Uchaguzi 2020 Aliyemshauri Lissu baada ya kuadhibiwa na NEC anaweza kuendelea na shughuli za chama amemshauri vibaya

Kwa hiyo unataka kutuaminisha hata Raisi anakosea sasa hivi pale anapoendelea kufanya shughuli za urais wakati yuko kwenye kipindi cha kampeni? maana yake naye anafanya kampeni kwa sababu huwezi tenganisha mtu kwa nafasi mbili

Waliofikiri kama wewe ndiyo wale tunao waitaga POYOYO

leta hoja za maana siyo tunapoteza muda wetu kusma utumbo

wewe ndiyo mwenye ushauri mbaya sasa
 
Hakuna chochote. Leo nimemuona Charles Hillary wa Azam News akimhoji mwanasheria wa NEC na mjumbe wa kamati ya maadili bwana Kawishe kuhusiana na matembezi anayofanya Lissu hasa matukio ya leo 07 Oktoba kama amekiuka sheria za uchaguzi, lakini majibu yalikuwa kama ifuatavyo; "Lissu hajakiuka sheria kwani hajafanya kampeni"
 
Imeandikwa, kiburi si maungwana na mtoto mkaidi hawezi kufaidi hadi siku ya Iddi. Tundu Lissu anaingia katika kundi hili kwa kushauriwa vibaya au kukaidi ushauri mzuri.

1. Aliemshauri Lissu kuwa baada ya kuadhibiwa na Kamati ya Maadili ya NEC anaweza kuendelea na shughuli za Chama kama Makam Mwenyekiti wa Chama amemshauri vibaya.

Tundu Lissu ni mmoja, hakuna nafsi mbili ktk mtu mmoja. Popote atakapokuwa Tundu Lissu ndipo alipo Mgombea wa Urais wa Chadema na Makam wa Mwenyekiti wa Chadema. Hakuna mstari wowote wa kutenganisha kati ya Lissu Mgombea na Lissu M/Mwenyekiti.

Kukosekana kwa tofauti hiyo ndio maana popote alipo mgombea wa CCM, Dr. John Pombe Magufuli ndipo alipo Rais wa JMT. Huwezi kuutofautisha ugombea wa John Pombe Joseph Magufuli na Urais wake au Uenyekiti wake wa CCM. Hivyo hivyo huwezi kuutofautisha ugombea wa Tundu Lissu na Umakam Mwenyekiti wake vinginevyo ni kujidanganya tu.

Aliemshauri Lissu kuwa baada ya kuadhibiwa anaweza kuendelea na kazi za kisiasa amemdanganya, amemshauri vibaya na amempotosha bure. Anachagiza vurumai za bila sababu. Lissu ashauriwe vizuri, ugombea wake na Umakam Mwenyekiti wake ni alfa na Omega, huwezi kuvitenganisha. Kimoja kinaathiri kingine!

2. Aliemshauri Lissu kuwa, kufungua matawi ya Chama au kutembelea masoko sio shughuli za Kampeni amemshauri vibaya, amemdanganya. Ni bahati mbaya kuwa Lissu licha ya kuwa Mwanasheria amedanganyika kirahisi mno. Mazingira na wakati vinanguvu zaidi ktk kuamua kesi, Lissu anafahamu hilo. Hakuna mstari wowote unaotenganisha kufungua matawi ya chama, kutembelea masoko na shughuli za Kampeni kwa wakati huu. Wakati uliopo sasa na mazingira anayokwenda kutembelea Tundu Lissu ni ushahidi wa wazi kuwa ameamua kufanya kampeni kwa mlango mwingine. Ni kosa, ni ukaidi.

Kampeni ni hamasa, kampeni ni ushawishi. Kufungua matawi ya vyama ni hamasa na ushawishi kuwa Chama kipo hai, hii ni kampeni zaidi kuliko kufanya mkutano wa hadhara.
Kuwatembelea watu ktk soko na maeneo ya wazi ni hamasa na ushawishi pia. Watu waliosoma elimu maalumu watanielewa vzr hapa kwamba kuna lugha ya picha na alama. Unaweza kufika mahala bila kuongea jambo lolote, ukasabahi kwa ishara na kuondoka lkn mavazi yako na muda vika-deliver ujumbe uliokusudiwa kwa watu. Kwenda Kibaha, kukutana na Wanachama au Wananchi hata bila kuongea jambo lolote ni kampeni kwa Lissu. Kati ya nafasi ya Umakam Mwenyekiti na nafasi ya Ugombea Urais kwa Lissu inayotangulia kwa sasa ni ya Ugombea. Hii ni principle ya wakati!!

Ushauri:

1. Mwambieni Tundu Lissu akili nyingi mbele ni giza. Awasikilize wenzake, aachane na mpango huu hauna faida. Polisi watamzuia kwa sababu hawawezi kutofautisha Ugombea wake na Umakam Mwenyekiti wake. Sio Polisi tu, hata wewe huwezi kwa sababu hakuna tofauti hiyo.

Polisi ndicho chombo chenye dhamana ya kusimamia na kushurutisha utekelezaji wa sheria. Ninahisi wataendelea na kusimamia utaratibu huu bila kujali kwa sababu ni wajibu wao, tusiwalaumu.

2. Mwambieni Tundu Lissu aache kukifanya kichwa chake kigumu, kitavunjika na asipate dawa. Aache kutukana watu kila kukicha, binadamu tumeumbwa na vinyongo. Siku Polisi wakikinai kuitwa wajinga au siku wakitamani kuufanya ujinga hadharani itakua hatari kwa nchi yetu. Hii ni nchi yetu sote, tuilinde!!

3. Mwambieni Lissu, walio nyuma yake ni ndugu zake ktk Chama, ndugu zake ktk damu na ni Watanzania wenzetu. Asiwatumie vibaya, majuto ni mjukuu. Likitokea la kutokea hasara ya kwanza ni kwetu sisi kama nchi, aachane na mzaha huo. Ni kosa kutumia njia haramu kuutafuta mwisho halali, Ikulu mtu hawezi kwenda kwa kupita ktk mifereji ya damu za watu. Aache mara moja!!
#MitanoTenaKwaJPM.

Unataka kutuambia akizuiwa kufanya kampeni asiende sokoni kununua mahitaji yake au NEC watakuwa wanamnunulia.
Ndugu yangu umeandika sana lakini ufahamu kuwa Mbowe na timu yake wanafanya makusudi ili Lissu aangamie moja kwa moja.Mbowe ni smart,anajua Lissu ni mpenda Sifa na atalipokea hilo kwa haraka bila kufikiria athari zake.Kwa ujumla hawamtaki.
 
Aahaa tangu lini Mamba akamshauri Swala avuke mto wenye Mamba kusudi asijeliwa na SImba upande aliopo? ahaa kumbe imewauma saana kesho anaenda kumkatia ticket ya basi shangazi yake anayeelekea Singida, alikuja kumtembelea na kumpa pole ya kupigwarisasi..sipati picha sasa hivi Mamlaka zinavyochanganyikwa na maagizo kutoka chama tawalaili kumzuia kesho asienda ubungo kwa visingizio vya kusababisha msongamano usiokuwa na haja ...changamoto waliyonayo ni kwamba hawajui atakwenda saa ngapi au anaweza asiende kesho au akaenda usiku pia ahaa...yaani hizi akili ni balaa
 
Polisi kwa Lissu washalegea kwa bao 3 bila tayari.
Polisi wamdhuru Lissu kwani wao hawajipendi na familia zao?
Usiwaingize chaka wenzio ndugu!!
 
Ushauri wako ungekuwa na mashiko kama usingeonyesha wazi kuwa unamfanyia Mtu fulani kampeni.

Rudi tena ulikotoa au ulikopatia bandiko lako kisha uje kivingine.

Mimi ningekushauri kitu kimoja: Ingekuwa ni busara kama ungeweza kumshauri yule aliyeleta utengano kwenye Taifa letu. Watangulizi wake wote waliweza kutuweka pamoja kama Watz bila kujali tofauti zetu za Kisiasa Kikabila na Kidini.

Siasa ilikuwa na ladha yake hasa ktk kipindi kama hiki cha kampeni. Lkn kwa sasa wewe mwenyewe ni shahidi kwa yanayoendelea hivi sasa. Yaani ni uadui chuki na hata visasi.

Ushauri wangu ni kwamba kwa sasa kinachohitajika kutumiwa na Watendaji wote wa Serikali/Vyombo vya Dola pamoja na Tume ya Taifa ya Uchaguzi ni BUSARA NA SI VITISHO/UBABE kuliko wakati mwingine wowote.

Watz wengi wameumizwa sana ktk Uongozi wa awamu ya tano. Hivyo wengi wana majeraha mioyoni mwao. Hivyo kundi kubwa liko tayari kwa lolote kwani hivi sasa wamechoka kudharauliwa.
 
Ndugu yangu umeandika sana lakini ufahamu kuwa Mbowe na timu yake wanafanya makusudi ili Lissu aangamie moja kwa moja.Mbowe ni smart,anajua Lissu ni mpenda Sifa na atalipokea hilo kwa haraka bila kufikiria athari zake.Kwa ujumla hawamtaki.
Am smart too.
 
Back
Top Bottom