Aliyetuhumiwa kwa ubakaji watoto 24 Arusha siyo ustadhi

M-TZ1

Member
Jun 3, 2020
79
132
ALIYETUHUMIWA KWA UBAKAJI WATOTO 24 ARUSHA SIYO USTADHI.

Tahariri.

Hivi karibuni Jamii ya Maustadhi ilijikuta imeingizwa kwenye mashaka makubwa kisaikolojia baada ya vichwa vya habari kuonyesha Kuwepo tuhuma kwa Ustadhi mkoani Arusha za ubakaji watoto 24 wa Shule ya Mkonoo kata ya Terati wilaya ya Arusha Jiji. Hata hivyo sasa imebainika mtuhumiwa siyo ustadhi wa madrasa.

Madrasa iliyolengwa ambayo ilifungwa kufuatia tukio la tuhuma hizo iko ndani ya Masjid Rosana Hamad ulio chini ya taasisi ya Islamic Foundation yenye Makao makuu Msamvu, Morogoro

Kwa Mujibu wa Sheikh wa wilaya ya Arusha Jiji Alhaj Ijunje Mtuhumiwa aliyetajwa Mbele ya mkuu wa wilaya siyo mwalimu wa Madrasa iliyofungwa na wala hajawahi kuwa mwalimu wa Madrasa yoyote na wanafunzi waliotajwa kuathiriwa hawajawahi kuwa wanafunzi wa Madrasa hiyo ambayo mpaka sasa imefungwa.

Naye katibu wa Islamic Foundation mkoani Arusha Bwana Mfinanga amesema Imamu na Mwalimu wa Madrasa hiyo ni Ustadh Shwaibu Suleiman Kifogo Na kwamba mtuhumiwa aliyetajwa siyo kiongozi wa msikiti au madrasa hiyo kwa namna yoyote. .Bwana Mfinanga anasema hajafahamu sababu hasa ya kuhusishwa mojakwamoja na kufungwa Madrasa hiyo.

Sheikh wa wilaya ya Arusha amesema Awali msikiti huo ulifungwa kwa Amri ya mkuu wa Wilaya. Baadaye waumini wakaruhusiwa kuswali lakini mpaka sasa Madrasa haijaruhusiwa kuendelea na mafunzo. Aidha Amesema imebainika wanafunzi wengi wanaodaiwa kufanyiwa vitendo hivyo siyo waislamu.

Mkuu wa wilaya naye hivi karibuni amesikika akisema kuwa mtuhumiwa siyo Ustadhi wa Madrasa. Na kwamba ni wanahabari tu waliongeza chumvi. Wala yeye hajamtuhumu mwalimu wa Madasa.

Kwa ujumla kosa kubwa lililofanyika ni kumtaja mtuhumiwa kuwa ni Ustadhi huku ikijulikana kwamba kufanya hivyo ni kuwadhalilisha maustadhi wote ambao siku ile waliathirika sana kisaikolojia.

Wala haijafahamika sababu ya BAKWATA kutoshirikishwa kwenye hatua za awali. Naamini uongozi wa BAKWATA mkoa, Wilaya au kata ungeshirikishwa mtuhumiwa asingehusishwa na ualimu wa Madrasa.

Je sekta nyingine ingepata shambulio kubwa la kisaikolojia kama hili kwa makusudi kungekalika?

Kwa mfano mtuhumiwa aitwe Polisi, Mkuu wa Wilaya, Diwani Mwalimu wa shule ilhali hana uhusiano na cheo au wadhifa huo waathirika wangekaa kimya? Au Mwalimu wa Madrasa anaendelea kuwa mnyonge mnyongeni na haki yake mnyimeni.
....

Dr. Harith Nkussa
Mwandishi Maalum wa Mufti
Ijumaa 27.5.2022
Dar es salaam
 
ALIYETUHUMIWA KWA UBAKAJI WATOTO 24 ARUSHA SIYO USTADHI.

Tahariri.

Hivi karibuni Jamii ya Maustadhi ilijikuta imeingizwa kwenye mashaka makubwa kisaikolojia baada ya vichwa vya habari kuonyesha Kuwepo tuhuma kwa Ustadhi mkoani Arusha za ubakaji watoto 24 wa Shule ya Mkonoo kata yaTerati wilaya ya Arusha Jiji. Hata hivyo sasa imebainika mtuhumiwa siyo ustadhi wa madrasa.

Madrasa iliyolengwa ambayo ilifungwa kufuatia tukio la tuhuma hizo iko ndani ya Masjid Rosana Hamad ulio chini ya taasisi ya Islamic Foundation yenye Makao makuu Msamvu, Morogoro

Kwa Mujibu wa Sheikh wa wilaya ya Arusha Jiji Alhaj Ijunje Mtuhumiwa aliyetajwa Mbele ya mkuu wa wilaya siyo mwalimu wa Madrasa iliyofungwa na wala hajawahi kuwa mwalimu wa Madrasa yoyote na wanafunzi waliotajwa kuathiriwa hawajawahi kuwa wanafunzi wa Madrasa hiyo ambayo mpaka sasa imefungwa.

Naye katibu wa Islamic Foundation mkoani Arusha Bwana Mfinanga amesema Imamu na Mwalimu wa Madrasa hiyo ni Ustadh Shwaibu Suleiman Kifogo Na kwamba mtuhumiwa aliyetajwa siyo kiongozi wa msikiti au madrasa hiyo kwa namna yoyote. .Bwana mfinanga anasema hajafahamu sababu hasa ya kuhusishwa mojakwamoja na kufungwa Madrasa hiyo.

Sheikh wa wilaya ya Arusha amesema Awali msikiti huo ulifungwa kwa Amri ya mkuu wa Wilaya. Baadaye waumini wakaruhusiwa kuswali lakini mpaka sasa Madrasa haijaruhusiwa kuendelea na mafunzo. Aidha Amesema imebainika wanafunzi wengi wanaodaiwa kufanyiwa vitendo hivyo siyo waislamu.

Mkuu wa wilaya naye hivi karibuni amesikika akisema kuwa mtuhumiwa siyo Ustadhi wa Madrasa. Na kwamba ni wanahabari tu waliongeza chumvi. Wala yeye hajamtuhumu mwalimu wa Madasa.

Kwa ujumla kosa kubwa lililofanyika ni kumtaja mtuhumiwa kuwa ni Ustadhi huku ikijulikana kwamba kufanya hivyo ni kuwadhalilisha maustadhi wote ambao siku ile waliathirika sana kisaikolojia.

Wala haijafahamika sababu ya BAKWATA kutoshirikishwa kwenye hatua za awali. Naamini uongozi wa BAKWATA mkoa, Wilaya au kata ungeshirikishwa mtuhumiwa asingehusishwa na ualimu wa Madrasa.

Je sekta nyingine ingepata shambulio kubwa la kisaikolojia kama hili kwa makusudi kungekalika?

Kwa mfano mtuhumiwa aitwe Polisi, Mkuu wa Wilaya, Diwani Mwalimu wa shule ilhali hana uhusiano na cheo au wadhifa huo waathirika wangekaa kimya? Au Mwalimu wa Madrasa anaendelea kuwa mnyonge mnyongeni na haki yake mnyimeni.
....

Dr. Harith Nkussa
Mwandishi Maalum wa Mufti
Ijumaa 27.5.2022
Dar es salaam
Dr. Umepitia fani ya uandishi wa habari au taarifa ya kitaalamu? Maana nimepitia mpangilio wa habari yako na weledi wa taaluma hiyo mara mbilimbili nione ujazo wa taarifa ya memaji wa taasisi muhimu sijashiba. Dr. Dr.Dr!!!!!
 
Acha kufunika wewe yule ni ustadhi kabisa sema mnaona aibu mbona wapo maustadhi wengine dar ukifuatilia matukio nao walikamatwa na matukio kama haya sema na nyie mmezidi kuficha ukiona limetapakaa ujue mwenye mtoto imemuuma sana msipende kuficha hayo ndio maana mitoto mingi pwani ni mishoga chunguza bila ushabiki na kufunika
 
Kwa Mujibu wa Sheikh wa wilaya ya Arusha Jiji Alhaj Ijunje Mtuhumiwa aliyetajwa Mbele ya mkuu wa wilaya siyo mwalimu wa Madrasa iliyofungwa na wala hajawahi kuwa mwalimu wa Madrasa yoyote na wanafunzi waliotajwa kuathiriwa hawajawahi kuwa wanafunzi wa Madrasa hiyo ambayo mpaka sasa imefungwa.

Naye katibu wa Islamic Foundation mkoani Arusha Bwana Mfinanga amesema Imamu na Mwalimu wa Madrasa hiyo ni Ustadh Shwaibu Suleiman Kifogo Na kwamba mtuhumiwa aliyetajwa siyo kiongozi wa msikiti au madrasa hiyo kwa namna yoyote. .Bwana mfinanga anasema hajafahamu sababu hasa ya kuhusishwa mojakwamoja na kufungwa Madrasa hiyo
Ina maana DC na msafara wake waliingizwa mkenge na waliomtaja mmiliki wa hiyo compound pamoja na shughuli zilizokuwa zikiendelea hapo ?
 
watu wametoa ufafanuzi kwa hoja za wazo, mfano wamesema Mtuhumiwa si wala hajawahi kuwa Mwalimu wa Madrasa yao pia wanafunzi waliodhalilishwa si wala hawajawahi kuwa Wanafunzi wa Madrasa tajwa


kujibu hoja zao ni kuthibitisha kuwa hao wanafunzi ni wa madrassa hiyo na Mwalimu ni wa madrasa hiyo

hizo hoja za kuoa ndoa za utotoni si sehemu ya mjadala na ukitaka iwe sehemu ya mjadala kasome sheria za Nchi ujue umri wa chini wa kuruhusiwa kuolewa ni miaka mingapi na wao wameolewa na umri gani
ACHENI KUKIMBIA LAWAMA HILI TATIZO NI HAI NA LINAISHI KWENYE MADRASA ZA WAISLAMU.
KINGINE WALE WAALIMU HUWA WANAOA WANAFUNZI WAO TENA NDOA ZA UTOTONI
 
ACHENI KUKIMBIA LAWAMA HILI TATIZO NI HAI NA LINAISHI KWENYE MADRASA ZA WAISLAMU.
KINGINE WALE WAALIMU HUWA WANAOA WANAFUNZI WAO TENA NDOA ZA UTOTONI
Ndio sababu iliipelekea mtu asihusuka kunasibishwa na tukio chafu,

Kama ni hivyo tutachelewa kufika au hatutafika kabisaaa.
 
kwa hiyo tabia za hao maustadhi ndio zilipelekea baadhi ya makanisa yaka halalisha ndoa za mashoga?

google hapo uone idadi ya malaki ya watoto waliopita Sunday school wanavyokiri kudhulumiwa kingono wakiwa mafunzoni.
Acha kufunika wewe yule ni ustadhi kabisa sema mnaona aibu mbona wapo maustadhi wengine dar ukifuatilia matukio nao walikamatwa na matukio kama haya sema na nyie mmezidi kuficha ukiona limetapakaa ujue mwenye mtoto imemuuma sana msipende kuficha hayo ndio maana mitoto mingi pwani ni mishoga chunguza bila ushabiki na kufunika
 
kwa hiyo tabia za hao maustadhi ndio zilipelekea baadhi ya makanisa yaka halalisha ndoa za mashoga?

google hapo uone idadi ya malaki ya watoto waliopita Sunday school wanavyokiri kudhulumiwa kingono wakiwa mafunzoni.
Sawa papa ameunga mkono ndoa za jinsia moja
 
Ila waislamu tunachekesha sana! Eti tumeona ni bora tufiche tatizo ili tuonekane bado tu wenye haki wakati watoto wetu wanaendelea kuharibiwa!

Mtoto wa miaka 8 wa kike wa huyu jilani yangu alibanduliwa 0713 na Mwalimu wake wa madrasa, mzazi akaona afiche, eti ni aibu!

Tunakoelekea siko! Mbona wenzetu yakiwakumba wanakubari kosa na kusahihisha! Tumezidi kujiona bora!
 
Back
Top Bottom