjwa wa Kiharusi Nyumbani kwake baada ya kuugua kwa muda mrefu.
Marehemu Mollel alifariki Mei 26 mwaka huu nyumbani kwake na kuzikwa Jana nyumbani kwake eneo la Selian katika mazishi yaliyotanguliwa na ibada ya kumwombea na kuhudhuliwa na viongozi mbalimbali wa chama na serikali akiwemo Mkuu wa wilaya ya Hai ,Sabaya Ole Lengai ambaye alipata fursa ya kusalimia
Akitoa salamu za rambirambi mwenyekiti wa ccm Mkoa wa Arusha,Zelothe Steven alimweleza marehemu Mollel kuwa alikuwa mzalendo ,mchapakazi na kuwataka wananchi pamoja na jamii yake kuyaenzi yale mema aliyoachwa na marehemu kwa kufuata nyayo zake za uchapa kazi ikiwemo uchangiaji wa ujenzi wa makanisa ujenzi wa visima na ujenzi wa barabara.
Aidha alisema kuwa marehemu aliongoza jimbo la Arumeru Magharibi kwa vipindi vitatu mfururizo na kuweza kuwatumikia wananchi wake kwa kipindi cha miaka 15 jambo lililompa heshima na umaarufu mkubwa katika kuisaidia jamii hasa katika nyaja za kujitolea kuchangua maendeleo.
Katika hatua nyingine Zelothe aliwakumbusha wananchi kuwa taifa linaelekea kwenye uchaguzi Mkuu hivyo wananchi hawanabudi kuwa macho kutumika kama daraja la kuwavusha wanansiasa kwa sababu ya njaa ya pesa.
Amesema jambo hilo ni hatari sana kwani watajikuta wakichagua viongozi wabovu watakao wafanya wajutie uamuzi wao katika kipindi cha miaka mitano ijayo..
"nibora mkala makande mkachagua kiongozi bora kuliko tamaa ya pesa mkapata kiongozi Bomu" Alisema Zelothe
Marehemu Mollel amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 75 na ameacha watoto wawili kati ya wanne na wajukuu 20 na atajumbukwa kwa mema mengi aliyoyafanya jimboni humo.
Ends.....
Marehemu Mollel alifariki Mei 26 mwaka huu nyumbani kwake na kuzikwa Jana nyumbani kwake eneo la Selian katika mazishi yaliyotanguliwa na ibada ya kumwombea na kuhudhuliwa na viongozi mbalimbali wa chama na serikali akiwemo Mkuu wa wilaya ya Hai ,Sabaya Ole Lengai ambaye alipata fursa ya kusalimia
Akitoa salamu za rambirambi mwenyekiti wa ccm Mkoa wa Arusha,Zelothe Steven alimweleza marehemu Mollel kuwa alikuwa mzalendo ,mchapakazi na kuwataka wananchi pamoja na jamii yake kuyaenzi yale mema aliyoachwa na marehemu kwa kufuata nyayo zake za uchapa kazi ikiwemo uchangiaji wa ujenzi wa makanisa ujenzi wa visima na ujenzi wa barabara.
Aidha alisema kuwa marehemu aliongoza jimbo la Arumeru Magharibi kwa vipindi vitatu mfururizo na kuweza kuwatumikia wananchi wake kwa kipindi cha miaka 15 jambo lililompa heshima na umaarufu mkubwa katika kuisaidia jamii hasa katika nyaja za kujitolea kuchangua maendeleo.
Katika hatua nyingine Zelothe aliwakumbusha wananchi kuwa taifa linaelekea kwenye uchaguzi Mkuu hivyo wananchi hawanabudi kuwa macho kutumika kama daraja la kuwavusha wanansiasa kwa sababu ya njaa ya pesa.
Amesema jambo hilo ni hatari sana kwani watajikuta wakichagua viongozi wabovu watakao wafanya wajutie uamuzi wao katika kipindi cha miaka mitano ijayo..
"nibora mkala makande mkachagua kiongozi bora kuliko tamaa ya pesa mkapata kiongozi Bomu" Alisema Zelothe
Marehemu Mollel amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 75 na ameacha watoto wawili kati ya wanne na wajukuu 20 na atajumbukwa kwa mema mengi aliyoyafanya jimboni humo.
Ends.....