Aliyepasuliwa kichwa badala ya mguu adai Sh800 milioni

Mshume Kiyate

JF-Expert Member
Feb 27, 2011
6,768
894
Kijana Emanuel Didas Marshai (24), ambaye madaktari walikosea na kumfanyia upasuaji wa kichwa badala ya mguu wa kulia, anakamilisha mchakato wa kuishataki Serikali na kuidai fidia ya Sh800 milioni.
Kwa sasa mgonjwa huyo ambae alifanyiwa upasuaji huo Novemba Mosi, 2008 na Madaktari bingwa wa Kitengo cha Mifupa (MOI) cha Hospitali ya Taifa Muhimubili, amepooza upande wa kulia wa mwili wake. Wakili wake, Cornelius Kariwa alisema jana kwamba mchakatato huo umeanza ikiwa ni pamoja na kuwasilisha maombi mahakama ili ateuliwe mtu atakayesimamia haki za kisheria.
"Tunachofanya sasa ni kufungua maombi ili tupate power of attorney (nguvu ya kisheria) ya mtu atakayesimamia haki zake kwa sababu kwa sasa haongei na hana uamuzi,"alisema.
Wakili huyo alisema kuwa baada ya kupatikana kwa mtu huyu atakayesimamama mahakamani kutetea haki za Emanuel watafungua kesi ya madai ya Sh800 milioni. Ndugu wa mgonjwa huyo, Raymond Marshai alisema: "pamoja na serikali kukubali kuwa itamfidia ndugu yangu lakini hadi sasa hawajathibitisha kwa maandishi kuwa watamlipa fidia ili tuwe na ushahidi."
SOURCE: MWANANCHI SEP 3 2011
 
Labda angekuwa anaishi Ulaya lakini kibongobongo alie tu.

mkuu hata Ulaya hawakuanzia hapo walipo
jambo ktk fani ya kitabibu vitu kama hivi vinatokea,, lakini kwahili ni uzembe na kutokujali kulikokidhiri kwa serekali na taasisi zake

hata kama hawatamlipa kumbukumbu zitabaki kwa vizazi vijavyo
 
Labda angekuwa anaishi Ulaya lakini kibongobongo alie tu.
Mwita, hata hivyo hivyo pesa ni ndogo sana $500.000 kwa matatizo aliopata uko ulaya unapopasema angelipwa zaidi ya hiyo pesa unayoiona nyingi
 
mkuu hata Ulaya hawakuanzia hapo walipo&lt;br /&gt;<br />
jambo ktk fani ya kitabibu vitu kama hivi vinatokea,, lakini kwahili ni uzembe na kutokujali kulikokidhiri kwa serekali na taasisi zake&lt;br /&gt;<br />
&lt;br /&gt;<br />
hata kama hawatamlipa kumbukumbu zitabaki kwa vizazi vijavyo
&lt;br /&gt;<br />
&lt;br /&gt;<br />
Sijui sheria zinasemaje lakini hospitali nyingi zinazidiwa na idadi ya wagonjwa ukilinganisha na namba ya watumishi. Haishangazi kuona makosa kama haya, madogo au makubwa, kutokea katika mazingira kama hayo ya kazi. Hospitali za Ulaya ziko well equipped in terms of both staff and medical supplies so such cases are rare occurance.
 
ni sahihi kudai fidia lakini je ataipata hiyo haki na je msimamizi wake atakuwa sahihi???
 
Hawa ndugu zake wasipokuwa makini wakitegemea Serikali yetu watoe fidia, usishangae mkapewa kifuta jasho cha mgonjwa laki tatu
 
Labda angekuwa anaishi Ulaya lakini kibongobongo alie tu.

Umeona eheee! hii ndo serkali unayoitetea kutwa kucha humu JF!!!!! kama kawaida yenu wenye mawazo ya kitumwa, unadhani kila zuri lipo na linastahili kuwa ulaya huku ukidharau na kudhihaki watanzania wenzetu wenye mtazamo na hoja za kutuleta mbadiliko ya kimaendeleo.
 
Labda angekuwa anaishi Ulaya lakini kibongobongo alie tu.
&lt;br /&gt;<br />
&lt;br /&gt;<br />
mwongeze na hii: MWAMBIE AMENG'ATWA NA NDAMA! Na labda angekuwa ni huko Ulaya labda mwenye ndama angemlipa lakini hapa TZ labda mashetani watamlipa. Cha kufanya kwake ni kama amepona akatowe SADAKA pale alipoelekezaga IMANI yake!
 
Mtu asiye na uwezo wa kuamua anapataje uamuzi wa kuishtaki serikali?naomba nielimishwe.
 
Naona ubinadamu tumeusahau kabisa, unafikiri wewe unayemwambia mwenzio alie tu upo salama kihivyo! Ungetumia lugha nzuri kidogo maana hakupenda haya yampate. Tutumie angalao lugha nzuri kwenye kujibu au kuzungumzia mambo kama haya jamani, huh!

Labda angekuwa anaishi Ulaya lakini kibongobongo alie tu.
 
Mtu asiye na uwezo wa kuamua anapataje uamuzi wa kuishtaki serikali?naomba nielimishwe.
Sina utaalamu wa sheria lakini logically inawezekana mtu kuact on behalf, kwa mfano kama angekuwa na mke au watoto wanao uwezo kabisa wa kuact on his behalf, kwa ndugu hapo ndio sifahamu perhaps wanasheria wanajua zaidi ndio maana amezungumzia power of attorney
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom