Aliyemfuata Rais Kikwete Ikulu apokewa kishujaa..................

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
219,470
911,173
Wednesday, 08 December 2010

NA PETER KATULANDA, GEITA

MKAZI wa Kasamwa wilayani Geita, Mussa Dotto, ambaye alitembea kwa baiskeli hadi Dar es Salaam, kumpongeza Rais Jakaya Kikwete, amerejea kijijini kwake na kupokelewa kishujaa.

Dotto (35), aliendesha baiskeli kutoka kijiji cha Chabulungo hadi Singida akiwa njiani kwenda Dar es Salaam, kumpongeza Rais Kikwete kwa kuchaguliwa kuongoza tena, alipokewa juzi huku akiwasilisha salamu za rais kwa kuwataka vijana kufanya kazi kwa bidii.

Aliwaeleza vijana wenzake kijijini hapo kuwa, hawana budi kusoma kwa bidii kwani ndiyo silaha ya mafanikio katika maisha.

Mapokezi na sherehe za kumpongeza Dotto, zilifanyika katika uwanja wa Shule ya Msingi Bungíwangoko na kuhudhuriwa viongozi mbalimbali wa CCM, wazazi na mamia ya wananchi.

"Rais Kikwete anawasalimia sana wana Bungíwangoko na Geita, anatuomba tujitahidi kuchapa kazi, vinginevyo tutaendelea kulaumu viongozi na kuichukia serikali," alisema huku akishangiliwa.


Alisema kuwa Rais Kikwete alimuasa kuwa kila mwananchi wakiwemo wakulima, watimize wajibu wao kwa kuchapa kazi na wasichukulie elimu kama jambo la mchezo.

"Vijana wenzangu Rais anatutaka tuchape kazi, maisha bora hayaji kwa kukaa tu bila kufanya kazi kwa bidii, wanafunzi someni kwa bidii, acheni kudharau elimu, maisha mazuri na bora yanataka elimu," alieleza.

Awali, Mwakilishi wa Rais Kikwete katika sherehe hizo, Joseph Makirikiri, alisema uhodari na mapenzi ya Chama alioonyesha Dotto yanapaswa kuigwa na vijana wengine.

Makirikiri, ambaye alionyesha kushtushwa na mapokezi hayo makubwa kwa Dotto, alisema wananchi wana kila sababu ya kufanya jambo kubwa la maendeleo kama kumbukumbu ya Dotto.

Katibu wa UVCCM wa Mkoa Mwanza Josephat Ndolango, alisema Dotto amekitangaza kijiji hicho na kwamba, hana budi kuenziwa na kusema milango ya CCM iko wazi kwa vijana wengine wenye nia kama yake.

Pamoja na zawadi za baiskeli mbili alizozawadiwa Dar es Salaam, Dotto pia alizawadiwa baiskeli nyingine na diwani wa Kata ya Nzela, Joseph Kasheku.
 
Vipi hakurudi kwa baiskeli tena? Ila bado siamini kama kweli aliendesha kwa mwendo huo wote..mwenye picha zake wakati yuko njiani atupandishie tafadhali..
 
Faida yake ni baiskeli 3,kwa kijijini ukiwa na baiskeli 3 tayari yeye ni tajiri kwa kuwa atakuwa akikodisha sh 200 kwa saa moja
 
Acha uzushi wako wewe unadanganya great thinkers, huyo mtu anatoka bagamoyo halafu mnapakaza geita kewnda zenu na propaganda zenu za uchakachuaji ili watu wasiseme mlichakachua bul..................................s.......................t wizi mtupuuuuuuuuuu mfike mahali mpate aibu jamani
 
Bungíwangoko?Nadhani ni mkazi wa kwanza kufika dar.
Sasa badala ya kumpa trekta la kumsaidia kwenye kilimo wanamjazia mabaiskeli ayafanyie nini?? CCM bwana.
 
baskeli tatu, waweza sasa kuzunguka tanzania yote bara na visiwani, yaonekani ni mwendeshaji mzuri, sipati picha hiyo miguu itakuwa na misuli kiwango gani. umekomaa kaka, nadhani kuna wenzio walio komaa kama wewe walikuja kukusaidia kurudi na hizo baskeli. hongera
 
Hana lolote huyo bongo lala!
Nguvu alizotumia kuendesha baskeli ni bora angezitumi kuchimba madini kwa sululu huko nyalugusu!
Kupanda/kuzawadiwa/kumiliki baiskeli kwa dunia ya sasa kutamsaidia nini?
Takataka!
 
wajinga kama hawa hawatakiwi kabisa.. wanafanya mambo kwa ushabiki wa kijinga
 
Huyo jamaa mpuuzi sana ,kwa lipi alilonalo Mkwere? yaani anashabikia uchakachuaji?? Kilichobaki awe anakodisha baiskeli kwa wanakijiji wenzake sh 200 kwa saa au awe anapakia abiria nasikia shinyanga hii biashara ya kusafirisha abiria kwa baiskeli inalipa kweli kweli :teeth:
 
....and a sad one, indeed.

Halafu mtu mzima miaka 35 bado anajiita kijana! Wa miaka 18 - 30 tuwaitaje, watoto?

No wonder taifa zima miaka 50 baada ya kupata uhuru, bado tunajiona ni taifa changa.

Kwani mkwere ana miaka mingapi?
Na mbona bado tunaambiwa ni Rais Kijana?
Yaani ni zero tu nchi hii
 
Watanzania bado ni maskini sana. Badala ya watu kukaa na kufanya maandamano kushinikiza katiba mpya, Tatizo la umeme, DOWANS, Bajeti fake na mengineyo eti tunafanya sherehe kumpongeza aliyetembea na baiskeli kwenda dar. Na hao Wasomi wa CHUO CHA KATA UDOM mbona hatuoni wakitoa tamko juu ya DOWANS na bajeti kukataliwa na wafadhili?
 
Ni mbinafsi ni kwa nini asinge organize waende wengi? na wawe na kauli mbiu moja nzuri yenye impact? alipandikizwa na hao hao!!
 
Vipi hakurudi kwa baiskeli tena? Ila bado siamini kama kweli aliendesha kwa mwendo huo wote..mwenye picha zake wakati yuko njiani atupandishie tafadhali..

Mazee hii paragraph unaielewa vipi? Au ni utovu wa umakini wa kawaida wa waandishi wetu tu ?

Dotto (35), aliendesha baiskeli kutoka kijiji cha Chabulungo hadi Singida akiwa njiani kwenda Dar es Salaam, kumpongeza Rais Kikwete kwa kuchaguliwa kuongoza tena, alipokewa juzi huku akiwasilisha salamu za rais kwa kuwataka vijana kufanya kazi kwa bidii.
 
Mazee hii paragraph unaielewa vipi? Au ni utovu wa umakini wa kawaida wa waandishi wetu tu ?
Paragraph ya kwanza ipo hivi
MKAZI wa Kasamwa wilayani Geita, Mussa Dotto, ambaye alitembea kwa baiskeli hadi Dar es Salaam, kumpongeza Rais Jakaya Kikwete, amerejea kijijini kwake na kupokelewa kishujaa.
 
Faida yake ni baiskeli 3,kwa kijijini ukiwa na baiskeli 3 tayari yeye ni tajiri kwa kuwa atakuwa akikodisha sh 200 kwa saa moja

Siwezi kuamini kama bado Tanzania kuna wajinga kiasi hiki. Whether this guy cycled from Geita or Bagamaoyo atakuwa ni mjinga wa mwaka. For what purpose? kama tukijua huko njiani alifanya nini, kama alihamaisha watu kuhusu jambo fulani la maana kwa jamii na kwa taifa naweza kukubaliana naye. Lakini kama ndio ule ujinga wa kutembea na kujitaftia sifa, atakuwa ni mjinga wa mwaka 2010.
Labda kama kweli lengo lake ni kupata baiskeli tatu na kufanya biashara ya kuzikodisha basi kweli ana akili sana.
 
Back
Top Bottom