Freed Freed
JF-Expert Member
- Jun 27, 2017
- 6,230
- 6,469
Wadau wa JF poleni na pilika zetu hizi za kila siku,
Hivi karibuni limetokea tukio la kuibwa mtoto wa miaka miwili ktk mji mdogo wa Kiomboi wilayani Iramba. Tukio hili lilitokea eneo la Soweto lenye watu wengi mjini hapo.
Aliyemuiba mtoto ni jirani ambaye ni mstaafu serikalini. Baada ya kumuiba mtoto huyo alimfungia kwake na inadaiwa Mzee huyu na Mkewe wana imani za kishirikina hivyo huenda ilikuwa kwa mambo ya makafara. Mzee huyu alishiriki vikao vyote vya mwano kama jirani ili kupanga namna ya kumpata mtoto huyu aliyepotea.
Za mwizi arobaini, wenye mtoto walimleta Mganga na mganga alisema mtoto kashikiliwa na jirani. Lahaulaaahh!!! Watu wakaivamia nyumba na kumkuta mtoto kafichwa akiwa na sufuria kubwa la wali. Mzee alipigwa kidogo na nyumba kuvunjwa vioo kabla polisi kufika na kumchukua na mtoto na pia wazazi wa mtoto.
Ajabu mzee huyu yupo mtaani anapeta kama kawaida. Hivi makosa ya utekaji watoto yamekaaje?
Hivi karibuni limetokea tukio la kuibwa mtoto wa miaka miwili ktk mji mdogo wa Kiomboi wilayani Iramba. Tukio hili lilitokea eneo la Soweto lenye watu wengi mjini hapo.
Aliyemuiba mtoto ni jirani ambaye ni mstaafu serikalini. Baada ya kumuiba mtoto huyo alimfungia kwake na inadaiwa Mzee huyu na Mkewe wana imani za kishirikina hivyo huenda ilikuwa kwa mambo ya makafara. Mzee huyu alishiriki vikao vyote vya mwano kama jirani ili kupanga namna ya kumpata mtoto huyu aliyepotea.
Za mwizi arobaini, wenye mtoto walimleta Mganga na mganga alisema mtoto kashikiliwa na jirani. Lahaulaaahh!!! Watu wakaivamia nyumba na kumkuta mtoto kafichwa akiwa na sufuria kubwa la wali. Mzee alipigwa kidogo na nyumba kuvunjwa vioo kabla polisi kufika na kumchukua na mtoto na pia wazazi wa mtoto.
Ajabu mzee huyu yupo mtaani anapeta kama kawaida. Hivi makosa ya utekaji watoto yamekaaje?