Aliyekuwa mbunge wa Temeke Abbas Mtemvu atuhumiwa na nduguze kudhulumu mirathi

YEHODAYA

JF-Expert Member
Aug 9, 2015
36,908
51,904
Dar es Salaam. Ndugu wa mbunge wa zamani wa Temeke, Abbas Mtemvu, wamekata rufaa wakipinga uteuzi wake kuwa msimamizi wa mirathi ya marehemu mama yao, Joyce Kilungo.

Abbas aliteuliwa kuwa msimamizi wa mirathi hiyo na Mahakama ya Mwanzo, Temeke katika shauri la mirathi namba 474 la mwaka 2017.

Lakini ndugu zake wawili, Ibrahimu Mtemvu na Jasmine Mtemvu wamekata rufaa Mahakama ya Wilaya ya Temeke, katika Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki kuhusu Masuala ya Kifamili (ndoa, talaka na mirathi), Temeke.

Mbali na Ibrahim na Jasmine, warufani wengine ni watoto watano wa kaka zao wawili, George Mtemvu na Modibo Mtemvu pamoja na wa dada yao mmoja Amina Mtemvu waliofariki dunia.

Katika rufaa hiyo wanadai kuwa uteuzi wake si halali kwa kuwa hakuwahi kupendekezwa wala kuteuliwa na kikao cha familia kuwa msimamizi wa mirathi hiyo.

Wanadai kuwa alifungua shauri hilo kinyemela bila kuwashirikisha wala kufuata taratibu za kisheria na baada ya kuteuliwa amekuwa akiuza mali za mirathi kinyemela na kutumia pesa peke yake bila kuwashirikisha wala kuwajulisha.

Ndugu zake hao jana walilieleza Mwananchi kuwa Abbas ameshauza nyumba mbili za urithi, ikiwemo ya Masaki katika ploti namba 1036/2, Haile Selasie Road.

Ibrahim alilieleza Mwananchi nyumba hiyo Abbas alimuuzia Mustafa Mohamed, ambaye ni mkurugenzi wa kampuni ya Delligent Group, kwa gharama ya Sh 900 milioni na pesa zote akatumia peke yake.

Hata hivyo akizungumzia madai hao, Abbas alisema kuwa hawezi kutoa maoni yoyote kuhusu hilo kwa kuwa shauri bado liko mahakamani.

Hata hivyo, alisema kuwa ndugu zake hao walishajaribu kufungua kesi Mahakama ya Temeke na Mahakama Kuu lakini wameshindwa.

“Mimi siwezi kuongeza zaidi, naiachia tu mahakama ndiyo itakayoamua,” alisema Abbas.

Source: Gazeti Mwananchi
 
Namfahamu Abbas tangu akiwa DC kibaha na baadae Mbunge, alikua mtu wa hovyo asiyeelezeka lakini ungeshangaa ni kwa merits zipi alikua akipita kwenye michujo mizito ya CCM na hata kufikia nafasi za juu za heshima.

CCM inalea uchafu sana na anachofanya ndio reflection ya kokoro CCM

Wivi, uchimvi, uchawi, uzinzi, liwati, husuda na mambo mengi ya hovyo ndivyo vimejificha miongoni mwa wana CCM.
 
Namfahamu Abbas tangu akiwa DC kibaha na baadae Mbunge, alikua mtu wa hovyo asiyeelezeka lakini ungeshangaa ni kwa merits zipi alikua akipita kwenye michujo mizito ya CCM na hata kufikia nafasi za juu za heshima.

CCM inalea uchafu sana na anachofanya ndio reflection ya kokoro CCM

Wivi, uchimvi, uchawi, uzinzi, liwati, husuda na mambo mengi ya hovyo ndivyo vimejificha miongoni mwa wana CCM.
Nakazia.....

Ova
 
Namfahamu Abbas tangu akiwa DC kibaha na baadae Mbunge, alikua mtu wa hovyo asiyeelezeka lakini ungeshangaa ni kwa merits zipi alikua akipita kwenye michujo mizito ya CCM na hata kufikia nafasi za juu za heshima.

CCM inalea uchafu sana na anachofanya ndio reflection ya kokoro CCM

Wivi, uchimvi, uchawi, uzinzi, liwati, husuda na mambo mengi ya hovyo ndivyo vimejificha miongoni mwa wana CCM.
1660090_FB_IMG_1514731600839.jpg
 
Dar es Salaam. Ndugu wa mbunge wa zamani wa Temeke, Abbas Mtemvu, wamekata rufaa wakipinga uteuzi wake kuwa msimamizi wa mirathi ya marehemu mama yao, Joyce Kilungo.

Abbas aliteuliwa kuwa msimamizi wa mirathi hiyo na Mahakama ya Mwanzo, Temeke katika shauri la mirathi namba 474 la mwaka 2017.

Lakini ndugu zake wawili, Ibrahimu Mtemvu na Jasmine Mtemvu wamekata rufaa Mahakama ya Wilaya ya Temeke, katika Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki kuhusu Masuala ya Kifamili (ndoa, talaka na mirathi), Temeke.

Mbali na Ibrahim na Jasmine, warufani wengine ni watoto watano wa kaka zao wawili, George Mtemvu na Modibo Mtemvu pamoja na wa dada yao mmoja Amina Mtemvu waliofariki dunia.

Katika rufaa hiyo wanadai kuwa uteuzi wake si halali kwa kuwa hakuwahi kupendekezwa wala kuteuliwa na kikao cha familia kuwa msimamizi wa mirathi hiyo.

Wanadai kuwa alifungua shauri hilo kinyemela bila kuwashirikisha wala kufuata taratibu za kisheria na baada ya kuteuliwa amekuwa akiuza mali za mirathi kinyemela na kutumia pesa peke yake bila kuwashirikisha wala kuwajulisha.

Ndugu zake hao jana walilieleza Mwananchi kuwa Abbas ameshauza nyumba mbili za urithi, ikiwemo ya Masaki katika ploti namba 1036/2, Haile Selasie Road.

Ibrahim alilieleza Mwananchi nyumba hiyo Abbas alimuuzia Mustafa Mohamed, ambaye ni mkurugenzi wa kampuni ya Delligent Group, kwa gharama ya Sh 900 milioni na pesa zote akatumia peke yake.

Hata hivyo akizungumzia madai hao, Abbas alisema kuwa hawezi kutoa maoni yoyote kuhusu hilo kwa kuwa shauri bado liko mahakamani.

Hata hivyo, alisema kuwa ndugu zake hao walishajaribu kufungua kesi Mahakama ya Temeke na Mahakama Kuu lakini wameshindwa.

“Mimi siwezi kuongeza zaidi, naiachia tu mahakama ndiyo itakayoamua,” alisema Abbas.

Source: Gazeti Mwananchi
Kuishi kwa kutegemea mirathi ni ufinyu wa akili
 
Namfahamu Abbas tangu akiwa DC kibaha na baadae Mbunge, alikua mtu wa hovyo asiyeelezeka lakini ungeshangaa ni kwa merits zipi alikua akipita kwenye michujo mizito ya CCM na hata kufikia nafasi za juu za heshima.

CCM inalea uchafu sana na anachofanya ndio reflection ya kokoro CCM

Wivi, uchimvi, uchawi, uzinzi, liwati, husuda na mambo mengi ya hovyo ndivyo vimejificha miongoni mwa wana CCM.
Hivi mtu wa hovyo anakuwa na sifa gani,tofauti na watu wengineo.
 
Back
Top Bottom