figganigga
JF-Expert Member
- Oct 17, 2010
- 25,492
- 54,890
Misungwi. Mahakama ya Hakimu Mkazi Wilaya ya Misungwi leo Ijumaa Julai 27, 2018 imemhukumu kifungo cha miezi sita jela, Samwel Kawiche (24) baada ya kumtia hatiani kwa kosa la uzembe uliosababisha kifo cha mkuu wa wilaya wa zamani, Danhi Makanga.
Kawiche aliyekuwa akiendesha gari lililogonga pikipiki aliyokuwa amepanda marehemu ambaye pia amewahi kuwa mbunge wa jimbo la Bariadi, pia leseni yake imefungiwa kwa miaka miwili.
Katika ajali hiyo dereva wa pikipiki hiyo, Marco Hamisi mkazi wa Kijiji cha Nyang’omango pia alifariki dunia.
Akitoa hukumu hiyo leo hakimu mkuu mfawidhi wa mahakama hiyo, Erick Marley amesema mahakama imefikia uamuzi huo baada ya mshtakiwa kukiri kutenda kosa hilo katika tukio lililotokea Juni 23, 2018 katika barabara kuu ya Mwanza Shinyanga eneo la Nyashishi kijiji cha Nyang’omango.
“Kutokana na kukiri kosa mahakama imekuhumu kwenda jela miezi sita na kuifungia leseni yako kwa miaka miwili ili iwe fundisho kwako na madareva wengine wanaoendesha magari kwa uzembe na kusababisha ajali zinazosababisha vifo na watu kupata majeraha,” amesema.
Awali, mwendesha mashtaka wa polisi, Ramsoney Salehe ameileza Mahakama kuwa mshtakiwa aliendesha gari kwa uzembe akitokea kijiji cha Usagara kwenda jijini Mwanza kwa kuigonga pikipiki na kusababisha kifo cha abiria na mwendesha pikipiki.
“Kosa hili ni kinyume cha kifungu cha 40 na 63 (2) (27) cha sheria ya usalama Barabarani sura ya 163 Iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2002,”amesema Salehe.
Akijtetea kabla ya hukumu katika shauri hilo la jinai namba 19/ 2018 mshitakiwa ameiomba mahakama kumpunguzia adhabu kwa kuwa hilo ni kosa lake la kwanza.
Chanzo: Mwananchi
Kawiche aliyekuwa akiendesha gari lililogonga pikipiki aliyokuwa amepanda marehemu ambaye pia amewahi kuwa mbunge wa jimbo la Bariadi, pia leseni yake imefungiwa kwa miaka miwili.
Katika ajali hiyo dereva wa pikipiki hiyo, Marco Hamisi mkazi wa Kijiji cha Nyang’omango pia alifariki dunia.
Akitoa hukumu hiyo leo hakimu mkuu mfawidhi wa mahakama hiyo, Erick Marley amesema mahakama imefikia uamuzi huo baada ya mshtakiwa kukiri kutenda kosa hilo katika tukio lililotokea Juni 23, 2018 katika barabara kuu ya Mwanza Shinyanga eneo la Nyashishi kijiji cha Nyang’omango.
“Kutokana na kukiri kosa mahakama imekuhumu kwenda jela miezi sita na kuifungia leseni yako kwa miaka miwili ili iwe fundisho kwako na madareva wengine wanaoendesha magari kwa uzembe na kusababisha ajali zinazosababisha vifo na watu kupata majeraha,” amesema.
Awali, mwendesha mashtaka wa polisi, Ramsoney Salehe ameileza Mahakama kuwa mshtakiwa aliendesha gari kwa uzembe akitokea kijiji cha Usagara kwenda jijini Mwanza kwa kuigonga pikipiki na kusababisha kifo cha abiria na mwendesha pikipiki.
“Kosa hili ni kinyume cha kifungu cha 40 na 63 (2) (27) cha sheria ya usalama Barabarani sura ya 163 Iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2002,”amesema Salehe.
Akijtetea kabla ya hukumu katika shauri hilo la jinai namba 19/ 2018 mshitakiwa ameiomba mahakama kumpunguzia adhabu kwa kuwa hilo ni kosa lake la kwanza.
Chanzo: Mwananchi