Mshume Kiyate
JF-Expert Member
- Feb 27, 2011
- 6,768
- 894
Kijana Emanuel Didas Marshai (24), ambaye madaktari walikosea na kumfanyia upasuaji wa kichwa badala ya mguu wa kulia, anakamilisha mchakato wa kuishataki Serikali na kuidai fidia ya Sh800 milioni.
Kwa sasa mgonjwa huyo ambae alifanyiwa upasuaji huo Novemba Mosi, 2008 na Madaktari bingwa wa Kitengo cha Mifupa (MOI) cha Hospitali ya Taifa Muhimubili, amepooza upande wa kulia wa mwili wake. Wakili wake, Cornelius Kariwa alisema jana kwamba mchakatato huo umeanza ikiwa ni pamoja na kuwasilisha maombi mahakama ili ateuliwe mtu atakayesimamia haki za kisheria.
"Tunachofanya sasa ni kufungua maombi ili tupate power of attorney (nguvu ya kisheria) ya mtu atakayesimamia haki zake kwa sababu kwa sasa haongei na hana uamuzi,"alisema.
Wakili huyo alisema kuwa baada ya kupatikana kwa mtu huyu atakayesimamama mahakamani kutetea haki za Emanuel watafungua kesi ya madai ya Sh800 milioni. Ndugu wa mgonjwa huyo, Raymond Marshai alisema: "pamoja na serikali kukubali kuwa itamfidia ndugu yangu lakini hadi sasa hawajathibitisha kwa maandishi kuwa watamlipa fidia ili tuwe na ushahidi."
SOURCE: MWANANCHI SEP 3 2011
Kwa sasa mgonjwa huyo ambae alifanyiwa upasuaji huo Novemba Mosi, 2008 na Madaktari bingwa wa Kitengo cha Mifupa (MOI) cha Hospitali ya Taifa Muhimubili, amepooza upande wa kulia wa mwili wake. Wakili wake, Cornelius Kariwa alisema jana kwamba mchakatato huo umeanza ikiwa ni pamoja na kuwasilisha maombi mahakama ili ateuliwe mtu atakayesimamia haki za kisheria.
"Tunachofanya sasa ni kufungua maombi ili tupate power of attorney (nguvu ya kisheria) ya mtu atakayesimamia haki zake kwa sababu kwa sasa haongei na hana uamuzi,"alisema.
Wakili huyo alisema kuwa baada ya kupatikana kwa mtu huyu atakayesimamama mahakamani kutetea haki za Emanuel watafungua kesi ya madai ya Sh800 milioni. Ndugu wa mgonjwa huyo, Raymond Marshai alisema: "pamoja na serikali kukubali kuwa itamfidia ndugu yangu lakini hadi sasa hawajathibitisha kwa maandishi kuwa watamlipa fidia ili tuwe na ushahidi."
SOURCE: MWANANCHI SEP 3 2011