Elections 2010 Aliyetuhumiwa Kumtukana Kikwete sasa Kugombea jimbo la Musoma Vijijini.......

Dickson Ng'hily

JF-Expert Member
Oct 22, 2010
451
485
Ndugu zangu Watanzania na wale wote wenye kuitakia mema Tanzania, nawasalimu,

Nimeona ni bora kuliweka hili wazi kwa kila Mtanzania ili ajue ni kitu gani kinaendelea. Baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka jana, yalisemwa mengi sana juu yangu kuwa nimerudi CCM n.k. Kama ilivyo kawaida yangu, nimechelewa sana kujibu hata hivyo sikuona umuhimu wa kujibu kwani wakati muafaka ulikuwa haijafika. Wahenga walisema, uwe mwepesi wa kusikia na sio kusema. Sasa wakati umefika na ninapenda kuwaambia habari hizo hakuwa na hazina ukweli wowote. Mimi bado ni mwanachama wa CDM na ninaipenda sana..

Baada ya kusema hayo, napenda pia kuchua fulsa hii kuwashukuru wakazi wa jimbo la Musoma Vijijini kwa mapenzi yao mema kwangu na kwa familia yangu. Pia niwashukuru kwa kuamua kuniunga mkono katika harakati hizi za ukombozi wa Taifa letu. Kutoka ndani ya moyo wangu, naomba Mpokee shukrani zangu. Pia niwashukuru wale wote waliosafiri kutoka Musoma kuja kuniomba nikubali kugombea jimbo la Musoma Vijijini katika uchaguzi mkuu ujao (2015) lakini pia wale wote walionipigia simu na kunitumia msgs kunitaka nikubali ombi hilo..SASA NASEMA KUWA NIMEKUBALI OMBI HILO LA KUGOMBEA UBUNGE JIMBO MUSOMA VIJIJINI IKIWA MWENYEZI MUNGU ATATUPATIA UZIMA NA AFYA NJEMA.....

Sababu za kukubali wito huo ni kutokana na ukweli kuwa nusu ya maisha yangu nimeyaishi Musoma both vijijini na mjini hivyo ninaijua vizuri Musoma. Huku ndiko Marehemu mama yangu alizaliwa na kukulia na ndiko alikokutana na Marehemu mzee wangu Dr Ng'hily..Huku ndiko ambako walezi wangu kwa maana ya Babu na Bibi Eliasaph magafu Samanyi wamezikwa...

Hata hivyo, kubwa kuliko yote ni maendeleo duni waliyonayo wakazi wa jimbo la Musoma Vijijini ambao wamekuwa nyuma kimaendeleo licha ya kuwa na natural resouces za kutosha...kama vile madini,uvuvi,utalii nk. Ninaamini kwa pamoja tunaweza kuibadilisha Musoma (V) na kuwa moja ya jimbo la kuigwa katika mkoa wa mara interms of maendeleo endelevu.

Ndg zangu, HAKUNA KULALA MPAKA KIELEWEKE...Ninawahakikishia ya kuwa sitawaangusha...Ujasiri nilionao nitautumia kudai haki na uhuru wa makazi wa jimbo la Musoma (V). Na kazi hii naifanya kuanzia sasa na ninawaomba ushirikiano wenu. Mungu awabriki sana kwa yote...
 
BIG UP; tuko pamoja. Fungueni matawi kila kijiji na kusimamia wanachama na wananchi vema kutambua harakati za CDM kuanzia sasa. Shirikiana na viongozi wilaya, mkoa, na taifa katika jitihada zako.
 
hii ni taarifa au habari mkuu......anyway nenda kaanze kujitangaza na kuwaambia utawanyia nini?
ndio muda wenyewe mkuu miaka minne siyo mingi
 
Mbona mapema. Chama na wananchi wakiteua mwingine? Acha vurugu kama za Kabwe na urais 2015
 
hii ni taarifa au habari mkuu......anyway nenda kaanze kujitangaza na kuwaambia utawanyia nini?
ndio muda wenyewe mkuu miaka minne siyo mingi

Mkuu hii ni taarifa...Kaka mimi nimeombwa na wao coz wameona kazi niliyoifanya kipindi nagombea TEMEKE...Siwezi kuwaahidi nitawanfanyia nini ila nitakchofanya ni kushirikiana nao ili sote kwa pamoja (Wao na MIMI) tuiletee Musoma Vijijini maendeleo endelevu...Wadogo zetu na watoto wetu wafurahie kuzaliwa katika jimbo hili...Asante sana kwa kunitia moyo...
 
Ndugu zangu Watanzania na wale wote wenye kuitakia mema Tanzania, nawasalimu,

Nimeona ni bora kuliweka hili wazi kwa kila Mtanzania ili ajue ni kitu gani kinaendelea. Baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka jana, yalisemwa mengi sana juu yangu kuwa nimerudi CCM n.k. Kama ilivyo kawaida yangu, nimechelewa sana kujibu hata hivyo sikuona umuhimu wa kujibu kwani wakati muafaka ulikuwa haijafika. Wahenga walisema, uwe mwepesi wa kusikia na sio kusema. Sasa wakati umefika na ninapenda kuwaambia habari hizo hakuwa na hazina ukweli wowote. Mimi bado ni mwanachama wa CDM na ninaipenda sana..

Baada ya kusema hayo, napenda pia kuchua fulsa hii kuwashukuru wakazi wa jimbo la Musoma Vijijini kwa mapenzi yao mema kwangu na kwa familia yangu. Pia niwashukuru kwa kuamua kuniunga mkono katika harakati hizi za ukombozi wa Taifa letu. Kutoka ndani ya moyo wangu, naomba Mpokee shukrani zangu. Pia niwashukuru wale wote waliosafiri kutoka Musoma kuja kuniomba nikubali kugombea jimbo la Musoma Vijijini katika uchaguzi mkuu ujao (2015) lakini pia wale wote walionipigia simu na kunitumia msgs kunitaka nikubali ombi hilo..SASA NASEMA KUWA NIMEKUBALI OMBI HILO LA KUGOMBEA UBUNGE JIMBO MUSOMA VIJIJINI IKIWA MWENYEZI MUNGU ATATUPATIA UZIMA NA AFYA NJEMA.....

Sababu za kukubali wito huo ni kutokana na ukweli kuwa nusu ya maisha yangu nimeyaishi Musoma both vijijini na mjini hivyo ninaijua vizuri Musoma. Huku ndiko Marehemu mama yangu alizaliwa na kukulia na ndiko alikokutana na Marehemu mzee wangu Dr Ng'hily..Huku ndiko ambako walezi wangu kwa maana ya Babu na Bibi Eliasaph magafu Samanyi wamezikwa...

Hata hivyo, kubwa kuliko yote ni maendeleo duni waliyonayo wakazi wa jimbo la Musoma Vijijini ambao wamekuwa nyuma kimaendeleo licha ya kuwa na natural resouces za kutosha...kama vile madini,uvuvi,utalii nk. Ninaamini kwa pamoja tunaweza kuibadilisha Musoma (V) na kuwa moja ya jimbo la kuigwa katika mkoa wa mara interms of maendeleo endelevu.

Ndg zangu, HAKUNA KULALA MPAKA KIELEWEKE...Ninawahakikishia ya kuwa sitawaangusha...Ujasiri nilionao nitautumia kudai haki na uhuru wa makazi wa jimbo la Musoma (V). Na kazi hii naifanya kuanzia sasa na ninawaomba ushirikiano wenu. Mungu awabriki sana kwa yote...

(wewe si ndiyo inasemekana ulilambishwa chapaa na yule jamaa wa Bank M? hahaha! yule jamaa anavaaga kibaragashia chenye mkia kama mzee small!?)

hapa ngoja niwe mwepesi wa kusikia kwanza; nisiwe mwepesi wa kusema,
 
Ndugu yangu Nyakageni...Shunghuli za kujiletea maendeleo, hazina muda maalum wa kuanza, so sio mapema kama ufikiriavyo...Kaka,CDM nna wananchi wanaweza kuteuwa mwingine kama ulivyosema hata hvivyo hiyo hainizuii kukubali maombi ya wanajimbo wenzangu tena wengine kutoka CCM...Kama CDM itateua mtu mwingine haina shinda, nitaungana naye kuleta ukombozi na labda niseme hivi...Cna fujo ya aina yeyote hata hivyo una haki ya kuoa maoni...Ubarikiwe.
 
Kumbe utaratibu wa kugombea ubunge kwa Chadema ni rahisi hivi, tunashukuru kwa kutuarifu. Yaani mimi nikiwa nataka kugombea jimbo fulani ninatangaza tu na basi tayari nimekuwa mgombea?

Hata hivyo nina mashaka na uwezo wako wa kujenga hoja. Kama hivyo ulivyoandika hapo juu ndivyo utakavyokuwa unajenga hoja Bungeni iwapo utachaguliwa basi Chadema tumepata seti tupu. Jimbo kuwa nyuma kimaendeleo siyo sababu ya wewe kugombea wakati hakuna ushahidi kwamba wewe ndiyo maendeleo yenyewe na bila mkakati vile utakavyofanya basi kutuletea hayo maendeleo.

Yaani ulichosema kama sapoti ya kugombea kwako ni sawa kabisa na kauli ambazo tumekuwa tukizisikia kwa wagombea wa ccm. Unaleta maendeleo gani, kwa vipi. Uwezo huo wa kuleta maendeleo wewe umeupata wapi? Kwamba umeishi huko siyo hoja, wengi wanaishi huko hadi sasa hivi. Kwamba wazazi wako walizaliwa huko siyo kigezo cha wewe kuwa mbunge wa eneo hilo, wengi wamezaliwa huko na bado hawana vigezo vya kugombea.

Kwanza umekiri kwamba umeshindwa kujibu hoja hapa janvini, na unatumia kigezo hicho eti kututangazia kwamba utagombea. Nashauri ukae kimya kama ulivyosema kwamba ulikaa kimya watu walipokuwa wanahoji uadilifu wako.

Ningependa wote wanaokusudia kugombea nafasi mbali mbali 2015 kujua kwamba it will not be business as usual, we want the best.
 
Mkuu hii ni taarifa...Kaka mimi nimeombwa na wao coz wameona kazi niliyoifanya kipindi nagombea TEMEKE...Siwezi kuwaahidi nitawanfanyia nini ila nitakchofanya ni kushirikiana nao ili sote kwa pamoja (Wao na MIMI) tuiletee Musoma Vijijini maendeleo endelevu...Wadogo zetu na watoto wetu wafurahie kuzaliwa katika jimbo hili...Asante sana kwa kunitia moyo...

Alaaaaa, kumbe ni wewe? Si ni wewe ndiye uliyeropoka ushuzi pale Mwembeyanga kwenye mkutano wa Dr. Slaa hadi polisi wakakuweka ndani na ikapelekea Chadema kukosa jimbo la Temeke?
 
BIG UP; tuko pamoja. Fungueni matawi kila kijiji na kusimamia wanachama na wananchi vema kutambua harakati za CDM kuanzia sasa. Shirikiana na viongozi wilaya, mkoa, na taifa katika jitihada zako.

Nsimba...Asante sana na ninakuhakikishia kuwa nitashirikiana nao na taarifa nilishaanza kuzisambaza kunakohusika na wakati huu ninaandaa safari ya kwenda huko...Nashukuru sana na asate kwa kuniunga mkono na kuwa pamoja nami...Tuna kazi kubwa kukijenga chama huko na nina aamini kuwa kwa pamoja tunaweza.
 

...

Baada ya kusema hayo, napenda pia kuchua fulsa hii kuwashukuru wakazi wa jimbo la Musoma Vijijini kwa mapenzi yao mema kwangu na kwa familia yangu. Pia niwashukuru kwa kuamua kuniunga mkono katika harakati hizi za ukombozi wa Taifa letu. Kutoka ndani ya moyo wangu, naomba Mpokee shukrani zangu. Pia niwashukuru wale wote waliosafiri kutoka Musoma kuja kuniomba nikubali kugombea jimbo la Musoma Vijijini katika uchaguzi mkuu ujao (2015) lakini pia wale wote walionipigia simu na kunitumia msgs kunitaka nikubali ombi hilo..SASA NASEMA KUWA NIMEKUBALI OMBI HILO LA KUGOMBEA UBUNGE JIMBO MUSOMA VIJIJINI IKIWA MWENYEZI MUNGU ATATUPATIA UZIMA NA AFYA NJEMA.....

...

Hapo kwenye bluu, kauli kama za wale jamaa wanaozeekea mjengoni. Wangapi wamesafiri kutoka Musoma just kuja tu kukuomba wewe ugombee ubunge 2015? Kauli mbiu hii imepitwa na wakati kaka.

By the way, kuna michakato mingi hadi kuteuliwa na "chama chako" kuwa mgombea hivyo pia chance ya kukosa hiyo nafasi ipo na naamini utakuwa mwaminifu na utakubali matokeo endapo lolote litatokea ikiwapo kutokisaliti chama kama wengine wafanyavyo. Labda tumwombe Mungu katiba mpya iwe imepatikana na taratibu ziwe zimebadilika ikiwepo ugombea binafsi.
 
Kumbe utaratibu wa kugombea ubunge kwa Chadema ni rahisi hivi, tunashukuru kwa kutuarifu. Yaani mimi nikiwa nataka kugombea jimbo fulani ninatangaza tu na basi tayari nimekuwa mgombea?

Hata hivyo nina mashaka na uwezo wako wa kujenga hoja. Kama hivyo ulivyoandika hapo juu ndivyo utakavyokuwa unajenga hoja Bungeni iwapo utachaguliwa basi Chadema tumepata seti tupu. Jimbo kuwa nyuma kimaendeleo siyo sababu ya wewe kugombea wakati hakuna ushahidi kwamba wewe ndiyo maendeleo yenyewe na bila mkakati vile utakavyofanya basi kutuletea hayo maendeleo.

Yaani ulichosema kama sapoti ya kugombea kwako ni sawa kabisa na kauli ambazo tumekuwa tukizisikia kwa wagombea wa ccm. Unaleta maendeleo gani, kwa vipi. Uwezo huo wa kuleta maendeleo wewe umeupata wapi? Kwamba umeishi huko siyo hoja, wengi wanaishi huko hadi sasa hivi. Kwamba wazazi wako walizaliwa huko siyo kigezo cha wewe kuwa mbunge wa eneo hilo, wengi wamezaliwa huko na bado hawana vigezo vya kugombea.

Kwanza umekiri kwamba umeshindwa kujibu hoja hapa janvini, na unatumia kigezo hicho eti kututangazia kwamba utagombea. Nashauri ukae kimya kama ulivyosema kwamba ulikaa kimya watu walipokuwa wanahoji uadilifu wako.

Ningependa wote wanaokusudia kugombea nafasi mbali mbali 2015 kujua kwamba it will not be business as usual, we want the best.


Kaka nashukuru kwa mchango wako..
 
Alaaaaa, kumbe ni wewe? Si ni wewe ndiye uliyeropoka ushuzi pale Mwembeyanga kwenye mkutano wa Dr. Slaa hadi polisi wakakuweka ndani na ikapelekea Chadema kukosa jimbo la Temeke?

Nashukuru kwa mchango ndugu yangu..
 
Hapo kwenye bluu, kauli kama za wale jamaa wanaozeekea mjengoni. Wangapi wamesafiri kutoka Musoma just kuja tu kukuomba wewe ugombee ubunge 2015? Kauli mbiu hii imepitwa na wakati kaka.

By the way, kuna michakato mingi hadi kuteuliwa na "chama chako" kuwa mgombea hivyo pia chance ya kukosa hiyo nafasi ipo na naamini utakuwa mwaminifu na utakubali matokeo endapo lolote litatokea ikiwapo kutokisaliti chama kama wengine wafanyavyo. Labda tumwombe Mungu katiba mpya iwe imepatikana na taratibu ziwe zimebadilika ikiwepo ugombea binafsi.


Ndo maana nimejibu kuwa tuombe uzima na afya, nilichofanya mimi ni kukubali ombi je kuna kosa hapo!Nihukumu kama kwa kukubali ombi nimefanya kosa...Hata hivyo nimesema na nitarudia kusema kuwa Chama kikiteua mtu mwingine, sina tatizo, nitashirikiana naye na mimi sitagombea jimbo lolote...
 
Ndugu zangu Watanzania na wale wote wenye kuitakia mema Tanzania, nawasalimu,

Nimeona ni bora kuliweka hili wazi kwa kila Mtanzania ili ajue ni kitu gani kinaendelea. Baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka jana, yalisemwa mengi sana juu yangu kuwa nimerudi CCM n.k. Kama ilivyo kawaida yangu, nimechelewa sana kujibu hata hivyo sikuona umuhimu wa kujibu kwani wakati muafaka ulikuwa haijafika. Wahenga walisema, uwe mwepesi wa kusikia na sio kusema. Sasa wakati umefika na ninapenda kuwaambia habari hizo hakuwa na hazina ukweli wowote. Mimi bado ni mwanachama wa CDM na ninaipenda sana..

Baada ya kusema hayo, napenda pia kuchua fulsa hii kuwashukuru wakazi wa jimbo la Musoma Vijijini kwa mapenzi yao mema kwangu na kwa familia yangu. Pia niwashukuru kwa kuamua kuniunga mkono katika harakati hizi za ukombozi wa Taifa letu. Kutoka ndani ya moyo wangu, naomba Mpokee shukrani zangu. Pia niwashukuru wale wote waliosafiri kutoka Musoma kuja kuniomba nikubali kugombea jimbo la Musoma Vijijini katika uchaguzi mkuu ujao (2015) lakini pia wale wote walionipigia simu na kunitumia msgs kunitaka nikubali ombi hilo..SASA NASEMA KUWA NIMEKUBALI OMBI HILO LA KUGOMBEA UBUNGE JIMBO MUSOMA VIJIJINI IKIWA MWENYEZI MUNGU ATATUPATIA UZIMA NA AFYA NJEMA.....

Sababu za kukubali wito huo ni kutokana na ukweli kuwa nusu ya maisha yangu nimeyaishi Musoma both vijijini na mjini hivyo ninaijua vizuri Musoma. Huku ndiko Marehemu mama yangu alizaliwa na kukulia na ndiko alikokutana na Marehemu mzee wangu Dr Ng'hily..Huku ndiko ambako walezi wangu kwa maana ya Babu na Bibi Eliasaph magafu Samanyi wamezikwa...

Hata hivyo, kubwa kuliko yote ni maendeleo duni waliyonayo wakazi wa jimbo la Musoma Vijijini ambao wamekuwa nyuma kimaendeleo licha ya kuwa na natural resouces za kutosha...kama vile madini,uvuvi,utalii nk. Ninaamini kwa pamoja tunaweza kuibadilisha Musoma (V) na kuwa moja ya jimbo la kuigwa katika mkoa wa mara interms of maendeleo endelevu.

Ndg zangu, HAKUNA KULALA MPAKA KIELEWEKE...Ninawahakikishia ya kuwa sitawaangusha...Ujasiri nilionao nitautumia kudai haki na uhuru wa makazi wa jimbo la Musoma (V). Na kazi hii naifanya kuanzia sasa na ninawaomba ushirikiano wenu. Mungu awabriki sana kwa yote...
Angalia sana hiyo nyekundu maana cku ukiambiwa uwataje utaweza?...Wakiulizwa wametumwa na nani kukwambia au kukutext watajibu?....Je hao waliokwambia au kukutext wao wanakubalika kwa wananchi???.......ni dhahiri kuwa hao ni ndugu zako tu ambao pia wanajua makazi yako kwa hao waliokuja na ambao walikutext wanajua number yako ya cmu?,(Jibu rahisi ni kuwa watakuwa ni ndugu zako).
Nina nia njema sana na wewe ndiyo maana nakutahadharisha ili ukienda kule uwe na propaganda za maana, Binafsi cpendi mbunge aliyepo kule maana amekuwa cyo mbunifu wa miradi ya maendeleo bali ana technique ya kugawia viongozi (Madiwani,Watendaji Kata?Vijiji, Headteachers/schools) vijisent vyake binafsi BADALA YA KUTETEA JIMBO LAKE LIPATE MIRADI INAYOTOKANA NA KODI YA WANANCHI/SERIKALI....Hivyo kaza buti sana maana amewateka na wamebweteka sana,Ukitoa Butiama,kiabakari,Busegwe( Kwao MB) na Mgango ambazo zina umeme pia kwa Advantage ya ''Butiama Tu''...Wilaya nzima haina umeme, haina Lami hata ya kutambikia, haina Irrigation scheme yoyote,Maji taabu wakati wako karibu na ziwa, hakuna makao makuu ya Wilaya.....Unakazi kubwa sana ya KUFANYA NDUGI YANGU...hebu anzia hapo, Pia ile fununu ya wagombea wa Musoma Vijijini kununuliwa kaa chonjo pia
Naomba kuwasilisha..........
 
Back
Top Bottom