Dickson Ng'hily
JF-Expert Member
- Oct 22, 2010
- 451
- 485
Ndugu zangu Watanzania na wale wote wenye kuitakia mema Tanzania, nawasalimu,
Nimeona ni bora kuliweka hili wazi kwa kila Mtanzania ili ajue ni kitu gani kinaendelea. Baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka jana, yalisemwa mengi sana juu yangu kuwa nimerudi CCM n.k. Kama ilivyo kawaida yangu, nimechelewa sana kujibu hata hivyo sikuona umuhimu wa kujibu kwani wakati muafaka ulikuwa haijafika. Wahenga walisema, uwe mwepesi wa kusikia na sio kusema. Sasa wakati umefika na ninapenda kuwaambia habari hizo hakuwa na hazina ukweli wowote. Mimi bado ni mwanachama wa CDM na ninaipenda sana..
Baada ya kusema hayo, napenda pia kuchua fulsa hii kuwashukuru wakazi wa jimbo la Musoma Vijijini kwa mapenzi yao mema kwangu na kwa familia yangu. Pia niwashukuru kwa kuamua kuniunga mkono katika harakati hizi za ukombozi wa Taifa letu. Kutoka ndani ya moyo wangu, naomba Mpokee shukrani zangu. Pia niwashukuru wale wote waliosafiri kutoka Musoma kuja kuniomba nikubali kugombea jimbo la Musoma Vijijini katika uchaguzi mkuu ujao (2015) lakini pia wale wote walionipigia simu na kunitumia msgs kunitaka nikubali ombi hilo..SASA NASEMA KUWA NIMEKUBALI OMBI HILO LA KUGOMBEA UBUNGE JIMBO MUSOMA VIJIJINI IKIWA MWENYEZI MUNGU ATATUPATIA UZIMA NA AFYA NJEMA.....
Sababu za kukubali wito huo ni kutokana na ukweli kuwa nusu ya maisha yangu nimeyaishi Musoma both vijijini na mjini hivyo ninaijua vizuri Musoma. Huku ndiko Marehemu mama yangu alizaliwa na kukulia na ndiko alikokutana na Marehemu mzee wangu Dr Ng'hily..Huku ndiko ambako walezi wangu kwa maana ya Babu na Bibi Eliasaph magafu Samanyi wamezikwa...
Hata hivyo, kubwa kuliko yote ni maendeleo duni waliyonayo wakazi wa jimbo la Musoma Vijijini ambao wamekuwa nyuma kimaendeleo licha ya kuwa na natural resouces za kutosha...kama vile madini,uvuvi,utalii nk. Ninaamini kwa pamoja tunaweza kuibadilisha Musoma (V) na kuwa moja ya jimbo la kuigwa katika mkoa wa mara interms of maendeleo endelevu.
Ndg zangu, HAKUNA KULALA MPAKA KIELEWEKE...Ninawahakikishia ya kuwa sitawaangusha...Ujasiri nilionao nitautumia kudai haki na uhuru wa makazi wa jimbo la Musoma (V). Na kazi hii naifanya kuanzia sasa na ninawaomba ushirikiano wenu. Mungu awabriki sana kwa yote...
Nimeona ni bora kuliweka hili wazi kwa kila Mtanzania ili ajue ni kitu gani kinaendelea. Baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka jana, yalisemwa mengi sana juu yangu kuwa nimerudi CCM n.k. Kama ilivyo kawaida yangu, nimechelewa sana kujibu hata hivyo sikuona umuhimu wa kujibu kwani wakati muafaka ulikuwa haijafika. Wahenga walisema, uwe mwepesi wa kusikia na sio kusema. Sasa wakati umefika na ninapenda kuwaambia habari hizo hakuwa na hazina ukweli wowote. Mimi bado ni mwanachama wa CDM na ninaipenda sana..
Baada ya kusema hayo, napenda pia kuchua fulsa hii kuwashukuru wakazi wa jimbo la Musoma Vijijini kwa mapenzi yao mema kwangu na kwa familia yangu. Pia niwashukuru kwa kuamua kuniunga mkono katika harakati hizi za ukombozi wa Taifa letu. Kutoka ndani ya moyo wangu, naomba Mpokee shukrani zangu. Pia niwashukuru wale wote waliosafiri kutoka Musoma kuja kuniomba nikubali kugombea jimbo la Musoma Vijijini katika uchaguzi mkuu ujao (2015) lakini pia wale wote walionipigia simu na kunitumia msgs kunitaka nikubali ombi hilo..SASA NASEMA KUWA NIMEKUBALI OMBI HILO LA KUGOMBEA UBUNGE JIMBO MUSOMA VIJIJINI IKIWA MWENYEZI MUNGU ATATUPATIA UZIMA NA AFYA NJEMA.....
Sababu za kukubali wito huo ni kutokana na ukweli kuwa nusu ya maisha yangu nimeyaishi Musoma both vijijini na mjini hivyo ninaijua vizuri Musoma. Huku ndiko Marehemu mama yangu alizaliwa na kukulia na ndiko alikokutana na Marehemu mzee wangu Dr Ng'hily..Huku ndiko ambako walezi wangu kwa maana ya Babu na Bibi Eliasaph magafu Samanyi wamezikwa...
Hata hivyo, kubwa kuliko yote ni maendeleo duni waliyonayo wakazi wa jimbo la Musoma Vijijini ambao wamekuwa nyuma kimaendeleo licha ya kuwa na natural resouces za kutosha...kama vile madini,uvuvi,utalii nk. Ninaamini kwa pamoja tunaweza kuibadilisha Musoma (V) na kuwa moja ya jimbo la kuigwa katika mkoa wa mara interms of maendeleo endelevu.
Ndg zangu, HAKUNA KULALA MPAKA KIELEWEKE...Ninawahakikishia ya kuwa sitawaangusha...Ujasiri nilionao nitautumia kudai haki na uhuru wa makazi wa jimbo la Musoma (V). Na kazi hii naifanya kuanzia sasa na ninawaomba ushirikiano wenu. Mungu awabriki sana kwa yote...