chilamanyika
JF-Expert Member
- Nov 20, 2016
- 405
- 272
Hama hama ya vyama inazidi kushika kasi, Leo wakati tukiazimisha miaka 41 ya kuzaliwa kwa chama cha mapinduzi, chama hicho kimewapokea wanachama zaidi ya 50 kutoka CHADEMA akiwemo ndg James Mwanilyela aliekuwa mgombea wa ubunge jimbo la Kwela kupitia tiketi ya Chadema, hata hivyo Mbwana aliangushwa na mwenzake ndg Daniel Ngigo kwenye hatua ya kura za maoni.
Mwingine ni bwana Peter Kakondele pia alikua mgombea wa udiwani kata ya Laela kupitia Act wazalendo, katika hotuba yake wakati wa kupokea kadi ya CCM bwana James alisema "cdm kwa sasa wamekosa Sera na mipango kama chama kisichohitaji kushika dola, pia aliongeza na kusema CHADEMA ni kama kinyago kilicho chongwa na CCM kwa hiyo hakiwezi kuogopwa na wachongaji".
Kwa upande wake Kakondele alisema " kule act nilisukumizwa tu na nikabatizwa ubatizo usio wa kawaida, naomba kurudi kwa baba na nichinjiwe ndama kwani nimejuta kule nilikokuwa in utumwani".